< Ezekiela 42 >
1 Nendese’e mb’an-kiririsa alafe’e ao iraho, mañavaratse mb’eo; le nente’e mb’amo efe-traño miatreke i kiririsay aolo’ i traño avaratseio.
Ndipo yule mtu akaniongoza kuelekea kaskazini mpaka kwenye ua wa nje na kunileta mpaka kwenye vyumba vinavyoelekeana na ua wa Hekalu na kuelekeana na ukuta wa nje upande wa kaskazini.
2 Kiho zato ty andava’ i fiatrefa’e avaratsey, tama’e ty lalambei’e, naho kiho limam-polo ty am-pohe’e,
Jengo ambalo mlango wake ulielekea kaskazini lilikuwa na urefu wa dhiraa mia moja na upana wa dhiraa hamsini.
3 ty toe’e le añate’ i kiririsay an-kiho roapolo naho miefetse amy damok’ an-kiririsa alafe’ey, vaho mifanongoa in-telo mañambone rekets’ o lavaranga’eo.
Mbele ya zile dhiraa ishirini za ule ua wa ndani unaoelekeana na ile njia ya ua wa nje, kuliinuka vyumba virefu kimoja baada ya kingine vya ghorofa tatu.
4 Aolo’ o efe-trañoo ty lalañe, kiho folo ty treha’e naho kiho zato i lalañey; mitolik’ avaratse o fiziliha’eo.
Mbele ya hivi vyumba kulikuwa na njia ya ndani yenye upana wa dhiraa kumi na urefu wa dhiraa mia moja. Milango yake ilikuwa upande wa kaskazini.
5 Bory o efe-traño amboneo fa nitomore’ o lavarangañeo mandikoatse ty nangala’e amy ambaney naho amy añivoy,
Basi vyumba vya juu vilikuwa vyembamba zaidi, kwa kuwa ujia ulichukua nafasi zaidi ndani yake kuliko katika vyumba vya sakafu ya chini na vya katikati ya jengo.
6 ie telo mifanongoa, fe tsy aman-tsotsòke manahake o efe-traño an-kiririsao; izay ty nampihànkañe i ambone’ o mananta’eoy te amy añivoy naho i ambaney.
Vyumba katika ghorofa ya tatu havikuwa na nguzo, kama kumbi zilivyokuwa nazo, kwa hiyo eneo la sakafu ya vyumba vya juu lilikuwa ni dogo kuliko la sakafu ya chini na ya kati.
7 Mifamalahañe amo efe-trañoo, an-kiririsa alafe’e, pak’ amo efe-trañon-kiririsa alafe’eo ty kijoly, kiho limampolo ty andava’e;
Kulikuwa na ukuta wa nje uliokuwa sambamba na vile vyumba na ukumbi wa nje, ulitokeza urefu wa dhiraa hamsini.
8 amy te kiho limampolo ty andava’ o efe-traño an-kiririsa alafe’eo, vaho kiho zato ty ila’e miatreke i kivohoy.
Wakati safu ya vyumba katika ua wa nje vilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini, vile vyumba vilivyokuwa karibu zaidi na Hekalu vilikuwa na urefu wa dhiraa mia moja.
9 Ambane’ i efetse rey añ’ila’e atiñanañe ty fizilihañe am’ iereo boak’an-kiririsa’ alafe’e.
Vyumba vya chini vilikuwa na ingilio upande wa mashariki unapoingia kutoka ukumbi wa nje.
10 Ami’ty treha’ i rindrin-kiririsa maniñanañe, tandrife’ i toetse miavakey naho tandrife’ i trañoy, le misy efe-traño,
Upande wa kusini kufuata urefu wa ukuta wa ukumbi wa nje, unaopakana na ukumbi wa Hekalu na kuelekeana na ukuta wa nje, kulikuwa na vyumba
11 le an-dalañe aolo’e eo ty hambañe amo efe-traño avaratseo, le mira amo azeo ty an-dava’e naho ty am-pohe’e, naho hambañe ty namoareñe o fiakara’eo vaho o fiziliha’eo.
