< 1 Mpanjaka 3 >
1 Nanao filongoañe am-panambaliañe amy Parò mpanjaka’ i Mitsraime t’i Selomò, ie nañenga ty anak’ampela’ i Parò, vaho nendese’e an-drova’ i Davide ampara’ te nifonitse ty anjomba nandranjia’e naho ty anjomba’ Iehovà naho ty kijoli’ Ierosalaime nañarikatoke aze.
Solomoni akafanya urafiki na Mfalme Farao wa Misri na kumwoa binti yake. Akamleta huyo binti katika Mji wa Daudi mpaka alipomaliza kujenga jumba lake la kifalme na Hekalu la Bwana, pamoja na ukuta kuzunguka Yerusalemu.
2 Nanao soroñe ankaboañe eñe ondatio, amy t’ie tsy aman’ anjomba rinafitse ho amy tahina’ Iehovày tañ’andro izay.
Hata hivyo, watu bado walikuwa wakitoa dhabihu huko kwenye vilima, kwa sababu Hekalu lilikuwa bado halijajengwa kwa ajili ya Jina la Bwana.
3 Nikokoa’ i Selomò t’Iehovà naho nañavelo amo fañèn-drae’eo; f’ie nanao soroñe an-kaboañe eo.
Solomoni akaonyesha upendo wake kwa Bwana kwa kuenenda sawasawa na amri za Daudi baba yake, ila yeye alitoa dhabihu na kufukiza uvumba huko mahali pa juu.
4 Nimb’e Gibone añe i mpanjakay hisoroñe amy te izay ty haboañe bey; soroñe arivo ty nengae’ i Selomò amy kitrely zay.
Mfalme akaenda Gibeoni kutoa dhabihu, kwa maana ndipo palipokuwa mahali pa juu pa kuabudia, naye Solomoni akatoa sadaka elfu moja za kuteketezwa juu ya hayo madhabahu.
5 Ie te Gibone añe, le nisodehañe amy Selomò haleñe ami’ty nofy t’Iehovà; le hoe t’i Andrianañahare: Mihalalia, Ino ty hatoloko azo?
Bwana akamtokea Solomoni huko Gibeoni wakati wa usiku katika ndoto, naye Mungu akasema, “Omba lolote utakalo nikupe.”
6 Le hoe t’i Selomò: Fañisoham-bey ty natolo’o amy Davide raeko mpitoro’o, ie nañavelo añatrefa’o an-katò naho an-kavantañañe, naho an-kavañonan’ arofo vaho nahaja’o ho aze o fatarihañe ra’elahy zao te tinolo’o anake hiambesatse amy fiambesa’ey manahake henanekeo.
Solomoni akajibu, “Umemfanyia mtumishi wako, baba yangu Daudi, fadhili nyingi, kwa kuwa alikuwa mwaminifu kwako na mwenye haki, tena mnyofu wa moyo. Nawe umemzidishia fadhili hii kuu kwani umempa mwana wa kuketi kwenye kiti chake cha ufalme, kama ilivyo leo.
7 Ie henane zao, ry Iehovà Andrianañahareko, fa nanoe’o mpanjaka handimbe i Davide raeko ty mpitoro’o; izaho mbe anak’ ajaja, tsy mahay miakatse ndra mimoake.
“Sasa, Ee Bwana Mungu wangu, umemfanya mtumishi wako mfalme badala ya baba yangu Daudi. Lakini mimi ni mtoto mdogo tu, wala sijui jinsi ya kutekeleza wajibu wangu.
8 Le añivo’ ondati’o jinobo’oo ty mpitoro’o, ondaty mitozantozañe tsy lefe iaheñe ami’ty havasiaña’e.
Mtumishi wako yuko hapa miongoni mwa watu uliowachagua: taifa kubwa, watu wengi wasioweza kuhesabika wala kutoa idadi yao.
9 Aa le toloro troke mahilala ty mpitoro’o hahafizaka’e ondati’oo, hahafitsakorea’e añivo’ ty soa naho ty raty; fa ia ty hahafizaka ondati’o ra’elahy retoañe?
