< Asan'ny Apostoly 20 >
1 Aa naho nijihetse i koràkey, le nampihitrife’ i Paoly mb’ ama’e o mpiòkeo naho nifetrehe’e vaho nionjoñe mb’e Makedonia añe.
Baada ya zile ghasia kumalizika, Paulo aliwaita wanafunzi pamoja akawatia moyo, akawaaga, akaanza safari kwenda Makedonia.
2 Nirangae’e o taneo, nañosike ondatio an-tsara maro vaho nandoake e Grisia añe,
Alipita katika sehemu zile, akinena na watu maneno mengi ya kuwatia moyo. Ndipo hatimaye akawasili Uyunani,
3 Nañialo telo volañe añe re. Aa naho nivoñoñ’ aze o Tehodao ie ho nijon-dakañe mb’e Sirià mb’eo, le sinafiri’e ty hibalik’ am-pirangañe i Makedonia.
ambako alikaa kwa muda wa miezi mitatu. Alipokuwa anakaribia kuanza safari kwa njia ya bahari kwenda Shamu, kwa sababu Wayahudi walikuwa wamefanya shauri baya dhidi yake, aliamua kurudi kupitia njia ya Makedonia.
4 Nindre ama’e t’i Sopatera ana’ i Pìro nte Berea naho i Aristarko naho i Sekondo nte Tesalonika naho i Gaio nte Derbe, le i Timoty naho i Tikìko vaho i Trofimo nte-Asia.
Paulo alikuwa amefuatana na Sopatro mwana wa Piro, Mberoya, Aristarko na Sekundo kutoka Thesalonike na Gayo, mtu wa Derbe, Timotheo pamoja na Tikiko na Trofimo kutoka sehemu ya Asia.
5 Niaolo anay iereo vaho nandiñe e Troasy ao.
Hawa watu walitutangulia wakaenda kutungojea Troa.
6 Aa naho niheneke o andro-Mofo-po-dalivaio le nijon-dakañe boak’e Filipy zahay; ie nimodo ty andro lime le nifanampe am’iereo e Troasy ao vaho nitambats’ ao fito andro.
Lakini sisi tukasafiri kwa njia ya bahari kwa siku tano kutoka Filipi baada ya siku za Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, nasi tukaungana na wengine huko Troa, ambako tulikaa kwa siku saba.
7 Ie tsofotse ty andro’ i Sabotsey, ie fa nivory hamolake mofo o mpiòkeo, le nitaroñe am’iereo t’i Paoly, fa satri’e ty hiavotse amy loak’ àndroy, aa le nitolom-pilañoñe ampara’ te antets’ aleñe re.
Siku ya kwanza ya juma tulikutana pamoja kwa ajili ya kumega mkate. Paulo akaongea na watu, naye kwa kuwa alikuwa amekusudia kuondoka kesho yake, aliendelea kuongea mpaka usiku wa manane.
8 Nimaro ty jiro am-batsa nivoria’ay ao,
Kwenye chumba cha ghorofani walimokuwa wamekutania kulikuwa na taa nyingi.
9 le nitobok’ an-dalan-kede eo ty ajalahy atao Eotika naho nikonkoñe, aa ie tinohitohi’ i Paoly i lañona’ey, le nilañake ty roro i ajalahiy naho nikapotrake intelo riha mb’an-tane mb’eo vaho fola-manta te nongaheñe.
Kijana mmoja jina lake Eutiko, alikuwa amekaa dirishani, wakati Paulo alipokuwa akihubiri kwa muda mrefu, alipatwa na usingizi mzito, akaanguka kutoka ghorofa ya tatu, wakamwinua akiwa amekufa.
10 Nizotso mb’eo t’i Paoly nihohok’ amy ajalahiy, ie nifihine’e, le hoe re, Ko hembañe, fa ama’e ty fiai’e!
Paulo akashuka chini, akajitupa juu yake na kumkumbatia, akasema, “Msishtuke, uzima wake bado umo ndani yake.”
11 Niañambone indraike t’i Paoly namolake mofo naho nikama, le nitolom-pitaroñe ampara’ te niporea ty maraindray vaho nienga.
Kisha Paulo akapanda tena ghorofani, akamega mkate na kula. Baada ya kuongea mpaka mapambazuko, akaondoka.
