< Isaia 5 >
1 Ho bekoeko i kokoakoy, toe beko’ i rañeko, ty amy tanem-balobo’ey, Aman-tanem-bahy ankaboan- kobokara añe i kokoakoy.
Nitaimba wimbo kwa ajili ya mmoja nimpendaye, kuhusu shamba lake la mizabibu: Mpendwa wangu alikuwa na shamba la mizabibu kwenye kilima chenye rutuba.
2 Nitrabahe’e, nahoro’e boak’ao o vato’eo, naketsa’e ao ty vahe soa-joboñe, rinanji’e tilik’abo an-teñateña ao, vaho nitsenea’e fipiritan-divay: le nitamà’e valoboke, f’ie namokatse valoboke vìlañe.
Alililima na kuondoa mawe na akaliotesha mizabibu bora sana. Akajenga mnara wa ulinzi ndani yake, na kutengeneza shinikizo la kukamulia divai pia. Kisha akatazamia kupata mazao ya zabibu nzuri, lakini lilizaa matunda mabaya tu.
3 Ie henane zao ry mpimoneñe e Ierosalaime ao, ry ondati’ Iehodào, ihalaliako: mizakà añivoko naho i tondam-balobokoy.
“Basi enyi wakazi wa Yerusalemu na watu wa Yuda, hukumuni kati yangu na shamba langu la mizabibu.
4 Ino ka ty hanoako amy tetem-bahekoy, ze mboe tsy nanoeko? Ie nitamàko hamokatse valoboke soa, ro nañomey valoboke lo?
Ni nini zaidi ambacho kingeweza kufanyika kwa shamba langu la mizabibu kuliko yale niliyofanya? Nilipotazamia kupata zabibu nzuri, kwa nini lilizaa zabibu mbaya tu?
5 Aa ie zao, hampahafohineko anahareo ty hanoako amy tanem-bahekoy; hombotako i fahe’ey, le horoañe; le harotsako ambane i kijoli’ey, ho lialiàñe.
Sasa nitawaambia lile nitakalolitendea shamba langu la mizabibu: Nitaondoa uzio wake, nalo litaharibiwa, nitabomoa ukuta wake, nalo litakanyagwa.
6 Hampangoakoaheko, tsy ho birabiraeñe, tsy havaeñe ka; fa hitirian-kisatse naho fatike: ho lilieko ka o rahoñeo ty tsy hampahavy orañe.
Nitalifanya nchi ya ukiwa isiyokaliwa na watu, halitakatiwa matawi wala kulimwa, nayo michongoma na miiba itamea huko, nitaamuru mawingu yasinyeshe mvua juu yake.”
7 Ty anjomba’Israele, ie ty tondam-bahe’ Iehovà’ i Màroy, ondati’ Iehodào, i hatae ifalea’ey, nipay to re fe nizò fanjamanañe; nitsoeke havañonañe fe inao ty kaikaike.
Shamba la mzabibu la Bwana Mwenye Nguvu Zote ni nyumba ya Israeli, na watu wa Yuda ni bustani yake ya kumpendeza. Alitazamia haki, lakini akaona umwagaji damu, alitazamia uadilifu, lakini akasikia vilio vya taabu.
8 Hankàñe amo mampifanoitoy kibohotse an-kivoho, naho tonda toien-tetekeo, ampara’ t’ie tsy malalake, vaho bangy irehe añivo’ i taney.
Ole wenu mnaoongeza nyumba baada ya nyumba na kuunganisha mashamba baada ya mashamba hadi hakuna nafasi iliyobaki, nanyi mnaishi peke yenu katika nchi.
9 Amo sofikoo ao! hoe t’Iehovà’ i Màroy, Toe maro ty anjomba ho kòake, ty jabajaba naho ty fanjaka tsy ho ama’ ondaty.
Bwana Mwenye Nguvu Zote amesema nikisikia: “Hakika nyumba kubwa zitakuwa ukiwa, nayo majumba ya fahari yatabaki bila kukaliwa.
10 Eka, hamokatse sajoa raike ty tanem-bahe folo lasarý, le hahafoe tsikotoke raike ty tabiry zahetse raike.
Shamba la mizabibu la eka kumi litatoa bathi moja ya divai, na homeri ya mbegu zilizopandwa itatoa efa moja tu ya nafaka.”
