< Asan'ny Apostoly 17 >
1 Ie niranga i Ampifolia naho i Apolonia le nandoake e Tesalonika fa ama’e ao ty Fitontonan-Jiosy.
Wakasafiri kupitia Amfipoli na Apolonia wakafika Thesalonike, ambako kulikuwa na sinagogi la Wayahudi.
2 Nizilik’ am-pitontonañ’ ao t’i Paoly amy lili’ey, le nitoroa’e boak’ amo Sokitse Masiñeo ami’ty Sabotse telo,
Kama desturi yake, Paulo aliingia ndani ya sinagogi, na kwa muda wa Sabato tatu akawa anahojiana nao kutoka kwenye Maandiko,
3 nampalange naho nampidodea te tsi-mahay tsy nijale i Norizañey vaho nitroatse amy havilasiy, ami’ty hoe, Iesoà itaroñakoy, ie ‘nio i Norizañey.
akidhihirisha wazi na kuthibitisha kwamba ilikuwa lazima Kristo ateswe na afufuke kutoka kwa wafu. Akasema, “Huyu Yesu ninayewaambia habari zake, ndiye Kristo.”
4 Niantoke ty ila’e le nirekets’ amy Paoly naho i Silasy; nanao zay ka ty maro amo Grika mpitalahoo, vaho maromaro amo roakemba beio.
Baadhi ya Wayahudi wakasadiki, wakaungana na Paulo na Sila, wakiwepo idadi kubwa ya Wayunani waliomcha Mungu na wanawake wengi mashuhuri.
5 Fe nañitrike ondaty tsivokatse boak’ an-tsena ao am-pikirañañe, o Tehodao, nitrobotrobo i lahialeñey, nampivalitsingorake i rovay; vaho nifajifajy mb’ añ’ anjomba’ i Jasona hañakarañe iareo mb’amy màroy.
Lakini Wayahudi ambao hawakuwa wameamini wakawa na wivu, wakawakodi watu waovu kutoka sokoni, wakakutanisha umati wa watu, wakaanzisha ghasia mjini. Wakaenda mbio nyumbani kwa Yasoni wakiwatafuta Paulo na Sila ili kuwaleta nje penye ule umati wa watu.
6 F’ie tsy nitendreke; le kinororòke mb’añatrefa’ o bei’ i rovaio mb’eo t’i Jasona naho ty roahalahy ila’e, vaho nitazataza ty hoe: Hehe te nivotrak’ atoy ka o mpampibalitaboake ty tane toio,
Lakini walipowakosa wakamburuta Yasoni na ndugu wengine mbele ya maafisa wa mji, wakipiga kelele: “Watu hawa ni wale walioupindua ulimwengu wamekuja huku,
7 mbore nampihovàe’ i Jasona. Mandilatse o lilin-Kaisarao ty sata’ iareo le inao eo ze o mpanjaka tovo’e atao Iesoà zao.
naye Yasoni amewakaribisha nyumbani mwake. Hawa wote wanaasi amri za Kaisari wakisema yuko mfalme mwingine aitwaye Yesu.”
8 Ie nahajanjiñe izay, le nitsiborehetoke i lahialeñey naho o bein-drovao.
Waliposikia haya, ule umati wa watu na maafisa wa mji wakaongeza ghasia.
9 Le nampandoà’ iareo àntoke t’i Jasona naho o rañe’eo vaho navotsotse.
Nao baada ya kuchukua dhamana kwa ajili ya Yasoni na wenzake wakawaacha waende zao.
10 Aa le nahitri’ o roahalahio aniany amy haleñey mb’e Berea mb’eo t’i Paoly naho i Silasy. Ie pok’ eo le nizilik’ am-pitontonan-Jiosy ao.
Usiku ule ule, wale ndugu walioamini wakawapeleka Paulo na Sila waende zao Beroya. Walipowasili huko wakaenda kwenye sinagogi la Wayahudi.
11 Nivañoñe te amo nte Tesalonikao iretoa, amy t’ie nandrambe o tsarao am-pahimbañañe vaho nañotsohotso o Sokitse Masiñeo lomoñandro handrendreke ty hatò’ o raha zao.
Hawa Waberoya walikuwa waungwana zaidi kuliko wale wa Thesalonike, kwa kuwa waliupokea ule ujumbe kwa shauku kubwa na kuyachunguza Maandiko kila siku ili kuona kama yale Paulo aliyosema yalikuwa kweli.
