< Asan'ny Apostoly 12 >

1 Ie henane zay, nañity fitàñe t’i Heroda mpanjaka hampisarerake ty ila’ i fivoriy.
Wakati huo huo Mfalme Herode Agripa aliwakamata baadhi ya watu wa kanisa.
2 Navetra’e am-pibara t’Iakobe rahalahi’ i Jaona.
Akaamuru Yakobo, ndugu yake Yohana, auawe kwa upanga.
3 Ie nifohi’e te nahafale o Tehodao, le tinovo’e ami’ty nitsepahañe i Petera. Nanoeñe amo andro’ i Sabadidak’ i Mofo tsy aman-dalivaiio zay.
Alipoona jambo hilo limewapendeza Wayahudi, akaendelea, akamkamata pia Petro. Hii ilitokea wakati wa Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu.
4 Tsinepa’e re naho najo’e am-porozò ao naho nanolotse mpiray lian-dahindefoñe efatse hañambeñe aze, ie nisinafiry ty hañakatse aze añatrefa’ ondatio naho fa tampetse i Fihelañey.
Baada ya kumkamata alimtia gerezani, chini ya ulinzi wa vikundi vinne vya askari, vyenye askari wanne kila kimoja. Herode alikuwa amekusudia kumtoa na kumfanyia mashtaka mbele ya watu baada ya Pasaka.
5 Aa le nitambozoreñe am-balabey ao t’i Petera vaho nimanea’ i Fivoriy halaly aman’ Añahare.
Kwa hiyo Petro akawekwa gerezani, lakini kanisa lilikuwa likimwombea kwa Mungu kwa bidii.
6 Ie amy aniankale’ ty hanesea’ i Heroda, le nirotse añivo’ ty lahin-defoñe roe ao t’i Petera nivahoran-tsilisily roe, vaho nijohañe an-dalam-bey eo o mpigaritse i porozòio.
Usiku ule kabla ya siku ambayo Herode Agripa alikuwa amekusudia kumtoa na kumfanyia mashtaka, Petro alikuwa amelala kati ya askari wawili, akiwa amefungwa kwa minyororo miwili. Nao walinzi wa zamu walikuwa wakilinda penye lango la gereza.
7 Tojo te nivotrake eo ty anjeli’ Iehovà, le nireandreañe amy trañoy ty hazavàñe. Nedrè’e an-deme’e t’i Petera naho nampitroare’e ami’ty hoe, Miongaha masìka! vaho nivitsok’ am-pità’e o silisilio.
Ghafula malaika wa Bwana akatokea na nuru ikamulika mle ndani ya gereza. Yule malaika akampiga Petro ubavuni na kumwamsha, akisema, “Ondoka upesi!” Mara ile minyororo ikaanguka kutoka mikononi mwa Petro.
8 Le hoe ty asa’ i anjeliy tama’e: Midiaña naho mihanà. Nanoe’e izay. Le hoe re tama’e: Saravio o lamba’oo le mañoriha.
Yule malaika akamwambia, “Vaa nguo zako na viatu vyako.” Petro akafanya hivyo. Kisha akamwambia, “Jifunge vazi lako na unifuate.”
9 Niakatse re, nanonjohy avao, fa tsy napota’e te ho tò i nanoe’ i anjeliy ama’ey; natao’e te nioniñ’ aroñaroñe.
Petro akatoka mle gerezani akiwa amefuatana na yule malaika. Hakujua wakati huo kuwa yaliyokuwa yakitukia yalikuwa kweli. Alidhani kuwa anaona maono.
10 Rinio’ iareo ty liam-pigaritse valoha’e naho ty faharoe vaho nigaoñe ami’ty lalam-bey viñe fimoahañe amy rovay ze nisokake ho a iareo an-tsatri’e le niakatse naho nizotso mb’ami’ty lalañe mb’ eo vaho nimiañe ama’e i anjeliy.
Wakapita lindo la kwanza na la pili, ndipo wakafika kwenye lango la chuma linaloelekea mjini. Lango likawafungukia lenyewe, nao wakapita hapo wakatoka nje. Baada ya kutembea umbali wa mtaa mmoja, ghafula yule malaika akamwacha Petro.
11 Ie nivañoñe t’i Petera, le hoe re: Apotako henaneo an-katò te nirahe’ Iehovà i anjeli’ey hañaha ahy am-pità’ i Heroda naho amy ze fitamà’ o Jiosy iabio.
Ndipo Petro akarudiwa na fahamu, akasema, “Sasa ninajua bila shaka yoyote kuwa Bwana amemtuma malaika wake na kuniokoa kutoka makucha ya Herode Agripa na kutoka matazamio yote ya Wayahudi.”
12 Ie naharendreke izay, le nimb’ añ’ anjomba’ i Marie rene’ i Jaona natao Marka, ze nivoria’ ty maro nihalaly.
Mara Petro alipotambua hili alikwenda nyumbani kwa Maria, mama yake Yohana aliyeitwa pia Marko, ambako watu wengi walikuwa wamekutana kwa maombi.