11 Hekoheko amo mitroatse handro hitolon-kamamoañeo; o mihenekeneke halem-bey ampara’ t’ie solebaren-divaio.
Ole wao wale waamkao asubuhi na mapema wakikimbilia kunywa vileo, wale wakawiao sana mpaka usiku, mpaka wamewaka kwa mvinyo.
12 Amo takataka’ iareo ty marovany naho ty mandolina, ty fikantsakantsàñe vaho ty divay: fe tsy oni’iareo ty sata’ Iehovà, mbore tsy ereñere’ iareo o fitoloñam-pità’eo.
Wana vinubi na zeze kwenye karamu zao, matari, filimbi na mvinyo, lakini hawayajali matendo ya Bwana, wala hawana heshima kwa ajili ya kazi ya mikono yake.
13 Aa le misese mb’an-drohy ondatikoo, amy te po-hilala, salikoeñe o androanavi’ iareoo, vaho miforejeje ami’ty hataliñiere’e ty valobohò’ iareo.
Kwa hiyo watu wangu watakwenda uhamishoni kwa sababu ya kukosa ufahamu, watu wao wenye vyeo watakufa kwa njaa na watu wao wengi watakauka kwa kiu.
14 Aa le nienatse ty fañiria’ i tsikeokeokey, nigorobahe’e ty vava’e tsy taka-zeheñe; hijoloboñe ao ty enge’ iareo, ty fivoamboa’e, ty fikoraha’e, rekets’ i mirebekey. (Sheol )
Kwa hiyo kaburi limeongeza hamu yake na kupanua mdomo wake bila kikomo, ndani mwake watashuka wakuu wao na wingi wa watu, pamoja na wagomvi wao, na wafanyao sherehe wote. (Sheol )
15 Haketrake ty fokonon-tsoa, harèke ty fanalolahy, vaho hampiambaneañe ty fihaino’ o mievotsevotseo:
Hivyo mwanadamu atashushwa, na binadamu kunyenyekezwa, macho ya wenye majivuno yatanyenyekezwa.
16 Ty hatò ro añonjonañe Iehovà’ i Màroy, ty havañonañe ro añamasiñañe i Andrianañahare Masiñe.
Lakini Bwana Mwenye Nguvu Zote atatukuzwa kwa ajili ya haki yake, naye Mungu Mtakatifu atajionyesha mwenyewe kuwa mtakatifu kwa haki yake.
17 Hierañerañe am-piandrazañe ao o anak’añondrio, naho hihinañe amo tete- lovodovo’ o vondrakeo ty mpirererere.
Kondoo watajilisha kwenye malisho yao wenyewe, wana-kondoo watajilisha katika magofu ya matajiri.
18 Feh’ohatse amo mpikozozo-kakeo an-taly hòakeo, naho o tahiñeo hoe an-talin-tsarete:
Ole wao wanaovuta dhambi kwa kamba za udanganyifu na uovu kama kwa kamba za mkokoteni,
19 Ie manao ty hoe: Ee t’ie halisa, hanaentaeñe i fitoloña’ey, hahaoniña’ay aze, le ee te hitotoke eo ty fanoroa’ i Masi’ Israeley homb’etoy hahafohina’ay Aze!
kwa wale wanaosema, “Mungu na afanye haraka, aharakishe kazi yake ili tupate kuiona. Huo mpango wa Aliye Mtakatifu wa Israeli na ukamilike, tena udhihirike ili tupate kuujua.”
20 Hekoheko ami’ty manao te raty ty soa, naho soa ty raty, o misolo ty ieñe ho hazavàñe naho ty hazavàñe ho ieñeo; o manao ty mafaitse ho mamy vaho ty mamy ho mafaitseo.
Ole wao wanaoita ubaya ni wema, na wema ni ubaya, wawekao giza badala ya nuru, na nuru badala ya giza, wawekao uchungu badala ya utamu, na utamu badala ya uchungu.
21 Hankàñe amo mahihitse am-pahaoniña’eo, naho o mahilala am-pahaisaha’eo!
Ole wao walio na hekima machoni pao wenyewe, na kujiona wenye akili machoni pao wenyewe.
