< Asan'ny Apostoly 5 >

1 Fe teo t’indaty atao Ananiasy; ie naho i Safirae vali’e ro nandeta-hanañañe,
Lakini mtu mmoja jina lake Anania pamoja na mkewe Safira waliuza kiwanja.
2 le nañaja’e i vili’ey ampahafohina’ i rakemba’ey naho nañendesa’e vaho napo’e am-pandia’ o Firàheñeo.
Huku mkewe akijua kikamilifu, Anania alificha sehemu ya fedha alizopata, akaleta kiasi kilichobaki na kukiweka miguuni pa mitume.
3 Aa le hoe t’i Petera: O Ananiasy, akore te nilifore’ i mpañìnjey ty tro’o handañitse amy Arofo Masiñey, ie nañajà’o i vilin-taney?
Petro akamuuliza, “Anania, mbona Shetani ameujaza moyo wako ili kumwambia uongo Roho Mtakatifu, ukaficha sehemu ya fedha ulizopata kutokana na kiwanja?
4 Tsy tama’o avao hao t’ie mbe tsy naletake? le ie naletake, tsy ihe ty nanandily ama’e? Akore te nikililie’o an-trok’ ao o raha zao? Tsy ondatio ty nandañira’o fa i Andrianañahare.
Je, kabla hujauza hicho kiwanja si kilikuwa mali yako? Hata baada ya kukiuza, fedha ulizopata si zilikuwa kwenye uwezo wako? Kwa nini basi umewaza hila hii moyoni mwako kufanya jambo kama hili? Wewe hukumwambia uongo mwanadamu bali Mungu.”
5 Ie jinanji’ i Ananiasy i tsaray le nikorovoke eo, nihomake; vaho nivotraha’ ty fangebahañe ze hene nahajanjiñe.
Anania aliposikia maneno haya akaanguka chini na kufa. Hofu kuu ikawapata wote waliosikia jambo lililokuwa limetukia.
6 Niongak’ amy zao o ajalahio, namolonkoñe naho nitakoñe aze mb’eo vaho nalenteke.
Vijana wakaja, wakaufunga mwili wake sanda, wakamchukua nje kumzika.
7 Ie miha-telo ora añe, le nizilik’ ao ka ty vali’e, fa namoea’e ty nizò.
Saa tatu baadaye mkewe Anania akaingia, naye hana habari ya mambo yaliyotukia.
8 Aa hoe ty ontane’ i Petera tama’e: Naleta’ areo amy vili’e zao v’i taney? le hoe re: Eka, ie.
Petro akamuuliza, “Niambie, je, mliuza kiwanja kwa thamani hii?” Akajibu, “Ndiyo, tuliuza kwa thamani hiyo.”
9 Le hoe t’i Petera tama’e: Akore ty nikinia’ areo hitsoke ty Arofo’ Iehovà? Hehe te an-dalañe eo ty fandia’ o nandeveñe i vali’oio, hitakoñ’ azo ka.
Ndipo Petro akamwambia, “Imekuwaje mkakubaliana kumjaribu Roho wa Bwana? Tazama! Nyayo za vijana waliomzika mumeo ziko mlangoni, wewe nawe watakuchukua nje.”
10 Le nidoñe am-pandia’e eo re namoe’ay. Naho nizilik’ ao i ajalahy rey, zoe’ iereo t’ie nivetrake, le nitakone’ iareo vaho naleveñe añ’ila’ i vali’ey.
Saa ile ile akaanguka chini miguuni mwake na kufa. Nao wale vijana wakaingia, wakamkuta amekufa, wakamchukua wakamzika kando ya mumewe.
11 Nangebahebake iaby i fivoriy naho ze hene nahajanjiñe.
Hofu kuu ikalipata kanisa lote pamoja na watu wote waliosikia juu ya matukio haya.
12 Maro ty viloñe naho raha tsi-tantane nanoeñe am-pità’ o Firàheñeo añivo’ ondatio. Ie fonga nitrao-drehak’ an-kiririsa’ i Solomona ao.
Mitume wakafanya ishara nyingi na miujiza miongoni mwa watu. Walioamini wote walikuwa wakikusanyika katika ukumbi wa Solomoni.
13 Tsy nahavany hirekets’ am’ iereo ka o ila’eo, f’ie nonjone’ ondatio.
Hakuna mtu mwingine aliyethubutu kuambatana nao ijapokuwa waliheshimiwa sana na watu.
14 Antsake te nitovoñe amy Talè o mpiatoo; toe lahialeñe: lahilahy naho rakemba.
Hata hivyo, waliomwamini Bwana wakazidi kuongezeka, wanaume na wanawake.
15 Aa le nasese añ’ olon-dalañe eo o matindrio, fonga nampandreañ’ an-tihy naho am-pan­dreañe, hera halofa’ ty talinjo’ i Petera t’ie niary eo.
