< Joba 13 >

1 Inao! fa nitreako iaby zao, tsinano’ ty sofiko vaho maharendreke.
“Macho yangu yameona hili lote, masikio yangu yamesikia na kulielewa.
2 Ze fohi’areo, apotako ka; Izaho tsy zai’ areo.
Hayo mnayoyajua mimi pia ninayajua; mimi si mtu duni kuliko ninyi.
3 Fe te hivolañe amy El-Sadai iraho, te hifanointoiñe aman’ Añahare.
Lakini ninayo shauku ya kuzungumza na Mwenyezi na kuhojiana shauri langu na Mungu.
4 Mpanosoke vande nahareo, songa mpanaha tsy manjofake.
Ninyi, hata hivyo, hunipakaza uongo; ninyi ni matabibu wasiofaa kitu, ninyi nyote!
5 Ehe t’ie vata’e nianjiñe, le ho natao hihitse!
Laiti wote mngenyamaza kimya! Kwa kuwa kwenu hilo lingekuwa hekima.
6 Ehe janjiño ty havereko, vaho janjiño ty fanoroan-tsoñiko
Sikieni sasa hoja yangu; sikilizeni kusihi kwangu.
7 Hisaontsy hamengohañ’ aman’Añahare hao, hilañona’areo famañahiañe?
Je, mtazungumza kwa uovu kwa niaba ya Mungu? Je, mtazungumza kwa udanganyifu kwa niaba yake?
8 Handombok’ aze v’inahareoo? h’ondati-aivo, mpihalaly ho an’Andrianañahare hao?
Mtamwonyesha upendeleo? Mtamtetea Mungu kwenye mashtaka yake?
9 Hahasoa anahareo hao te itsikaraha’e? Hamañahy Aze hao nahareo manahake ty famañahiañe ondaty?
Je, ingekuwa vyema Mungu akiwahoji ninyi? Je, mngeweza kumdanganya kama ambavyo mngeweza kuwadanganya wanadamu?
10 Ie ho trevohe’e te mirihy añ’etake.
Hakika angewakemea kama mkiwapendelea watu kwa siri.
11 Tsy hampangebahebak’ anahareo hao ty enge’e? naho hivotrak’ ama’ areo ty fañeveñañe.
Je, huo ukuu wake haungewatisha ninyi? Je, hofu yake isingewaangukia ninyi?
12 Oha-drehan-davenoke ty onin-taro’ areo, fiaron-dietse ty fikala’ areo.
Maneno yenu ni mithali za majivu; utetezi wenu ni ngome za udongo wa mfinyanzi.
13 Mianjiña, apoho iraho hivolañe le adono ho amako ty toly.
“Nyamazeni kimya nipate kusema; kisha na yanipate yatakayonipata.
14 Ino ty andrambesako? ami’ty nifeko ty nofoko, vaho apoko an-tañako ty fiaiko.
Kwa nini nijiweke mwenyewe kwenye hatari na kuyaweka maisha yangu mikononi mwangu?
15 Ndra te havetra’e, ie ty fatokisako fe hiverok’ añ’atrefa’e raho ty amo satakoo,
Ingawa ataniua, bado nitamtumaini; hakika nitazitetea njia zangu mbele zake.
16 Vaho zao ty ho fandrombahañe ahy: te tsy hiatrek’aze ty tsy aman-Kake
Naam, hili litanigeukia kuwa wokovu wangu, kwa maana hakuna mtu asiyemcha Mungu atakayethubutu kuja mbele yake!
17 Tsendreño o entakoo, naho ty lañonako an-dravembia’ areo.
Sikilizeni maneno yangu kwa makini; nayo masikio yenu yaingize kile nisemacho.
18 Ingo, fa nalahako i tarokoy, apotako te hahazo to.
Sasa kwamba nimekwisha kutayarisha mambo yangu, ninajua mimi nitahesabiwa kuwa na haki.
19 Ia ty hifanjomotse amako? le ho nitsiñe amy zao raho vaho nikenkañe.
Je, kuna yeyote anayeweza kuleta mashtaka dhidi yangu? Kama ndivyo, nitanyamaza kimya na nife.
20 Ehe ty raha roe avao ty tsy hanoa’o ahy, le tsy hietahako o lahara’oo.
“Ee Mungu, unijalie tu mimi haya mambo mawili, nami sitajificha uso wako:
21 Ahankaño amako ty fità’o, le ehe tsy hampianifañe ahy ty fañeveñako ama’o
Ondoa mkono wako uwe mbali nami, nawe uache kuniogofya kwa hofu zako kuu.
22 Ie amy zao koiho, le hanoiñe iraho, ke angao hivolan-draho vaho toiño.
Niite kwenye shauri nami nitajibu, au niache niseme, nawe upate kujibu.
23 Fire o fandilarako naho hakeokoo? Ampahafohino ahy ty fiolako naho o tahikoo,
Ni makosa na dhambi ngapi nilizotenda? Nionyeshe kosa langu na dhambi yangu.
24 Akore te añetaha’o laharañe, vaho manao ahy ho rafelahi’o?
Kwa nini kuuficha uso wako na kunihesabu mimi kuwa adui yako?
25 Hampititititihe’o hao ty ravets-atae asiotsion-tioke, ho heañe’o hao ty kafo maike?
Je, utaliadhibu jani lipeperushwalo na upepo? Je, utayasaka makapi makavu?
26 Fa anokira’o raha mafaitse iraho, vaho ampandova’o ahy o hakeoko te niajalahy.
Kwa kuwa unaandika mambo machungu dhidi yangu na kunifanya nizirithi dhambi za ujana wangu.
27 Añombea’o longòke o tombokoo, naho efera’o ty ho nilian-tombokoo.
Umeifunga miguu yangu kwenye pingu. Unazichunga kwa makini njia zangu zote kwa kutia alama kwenye nyayo za miguu yangu.
28 ie mihamomoke hoe raha lo iraho, hoe saroñe nihanem-bararaoke.
“Hivyo mwanadamu huangamia kama kitu kilichooza, kama vazi lililoliwa na nondo.

< Joba 13 >