< 2 Samoela 11 >
1 Ie an-tsam-pamalihan-taoñe, i sam-piavotam-panjaka hihotakotakey, le nirahe’ i Davide t’Ioabe, rekets’ o mpitoro’eo, naho Israele iaby; le rinotsa’ iereo o ana’ i Amoneo vaho niarikatohe’ iereo t’i Ramà. F’ie nitambatse e Ierosalaime ao t’i Davide.
Katika mwanzo wa mwaka mpya, wakati wafalme watokapo kwenda vitani, Daudi akamtuma Yoabu pamoja na watu wa mfalme na jeshi lote la Israeli. Wakawaangamiza Waamoni na kuuzunguka kwa jeshi mji wa Raba. Lakini Daudi akabaki Yerusalemu.
2 Aa teo ty hariva te nitroatse am-pandrea’e t’i Davide, naho nidraidraitse an-tafon’ anjomba’ i mpanjakay; ie an-tafo ey ro nahatalake ty rakemba niandro; nimontramontra i rakembay, hasoa-vintañe.
Ikawa siku moja wakati wa jioni Daudi aliinuka kitandani mwake na kutembeatembea juu ya paa la jumba lake la kifalme. Kutokea kule kwenye paa, akamwona mwanamke akioga. Mwanamke huyo alikuwa mzuri sana wa sura,
3 Nampañitrike hañontane i rakembay t’i Davide. Le hoe re: Tsy ie hao i Batesevae, ana’ i Eliame, tañanjomba’ i Orià nte-Kite?
naye Daudi akatuma mtu mmoja kuuliza habari za huyo mwanamke. Huyo mtu akamwambia Daudi, “Je, huyu si Bathsheba binti Eliamu, naye ni mke wa Uria, Mhiti?”
4 Aa le nampihitrife’ i Davide; ie niheo mb’ama’e ao, niolora’e, aa ie fa nañefe-batañe amy haleora’ey ro nimpoly añ’anjomba’e ao.
Ndipo Daudi akatuma wajumbe kumleta. Huyo mwanamke akaja kwa Daudi, Daudi akakutana naye kimwili. (Huyo mwanamke ndipo tu alikuwa amejitakasa kutoka siku zake za hedhi.) Kisha akarudi nyumbani kwake.
5 Niareñe i rakembay vaho nirahe’e amy Davide ty hoe: Mivesatse iraho.
Huyo mwanamke akapata mimba akampelekea Daudi ujumbe, kusema, “Mimi ni mjamzito.”
6 Aa le nafanto’ i Davide amy Ioabe ty hoe: Iraho mb’amako mb’etoa t’i Orià nte-Kite. Aa le nirahe’ Ioabe mb’ amy Davide t’i Orià.
Ndipo Daudi akapeleka ujumbe kwa Yoabu, “Unipelekee Uria, Mhiti.” Naye Yoabu akamtuma Uria kwa Daudi.
7 Aa ie pok’ ama’e t’i Orià, le nañontanea’ i Davide te nanao akore t’Ioabe, naho ondatio naho i fañotakotaha’ i aliy.
Uria alipofika, Daudi akamuuliza habari za Yoabu, hali za askari na vita kwamba inaendeleaje.
8 Le hoe t’i Davide amy Orià: Akia, mizotsoa mb’añ’ akiba’o mb’eo, naho manasà fandia. Aa le niavotse añ’ anjomba’ i mpanjakay t’i Orià vaho nampañoriheñ’ aze ty mahakama, ravoravo boak’ amy mpanjakay.
Kisha Daudi akamwambia Uria, “Teremka nyumbani kwako ukanawe miguu yako.” Basi Uria akaondoka kutoka kwenye jumba la kifalme, tena zawadi zikamfuata kutoka kwa mfalme.
9 Fe nirotse an-dalan’ anjomba’ i mpanjakay t’i Orià mindre amo mpitoro’ i talè’ey iabio vaho tsy nizotso mb’ añ’anjomba’e mb’eo.
Lakini Uria akalala kwenye ingilio la jumba la kifalme pamoja na watumishi wote wa bwana wake, na hakuteremka kwenda nyumbani kwake.