Hata wakawa wanawaleta wagonjwa na kuwalaza kwenye magodoro na kwenye vitanda barabarani ili yamkini Petro akipita kivuli chake kiwaguse baadhi yao.
16 Maro ka ty nifanontoñe hirik’ amo rova amparipari’ Ierosalemeo ninday ty marare naho ze nitokoen-kokolampa vaho hene nijangañe.
Pia watu wakakusanyika kutoka miji iliyokuwa karibu na Yerusalemu, wakileta wagonjwa na watu walioteswa na pepo wachafu. Hao wote wakaponywa.
17 Niongak’ amy zao ty talèm-pisoroñe naho ze vavea’e amo Tsadokeo, lifo-pamarahiañe,
Kisha kuhani mkuu na wenzake wote waliokuwa pamoja naye, waliokuwa wa kundi la Masadukayo, wakajawa na wivu.
18 le nipao-pitañe amo Firàheñeo vaho najorobo’ iareo am-balabei’ i màroy ao;
Wakawakamata mitume na kuwatia gerezani.
19 fe sinoka’ ty anjelin’ Añahare amy haleñey o lalam-beim-porozòo naho nakare’e vaho hoe ty asa’e:
Lakini wakati wa usiku, malaika wa Bwana akaja, akafungua milango ya gereza na akawatoa nje. Akawaambia,
20 Akia, mijohaña an-kiririsan’ anjomban’ Añahare ey vaho taroño am’ondatio ze hene enta’ ty haveloñe toy.
“Nendeni, mkasimame Hekaluni mkawaambie watu maneno yote ya uzima huu mpya.”
21 Ie nahajanjiñe le nimoak’ añ’ anjomban’ Añahare ao te maraindrain-tsikiake, nañoke. Aa naho niavy ao ty talèm-pisoroñe naho o mpiama’eo le kinoi’ iereo i fivoriy hifanontoñe naho ze hene roandria’ o nte-Israeleo, vaho nañitrik’ am-porozò ao haneseañe iareo.
Waliposikia haya wakaenda Hekaluni alfajiri wakaendelea kufundisha watu. Kuhani mkuu na wale waliokuwa pamoja nao walipowasili, alikusanya baraza na wazee wote wa Israeli wakatuma wale mitume waletwe kutoka gerezani.
22 Fe naho pok’eo o mpifelekeo, tsy nahaoniñe iareo am-porozò ao, le nibalike vaho nitalily
Lakini wale walinzi wa Hekalu walipokwenda gerezani hawakuwakuta mitume mle. Kwa hiyo wakarudi na kutoa habari.
23 ty hoe: Toe nizoe’ay nigabeñe soa i porozòoy songa nijaridiñe amo lalañeo o mpigaritseo; fa ie sinoka’ay le tsy nahaoniñe ondaty ao zahay.
Wakasema, “Tumekuta milango ya gereza imefungwa sawasawa na askari wa gereza wamesimama nje ya mlango, lakini tulipofungua milango hakuwepo mtu yeyote ndani.”
24 Ie jinanji’ i talèn-anjombay naho o mpisorom-beio i hoe zay, le niveren-draha vaho nañarahara ze mete ho nizò.
Basi mkuu wa walinzi wa Hekalu na viongozi wa makuhani waliposikia haya, wakafadhaika na kushangaa sana kwa ajili yao kwamba jambo hili litakuwaje.
25 Nimb’eo amy zao ty nitalily ty hoe: Inao, mijohañe añ’ anjomban’ Añahare ao mañòke ondatio indaty najò’ areo an-drohy ao rey!
Ndipo mtu mmoja akaja akawaambia, “Tazameni watu mliowatia gerezani wako Hekaluni wakiwafundisha watu.”
26 Aa le nimb’eo i mpifehey rekets’ o mpañambeñeo nangalake iareo mora fa nihembañe am’ ondatio, ke hametsaham-bato.
Ndipo yule mkuu wa walinzi wa Hekalu wakaenda pamoja na askari wakawaleta wale mitume, lakini bila ghasia kwa sababu waliogopa kupigwa mawe na watu.
27 Ie nasese’ iareo, le navotra’ iereo añatrefa’ i fivoriy vaho hoe ty ontane’ i talèm-pisoroñey am’ iereo:
Wakiisha kuwaleta mitume wakawaamuru kusimama mbele ya baraza ili kuhani mkuu awahoji.
28 Tsy linili’ay mafe hao t’ie tsy hañoke amy añarañe zay? Te mone nitsitsihe’ areo t’Ierosaleme amo fañòha’ areoo, vaho kililie’ areo zahay hivave ty lio’ Indatiy!
“Tuliwaonya kwa nguvu msifundishe kwa jina hili, lakini ninyi mmeijaza Yerusalemu yote mafundisho yenu na tena mmekusudia kuleta damu ya mtu huyu juu yetu.”
