< Jaona 21 >

1 Añe irezay, le niboak’ amo mpi­ama’eo indraike t’Iesoà an-driake Tiberiasy eo; le zao ty niboaha’e:
Baada ya haya Yesu akawatokea tena wanafunzi wake kando ya Bahari ya Tiberia. Yeye alijionyesha kwao hivi:
2 Nifandrimboñe t’i Simona Petera naho i Tomasy atao Didimo, naho i Natanaela nte-Kana’ i Galilia miharo amy ana’ i Zebedio rey vaho ty mpiama’e roe ila’e.
Simoni Petro, Tomaso aitwaye Didimasi, yaani Pacha, Nathanaeli wa Kana ya Galilaya, wana wa Zebedayo na wanafunzi wengine wawili walikuwa pamoja.
3 Le hoe t’i Simona Petera tam’ iereo: Hikara fian-draho. Hoe iereo tama’e: Hindre ama’o zahay. Aa le nionjom-beo iereo vaho nijon-dakañe, fe tsy nahazo leo raik’ amy haleñey.
Simoni Petro akawaambia wenzake, “Mimi naenda kuvua samaki.” Nao wakamwambia, “Tutakwenda pamoja nawe.” Wakatoka, wakaingia ndani ya mashua, lakini usiku ule hawakupata chochote.
4 Aa ie nanjirike i àndroy, nijohañe añ’olotse ey t’Iesoà, fe tsy napota’ o mpiama’eo t’ie Iesoà.
Mara baada ya kupambazuka, Yesu akasimama ufuoni, lakini wanafunzi hawakumtambua kwamba alikuwa Yesu.
5 Le hoe t’Iesoà tam’ iereo: O Anake, nahazo fiañe v’inahareo? Hoe ty natoi’ iareo aze: Aiy.
Yesu akawaambia, “Wanangu, je, mna samaki wowote?” Wakamjibu, “La.”
6 Le nanoa’e ty hoe: Ahifiho an-kavana’ o lakañeo i haratoy handrendreke. Aa le nahifi’ iereo, fe tsy nahatarike i haratoy ami’ty fifamorohota’ o fiañeo.
Akawaambia, “Shusheni nyavu upande wa kuume wa mashua yenu nanyi mtapata samaki.” Wakashusha nyavu na tazama wakapata samaki wengi mno hata wakashindwa kuvutia zile nyavu zilizojaa samaki ndani ya mashua.
7 Aa le hoe i mpiama’e nikokoa’ Iesoày amy Petera: I Talè ‘nio. Ie jinanji’ i Simona Petera t’ie i Talè, le nidiaña’e ty saro’e, (amy t’ie nihalo), le nijorobo an-driak’ ao.
Yule mwanafunzi aliyependwa na Yesu akamwambia Petro, “Huyu ni Bwana!” Simoni Petro aliposikia haya, akajifunga nguo yake kwa kuwa alikuwa uchi, naye akajitosa baharini.
8 Nanonjohy amy lakañey o mpiama’e ila’eo; tsy nilavitse i olon-driakey fa niha-roanjato kiho avao, le nikororohe’ iereo i harato vokatse fiañey.
Wale wanafunzi wengine wakaja kwa ile mashua huku wakikokota ule wavu uliyojaa samaki, maana hawakuwa mbali na nchi kavu, ilikuwa yapata dhiraa 200
9 Ie nitoly an’ tamboho ey iereo, ro nahaoniñe foroha mirekake naho fiañe misale ama’e vaho mofo.
Walipofika ufuoni, wakaona moto wa makaa na samaki wakiokwa juu yake na mikate.
10 Hoe t’Iesoà tama’e: Andeso amo fiañe niazo’ areoo.
Yesu akawaambia, “Leteni baadhi ya hao samaki mliovua sasa hivi.”
11 Niongake t’i Petera le nikororohe’e mb’an-tamboho mb’eo i harato vokatse fiañe jabajabay, toe zato tsy limampolo telo amby; fe tsy nianto i haratoy ndra te nimaro.
Simoni Petro akapanda kwenye mashua na kuukokota ule wavu pwani. Ulikuwa umejaa samaki wakubwa 153. Ingawa samaki walikuwa wengi kiasi hicho, ule wavu haukuchanika.
12 Hoe t’Iesoà tam’ iereo: Antao hikama. Aa ndra iaia amo mpiama’eo tsy nahavany nañontane aze ty hoe: Ia v’iheo? fa nirendreke t’ie i Talè.
Yesu akawaambia, “Njooni mpate kifungua kinywa.” Hakuna hata mmoja wa wanafunzi aliyethubutu kumuuliza, “Wewe ni nani?” Kwa sababu walijua ya kuwa ni Bwana.
13 Nisitse mb’eo t’Iesoà nandrambe i mofoy naho nazotso’e, vaho o fiañeo.
Yesu akaja, akachukua ule mkate, akawapa na vivyo hivyo akawagawia pia wale samaki.
14 Izay ty nisodehà’ Iesoà fañintelo’e amo mpiama’eo hirik’ amy nitroara’e an-kavilasiy.
Hii ilikuwa mara ya tatu Yesu kuwatokea wanafunzi wake baada yake kufufuliwa kutoka kwa wafu.