12 Aa le maro ty niantoke, miharo ami’ty roakemba maromaro aman-kasy naho amo lahilahy Grikao.
Wayahudi wengi wakaamini pamoja na wanawake na wanaume wa Kiyunani wa tabaka la juu.
13 Aa ie nifohi’ o Jiosy nte Tesalonikao te mbore nitaroñe i tsaran’ Añaharey e Berea t’i Paoly, le niheo mb’eo ka iereo nitrobo i lahialeñey.
Lakini wale Wayahudi wa Thesalonike waliposikia kuwa Paulo anahubiri neno la Mungu huko Beroya, wakaenda huko ili kuwashawishi watu na kuwachochea.
14 Le nampihitrife’ o roahalahio pak’an-driak’ añe aniany t’i Paoly, fe mbe nitambatse eo t’i Silasy naho i Timoty.
Mara hiyo, wale ndugu wakamsafirisha Paulo hadi pwani, lakini Sila na Timotheo wakabaki Beroya.
15 Nasese’ o lahilahio pak’ Atena añe t’i Paoly; le nimpoly ninday saontsy amy Silasy naho i Timoty ty homb’ama’e añe masìka.
Wale waliomsindikiza Paulo wakaenda naye mpaka Athene, kisha wakarudi Beroya wakiwa na maagizo kutoka kwa Paulo kuhusu Sila na Timotheo kwamba wamfuate upesi iwezekanavyo.
16 Nandiñe iareo e Atena ao t’i Paoly fe nitsimboetse añ’arofo t’ie nahaisake te lifo-kazomanga i rovay.
Paulo alipokuwa akiwasubiri huko Athene, alisumbuka sana moyoni mwake kuona vile mji huo ulivyojaa sanamu.
17 Aa le nitaroñe lomoñandro amo Jiosio naho amo mpañeveñe aman’ Añahareo am-pitontonañe ao naho an-tsena ey amy ze nifanampe ama’e.
Hivyo akahojiana kwenye sinagogi na Wayahudi pamoja na Wayunani waliomcha Mungu, na pia sokoni kila siku na watu aliopatana nao huko.
18 Nifanaontsy ama’e ka o mpikaro-kihitse amo Epikoreo naho amo Stoikao. Hoe ty ila’e: Ino ty ho volañe’ ty mpangaradadake tìa? Hoe ka ty ila’e: Hoe t’ie mpitalily ndrañahare hafa, amy t’ie nitaroñe Iesoà naho i fivañonambelo’ey.
Kisha baadhi ya Waepikureo na Wastoiko wenye falsafa wakakutana naye. Baadhi yao wakasema, “Je, huyu mpayukaji anajaribu kusema nini?” Wengine wakasema, “Inaonekana anasema habari za miungu ya kigeni.” Walisema haya kwa sababu Paulo alikuwa anahubiri habari njema kuhusu Yesu na ufufuo wa wafu.
19 Rinambe’ iereo naho nasese mb’ami’ty Areopagò mb’eo, le nanao ty hoe: Ehe ampahafohino anay te inoñe o fañòhañe vao saontsie’oo;
Hivyo wakamchukua na kumleta kwenye mkutano wa Areopago, walikomwambia, “Je, tunaweza kujua mafundisho haya mapya unayofundisha ni nini?
20 amy t’ie minday enta ankafankafa an-dravembia’ay, paia’ay ty hahafohiñe ty lengo’ o raha zao.
Wewe unaleta mambo mapya masikioni mwetu, hivyo tungetaka kujua maana yake ni nini.”
21 (Toe fonga tsy nanao inoñ’ inoñe o nte Atenao naho ze ambahiny ao naho tsy ty hitalily ndra ty hijanjiñe ze atao vao lomoñandro.)
(Waathene na wageni wote walioishi humo hawakutumia muda wao kufanya chochote kingine isipokuwa kueleza au kusikia mambo mapya).
22 Aa le nijohañe añivo’ i Vohi-Arese eo t’i Paoly nanao ty hoe: O ry nte Atenao! Treako t’ie vata’e mpitalaho amy ze he’e.
Ndipo Paulo akasimama katikati ya Areopago akasema, “Enyi watu wa Athene! Ninaona kwamba katika kila jambo ninyi ni watu wa dini sana.
23 Izaho nijenlajelañe, nisamba o fitalahoa’ areoo, le nizoeko ty kitrely nipatereñe ty hoe: Ho amy t’i Andrianañahare tsy Fohiñe. Aa le hitaroñako i italahoa’ areo fa tsy apota’ areoy.