Hivyo mpe mtumishi wako moyo wa ufahamu ili kutawala watu wako na kupambanua kati ya mema na mabaya. Kwa maana, ni nani awezaye kutawala watu wako hawa walio wengi hivi?”
10 Nisoa ampihaino’ i Talè, i nihalalia’ i Selomòy.
Bwana akapendezwa kwamba Solomoni ameliomba jambo hili.
11 Le hoe t’i Andrianañahare ama’e: Kanao izay ty nihalalia’o, naho tsy hinalali’o ho azo ty halava-haveloñe, tsy hinalali’o ho azo ty vara-bey, tsy hinalali’o ty fiain-drafelahi’o; fe nihalalie’o ty fahafohinañe hahatsikaritse ty hatò.
Basi Mungu akamwambia, “Kwa kuwa umeomba neno hili na hukuomba maisha marefu au upate utajiri kwa nafsi yako, wala adui zako wafe, bali umeomba ufahamu katika kutoa haki,
12 Inao, nanoeko i sinaontsi’oy: ingo te nitolorako arofo mahihitse naho mahilala; kanao tsy eo ty nanahak’ azo taolo’o, naho tsy ho amam-panonjohy hitroatse hañirinkiriñe azo;
nitafanya lile uliloomba. Nitakupa moyo wa hekima na wa ufahamu, kiasi kwamba hajakuwepo mtu mwingine kama wewe, wala kamwe hatakuwepo baada yako.
13 vaho natoloko azo ka o tsy nihalalie’oo, ty vara naho ty asiñe, soa tsy eo ty mpanjaka hanahak’ azo amo hene andro’oo.
Zaidi ya hayo, nitakupa yale ambayo hukuomba, yaani utajiri na heshima, ili kwamba maisha yako yote hapatakuwa na mtu kama wewe miongoni mwa wafalme.
14 Aa naho añaveloa’o o lalakoo, hañambeñe o fañèkoo naho o lilikoo, manahake ty fañaveloan-drae’o Davide, le halavaeko o andro’oo.
Nawe kama ukienenda katika njia zangu na kutii sheria na amri zangu kama baba yako Daudi alivyofanya, nitakupa maisha marefu.”
15 Nivañoñe amy zao t’i Selomò le naheo’e t’ie nofy; nomb’e Ierosalaime mb’eo re, nijohañe añatrefa’ i vatam-pañina’ i Talèy eo le nañenga soroñe naho engam-panintsiñañe, vaho nanoa’e sabadidake o mpitoro’e iabio.
Ndipo Solomoni akaamka, akatambua kuwa ilikuwa ndoto. Akarudi Yerusalemu, akasimama mbele ya Sanduku la Agano la Bwana, naye akatoa dhabihu za kuteketezwa na sadaka za amani. Kisha akawafanyia watumishi wake wote karamu.
16 Niheo mb’amy mpanjakay amy zao ty karapilo roe, nijohañe añatrefa’e eo
Basi wanawake wawili makahaba walikuja kwa mfalme na kusimama mbele yake.
17 le hoe ty rakemba raike: O ry talèko, mitrao-pimoneñe an-kibohotse ami’ty rakemba tiañe iraho; vaho nahatoly ajaja t’ie an-traño ao.
Mmojawapo akasema, “Bwana wangu, mimi na mwanamke huyu tunaishi kwenye nyumba moja. Nilikuwa nimezaa alipokuwa pamoja nami.
18 Aa ie amy andro fahatelo’ i niterahakoiy le nahatoly ka o rakembao, vaho niharo ao zahay; tsy aman’ ambahiny i kibohotsey naho tsy zahay roe avao ty an-traño ao.
Siku ya tatu baada ya mtoto wangu kuzaliwa, mwanamke huyu pia naye akazaa mtoto. Tulikuwa peke yetu, hapakuwa na mtu mwingine yeyote katika nyumba isipokuwa sisi wawili.
19 Nisimba haleñe ty ana’ i rakembay, amy te nandrea’e.
“Wakati wa usiku mwana wa huyu mwanamke akafa kwa sababu alimlalia.