15 Ie fa nitendre iereo, le hoe t’Ie­soà amy Simona Petera: O Simona, ana’ i Jonà, tea’o mandikoatse o retoañe v’ irahoo? Hoe re tama’e: Eka, Talè, arofoana’o te ikokoako. Hoe re tama’e: Fahano o vik’ añondrikoo.
Walipokwisha kula, Yesu akamuuliza Simoni Petro, “Je, Simoni mwana wa Yohana, unanipenda kweli kuliko hawa?” Yeye akamjibu, “Ndiyo Bwana, wewe unajua ya kuwa ninakupenda.” Yesu akamwambia, “Lisha wana-kondoo wangu.”
16 Nindrai’ Iesoà ama’e fañindroe’e: Simona, ana’ i Jonà, tea ahy v’iheo? Hoe re tama’e: Eñ’anio, Talè, arofoana’o te ikokoako. Hoe t’Iesoà: Andrazo o vik’ añondrikoo.
Yesu akamwambia tena, “Simoni, mwana wa Yohana, wanipenda?” Petro akamjibu, “Ndiyo Bwana, wewe unajua ya kuwa ninakupenda.” Yesu akamwambia, “Chunga kondoo zangu.”
17 Mbe nanoe’e fañintelo: O Simona, ana’ i Jonà, kokoa’o v’Irahoo? Nangoae t’i Simona amy nanoa’e fañintelo’ey ty hoe: Ko­koa’o hao iraho? le hoe re tama’e: O Rañandria, kila arofoana’o; fohi’o t’ie kokoako. Hoe t’Iesoà tama’e: Fahano o añondrikoo.
Kwa mara ya tatu Yesu akamuuliza Petro, “Simoni mwana wa Yohana, unanipenda?” Petro akahuzunika sana kwa kuwa Yesu alimuuliza mara ya tatu, “Unanipenda?” Akamjibu, “Bwana, wewe unajua yote, unajua ya kuwa ninakupenda.” Yesu akamwambia, “Lisha kondoo wangu.
18 Ita­roñako an-katò t’ie nidiañe te ni-ajalahy, naho nandenà’o ze ni-tea’o, f’ie bey le hahiti’o o fità’oo hampidiaña’ ty ila’e hinday azo mb’ami’ty tsy tea’o hombañe.
Amin, amin nakuambia, ulipokuwa kijana ulivaa na kwenda unakotaka, lakini utakapokuwa mzee utanyoosha mikono yako na mtu mwingine atakuvika na kukupeleka usipotaka kwenda.”
19 I hoe zay ty nisaontsie’e ho fitaliliañe aze ty karazan-kavilasy handrengea’e an’ Andrianañahare. Ie sinaontsi’e, le hoe re tama’e: Oriho iraho.
Yesu alisema haya ili kuashiria ni kifo cha aina gani Petro atakachomtukuza nacho Mungu. Kisha Yesu akamwambia Petro, “Nifuate!”
20 Ie nitolike t’i Petera le niisa’e i mpiòke nikokoa’ Iesoày nanonjohy ey—i nitoñoñe añ’araña’ Iesoà amy sabadidakey, nañontane aze ty hoe: O Talè, ia ty hifotetse ama’o?
Petro akageuka, akamwona yule mwanafunzi aliyependwa na Yesu akiwafuata. (Huyu ndiye yule mwanafunzi aliyeegama kifuani mwa Yesu walipokula naye chakula cha mwisho na kuuliza, “Bwana, ni nani atakayekusaliti?”)
21 Ie nioni’ i Petera, le hoe re amy Iesoà: O Talè, akore ondaty roañe?
Petro alipomwona huyo mwanafunzi, akamuuliza Yesu, “Bwana na huyu je?”
22 Hoe t’Iesoà tama’e: Naho satriko t’ie handiñe ty fibaliko, akore ama’o izay? Oriho iraho.
Yesu akamjibu, “Ikiwa nataka aishi mpaka nitakaporudi, inakuhusu nini? Wewe inakupasa unifuate!”
23 Aa le niboele amo longoo ty tsara te tsy hivetrake i mpiama’ey; fe tsy nanao ty hoe t’Iesoà t’ie tsy ho vilasy, fa, Naho lahako t’ie handiñe ty fihereñako, akore ama’o vi’zay?
Kwa sababu ya maneno haya ya Yesu, uvumi ukaenea miongoni mwa ndugu kwamba huyu mwanafunzi hangekufa. Lakini Yesu hakusema kuwa hangekufa. Yeye alisema tu kwamba, “Ikiwa nataka aishi mpaka nitakaporudi, inakuhusu nini?”
24 Itoy ty mpiama’e mitalily irezay, naho nanokitse iretoañe. Fohi’ay te mahity i talili’ey.
Huyu ndiye yule mwanafunzi anayeshuhudia mambo haya na ndiye ambaye ameandika habari hizi. Nasi tunajua ya kuwa ushuhuda wake ni kweli.
25 Mbe maro ka ty raha nanoe’ Iesoà, t’ie ro hene sinokitse, ataoko te, ndra ty voatse toy tsy nahatsake o boke ho nisokireñeo. Amena.
Lakini kuna mambo mengine mengi ambayo Yesu alifanya. Kama yote yangeliandikwa, nadhani hata ulimwengu wote usingekuwa na nafasi ya kutosha kuweka vitabu vyote ambavyo vingeandikwa. Amen.

< Jaona 21 >