< Salamo 143 >
1 Sabo’ i Davide Ry Iehovà, janjiño ty filolohako, atokilaño mb’amo halalikoo ty ravembia’o ty amo figahiña’oo naho o havantaña’oo.
Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, sikia sala yangu, sikiliza kilio changu unihurumie; katika uaminifu na haki yako njoo unisaidie.
2 Ko ampanesefe’o an-jaka ty mpitoro’o; fa tsi-mbia tsy ho añatrefa’o ty veloñe.
Usimhukumu mtumishi wako, kwa kuwa hakuna mtu anayeishi aliye mwenye haki mbele zako.
3 Fa nampisòañe ty fiaiko o rafelahio, nigorè’e an-tane ty haveloko; nampitoboheñe añ’ieñe ao, manahake t’ie nilolo ela.
Adui hunifuatilia, hunipondaponda chini; hunifanya niishi gizani kama wale waliokufa zamani.
4 Aa le mitsikorak’ amako ty troko; mioremeñe ty añovako ao.
Kwa hiyo roho yangu inazimia ndani yangu, moyo wangu ndani yangu unakata tamaa.
5 Tiahiko o andro taoloo, niniheko iaby o fitoloña’oo tsakorèko o satam-pità’oo.
Nakumbuka siku za zamani; natafakari juu ya kazi zako zote, naangalia juu ya kazi ambazo mikono yako imezifanya.
6 Ahitiko mb’ama’o o tañakoo; limpoañe ty ama’o ty fiaiko hoe tane mivaràkivaràky. Selà
Nanyoosha mikono yangu kwako, nafsi yangu inakuonea kiu kama ardhi kame.
7 Toiño masìka ry Iehovà; fa mimoremoretse ty troko. ko aeta’o amako ty lahara’o (hera) hanahake o mizotso mb’an-kaly aoo.
Ee Bwana, unijibu haraka, roho yangu inazimia. Usinifiche uso wako, ama sivyo nitafanana na wale washukao shimoni.
8 Ampitsanoño ahy ty fiferenaiña’o te maraiñe, amy te Ihe ro iatoako. ampandrendreho ty lala hombako, fa ama’o ty fañonjonañe ty fiaiko.
Asubuhi uniletee neno la upendo wako usiokoma, kwa kuwa nimeweka tumaini langu kwako. Nionyeshe njia nitakayoiendea, kwa kuwa kwako nainua nafsi yangu.
9 Ihahao amo rafelahikoo, ry Iehovà; Ihe ro fitsolohako.
Ee Bwana, uniokoe na adui zangu, kwa kuwa nimejificha kwako.
10 Anaro ahy ty hanao o satri’oo, Ihe ro Andrianañahareko; le ampiaolò ahy an-tane mira ty Arofo’o soa.
Nifundishe kufanya mapenzi yako, kwa maana wewe ndiwe Mungu wangu, Roho wako mwema na aniongoze katika nchi tambarare.
11 Isotrafo amy tahina’oy, ry Iehovà, afaho amo hasosorañeo, ty amy havantaña’oy.
Ee Bwana, kwa ajili ya jina lako, hifadhi maisha yangu, kwa haki yako nitoe katika taabu.
12 Aitò amako o rafelahikoo ty amy fiferenaiña’oy, vaho fonga rotsaho o mitsibore ty fiaikoo, fa mpitoro’o iraho.
Kwa upendo wako usiokoma, nyamazisha adui zangu; waangamize watesi wangu wote, kwa kuwa mimi ni mtumishi wako.