vyenye ujia unayopita mbele yake. Hivi vilifanana na vile vyumba vya upande wa kaskazini, vilikuwa na urefu na upana ulio sawa, mahali pa kutokea na vipimo vyake vilikuwa sawa. Kama ilivyokuwa milango ya upande wa kaskazini,
12 Añ’ila o fiziliha’ i efe-traño atimo reio ty fizilhañe am-pigadoña’ i lalañey eo, toe i lalañe mioza aolo’ i kijoliiy momb’amy fizilihañe atiñanañe rey.
ndivyo ilivyokuwa milango ya vyumba vya upande wa kusini. Kulikuwa na ingilio kuanzia mwanzo wa njia ambao ulikuwa sambamba na ukuta wa pili uliokuwa upande wa mashariki, ambako ndiko kwa kuingia vyumbani.
13 Le hoe re tamako, I efe-traño avaratse rey naho i efe-traño atimo rey tandrife i kiririsay ro traño miavake, toem-pikamà’ o mpisoroñe miatreke Iehovào o enga miavake do’eo; ao ty hampipoha’ iareo o enga miavake do’eo: o enga mahakamao, o engan-tahiñeo, naho o engan-kakeoo: miavake i efetsey.
Kisha akaniambia, “Vyumba vya upande wa kaskazini na vya upande wa kusini ambavyo vinaelekeana na ukumbi wa Hekalu ni vyumba vya makuhani, mahali ambapo wale makuhani ambao humkaribia Bwana watakula zile sadaka takatifu sana. Huko ndiko watakakoweka zile sadaka takatifu sana, yaani, sadaka za nafaka, sadaka za dhambi na sadaka za hatia, kwa kuwa mahali ni patakatifu.
14 Ie mizilik’ ao o mpisoroñeo, le tsy hiavotse i toetse miavakey mb’an-kiririsa alafe’e ao iereo, naho tsy apo’ iareo eo hey o sikiñe nitoroñe’ iareoo, amy t’ie miavake; vaho hisikiñe hafa, hionjona’ iareo mb’an-toe’ ondatio mb’eo.
Mara makuhani waingiapo mahali patakatifu, hawaruhusiwi kwenda kwenye ukumbi wa nje mpaka wayaache mavazi ambayo walivaa wakiwa wanahudumu, kwa kuwa hayo mavazi ni matakatifu. Inawapasa kuvaa mavazi mengine kabla hawajakaribia eneo lililo wazi kwa ajili ya watu.”
15 Aa ie nihenefe’e zehe ty toe’ i kivohoy, le nendese’e niakatse mb’ amy lalam-bey miatrek’ atiñanañey iraho le nizehe añ’ ariary aze.
Alipomaliza kupima vile vilivyokuwa katika eneo la ndani la Hekalu, akanitoa nje kupitia lango la upande wa mashariki na kupima eneo lote linalozunguka:
16 Zinehe’e amy kobaim-panjeheañey i lafe’e atiñanañey, kobay liman-jato amy kobaim-panjeheañey, le nitolike re
Akapima upande wa mashariki kwa ule ufito wa kupimia, nao ulikuwa dhiraa 500
17 nanjehe ty lafe’e avaratse, kobay liman-jato amy kobaim-panjeheañey, le nitolike
Akapima upande wa kaskazini, nao ulikuwa dhiraa 500 kwa ufito ule wa kupimia.
18 nanjehe ty lafe’e atimo, kiho liman-jato amy kobaim-panjeheañey.
Tena akapima upande wa kusini, nao ulikuwa dhiraa 500 kwa ufito ule wa kupimia.
19 Nitolike mb’ ahandrefañe vaho nanjehe kobay liman-jato amy kobaim-panjeheañey.
Kisha akageukia upande wa magharibi na kuupima, ulikuwa dhiraa 500 kwa ufito ule wa kupimia.
20 Aa le hene zinehe’e i lafe’e efatse rey, toe niarikatohe’ ty kijoly, liman-jato ty an-dava’e le liman-jato ty am-pohe’e, hampiambake ty masiñe ami’ty tsotra.
Hivyo akapima eneo katika pande zote nne. Lilikuwa na ukuta kulizunguka wenye urefu wa dhiraa 500 na upana wa dhiraa 500, uliotenganisha mahali Patakatifu na eneo la watu wote.