20 Nitroatse amy haleñey re nandrambe i anadahiko marine ahiy, ie niroro ty anak’ ampata’o, le nampandre’e añ’ araña’e; vaho napo’e añ’ arañako eo i ana’e niopoy.
Hivyo akaondoka katikati ya usiku na kumchukua mwanangu kutoka ubavuni pangu wakati mimi mtumishi wako nilipokuwa nimelala. Akamweka kifuani mwake na kumweka mwanawe aliyekufa kifuani mwangu.
21 Aa izaho nañente te maraindray hampinono i anakoy, hehe te mate; f’ie nibiribirieko amy maraiñey; hete! tsy i ana-dahy naterakoy toke.
Asubuhi yake, nikaamka ili kumnyonyesha mwanangu, naye alikuwa amekufa! Lakini nilipomwangalia sana katika nuru ya asubuhi, niliona kuwa hakuwa yule mwana niliyekuwa nimemzaa.”
22 Le hoe ka i rakemba raikey: Aiy! i veloñey ro anako, vaho simba i azoy; Fa hoe ka ty asa’ itiañe: Tsie fa toe ana’o i nisimbay, vaho veloñe i anadahiko. Izay ty enta’ iareo añ’ atrefa’ i mpanjakay.
Huyo mwanamke mwingine akasema, “Hapana! Mwana aliye hai ndiye wangu, aliyekufa ni wako.” Lakini yule wa kwanza akasisitiza, “Hapana! Mwana aliyekufa ni wako, aliye hai ni wangu.” Hivi ndivyo walivyobishana mbele ya mfalme.
23 Le hoe i mpanjakay: Hoe ty asa’ ty raike: Anadahiko ty veloñe toy, naho mate i ana-dahi’oy; hoe ka i raikey: Aiy! fa i ana’oy ty mate vaho veloñe i anadahikoy.
Mfalme akasema, “Huyu anasema, ‘Mwanangu ndiye aliye hai, na aliyekufa ndiye mwanao,’ maadamu yule anasema, ‘Hapana! Aliyekufa ni wako, na aliye hai ni wangu.’”
24 Le hoe i mpanjakay: Angalao fibara, le nindesa’ iareo fibara i mpanjakay.
Kisha mfalme akasema, “Nileteeni upanga.” Basi wakamletea mfalme upanga.
25 Le hoe i mpanjakay: Tampaho roe i ajaja veloñey, le atoloro amy raikey ty vaki’e naho amy ila’ey ty vaki’e.
Ndipo mfalme akatoa amri: “Mkate mtoto aliye hai vipande viwili; mpe huyu nusu na mwingine nusu.”
26 fe nitoreo amy mpanjakay i rakemba rene’ i ajaja veloñeiy, ie niferenaiñan-tro’e i ana-dahi’ey, ami’ty hoe: O talèko, atoloro aze i ajaja veloñey, ehe tsy vonoeñe, Fa hoe ka i raikey, Tsy ho ahy tsy ho azo; salàho!
Mwanamke ambaye mwanawe alikuwa hai akajawa na huruma kwa ajili ya mwanawe na kumwambia mfalme, “Tafadhali, bwana wangu, mpe yeye mtoto aliye hai! Usimuue!” Lakini yule mwanamke mwingine akasema, “Mkate vipande viwili. Asiwe wangu au wake!”
27 Aa le hoe ty navale’ i mpanjakay: Atoloro aze i ajaja veloñey le ko vonoeñe! ie ty rene’e.
Kisha mfalme akatoa uamuzi wake: “Mpeni mama wa kwanza mtoto aliye hai. Msimuue; ndiye mama yake.”
28 Jinanji’ Israele iaby i zaka tinaro’ i mpanjakaiy; vaho nañeveñe amy mpanjakay, amy te nioni’ iareo te ama’e ty hihin’ Añahare hahahenefa’e zaka.
Wakati Israeli yote iliposikia hukumu aliyotoa mfalme, wakamwogopa mfalme, kwa sababu waliona kuwa alikuwa na hekima kutoka kwa Mungu kwa kutoa haki.