< 1 Tesaloniana 5 >
1 Aa ty amo androo naho o sa-ao, ry longo, tsy ipaia’ areo ho sokireñe.
Sasa, kwa habari ya muda na nyakati, ndugu, hamna haja kwamba kitu chochote kiandikwe kwenu.
2 Fa toe fohi’ areo te ho tondroke manahake ty mpamaoke haleñe ty andro’ i Talè.
Kwa kuwa ninyi wenyewe mwajua kwa usahihi ya kuwa siku ya Bwana inakuja kama mwizi ajapo usiku.
3 Ie manao ty hoe, Fierañerañañe naho Fañanintsiñe! te mone hiambotrahan-karotsahañe, manahake ty fitsongoan-drakemba mivesatse, ie tsy hahabolititse.
Pale wasemapo kuna “Amani na usalama”, ndipo uharibifu huwajia ghafla. Ni kama utungu umjiavyo mama mwenye mimba. Hawataepuka kwa njia yeyote.
4 Fe tsy añ’ieñe ao nahareo ry longo, hivovoa’ i andro zay hoe malaso.
Lakini ninyi, ndugu hampo kwenye giza hata ile siku iwajie kama mwizi.
5 F’ie songa an-kazavàñe naho ana’ ty atoandro, tsy mpiamo haleñeo ndra o fimoromoroñañeo.
Kwa maana ninyi nyote ni wana wa nuru na wana wa mchana. Sisi siyo wana wa usiku au wa gizani.
6 Aa ee t’ie tsy hirotse, manahake o ila’eo, fa hitao naho hilie-batañe.
Hivyo basi, tusilale kama wengine walalavyo. Bali tukeshe na kuwa makini.
7 Mirotse haleñe o mirotseo naho mamo haleñe o mpijikeo.
Kwa kuwa wanaolala hulala usiku na wanao lewa hulewa usiku.
8 Aa kanao mpiamo atoandroo, antao ho marea, hampitsetake ty fikalañan’ arañam-patokisañe naho fikokoañe vaho hisabaka i fitamàm-pandrombahañey.
Kwa kuwa sisi ni wana wa mchana, tuwe makini. Tuvae ngao ya imani na upendo, na, kofia ya chuma, ambayo ni uhakika wa wokovu wa wakati ujao.
9 Tsy tinendren’ Añahare ho an-kaviñerañe tika, fa t’ie ho rombaheñe añamy Talèntika Iesoà Norizañey,
Kwa kuwa Mungu hakutuchagua mwanzo kwa ajili ya gadhabu, bali kwa kupata wokovu kwa njia ya Bwana Yesu Kristo.
10 ie nivilasy ho antikañe, le he mañente ke mirotse ro hitraofan-tika haveloñe.
Yeye ndiye aliyetufia ili kwamba, tukiwa macho au tumelala, tutaishi pamoja naye.
11 Aa le mifañosiha, naho mifampiraoraòa, hambañe ami’ty fanoe’ areo avao.
Kwa hiyo, farijianeni na kujengana ninyi kwa ninyi, kama ambavyo tayari mnafanya.
12 Mihalaly ama’ areo zahay, ry longo, ty hiasia’ areo o mpifanehake ama’ areo naho mpifehe vaho mpanoro anahareoo amy Talè ao.
Ndugu, twawaomba muwatambue wale wanaotumika miongoni mwenu na wale walio juu yenu katika Bwana na wale wanao washauri.
13 Le aonjono am-pikokoañe o fitoloña’ iareoo, vaho mifampilongoa.
Tunawaomba pia muwatambue na kuwapa heshima katika upendo kwa sababu ya kazi yao. Muwe na amani miongoni mwenu ninyi wenyewe.
14 Risihe’ay nahareo ry longo, hatahatào o mañarinjeñeo, ohoño o mimoremoretseo, imbao o midazidazìtseo vaho hene ilofiho.
Twawasihi, ndugu: muwaonye wasio kwenda kwa utaratibu, watieni moyo walio kata tamaa, Wasaidieni walio wanyonge, na muwe wavumilivu kwa wote.
15 Asoao tsy hamalean-draty ty raty ndra ama’ ia ia, fe paiao nainai’e ty hañasoa ty ila’e naho ze fonga ondaty.
Angalieni asiwepo mtu yeyote anayelipa baya kwa baya kwa mtu yeyote. Badala yake, fanyeni yaliyo mema kwa kila mmoja wenu na kwa watu wote.
18 kila andriañeñe; fa izay ty satrin’ Añahare ho anahareo am’ Iesoà Norizañey.
Mshukuruni Mungu kwa kila jambo, kwa sababu hayo ndiyo mapenzi ya Mungu kwenu katika Yesu Kristo.
20 Ko mavoeñe o fitokiañeo,
Msiudharau unabii.
21 fa biribirio ze he’e; tambozoro ty soa.
Yajaribuni mambo yote. Mlishike lililo jema.
22 Ifoneño ze atao haratiañe.
Epukeni kila mwonekano wa uovu.
23 I Andrianañaharem-pañanintsiñey abey ro hañeneke ty fiavaha’areo, hañaro ty arofo naho ty fiaiñe vaho ty sandri’ areo ho fonitse tsy aman-kila amy fitotsaha’ i Talèntika Iesoà Norizañeiy.
Mungu wa amani awakamilishe katika utakatifu. Roho, nafsi na mwili vitunzwe pasipo mawaa katika kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo.
24 Migahiñe t’i mikanjy anahareo, Ie ro hañeneke izay.
Yeye aliyewaita ni mwaminifu, naye ndiye mwenye kutenda.
25 Ry rahalahio, mihalalia ho anay.
Ndugu, tuombeeni pia.
26 Añontaneo an’ oroke miavake o longo iabio,
Wasalimuni ndugu wote kwa busu takatifu.
27 Afantoko ama’ areo amy Talè ty hamaky ty taratasy toy amo longo iabio.
Nawasihi katika Bwana kwamba barua hii isomwe kwa ndugu wote.
28 Ho ama’ areo abey ty hasoa’ i Talèntika Iesoà Norizañey.
Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe pamoja nanyi.