10 Aa ie natalily amy Davide ty hoe: Tsy nizotso mb’añ’ anjomba’e mb’eo t’i Orià. Le hoe t’i Davide amy Orià, Tsy vaho nihirik’ an-dia-lava v’iheo? Aa vaho akore t’ie tsy nizotso mb’ añ’anjomba’o mb’eo?
Daudi alipoambiwa kwamba, “Uria hakwenda nyumbani,” Daudi akamuuliza, “Je, si ndiyo tu umefika kutoka safari ya mbali? Kwa nini hukwenda nyumbani?”
11 Le hoe t’i Orià amy Davide: Songa mimoneñe an-kibohotse i vatam-pañinay, naho Israele, vaho Iehodà; mbore mitobe an-kivok’ ey t’Ioabe talèko mindre amo mpitoron-talèkoo; aa le himoak’ añ’ anjombako ao hao iraho hihinañe naho hinoñe, vaho handre amy valikoy? Kanao velon-drehe naho veloñe ty arofo’o, tsy hanoeko.
Uria akamwambia Daudi, “Sanduku la Mungu, na Israeli na Yuda wanakaa kwenye mahema, naye bwana wangu Yoabu na watu wa bwana wangu wamepiga kambi mahali pa wazi. Ningewezaje kwenda nyumbani kwangu ili nile, ninywe na kukutana na mke wangu? Hakika kama uishivyo sitafanya jambo la namna hiyo!”
12 Le hoe t’i Davide amy Orià: Mahaliñisa atoy hey te anito, le hengako hiavotse te maray. Aa le niambesatse e Ierosalaime ao t’i Orià amy andro zay; le ie loakandro
Ndipo Daudi akamwambia, “Kaa hapa siku moja zaidi, nami kesho nitakutuma urudi.” Kwa hiyo Uria akakaa Yerusalemu siku ile na siku iliyofuata.
13 nikanjie’ i Davide naho nikama naho ninoñe ama’e; vaho nimamoe’e; le niakatse añe re te hariva nandre am-pandreañe mindre amo mpitoro’ i taleio, fe tsy nizotso mb’ añ’ anjomba’e mb’eo.
Kwa ukaribisho wa Daudi, Uria akala na kunywa pamoja naye, Daudi akamlevya. Lakini jioni Uria alitoka kwenda kulala juu ya mkeka wake miongoni mwa watumishi wa bwana wake, hakwenda nyumbani.
14 Aa ie maraiñe, nanokitse taratasy am’ Ioabe t’i Davide, vaho nampisangitrifa’e am-pità’ i Orià.
Asubuhi yake Daudi akamwandikia Yoabu barua, akamtuma Uria kuipeleka.
15 Le hoe ty sinoki’e amy taratasiy: Apoho aolo amy hotakotake miforoforoy t’i Orià, le isitaho, soa t’ie ho fofoheñe hivetrake.
Ndani ya barua aliandika, “Mweke Uria mstari wa mbele mahali ambapo mapigano ni makali sana. Kisha wewe uondoke ili Uria aangushwe chini na kuuawa.”
16 Ie amy zao, naho nisary i aliy t’Ioabe le nafanto’e hitoetse amo fanalolahio t’i Orià.
Hivyo Yoabu alipokuwa ameuzingira mji kwa jeshi, akamweka Uria mahali ambapo alijua kuwa ulinzi wa adui ulikuwa imara sana.
17 Aa le niavotse ondati’ i rovaio, nifandraparapak’ am’ Ioabe; nitsingoro eo ty ila’ ondatio, naho ty ila’ o mpitoro’ i Davideo; vaho nihomake ka t’i Orià nte-Kite.
Wakati watu wa mjini walipotoka kwenda kupigana dhidi ya Yoabu, baadhi ya watu katika jeshi la Daudi wakauawa, zaidi ya hayo, Uria, Mhiti, akafa.
18 Le nañirake t’Ioabe naho nitalily i aliy amy Davide;
Yoabu akampelekea Daudi maelezo yote ya vita.