22 Feh’ ohatse o fanalolahy am-pinon-divaio, naho ondaty maozatse am-pampilaroañe toakeo;
Ole wao walio mashujaa kwa kunywa mvinyo, nao walio hodari katika kuchanganya vileo,
23 ie mañatò ty lo-tsereke hahazoam-bokàñe vaho mañafake ty havañona’ o vantañeo!
wale wanaoachilia wenye hatia kwa kupokea hongo, lakini huwanyima haki wasio na hatia.
24 Aa le manahake ty fipiloran-afo ty ahetse, naho ty fampibotseha’ ty lel’afo ty kafokafo’e, ty hañamomohañe ty vaha’ iareo, vaho hiboele hoe deboke o voñe’ iareoo; fa napo’ iareo ty Hà’ Iehovà’ i Màroy, naho nimavoe’ iareo ty nafè’ i Masi’ Israeley.
Kwa hiyo, kama ndimi za moto zirambavyo nyasi, na kama vile majani makavu yazamavyo katika miali ya moto, ndivyo mizizi yao itakavyooza na maua yao yatakavyopeperushwa kama mavumbi; kwa kuwa wameikataa sheria ya Bwana Mwenye Nguvu Zote na kulisukumia mbali neno la Aliye Mtakatifu wa Israeli.
25 Toly ndra miforoforo am’ ondati’eo ty haviñera’ Iehovà, naho natora-kitsi’e am’ iereo ty fità’e, naho trinabotrabo’e; nihondrahondra iaby o tambohoo, natao litsake an-dalambey eo ty lolo’ iareo. Amy hoe zay iaby mbe tsy nivike ty haviñera’e, vaho mbe mihity avao ty fità’e.
Kwa hiyo hasira ya Bwana inawaka dhidi ya watu wake, mkono wake umeinuliwa na anawapiga. Milima inatetemeka, maiti ni kama takataka kwenye barabara. Hata kwa haya yote, hasira yake haijageukia mbali, mkono wake bado umeinuliwa juu.
26 Hañonjo kobaiñe amo kilakila ondaty tsietoitaneo Re, naho hifioke ama’e boak’ añ’olo-ty tane toy añe, le hehe, hiherereake mb’etoy masika.
Yeye anainua bendera kwa ajili ya mataifa yaliyo mbali, anapiga filimbi kwa ajili ya wale walio kwenye miisho ya dunia. Tazama wamekuja, kwa kasi na kwa haraka!
27 Tsy ho am’ iereo ty ho mokotse ndra hitsikapy; tsy eo ty hiroro ndra hirotse; tsy habalake ty sadiam-bania’ iareo, vaho tsy hianto ty fihilin-kana’ iareo;
Hakuna hata mmoja wao anayechoka wala kujikwaa, hakuna hata mmoja anayesinzia wala kulala, hakuna mkanda uliolegezwa kiunoni, hakuna gidamu ya kiatu iliyokatika.
28 Masioñe o ana-pale’eo, fonga mivohotse o fale’eo, hoe vato-pilake o tombon-tsoavala’eo, vaho talio o larò’eo;
Mishale yao ni mikali, pinde zao zote zimevutwa, kwato za farasi wao ziko kama jiwe la gumegume, magurudumu ya magari yao ya vita ni kama upepo wa kisulisuli.
29 Hirohake hoe liona vave iereo, hiroharoha hoe anan-diona, Eka, mitrè iereo mitsepake i horoñeñey, naho hendese’e añe, ie tsy amam-pandrombake.
Ngurumo yao ni kama ile ya simba, wananguruma kama wana simba, wanakoroma wanapokamata mawindo yao, na kuondoka nayo pasipo yeyote wa kuokoa.
30 Hitròñe amy andro zay iereo, manahake ty fitròña’ i riakey, ie mahaisake i taney, heheke ty hamoromoroñañe, naho faloviloviañe, ndra i hazavañey ro ampigodoñen-drahoñe.
Katika siku ile watanguruma juu yake kama ngurumo za bahari. Kama mtu akiitazama nchi, ataona giza na dhiki; hata nuru itatiwa giza kwa mawingu.