< Nomery 8 >
1 Le hoe ty nitsara’ Iehovà amy Mosè:
Bwana akamwambia Mose,
2 Saontsio amy Aharone vaho ano ty hoe: Ie hañajary o jiroo, le ampañazavao mb’aolo mb’eo i fitàn-jiroy i jiro fito rey.
“Sema na Aroni umwambie, ‘Wakati utakapoziweka zile taa saba, zinatakiwa kuangaza eneo lililo mbele ya kinara cha taa.’”
3 Le nanoe’ i Aharone izay; nalaha’e i jiro rey hañazava’e mañaolo i fitàn-jiroy amy nandilia’ Iehovà i Mosè.
Aroni akafanya hivyo; akaziweka zile taa ili zielekee mbele kwenye kinara cha taa, kama vile Bwana alivyomwamuru Mose.
4 Inao ty nanoeñe i fitàn-jiroy: volamena pinepeke i taho’ey pak’ amboñe’e eo; toe satam-pipepehañe, amy sare natoro’ Iehovà amy Mosèy, izay ty nanoe’e i fitàn-jiroy.
Hivi ndivyo kinara cha taa kilivyotengenezwa: Kilitengenezwa kwa dhahabu iliyofuliwa, kuanzia kwenye kitako chake hadi kwenye maua yake. Kinara cha taa kilitengenezwa sawasawa kabisa na kielelezo ambacho Bwana alikuwa amemwonyesha Mose.
5 Le hoe ty nitsara’ Iehovà amy Mosè:
Bwana akamwambia Mose:
6 Aviho amo ana’ Israeleo o nte-Levio vaho efero.
“Watwae Walawi kutoka miongoni mwa Waisraeli wengine na uwatakase kwa kawaida ya ibada.
7 Zao ty hañefera’o iareo: amitsezo am’ iereo ty ranon’ enga-kakeo, le ampiozàñem-piharatse ty fañòva’ iareo iaby, naho ampanasao sikiñe vaho ampiliovo.
Ili kuwatakasa fanya hivi: Nyunyizia maji ya utakaso juu yao; kisha uwaambie wanyoe nywele kwenye mwili mzima, wafue nguo zao na hivyo wajitakase wenyewe.
8 Le ampangalao iareo ty bania rekets’ i enga-mahakama’ey, i mona linaro menakey, vaho ampangalao bania raike ho engan-kakeo.
Waambie wamchukue fahali mchanga pamoja na sadaka yake ya nafaka ya unga laini uliochanganywa na mafuta; kisha utamchukua fahali mchanga wa pili kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
9 Le aseseo mb’ añatrefa’ i kibohom-pamantañañey mb’eo o nte-Levio vaho atontono ty valobohò’ Israele;
Walete Walawi mbele ya Hema la Kukutania na ukusanye jumuiya yote ya Waisraeli.
10 Aa naho fa navori’o añatrefa’ Iehovà o nte-Levio le hanampe fitàñe amo nte-Levio o ana’ Israeleo;
Utawaleta Walawi mbele za Bwana, na Waisraeli wataweka mikono yao juu ya Walawi.
11 le hengae’ i Aharone ho engan-kelahela am’ Iehovà o nte-Levy boak’ amo ana’ Israeleoo hitoroñe Iehovà.
Aroni atawaweka Walawi mbele za Bwana kama sadaka ya kuinua kutoka kwa Waisraeli, ili kwamba wawe tayari kuifanya kazi ya Bwana.
12 Le hanampeza’ o nte-Levio fitàñe i bania rey, naho hengae’o ho engan-kakeo ty raike vaho ho soroñañe am’ Iehovà ty raike, hijebaña’o o nte-Levio.
“Baada ya Walawi kuweka mikono yao juu ya vichwa vya hao mafahali wawili, tumia mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi kwa Bwana, na mwingine kuwa sadaka ya kuteketezwa, ili kufanya upatanisho kwa ajili ya Walawi.
13 Aa le ajohaño añatrefa’ i Aharone naho o ana’eo o nte-Levio vaho engao am’ Iehovà ho engan-kelahela.
Waambie hao Walawi wasimame mbele ya Aroni na wanawe, kisha wawatoe kama sadaka ya kuinuliwa kwa Bwana.
14 Izay ty hañambaha’o amo ana’ Israeleo o nte-Levio le ho ahiko o nte-Levio.
Kwa njia hii utakuwa umewatenga Walawi kutoka kwa Waisraeli wengine, nao Walawi watakuwa wangu.