19 le hoe ty nafanto’e amy nampihitrifa’ey: Ie fa nitalilie’o amy mpanjakay i aly iabiy,
Akamwagiza mjumbe hivi, “Utakapokuwa umemaliza kumpa mfalme maelezo ya vita,
20 naho miforoforo ty haviñera’ i mpanjakay, manao ama’o ty hoe: Aa vaho akore t’ie niheo mb’eo hialy marine i rovay hoe zao? Tsy nifohi’ areo t’ie hitifitse boak’ ambone’ i kijoliy ey?
hasira ya mfalme yaweza kuwaka, naye aweza kukuuliza, ‘Kwa nini mlisogea karibu hivyo na mji kupigana? Hamkujua kuwa wangeweza kuwapiga mishale kutoka ukutani?
21 ia ty nañoho-doza amy Akimelek’ ana’ Ierobesete? tsy roakemba hao ty nametsake vato-fandisanañe-ambone ama’e boak’ an-kijoly ey nampihomak’ aze e Tebetse añe? Aa vaho manao akore te niharinea’ areo i rindriñey? le hoe ty hatao’o: Nihomake ka i mpitoro’o Orià nte-Kitey.
Ni nani aliyemuua Abimeleki mwana wa Yerub-Besheth? Je, mwanamke hakutupa juu yake jiwe la juu la kusagia kutoka ukutani, kwa hiyo akafa huko Thebesi? Kwa nini mlisogea hivyo karibu ya ukuta?’ Ikiwa atakuuliza hivi, ndipo umwambie, ‘Pia mtumishi wako Uria, Mhiti, amekufa.’”
22 Aa le nimb’eo i nafantokey vaho natalili’e amy Davide iaby i nampañitrife’ Ioabe azey.
Mjumbe akaondoka. Alipowasili akamwambia Daudi kila kitu alichokuwa ametumwa na Yoabu kusema.
23 Le hoe i ìrakey amy Davide: Toe naname anay ondatio naho niakatse mb’ ama’ay an-kivoke ey fe nampolie’ay pak’ am-pimoahañe an-dalam-bey eo.
Mjumbe akamwambia Daudi, “Watu walituzidi nguvu wakatoka nje ya mji dhidi yetu kwenye eneo la wazi, lakini tuliwarudisha nyuma mpaka kwenye ingilio la mji.
24 Le hiniriri’ o mpitàm-paleo o mpitoro’oo boak’ amy kijoliy, naho amo mpitoro’ i mpanjakaio ty nivetrake, vaho nihomake ka t’i Orià nte-Kite mpitoro’oy.
Ndipo wapiga upinde walitupa mishale kwa watumishi wako kutoka ukutani, na baadhi ya watu wa mfalme wakafa. Zaidi ya hayo, Uria, Mhiti, mtumishi wako amekufa.”
25 Aa le hoe t’i Davide amy nihitrikey: Ty hoe ty ho enta’o am’ Ioabe: Ehe te tsy hampioremeñe azo o raha zao fa tsy mete tsy mampibotseke mb’eo mb’eo avao i fibaray; ampaozaro ty fihotakotaha’o amy rovay vaho rotsaho. Osiho re.
Daudi akamwambia mjumbe, “Ukamwambie Yoabu hivi, ‘Jambo hili lisikutie wasiwasi, upanga hula huyu sawa na ulavyo mwingine. Zidisha mashambulizi dhidi ya mji na uangamize.’ Mwambie Yoabu hivi ili kumtia moyo.”
26 Ie jinanji’ i tañanjomba’ i Oriày te vilasy t’i Orià vali’e le nandala’e.
Mke wa Uria aliposikia kwamba mumewe amekufa, akamwombolezea.
27 Ie añe i fandalà’ey le nahitri’ i Davide ty holia’e añ’anjomba’e ao naho nengae’e ho vali’e vaho nisamak’ ana-dahy ho aze. Fe tsy ninò’ Iehovà i nanoe’ i Davidey.
Baada ya muda wa maombolezo kwisha, Daudi akamtaka aletwe nyumbani kwake, naye akawa mkewe, na akamzalia mwana. Lakini jambo alilokuwa amefanya Daudi lilimchukiza Bwana.