13 Aa ie nañonkòñe amy lalam-bey fimoahañey t’i Petera, le nimb’eo ty mpitoroñ’ ampela atao Rodae handrendreke.
Petro alipobisha hodi kwenye lango la nje, mtumishi wa kike jina lake Roda, akaja kumfungulia.
14 Ie nirendre’e ty fiarañanaña’ i Petera, le akore ty hafalea’e, kanao tsy nanokake lalañe, te mone nilay añe nitalily te nijohañe an-dalambey ao t’i Petera!
Alipoitambua sauti ya Petro, alifurahi mno akarudi bila kufungua na kuwaeleza kwamba, “Petro yuko langoni!”
15 Veren-draha n’iheo, hoe iareo. Fe mbe nitambozore’e te to, le hoe iereo: I anjeli’ey ‘nio.
Wakamwambia yule mtumishi wa kike, “Umerukwa na akili.” Alipozidi kusisitiza kuwa ni kweli, wakasema, “Lazima awe ni malaika wake.”
16 Mbe nañonkòñe avao t’i Petera. Aa naho sinoka’ iareo i lalañey, nizoe’ iereo re vaho nilatsa,
Lakini Petro aliendelea kugonga langoni, nao walipofungua lango na kumwona Petro, walistaajabu sana.
17 le tinondrotondro’ i Petera am-pitañe hianjiña’ iareo naho natalili’e ty nampiakara’ i Talè aze amy porozòy. Le hoe re: Italilio t’Iakobe naho o roahalahio; vaho nienga mb’an-toetse hafa añe.
Yeye akawaashiria kwa mkono wake wanyamaze kimya, akawaeleza jinsi Bwana alivyomtoa gerezani. Naye akaongeza kusema, “Waelezeni Yakobo na ndugu wengine habari hizi.” Kisha akaondoka akaenda sehemu nyingine.
18 Ie nimaraindray, hay aia ty fivalitaboa’ o lahin-defoñeo ami’ty nanjò’ i Petera.
Kulipokucha kukawa na fadhaa kubwa miongoni mwa wale askari kuhusu yaliyomtukia Petro.
19 Ie nampitsoehe’ i Heroda soa fa tsy nioniñe, le nilohize’e o mpigari­tseo vaho nampanese’e añe. Nizotso boake Iehodà mb’e Kaisaria añe t’i Heroda le nitambatse ao.
Baada ya Herode kuamuru atafutwe kila mahali na bila kumpata, aliwahoji wale askari walinzi kisha akatoa amri wauawe. Basi Herode Agripa akatoka Uyahudi akaenda Kaisaria, akakaa huko kwa muda.
20 Ie amy zao ro nioroñoroñe amy Tirò naho i Sidona, f’ie nifamantañe le nimb’ ama’e mb’eo re, naho nampivavè’ iareo t’i Blasto, mpiatra’ i mpanjakay, le nihalaly fifampilongoañe ama’e amy te mpamahañe ty tane’ i mpanjakay ty tane’ iareo.
Basi Herode Agripa alikuwa amekasirishwa sana na watu wa Tiro na Sidoni. Hivyo watu wa miji hiyo miwili wakaungana pamoja wakatafuta kukutana naye. Wakiisha kuungwa mkono na Blasto, mtumishi maalum wa Mfalme Herode Agripa aliyeaminika, wakaomba mapatano ya amani maana nchi zao zilitegemea nchi ya huyo mfalme kwa mahitaji yao ya chakula.
21 Aa ie amy andro tinendrey, nisikin-dambam-panjaka t’i Heroda, niambesatse am-piambesa’e eo nilañoñe am’ondatio.
Katika siku iliyochaguliwa Herode Agripa akavaa mavazi yake ya kifalme, akaketi kwenye kiti chake cha enzi na kuwahutubia watu.
22 Aa le nipazapazake ty hoe ondatio: Fiarañanañan-drañahare zao fa tsy a ondaty.
Watu waliokuwa wamekusanyika wakapiga kelele, wakisema, “Hii si sauti ya mwanadamu, bali ni ya Mungu.”
23 Toly ndra pinao’ ty anjeli’ Iehovà amy zao, ie tsy nandrenge an’ Andrianañahare, le nihànen’ oletse vaho nihomake.
Ghafula, kwa kuwa Herode hakumpa Mungu utukufu, malaika wa Bwana akampiga, naye akaliwa na chango, akafa.
24 Niraorao avao naho niboele ty tsara’ i Talè.
Lakini neno la Mungu likaendelea mbele na kuenea, nao wengi wakaambatana nalo.
25 Naho niheneke ty lia’ i Barna­basy naho i Saole e Ierosaleme ao le nimpoly vaho nindese’ iereo t’i Jaona, atao Marka mindre ama’e.
Barnaba na Sauli walipomaliza ile huduma yao iliyowapeleka, wakarudi Yerusalemu wakiwa pamoja na Yohana aitwaye Marko.

< Asan'ny Apostoly 12 >