12 Nindese’ iareo veloñe, am-panintsiñañe, i ajalahiy.
Watu wakamrudisha yule kijana nyumbani akiwa hai nao wakafarijika sana.
13 Fa niaolo aze an-dakan-jahay, nionjoñe mb’e Aso mb’eo, hampijoñe i Paoly añe amy namotoaña’ey, ie nañavelo am-pandia.
Tukatangulia melini tukasafiri mpaka Aso ambako tungempakia Paulo. Alikuwa amepanga hivyo kwa maana alitaka kufika kwa miguu.
14 Aa ie nifanampe ama’ay e Aso ao, le najo’ay vaho nitolom-b’e Mitilena mb’eo.
Alipotukuta huko Aso, tulimpakia melini, tukasafiri wote mpaka Mitilene.
15 Nionjoñe boak’ao zahay le niporopotìtse tandrife’ i Kio te loak’ àndro. Amy hamarai’ey ka le nivotrake e Samo, vaho nandoake e Mileto añe amy loak’ àndroy.
Kutoka huko tuliendelea kwa njia ya bahari, na kesho yake tukafika mahali panapokabili Kio. Siku iliyofuata tukavuka kwenda Samo, na kesho yake tukawasili Mileto.
16 Sinafiri’ i Paoly ty handrioñe i Efesosy tsy handrìta’e andro maro e Asia ao, fa sinda te hañambeñe ty andro’ i Halimampoloy e Ierosaleme ao.
Paulo alikuwa ameamua tusipitie Efeso ili asitumie muda mwingi huko sehemu za Asia, kwa sababu alikuwa anatamani kama ikiwezekana kufika Yerusalemu kabla ya siku ya Pentekoste.
17 Nampihitrike Efesosy añe boak’e Mileto re, nikoike o beim-Pivorio.
Paulo akiwa Mileto, alituma mjumbe kwenda Efeso kuwaita wazee wa kanisa waje wakutane naye.
18 Ie nitotsak’ ama’e, le hoe re: Fohi’ areo, boak’amy andro valoha’e nivotrahako Asia atoiy, ty fivelomako ama’ areo ze hene sà nitraofan-tika rezay,
Walipofika akawaambia, “Ninyi wenyewe mnajua jinsi nilivyoishi katikati yenu muda wote tangu siku ya kwanza nilipokanyaga hapa Asia.
19 nitoroñe i Talè am-pirèhan-troke naho ranomaso maro ndra te teo ty fitsohañe ahy amo fikinià’ o Tehodaoo;
Nilimtumikia Bwana kwa unyenyekevu wote na kwa machozi nikivumilia taabu na mapingamizi yaliyonipata kutokana na hila za Wayahudi.
20 tsy nitsikifotse tsy hitaroñako ze mete mañasoa, fe nanoro anahareo an-tameañe vaho ki-anjomba-anjomba.
Mnajua kwamba sikusita kuhubiri jambo lolote ambalo lingekuwa la kuwafaa ninyi, lakini nilifundisha hadharani na nyumba kwa nyumba.
21 Nafèko amo Jiosio naho amo Grikao ty fisolohoañe aman’Añahare naho ty fatokisañe Iesoà Talèntika Norizañey.
Nimewashuhudia Wayahudi na Wayunani kwamba inawapasa kumgeukia Mungu kwa kutubu dhambi na kumwamini Bwana wetu Yesu Kristo.
22 Ie henanekeo, oniño te mionjoñe mb’e Ierosaleme mb’eo an-troke mirohy le nofiko o raha mete hizò ahy añe;
“Nami sasa nimesukumwa na Roho, ninakwenda Yerusalemu wala sijui ni nini kitakachonipata huko.
23 naho tsy te mañatahata ahy amy ze rova iaby i Arofo Masiñey t’ie mandiñe rohy naho sarerake.
Ila ninachojua tu ni kwamba Roho Mtakatifu amenionya kuwa vifungo na mateso vinaningoja.
24 Fe tsy volilieko ho vara amako ty fiaiko, hañenefako an-drebeke ty filaisako naho i fitoroñañe rinambeko am’ Iesoà Talèy, t'ie mitaroñe i talili-soa’ o falalàn’ Añahareoy.
Lakini siyahesabu maisha yangu kuwa ya thamani kwangu, kama kuyamaliza mashindano na kukamilisha ile kazi Bwana Yesu aliyonipa, yaani, kazi ya kuishuhudia Injili ya neema ya Mungu.