15 Henane zay, himoake hitoroñe amy kibohom-pamantañañey o nte-Levio, ie fa neferañe naho nengaeñe ho engan-kelahela.
“Utakapokuwa umekwisha kuwatakasa Walawi na kuwatoa kama sadaka ya kuinuliwa, watakuja kufanya kazi yao katika Hema la Kukutania.
16 Songa natolotse ahiko boak’ amo ana’ Israeleo; fa rinambeko ho amako ho solo’ ze hene manoka-koviñe; ze fonga tañoloñoloñan’ ana’ Israele.
Wao ndio Waisraeli ambao watatolewa kabisa kwangu. Nimewatwaa kama mali yangu mwenyewe badala ya mzaliwa wa kwanza, mzaliwa wa kwanza wa kiume kutoka kwa kila mwanamke wa Kiisraeli.
17 Toe anjarako ze hene valohan’ ana’ o ana’ Israeleo, ondaty naho hare; tamy andro nipaohako ze fonga valohan’ ana’ i Mitsraimey ty nañambahako iareo ho ahy.
Kila mzaliwa wa kwanza wa kiume katika Israeli, awe wa mwanadamu au mnyama, ni wangu. Wakati nilipowaua wazaliwa wote wa kwanza huko Misri, niliwatenga kwa ajili yangu mwenyewe.
18 Le rinambeko ho soloe’ o nte-Levio o tañoloñoloñan’ ana’ Israeleo;
Nami nimewatwaa Walawi badala ya wazaliwa wote wa kwanza wa kiume katika Israeli.
19 vaho natoloko amy Aharone naho amo ana’eo aivo o ana’ Israeleo ho ravoravo o nte-Levio, hitoloñe ami’ty fitoloña’ o ana’ Israeleo amy kibohom-pamantañañey, naho hanao fijebañañe ho amo ana’ Israeleo tsy mone hiboak’ amo ana’ Israeleo ty angorosy naho harinea’ o ana’ Israeleo i efe-miavakey.
Kati ya Waisraeli wote, nimempa Aroni na wanawe Walawi kama zawadi ili wafanye kazi katika Hema la Kukutania kwa niaba ya Waisraeli, na kufanya upatanisho kwa ajili yao ili pasiwepo na pigo lolote litakalowapata Waisraeli wakati watakapokaribia mahali patakatifu.”
20 Izay ty nanoe’ i Mosè naho i Aharone vaho ty valobohò’ Israele amo nte-Levio; ze hene nandilia’ Iehovà i Mosè ty amo nte-Levio ty nanoe’ o ana’ Israeleo.
Mose, Aroni na jumuiya yote ya Waisraeli wakawafanyia Walawi kama Bwana alivyomwamuru Mose.
21 Le nañalio vatañe o nte-Levio naho nanasa’ o siki’eo iareo, naho nengae’ i Aharone am’ Iehovà ho ravoravo miavake, vaho nanao fijebañañe hañaliova’e iareo.
Walawi wakajitakasa wenyewe na wakafua nguo zao. Kisha Aroni akawasogeza mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa, na kufanya upatanisho kwa ajili yao ili kuwatakasa.
22 Ie henane zay nimoak’ an-kibohom-pamantañañe ao o nte-Levio hitoloñe añatrefa’ i Aharone naho o ana’eo; i nandilia’ Iehovà amy Mosè ty amo nte-Levio ty nanoañe am’iareo.
Baada ya hayo, Walawi walikuja kufanya kazi yao katika Hema la Kukutania chini ya usimamizi wa Aroni na wanawe. Waliwafanyia Walawi kama vile Bwana alivyomwamuru Mose.
23 Le hoe ty nitsara’ Iehovà amy Mosè:
Bwana akamwambia Mose,
24 Inao ty amo nte-Levio: ie roapolo-taoñe lim’ amby mañambone ro hizilike hitoloñe an-kibohom-pamantañañe ao;
“Hili linawahusu Walawi: Wanaume wenye umri wa miaka ishirini na mitano au zaidi watakuja kushiriki katika kazi kwenye Hema la Kukutania,
25 ie limampolo taoñe ro hitroatse amo fitoroña’eo, le tsy hitoloñe ao ka.
lakini watakapofika umri wa miaka hamsini, ni lazima waache kazi zao za kawaida wala wasiendelee.
26 F’ie mete hañimba o rahalahi’eo an-kibohom-pamantañañe ao, hisary o tolon-draha’eo fe tsy hitromake. Izay ty hanoe’o amo nte-Levio amo fitoloña’eo.
Wanaweza kuwasaidia ndugu zao kufanya wajibu wao katika Hema la Kukutania, lakini wao wenyewe kamwe hawatafanya hiyo kazi. Basi, hivi ndivyo utakavyogawa wajibu kwa Walawi.”