Kwa kuwa nilipokuwa nikitembea mjini na kuangalia kwa bidii vitu vyenu vya kuabudiwa, niliona huko madhabahu moja iliyoandikwa: Kwa Mungu Asiyejulikana. Basi sasa kile ambacho mmekuwa mkikiabudu kama kisichojulikana, ndicho ninachowahubiria.
24 I Andrianañahare nanao ty voatse toy naho ze he’e ama’ey, ie i Talè i likerañey naho ty tane toiy vaho tsy mpimoneñe an-kibohotse nanoem-pitàñe re;
“Mungu aliyeumba dunia na vyote vilivyomo ndani yake, yeye ndiye Bwana wa mbingu na nchi, hakai katika mahekalu yaliyojengwa kwa mikono ya wanadamu.
25 mbore tsy atràm-pità’ ondaty—ino ty paiae’e? Ie ty mpanolo-kaveloñe naho arofo vaho ze he’e.
Wala hatumikiwi na mikono ya wanadamu kana kwamba anahitaji chochote, kwa sababu yeye mwenyewe ndiye awapaye watu wote uhai na pumzi na vitu vyote.
26 Le songa namboare’e an-dio raike ze foko’ ondaty, himoneña’e an-tane atoy, le ie ty nisafiry o sàn’ andro hiraoraoa’ iareo, vaho ty efem-pimoneña’ iareo;
Kutoka kwa mtu mmoja, yeye aliumba mataifa yote ya wanadamu ili waikalie dunia yote, naye akaweka nyakati za kuishi.
27 soa te hipay an’ Andrianañahare, hitsoek’ aze, he ho tendreke, ie tsy lavitse an-tikañ’ iaby.
Mungu alifanya hivyo ili wanadamu wamtafute na huenda wakamfikia ingawa kwa kupapasapapasa ijapokuwa kwa kweli hakai mbali na kila mmoja wetu.
28 Fa ama’e ao tika ro veloñe naho mihetseke vaho manañ’ aiñe, manahake ty fitaroña’ o mpahay sabo’ areoo, ty hoe: Tarira’e ka tikañe.
‘Kwa kuwa katika yeye tunaishi, tunatembea na kuwa na uzima wetu.’ Kama baadhi ya watunga mashairi wenu walivyosema, ‘Sisi ni watoto wake.’
29 Aa kanao tariran’ Añahare tika, le tsy mete ty fitsakorean-tika te ampihambañeñe ami’ty volamena ndra volafoty ndra vato nisokireñe an-kilala naho ami’ty hihi’ ondatio i Masiñey.
“Kwa kuwa sisi ni watoto wa Mungu, haitupasi kudhani kuwa uungu ni kama sanamu ya dhahabu au ya fedha au ya jiwe, mfano uliotengenezwa kwa ubunifu na ustadi wa mwanadamu.
30 Ie nihevea’e heike an-tsa habahimoañe, ro taroñen’ Añahare henaneo te tsi-mete tsy hene misoloho ondatio ndra aia aia,
Zamani wakati wa ujinga, Mungu alijifanya kama haoni, lakini sasa anawaamuru watu wote kila mahali watubu.
31 amy te nifotoàña’e andro zaka an-katò ty voatse toy añam’ indaty tinendre’ey; ie niventè’e amy ze kila ondaty amy nampitroara’e an-kavilasy.
Kwa kuwa ameweka siku ambayo atauhukumu ulimwengu kwa haki akimtumia mtu aliyemchagua. Amewahakikishia watu wote mambo haya kwa kumfufua Kristo kutoka kwa wafu.”
32 Aa ie jinanji’ iereo ty hoe: Fitroarañ’ an-kavilasy, le nikobìha’ ty ila’e, vaho hoe ka ty ila’e: Mbe hijanjiña’ay indraike.
Waliposikia habari za ufufuo wa wafu, baadhi yao wakadhihaki, lakini wengine wakasema, “Tunataka kukusikia tena ukizungumza juu ya jambo hili.”
33 Aa le nienga iareo t’i Paoly.
Kwa hiyo Paulo akaondoka katikati yao.
34 Fe nipitek’ ama’e t’indaty ila’e vaho niato. Tam’ iereo t’i Dionisio, mpiamy Areopagoy, naho ty rakemba atao Damarie vaho ty ila’e.
Lakini baadhi yao wakaungana naye wakaamini. Kati yao alikuwepo Dionisio, Mwareopago na mwanamke mmoja aliyeitwa Damari na wengine wengi.