< Asan'ny Apostoly 18 >
1 Ie añe, le nienga i Atena t’i Paoly mb’e Korinto mb’eo.
Baada ya haya, Paulo akaondoka Athene akaenda Korintho.
2 Le tendreke ty Jiosy atao Akoila, nisamak’ e Ponto, ie vaho nivotrake boak’e Italia rekets’ i Prisilae, vali’e, (ami’ty nandilia’ i Klaodio te hakareñ’ amy Roma ze atao Jiosy.) Le niheova’e,
Huko akakutana na Myahudi mmoja jina lake Akila, mwenyeji wa Ponto, ambaye alikuwa amewasili karibuni kutoka Italia pamoja na mkewe Prisila, kwa sababu Klaudio alikuwa ameamuru Wayahudi wote waondoke Rumi. Paulo akaenda kuwaona,
3 aa kanao nihamban-tolon-draha, le nimoneñe am’ iereo ao, nitrao-pitoroñe, fa sindre mpamboatse lamban-kibohotse.
naye kwa kuwa alikuwa mtengeneza mahema kama wao, akakaa na kufanya kazi pamoja nao.
4 Boa-tSabotse re nañoke am-pitontonañe ao, nandrekets’ o Jiosio naho o Grikao.
Kila Sabato Paulo alikuwa akihojiana nao katika sinagogi, akijitahidi kuwashawishi Wayahudi na Wayunani.
5 Ie pok’eo boake Makedonia añe t’i Silasy naho i Timoty, le nazìn’ arofo t’i Paoly hitaroñe amo Jiosio te Iesoà i Norizañey.
Sila na Timotheo walipowasili kutoka Makedonia, walimkuta Paulo akiwa amejitolea muda wake wote katika kuhubiri, akiwashuhudia Wayahudi kwamba Yesu ndiye Kristo
6 Aa ie nandietse naho nanivetive avao, le nakopi’e o saro’eo, nanao ty hoe: Ami’ty añambone’ areo o lio’ areoo! Malio iraho, fa homb’ amo kilakila ondatio henane zao.
Wayahudi walipompinga Paulo na kukufuru, yeye aliyakungʼuta mavazi yake, akawaambia, “Damu yenu na iwe juu ya vichwa vyenu! Mimi sina hatia, nimetimiza wajibu wangu. Kuanzia sasa nitawaendea watu wa Mataifa.”
7 Niakatse re, niheo mb’ añ’ anjomba’ ty atao Titosy Josto, mpitalaho aman’ Añahare, ie nipitek’ amy fitontonañey i anjomba’ey.
Kisha akaondoka mle kwenye sinagogi, akaenda nyumbani kwa mtu mmoja jina lake Tito Yusto, aliyekuwa mcha Mungu. Nyumba yake ilikuwa karibu na sinagogi.
8 Niantoke i Talè t’i Krispo, bei’ i fitontonañey, naho o añ’ anjomba’e iabio; le maro amo nte-Korinto ro nahajanjiñe naho niato vaho nalipotse.
Kiongozi wa hilo sinagogi, aliyeitwa Krispo, akamwamini Bwana, yeye pamoja na watu wote wa nyumbani mwake. Nao Wakorintho wengi waliomsikia Paulo pia wakaamini na kubatizwa.
9 Nañento i Paoly haleñe añ’ aroñaroñe t’i Talè, ami’ty hoe: Ko hembañe, fa mitaròña, le ko mianjiñe,
Usiku mmoja Bwana akamwambia Paulo katika maono, “Usiogope, lakini endelea kusema wala usinyamaze,
10 amy te mindre ama’o iraho vaho tsy ao ty hiambotrak’ ama’o hijoy, fa maro ty ondatiko an-drova atoy.
kwa maana mimi niko pamoja nawe, wala hakuna mtu atakayeweza kukushambulia ili kukudhuru, kwa kuwa ninao watu wengi katika mji huu ambao ni watu wangu.”
11 Aa le nitoloñe ao taoñe raike tsy enem-bolañe re nañoke o tsaran’ Añahareo am’iareo.
Hivyo Paulo akakaa huko kwa muda wa mwaka mmoja na nusu, akiwafundisha neno la Mungu.
12 Ie nimpifehe’ i Akaia t’i Galio, le nifandrimboñe o Tehodao nañoridañe i Paoly, vaho nasese’ iareo mb’an-jaka.
Lakini wakati Galio alipokuwa msaidizi wa mwakilishi wa mtawala huko Akaya, Wayahudi waliungana kumshambulia Paulo, wakamkamata na kumpeleka mahakamani.
13 T’indaty tìañe, hoe iareo, manigìke ondatio hitalaho aman’ Añahare am-pirangañe Hake.
Wakamshtaki wakisema, “Mtu huyu anawashawishi watu wamwabudu Mungu kinyume cha sheria.”
14 Ie fa ho nanoka-palie t’i Paoly, le hoe t’i Galio amo Tehodao, Naho ie mioza an-dilatse ndra halolòañe, ry Tehodao, le ho nitò te nifeahako.
Paulo alipotaka kujitetea, Galio akawaambia Wayahudi, “Kama ninyi Wayahudi mlikuwa mkilalamika kuhusu makosa makubwa ya uhalifu ingekuwa haki kwangu kuwasikiliza.
