< Matio 20 >
1 Ie añe izay le hoe t’i Iesoà amo mpiama’eo: Ampanahafeñe ami’ty talèn’ anjomba, i fifehean-dikerañey, ie nañaleñaleñe nañèke ondaty ho amy tetem-bahe’ey.
“Kwa maana Ufalme wa Mbinguni unafanana na mtu mwenye shamba aliyetoka alfajiri ili kwenda kuajiri vibarua kufanya kazi katika shamba lake la mizabibu.
2 Naè’e ami’ty bogady raike iereo ho ami’ty andro raike, le nirahe’e mb’an-tetem-bahe’e mb’eo.
Baada ya kukubaliana na hao vibarua kuwalipa ujira wa dinarimoja kwa siku, akawapeleka kwenye shamba lake la mizabibu.
3 Niavotse indraike re ami’ty ora faha telo vaho nitendreke ondaty nisarasara an-tsena ao,
“Mnamo saa tatu akatoka tena, akawakuta wengine wamesimama sokoni bila kazi.
4 hoe re tam’ iereo: Akia mb’an-teteko ao ka, vaho hatoloko anahareo ze mañeva. Le nimb’eo iereo.
Akawaambia, ‘Ninyi nanyi nendeni mkafanye kazi katika shamba langu la mizabibu, nami nitawalipa chochote kilicho haki yenu.’
5 Niavotse indraike re nanao if zay ami’ty ora fah’ eneñe naho amy faha-sivey, le nampanahafe’ amy teoy.
Kwa hiyo wakaenda. “Akatoka tena mnamo saa sita na pia saa tisa akafanya vivyo hivyo.
6 Niakatse amy ora faha folo-raik’ ambiy re nahaoniñe ty ila’e nihenekeneke ey, le hoe ty nanoa’e: Akore t’ie mijohajohañe etoañe lomoñandro?
Mnamo saa kumi na moja akatoka tena akawakuta wengine bado wamesimama bila kazi. Akawauliza, ‘Kwa nini mmesimama hapa kutwa nzima pasipo kufanya kazi?’
7 Hoe ty natoi’ iareo: Ie tsy amam-pañeke, le hoe re am’iereo: Akia mb’an-teteko mb’eo ka.
“Wakamjibu, ‘Ni kwa sababu hakuna yeyote aliyetuajiri.’ “Akawaambia, ‘Ninyi nanyi nendeni mkafanye kazi katika shamba langu la mizabibu.’
8 Ie hariva, hoe ty asa’ i talèn-tetem-bahey amy mpisarim-piekey: Ikoiho hanolorako ty karama’ iareo, mifototse ami’ty fara’e, pak’ ami’ty valoha’e.
“Ilipofika jioni, yule mwenye shamba la mizabibu akamwambia msimamizi, ‘Waite hao vibarua na uwalipe ujira wao, ukianzia na wale walioajiriwa mwisho na kuishia na wale walioajiriwa kwanza.’
9 Nandrambe bogady raike o am-para’eo.
“Wale vibarua walioajiriwa mnamo saa kumi na moja, wakaja na kila mmoja wao akapokea dinari moja.
10 Aa le natao’ o valoha’eo t’ie ho nandrambe mandikoatse, te mone songa natolo’e bogady raike.
Hivyo wale walioajiriwa kwanza walipofika, walidhani watalipwa zaidi. Lakini kila mmoja wao pia alipokea dinari moja.
11 Le nitreontreoñe amy talèn-tetem-bahey i valoha’e rey
Walipoipokea, wakaanza kulalamika dhidi ya yule mwenye shamba,
12 ami’ty hoe: Ora raike ty nitoloña’ i fara’e retia, fe nampirae’o ama’ay nifanehake ami’ty hatrovoha’ i àndroy.
wakisema, ‘Hawa watu walioajiriwa mwisho wamefanya kazi kwa muda wa saa moja tu, nawe umewafanya sawa na sisi ambao tumestahimili taabu na joto lote la mchana kutwa?’
13 Tinoi’e ty hoe ty raike ama’e: O rañeko, Tsy nanoeko ama’o ty tsi-to; tsy nañeke azo ami’ty bogady raike hao?
“Yule mwenye shamba akamjibu mmoja wao, ‘Rafiki, sijakudhulumu. Je, hukukubaliana nami kwa ujira wa kawaida wa dinari moja?
14 Rambeso le akia, he satriko ty manolotse ami’ty hengaha’e tia mira amy azoy,
Chukua ujira wako na uende. Mimi nimeamua kumlipa huyu mtu aliyeajiriwa mwisho kama nilivyokupa wewe.
15 tsy mete hao te hanoeko i satrikoy? maha-mandofirim-pihaino’o hao te izaho matarike?
Je, sina haki yangu kufanya kile nitakacho na mali yangu mwenyewe? Au unaona wivu kwa kuwa nimekuwa mkarimu?’
16 Aa le ho valoha’e ty fara’e, vaho ho fara’e ty valoha’e. Maro ty koiheñe fe tsy ampeampe ty ho joboñeñe.
“Vivyo hivyo, wa mwisho watakuwa wa kwanza, na wa kwanza watakuwa wa mwisho.”
17 Ie narivo’ Ierosaleme t’i Iesoà, le natola’e i mpiama’e folo ro’amby rey, vaho nanoa’e ty hoe:
Basi Yesu alipokuwa anapanda kwenda Yerusalemu, aliwachukua kando wale wanafunzi wake kumi na wawili na kuwaambia,
18 Inao! mionjoñe mb’e Ierosaleme mb’eo tika; le hatolotse amo Androanavy naho mpisoroñe lohà’eo i Ana’ ondatiy vaho hafà’ iereo havetrake,
“Tunapanda kwenda Yerusalemu, na Mwana wa Adamu atatiwa mikononi mwa viongozi wa makuhani na walimu wa sheria. Nao watamhukumu kifo
19 le hasese amo kilakila ondatio ho lafañe naho hohofan-doza; f’ie hitroatse ami’ty andro fahatelo.
na kumtia mikononi mwa watu wa Mataifa ili wamdhihaki na kumpiga mijeledi na kumsulubisha msalabani. Naye atafufuliwa siku ya tatu!”
