< 2 Mpanjaka 1 >
1 Ie nihomake t’i Akabe, le niola am’ Israele t’i Moabe.
Baada ya kifo cha Mfalme Ahabu, nchi ya Moabu iliasi dhidi ya Israeli.
2 Nitsirikoake boak’ amy tsingarakara’ i efe’e ambone eo e Someroney t’i Ahkazià le nisiloke vaho nampañitrife’e ty ìrake, ami’ty hoe: Akia. añontaneo amy Baalezebobe, ‘ndrahare’ i Ekrone, ke hiambeñe iraho amo areteko zao.
Basi Ahazia alikuwa ameanguka huko Samaria kutoka baraza ya chumba chake cha juu, akaumia. Hivyo akatuma wajumbe, akiwaambia, “Nendeni mkaulize kwa Baal-Zebubu, mungu wa Ekroni, mkaone kama nitapona kutokana na kuumia huku.”
3 Fe hoe ty tsara’ i anjeli’ Iehovà amy Elià nte-Tisbý: Miongaha, akia mifanalakà amo ìra’ i mpanjaka’ i Someroneio, le ano ty hoe: Aa vaho tsy aman’ Añahare hao t’Israele, t’ie homb’ amy Baalezebobe ‘ndrahare’ i Ekrone hañontane aze?
Lakini malaika wa Bwana akamwambia Eliya, Mtishbi, “Panda ukakutane na wajumbe wa mfalme wa Samaria, uwaulize, ‘Je, ni kwa sababu hakuna Mungu katika Israeli ndiyo maana mnakwenda kumuuliza Baal-Zebubu, mungu wa Ekroni?’
4 Aa le hoe ty nafè’ Iehovà: Tsy hizotso amy fandreañe nijoña’oy irehe, fa toe hivetrake. Le nienga t’i Elià.
Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana, ‘Hutaondoka kwenye kitanda unachokilalia. Hakika utakufa!’” Hivyo Eliya akaenda.
5 Nimpoly ama’e o ìra’eo, le hoe re ama’e: Ino ty nimpolia’ areo?
Wajumbe waliporudi kwa mfalme, akawauliza, “Kwa nini mmerudi?”
6 Le nanoa’ iareo ty hoe: Nifanampe ama’ay t’indaty nanao ty hoe: Akia mimpolia mb’ amy mpanjaka nañirak’ anahareoy, vaho isaontsio ty hoe: Hoe ty nafè’ Iehovà: Aa vaho tsy aman’ Añahare hao t’Israele te ihe mañitrike hañontane e Baalezebobe ‘ndrahare’ i Ekrone? Aa le tsy hizotsoa’o i fandreañe nijoña’o, fa toe hihomake.
Wakamjibu, “Mtu fulani alikuja kukutana nasi, naye akatuambia, ‘Rudini kwa mfalme aliyewatuma na mkamwambie, “Hili ndilo asemalo Bwana: Je, ni kwa sababu hakuna Mungu katika Israeli ndiyo maana unawatuma watu kwenda kuuliza kwa Baal-Zebubu, mungu wa Ekroni? Kwa hiyo hutaondoka kwenye kitanda unachokilalia. Hakika utakufa!”’”
7 Le hoe re am’ iereo: T’indaty manao akore ty nifanalaka ama’ areo, nisaontsy i entañe zay ama’ areo?
Mfalme akawauliza, “Alikuwa mtu wa namna gani ambaye mlikutana naye, akawaambia hili?”
8 Le hoe ty natoi’ iareo: Ondaty volovoloeñe, midian-kolitse an-toha’e. Le hoe re: I Elià nte-Tisbý izay.
Wakamjibu, “Alikuwa mtu aliyekuwa na vazi la manyoya na mkanda wa ngozi kiunoni mwake.” Mfalme akasema, “Huyo alikuwa ni Eliya, Mtishbi.”
9 Aa le nañirake ty mpifehe-limampolo rekets’ i limampolo’ey i mpanjakay. Niañambone mb’ama’e mb’eo iereo, le ingo ie niambesatse an-dengom-bohitse ey. Le hoe re ama’e: O ondatin’ Añahareo, hoe ty enta’ i mpanjakay: Mizotsoa.
Ndipo mfalme akamtuma mkuu mmoja wa kikosi pamoja na kikosi chake cha askari hamsini kwa nabii Eliya. Yule mkuu wa kikosi akamwendea Eliya, aliyekuwa ameketi juu ya kilima, na kumwambia, “Mtu wa Mungu, mfalme anasema, ‘Shuka chini!’”
10 Le hoe ty natoi’ i Elià i mpifehe limampoloy: Naho toe ondatin’ Añahare iraho le ee te hizotso boak’ andikerañe ey ty afo hamorototo azo naho o limampolo’oo, Aa le nikodoiñe boak’ andikerañe añe ty afo namorototo aze rekets’ i limampolo rey.