25 Inao, apotako henane zao te tsy hahaisake ty tareheko ka nahareo nindre amako amy fitaroñako i fifeheañeiy.
“Nami sasa najua ya kuwa hakuna hata mmoja miongoni mwenu ambaye nimemhubiria Ufalme wa Mungu katika kwenda kwangu huku na huko, atakayeniona uso tena.
26 Ataliliko ama’ areo androany, te malio tahin-draho amy ze hene lio’ ondaty,
Kwa hiyo nawatangazia leo, sina hatia ya damu ya mtu awaye yote.
27 le tsy nifimpìñe tsy hitaroñe ama’ areo ze fonga famerean’ Añahare.
Kwa kuwa sikusita kuwatangazia mapenzi yote ya Mungu.
28 Mitaoa, naho itaò o mpirai-lia’e iabio, o nampiandraze’ i Arofo Masiñeio, hamahana’ areo i Fivorin’ Añahare vinili’e amy lio’eiy.
Jilindeni nafsi zenu na mlilinde lile kundi lote ambalo Roho Mtakatifu amewaweka ninyi kuwa waangalizi wake. Lichungeni kanisa lake Mungu alilolinunua kwa damu yake mwenyewe.
29 Apotako te izaho fa nienga, le hizilik’ ama’ areo ao o amboa romotseo vaho tsy hapo’e i lia-raikey.
Najua kwamba baada yangu kuondoka, mbwa mwitu wakali watakuja katikati yenu ambao hawatalihurumia kundi.
30 Toe hiboak’ ama’ areo ty ‘ndaty hiongake naho hivolan-kamengohañe, hanintake ty mpiòke ho am’iereo.
Hata kutoka miongoni mwenu watainuka watu na kuupotosha ukweli ili wawavute wanafunzi wawafuate.
31 Aa le mitomira! naho mitiahia te nañeneke ty telo taoñe iraho tsy nitroatse namere anahareo haleñe naho handro an-dranomaso.
Hivyo jilindeni! Kumbukeni kwamba kwa miaka mitatu sikuacha kamwe kuwaonya kila mmoja kwa machozi usiku na mchana.
32 Aa ie henaneo, tolorako aman’ Añahare naho ami’ty Tsara’ i hasoa’ey, ie ty mahatomambao anahareo, hanolotse anjara lova amy ze hene ondaty navaheñe.
“Sasa nawakabidhi kwa Mungu na kwa neno la neema yake, linaloweza kuwajenga na kuwapa ninyi urithi miongoni mwa wote ambao wametakaswa.
33 Tsy eo ty nikirañako volafoty ndra volamena ndra sarimbo.
Sikutamani fedha wala dhahabu wala vazi la mtu yeyote.
34 Toe fohi’ areo te nañeneke o nipaiakoo naho o nitraok’ amakoo o tañako retoa.
Ninyi wenyewe mnajua kwamba mikono yangu hii imetumika kwa mahitaji yangu na ya wale waliokuwa pamoja nami.
35 Fa nitoroako amy ze he’e amy fifanehafañe zay, ty hañimbà’ areo o malemeo, ie mitiahy ty tsara’ i Talè Iesoà manao ty hoe: Haha ty manjotso ta ty mandrambe.
Katika kila jambo nimewaonyesha kwamba kwa njia hii ya kufanya kazi kwa bidii imetupasa kuwasaidia wadhaifu, mkikumbuka maneno ya Bwana Yesu mwenyewe jinsi alivyosema, ‘Ni heri kutoa kuliko kupokea.’”
36 Ie niheneke i saontsi’ey, le nitongaleke vaho nitrao-pilolok’ am’iereo iaby.
Paulo alipomaliza kusema haya akapiga magoti pamoja nao wote akaomba.
37 Sindre nirovetse, namontititse ty fititia’e naho nañondrok’ aze.
Wote wakalia, wakamkumbatia Paulo na kumbusu,
38 Loho nampihontoke iareo i tsara nanoe’e te tsy ho isa’ iereo ka i lahara’eiy; le nasese’ iereo mb’ an-dakañe mb’eo.
Kilichowahuzunisha zaidi ni kwa sababu ya yale maneno aliyosema kwamba kamwe hawatauona uso wake tena. Wakaenda naye mpaka kwenye meli.