20 Nimb’ama’e mb’eo ty tañanjomba’ i Zebedia rekets’ i ana’e rey, niambane vaho nihalaly ama’e.
Kisha mama yao wana wa Zebedayo akamjia Yesu pamoja na wanawe, naye akapiga magoti mbele yake, akamwomba Yesu amfanyie jambo fulani.
21 Hoe re tama’e: Inoñe o paia’oo? le hoe re. Te ihe handily ty amo anako roe retoañe te hitoboke am-pità’o havàna eo ty raike vaho ankavia’o eo ty raike am-pifehea’o ao.
Yesu akamuuliza, “Unataka nini?” Akajibu, “Tafadhali, wajalie wanangu hawa ili mmoja aketi upande wako wa kuume, na mwingine upande wako wa kushoto katika Ufalme wako.”
22 Natoi’ Iesoà ty hoe: Tsy apota’ areo ty halali’ areo. Lefe’ areo hao ty hinoñe amy fitovy hinomakoy? Tinoi’ iereo ty hoe: Lefe’ay.
Yesu akawaambia, “Ninyi hamjui mnaloliomba. Je, mnaweza kukinywea kikombe nitakachonywea mimi?” Wakajibu, “Tunaweza.”
23 Le hoe re am’iereo: Nomo i fitovikoy, fe ty hiambesatse an-kavanako naho an-kaviako eo, tsy ahiko hatolotse, fa ho a i nihalankañañe aze aolon-dRaey.
Yesu akawaambia, “Kwa kweli kikombe changu mtakinywea, lakini kuketi upande wangu wa kuume au wa kushoto si langu mimi kuwapa. Nafasi hizo ni za wale ambao wameandaliwa na Baba yangu.”
24 Ie jinanji’ i folo rey, le nitorifiheñe am-pihaino’ iareo i mpirahalahy roe rey.
Wale wanafunzi wengine kumi waliposikia haya, waliwakasirikia hao ndugu wawili.
25 Tsinikao’ Iesoà iereo, le nanoa’e ty hoe: Fohino te felehe’ o roandria’ ze kilakila ondatio iereo, naho mifehe’iareo ka ty bey.
Lakini Yesu akawaita wote pamoja na kuwaambia, “Mnafahamu kuwa watawala wa watu wa Mataifa huwatawala kwa nguvu, nao wenye vyeo huonyesha mamlaka yao.
26 Tsy ho izay ty ama’ areo, amy te, ze mipay ho bey ama’areo le ampitoroño anahareo,
Isiwe hivyo kwenu. Badala yake, yeyote anayetaka kuwa mkuu miongoni mwenu hana budi kuwa mtumishi wenu,
27 vaho ze te ho jabajaba ama’areo ty h’ondevo’ areo,
naye anayetaka kuwa wa kwanza miongoni mwenu hana budi kuwa mtumwa wenu:
28 manahake te tsy niavy ho toroñeñe i Ana’ ondatiy, fa ty hitoroñe, hanolo-batañe ho vilin’ ai’ i màroy.
kama vile ambavyo Mwana wa Adamu hakuja ili kutumikiwa, bali kutumika na kuutoa uhai wake uwe fidia kwa ajili ya wengi.”
29 Nigodañe e Hieriko ao iereo, ie norihe’ i lahialeñey.
Yesu na wanafunzi wake walipokuwa wakiondoka Yeriko, umati mkubwa wa watu ulimfuata.
30 Ingo niakatse mb’ añ’olon-dalañe mb’eo ty ‘ndaty fey roe naho nahajanjiñe ty fizakozakoa’ i lahialeñey le nañontane ty ama’e, naho nisaontsiañe te mañavelo mb’eo t’Iesoà nte-Nazareta, vaho nipoñafa’ iereo ty hoe: Ry Ana’ i Davide, ferenaiño zahay.
Vipofu wawili walikuwa wameketi kando ya barabara. Waliposikia kwamba Yesu alikuwa anapita, wakapiga kelele wakisema, “Bwana, Mwana wa Daudi, tuhurumie!”
31 Fe nendaha’ i lahialeñey ami’ty hoe: Mamatsy; te mone nindrae’ iereo am-pazake ty hoe: O Rañandria, Ana’ i Davide, itretrezo.
Ule umati wa watu ukawakemea na kuwaambia wanyamaze, lakini wao wakazidi kupaza sauti, wakisema, “Bwana, Mwana wa Daudi, tuhurumie.”
32 Nijohañe t’i Iesoà, le kinanji’e, vaho nanoa’e ty hoe: Inoñe o paia’ areo hanoeko?
Yesu akasimama na kuwaita, akawauliza, “Mnataka niwafanyie nini?”
33 Hoe iareo: O Rañandria, ty hampibarababeake o maso’aio.
Wakamjibu, “Bwana, tunataka kuona.”
34 Niferenaiña’ Iesoà, le tsinapa’e o fihaino’ iareoo, naho nanoa’e ty hoe: Nampijangañe anahareo ty fatokisa’ areo, le nahaisake amy zao iereo naho nandrenge an’ Andrianañahare naho nañorike aze vaho hene nañonjoñe an’Andrianañahare ondatio ty am’izay.
Yesu akawahurumia na kuwagusa macho yao. Mara macho yao yakapata kuona, nao wakamfuata.