Eliya akamjibu yule mkuu wa kikosi, “Ikiwa mimi ni mtu wa Mungu, moto na ushuke kutoka mbinguni ukuteketeze wewe na watu wako hamsini!” Ndipo moto ukashuka kutoka mbinguni na kuwateketeza yule mkuu wa kikosi pamoja na watu wake.
11 Nañirake mpifehe limampolo indraike re rekets’ i limampolo’ey. Le nisaontsia’e ty hoe: Ry ‘ndatin’ Añahareo, hoe i mpanjakay: Mizotsoa ami’ty manao zao.
Aliposikia hili, mfalme akatuma kwa Eliya mkuu wa kikosi mwingine na askari wake hamsini. Yule mkuu wa kikosi akamwambia Eliya, “Mtu wa Mungu, hili ndilo asemalo mfalme, ‘Shuka chini mara moja!’”
12 Le hoe ty natoi’ i Elià: Naho toe ‘ndatin’ Añahare iraho, le ee te hizotso boak’ an-dikerañe ey ty afo hamorototo azo naho o limampolo’oo. Le nizotso boak’ aman’ Añahare an-dikerañe añe ty afo namorototo aze rekets’ i limampolo’ey.
Eliya akajibu, “Ikiwa mimi ni mtu wa Mungu, moto na ushuke kutoka mbinguni ukuteketeze wewe na watu wako hamsini!” Ndipo moto wa Mungu ukashuka kutoka mbinguni, ukamteketeza yeye na watu wake hamsini.
13 Nañirake indraike re, le ty mpifehe limampolo fahatelo reketse ty limam-polo’e. Nitroatse mb’eo i mpifehe limampoloy, le nitongalek’ añatrefa’ i Elià eo vaho nihalalia’e ami’ty hoe: Ry ondatin’ Añahare, miambane ama’o, ehe te ho vara am-pahaisaha’o ty fiaiko naho ty fiai’ o mpitoro’o limampolo retoañe.
Hivyo mfalme akatuma mkuu wa kikosi wa tatu na watu wake hamsini. Huyu mkuu wa kikosi wa tatu akapanda na kupiga magoti mbele ya Eliya, akiomba, “Mtu wa Mungu, tafadhali niachie uhai wangu na uhai wa hawa watu hamsini, watumishi wako!
14 Toe nihotrake boak’ andikerañe ey ty afo namorototo i mpifehe limampolo taolo rey rekets’ i limampolo’ iareoy; fe ee te ho sarotse ampahaoniña’o henaneo ty fiaiko.
Tazama, moto umeshuka kutoka mbinguni na kuwateketeza wale wakuu wa vikosi viwili vya kwanza pamoja na watu wao. Lakini sasa niachie uhai wangu!”
15 Le hoe ty tsara’ i anjeli’ Iehovày amy Elià: Mindreza fizotso ama’e, ko hembañe. Le niongake re nizotso mindre ama’e mb’ amy mpanjakay mb’eo.
Malaika wa Bwana akamwambia Eliya, “Shuka pamoja naye, usimwogope.” Hivyo Eliya akainuka na kushuka pamoja naye kwa mfalme.
16 Le hoe re tama’e: Hoe ty nafè’ Iehovà: Ie nañitrik’ ìrake hañontane i Baalezebobe, ‘ndrahare’ i Ekrone; tsy aman’Añahare hao t’Israele hañontanea’o i tsara’ey? Toly ndra tsy hizotsoa’o o fandreañe nijoña’oo fa toe hivetrake.
Akamwambia mfalme, “Hili ndilo asemalo Bwana: Je, ni kwa sababu hakuna Mungu katika Israeli wa kumuuliza habari, ndiyo maana ukatuma wajumbe kuuliza Baal-Zebubu, mungu wa Ekroni? Kwa sababu umefanya hili, kamwe hutaondoka kwenye kitanda unachokilalia. Hakika utakufa!”
17 Aa le nihomake re ty amy tsara’ Iehovà nisaontsie’ i Eliày. Le niorotse nandimbe aze nifehe t’Iehorame amy taom-paharoe’ Iehorame ana’ Iehosafate mpanjaka’ Iehoday; amy t’ie tsy nanañ’ ana-dahy.
Hivyo akafa, sawasawa na lile neno la Bwana ambalo Eliya alikuwa amesema. Kwa kuwa Ahazia hakuwa na mwana, Yoramu akawa mfalme baada yake katika mwaka wa pili wa Yehoramu mwana wa Yehoshafati mfalme wa Yuda.
18 Le o fitoloñañe ila’e nanoe’ i Ahkaziào, tsy fa sinokitse amy bokem-pamoliliañe o mpanjaka’ Israeleoy hao?
Kwa matukio mengine ya utawala wa Ahazia na yale aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?