15 Fe kanao ontane ty amo tsarao naho o tahinañeo vaho i lili’ areoy—le mifandahara, fa tsy ho zakaeko.
Lakini kwa kuwa linahusu maneno, majina na sheria yenu, amueni ninyi wenyewe. Mimi sitakuwa mwamuzi wa mambo haya.”
16 Le rinoa’e hisitak’ amy fiambesam-pizakañey.
Akawafukuza kutoka mahakamani.
17 Aa le niambotraha’ i màroy t’i Sostena, bei’ i fitontonañey le kinabokabo’ iereo añatrefa’ i fiambesam-pizakañey, fe tsy nihaoñe’ i Galio.
Ndipo wote wakamkamata Sosthene kiongozi wa sinagogi, wakampiga mbele ya mahakama, lakini Galio hakujali kitendo chao hata kidogo.
18 Ie nitambatse ela ao t’i Paoly, le niavotse amo roahalahio, vaho nijon-dàkañe mb’e Sirià añe mindre amy Prisilae naho i Akoila, ie fa nihitsife’e e Kenkrea ao hey o maroi’eo ami’ty fanta nanoe’e.
Baada ya kukaa Korintho kwa muda, Paulo akaagana na wale ndugu walioamini, akasafiri kwa njia ya bahari kwenda Shamu akiwa amefuatana na Prisila na Akila. Walipofika Kenkrea, Paulo alinyoa nywele zake kwa kuwa alikuwa ameweka nadhiri.
19 Ie nivotrake Efesosy añe, le nenga’e eo iereo, vaho nizilik’ am-pitontonañ’ ao nifañotsohotso amo Jiosio.
Walipofika Efeso, Paulo aliwaacha Prisila na Akila huko, lakini yeye akaingia kwenye sinagogi akawa anajadiliana na Wayahudi.
20 Nihalalie’ iereo t’ie hitambatse ao, fe tsy nimete.
Walipomwomba akae nao kwa muda mrefu zaidi hakukubali.
21 Fa hoe re amy fienga’ey: Tsy mete tsy ambenako e Ierosaleme ao i sabadidake fa antitotsey, f’ie hibalike naho non’ Añahare; le nijon-dakañe Efesosy ao.
Lakini alipokuwa akiondoka, akaahidi, “Nitarudi kama Mungu akipenda.” Kisha akasafiri kwa njia ya bahari kutoka Efeso.
22 Ie nandoake e Kaisaria añe, le nionjoñe mb’eo nifañontane amy Fivoriy, vaho nizotso mb’e Antiokia mb’eo.
Alitia nanga Kaisaria, akaenda Yerusalemu na kulisalimu kanisa, kisha akaenda Antiokia.
23 Teo hey re, vaho nienga nañariary an-tane Galate naho e Frigià añe nampaozatse o mpiòke iabio.
Baada ya kukaa huko kwa muda, akaondoka na kwenda sehemu moja hadi nyingine huko Galatia na Frigia, akiwaimarisha wanafunzi wote.
24 Ie amy zao nivotrake Efesosy ao ty Jiosy atao Apolosy, nte Aleksandria; ondaty fonitse hilala, maozatse amo Sokitse Masiñeo.
Basi akaja Efeso Myahudi mmoja, jina lake Apolo, mwenyeji wa Iskanderia. Yeye alikuwa na elimu kubwa, pia alikuwa hodari katika Maandiko.
25 Toe naòke ami’ty lala’ i Talè indatiy, le naringatse an-troke, nitalily naho nañanatse Iesoà an-katò, fe ty fampilipora’ i Jaona avao ty nifohi’e.
Alikuwa amefundishwa katika njia ya Bwana, naye alikuwa na bidii katika roho, akafundisha kwa usahihi juu ya Yesu, ingawa alijua tu ubatizo wa Yohana.
26 Niorotse nilañoñe an-kasibehañe am-pitontonañ’ao re; aa naho nahajanjiñe aze t’i Prisilae naho i Akoila, le natola’ iareo, vaho nampalangesañe an-katò o satan’ Añahareo.
Apolo alianza kunena kwa ujasiri mkubwa katika sinagogi. Lakini Prisila na Akila walipomsikia, walimchukua kando na kumweleza njia ya Mungu kwa ufasaha zaidi.
27 Ie nisalalae’e ty homb’ Akaia mb’eo, le nirisihe’ o roahalahio an-tsokitse o mpiòke añeo ty handrambe aze. Ie pok’ eo le vata’e nimbae’e o nahafiato amy hasoaio.
Naye Apolo alipotaka kwenda Akaya, ndugu wa Efeso walimtia moyo, wakawaandikia wanafunzi huko ili wamkaribishe. Alipofika huko, aliwasaidia sana wale ambao, kwa neema ya Mungu, walikuwa wameamini.
28 Amy te niliere’e an-ozatse am-batraike ey o Jiosio le naboa’e amo Sokitse Masiñeo te toe Iesoà i Norizañey.
Kwa uwezo mkubwa aliwakanusha hadharani Wayahudi waliokuwa wakipinga, akionyesha kwa njia ya Maandiko kwamba Yesu ndiye Kristo.