29 Hoe ty natoi’ i Petera naho o Firàheñeo: Tsy mete tsy mañorike an’ Andrianañahare zahay fa tsy ondaty.
Petro na wale mitume wengine wakajibu, “Imetupasa kumtii Mungu kuliko wanadamu.
30 Natroan’ Añaharen-droaen-tikañey t’Iesoà vinono naho naradorado’areo an-katae.
Mungu wa baba zetu alimfufua Yesu kutoka kwa wafu, ambaye ninyi mlimuua kwa kumtundika kwenye msalaba.
31 Ie ro naonjon’ Añahare am-pità’e havana ho Talè naho Mpandrom­bake, hanolotse fisolohoañe naho fañahan-kakeo amy Israele.
Mungu alimtukuza, akamweka mkono wake wa kuume kuwa Kiongozi na Mwokozi ili awape Israeli toba na msamaha wa dhambi.
32 Valolombeloñe amy rezay zahay naho i Arofo Masiñe natolon’ Añahare amo mpañorik’ azeoy.
Nasi tu mashahidi wa mambo haya, vivyo hivyo na Roho Mtakatifu ambaye Mungu amewapa wale wanaomtii.”
33 Ie nahajanjiñe, le niondro­ñon­droñe naho nikilily t’ie hohofan-doza.
Wale wajumbe wa baraza la wazee waliposikia haya, walijawa na ghadhabu, wakataka kuwaua mitume.
34 Fe niongake amy fivoriy t’i Gamaliela, Fariseo, mpañoke Hake, niasia’ ze hene ondaty, le linili’e te hakareñe alafe ao heik’ indaty rey.
Lakini Farisayo mmoja, jina lake Gamalieli, aliyekuwa mwalimu wa sheria, aliyeheshimiwa na watu wote, akasimama mbele ya baraza akaamuru mitume watolewe nje kwa muda.
35 Le hoe re am’iereo: Ry nte-Israeleo, mitaoa amy ze hikililiañe am’ indaty rey.
Ndipo alipowaambia wajumbe wa baraza, “Enyi watu wa Israeli, fikirini kwa uangalifu mnayotaka kuwatendea watu hawa.
36 Ie omalemale, nitroatse t’i Teodasy le nirengevoke h’ondaty vaho nirekets’ ama’e t’indaty miha-efa-jato. F’ie vinono le fonga nabaibay o nañorik’ azeo vaho nihelañe añe.
Kwa maana wakati uliopita, aliinuka mtu mmoja jina lake Theuda, alijidai kuwa yeye ni mtu maarufu, akapata wafuasi wapatao 400 walioambatana naye. Lakini aliuawa, na wafuasi wake wote wakatawanyika, wakawa si kitu.
37 Ie añe, niongake nandimbe aze t’i Jodasy nte Galilia amy andro fañiahañe rezay; nampañorihe’e t’indaty, f’ie nihomake naho niparaitake iaby ze nañorik’ aze.
Baada yake, alitokea Yuda Mgalilaya wakati wa kuorodhesha watu, naye akaongoza kundi la watu kuasi. Yeye pia aliuawa, nao wafuasi wake wakatawanyika.
38 Aa le hoe ty taroko ama’ areo henaneo, isitaho ondatio, apoho; fa naho a ondaty i safiry naho fitoloñañey, le hihotrake;
Kwa hiyo, kwa habari ya jambo hili nawashauri, jiepusheni na watu hawa. Waacheni waende zao! Kwa maana kama kusudi lao na shughuli yao imetokana na mwanadamu, haitafanikiwa.
39 fe naho an’An­drianañahare, tsy ho mete’ areo harotsake, hera ho zoeñe te mifanjomotse aman’ Añahare.
Lakini ikiwa imetoka kwa Mungu, hamtaweza kuwazuia watu hawa. Badala yake mtajikuta mnapigana na Mungu.”
40 Niantofa’ iareo i namerea’ey; le kinanji’ iareo o Firàheñeo naho nilafaeñe naho nililieñe tsy hivolañe ami’ty tahina’ Iesoà ka, vaho nihahañe.
Wakapokea ushauri wa Gamalieli. Wakawaita mitume ndani, wakaamuru wachapwe mijeledi, kisha wakawaagiza wasinene tena kwa jina la Yesu, wakawaachia waende zao.
41 Nienga i fivoriy iereo, niankahake te natao mañeva nisalareñe ho amy tahina’ey.
Nao mitume wakatoka nje ya baraza, wakiwa wamejaa furaha kwa sababu wamehesabiwa kustahili kupata aibu kwa ajili ya jina la Yesu.
42 Boak’ andro iereo tañ’ anjomban’ Añahare ao naho nitsatsàk’ akiba nitolom-pañoke vaho nitaroñe te Iesoà i Norizañey.
Kila siku, Hekaluni na nyumba kwa nyumba, hawakuacha kufundisha na kuhubiri habari njema kwamba Yesu ndiye Kristo.

< Asan'ny Apostoly 5 >