< 1 Tantara 27 >
1 Ty famoliliañe o ana’ Israeleo, o talèn’ anjomban-droae naho o mpifelek’ arivo naho zatoo naho o roandriañe mpitoroñe i mpanjakaio aman-dra inoñ’ inoñe amo firimboñañe mimoak’ ao naho miavotse mb’eo am-bolañ’ am-bolañe amo hene volan-taoñeo, ie songa ro’ale-tsi-efats’ arivo ami’ty firimboñañe.
Hii ndiyo orodha ya Waisraeli: viongozi wa jamaa, majemadari wa maelfu, majemadari wa mamia na maafisa wao, waliomtumikia mfalme kwa lolote lililohusu vikosi vya jeshi vilivyokuwa zamu mwezi baada ya mwezi katika mwaka mzima. Kila kikosi kimoja kilikuwa na watu 24,000.
2 Ambone’ ty firimboñam-bolam-baloha’e t’Iasobeame ana’ i Zabdiele,
Msimamizi wa kikosi cha kwanza kwa mwezi wa kwanza alikuwa Yashobeamu mwana wa Zabdieli. Kulikuwa na watu 24,000 katika kikosi chake.
3 tarira’ i Peretse, ie nitalèm-pifehe’ i valobohòkey amy volam-baloha’ey.
Yeye alikuwa mzao wa Peresi, na mkuu wa maafisa wote wa jeshi kwa mwezi wa kwanza.
4 Ambone’ i firimboñam-bolam-paharoey t’i Doday nte Akoký, i Miklote nitalè’ i firimboñañey; ro’ale-tsi-efats’ arivo ro amy firimboña’ey.
Msimamizi wa kikosi kwa mwezi wa pili alikuwa Dodai Mwahohi. Miklothi ndiye alikuwa kiongozi wa kikosi chake. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
5 I Benaià ana’ Iehoiada, mpisoroñe, mpiaolo, nimpifehe’ fahatelo’ i valobohòkey ho am-bolam-pahatelo, ro’ale-tsi-efats’ arivo ro amy firimboña’ey.
Jemadari wa kikosi cha tatu kwa mwezi wa tatu alikuwa Benaya mwana wa kuhani Yehoyada. Ndiye alikuwa mkuu wa kikosi chake kilichokuwa na watu 24,000.
6 Ie i Benanià nifanalolahy amy telopoloy naho nifehe i telopoloy; talè i firimboña’ey t’i Amizabade ana’e.
Huyu ndiye yule Benaya aliyekuwa shujaa miongoni mwa wale Thelathini na ndiye alikuwa juu yao hao Thelathini. Mwanawe Amizabadi ndiye alikuwa mkuu katika kikosi chake.
7 Ty fah’ efatse ho am-bolam-pahefatse le i Asaele, rahalahi’ Ioabe naho i Zebadià ana’e ty nandimbe aze; ro’ ale-tsi-efats’ arivo ro amy firimboña’ey.
Jemadari wa nne kwa mwezi wa nne alikuwa Asaheli nduguye Yoabu, mwanawe Zebadia ndiye aliingia mahali pake kwenye uongozi. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
8 Ty fahalime ho am-bolam-pahalime i Samhote nte Iizrake; ni-ro’ ale-tsi-efats’ arivo amy firimboña’ey.
Jemadari wa kikosi cha tano kwa mwezi wa tano alikuwa Shamhuthi Mwizrahi. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
9 Ty fah’ eneñe ho am-bolam-pah’ eneñe i Irà ana’ Ikese nte-Tekoy; ro’ale-tsi-efats’ arivo ro amy firimboña’ey.
Jemadari wa kikosi cha sita kwa mwezi wa sita alikuwa Ira, mwana wa Ikeshi Mtekoa. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
10 Ty faha-fito ho am-bolam-pahafito, i Keletse, nte-Pelone, tarira’ i Efraime; ro’ale-tsi-efats’ arivo ro amy firimboña’ey.
Jemadari wa kikosi cha saba kwa mwezi wa saba alikuwa Helesi Mpeloni wa Waefraimu. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
11 Ty fahavalo ho am-bolam-pahavalo i Sibekay nte Kosate, tarira’ i Zerake; ro’ale-tsi-efats’ arivo ro amy firimboña’ey.
Jemadari wa nane kwa mwezi wa nane, alikuwa Sibekai Mhushathi wa Wazera. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
12 Ty fahasive ho am-bolam-pahasive, i Abiezere, nte Anatote, tarira’ i Beniamine; ro’ale-tsi-efats’ arivo ro amy firimboña’ey.
Jemadari wa tisa kwa mwezi wa tisa alikuwa Abiezeri Mwanathothi wa Wabenyamini. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
13 Ty fahafolo ho am-bolam-pahafolo, i Makray, nte Netofate, tarira’ i Zarkry, ro’ ale-tsi-efats’ arivo ro amy firimboña’ey.
Jemadari wa kumi kwa mwezi wa kumi alikuwa Maharai Mnetofathi wa Wazera. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
14 Ty fahafolo-raik’ amby ho am-bolam-pahafolo-raik’ amby, i Benaià, nte Pirato, tarira’ i Efraime; ro’ale-tsi-efats’ arivo ro amy firimboña’ey.
Jemadari wa kumi na moja kwa mwezi wa kumi na moja alikuwa Benaya Mpirathoni wa Waefraimu. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
15 Ty fahafolo-ro’ amby ho am-bolam-pahafolo-ro’ amby, i Keldày nte-Netofate, tarira’ i Otniele, ro’ ale-tsi-efats’ arivo ro amy firimboña’ey.
Jemadari wa kumi na mbili kwa mwezi wa kumi na mbili alikuwa Heldai Mnetofathi kutoka jamaa ya Othnieli. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
16 Aa naho ty nifehe’ o fifokoa’ Israeleo: Amo nte-Reobeneo, i Eliezere ana’ i Zikrý, nitalè; amo nte-Simoneo, i Sefatià, ana’ i Maakà;
Maafisa waliokuwa wanaoongoza makabila ya Israeli walikuwa: Kwa Wareubeni: Eliezeri mwana wa Zikri; kwa Wasimeoni: Shefatia mwana wa Maaka;
17 amy Levý, i Kasabià, ana’ i Kemoele; amy Aharone, i Tsadoke;
kwa Walawi: Hashabia mwana wa Kemueli; kwa Aroni: Sadoki;
18 amy Iehodà, i Elihò, rahalahi’ i Davide; amy Isakare, i Omrý ana’ i Mikaele;
kwa Yuda: Elihu, nduguye Daudi; kwa Waisakari: Omri mwana wa Mikaeli;
19 amy Zebolone, Ismaià ana’ i Obadià; amy Naftalý, Ierimote ana’ i Azriele;
kwa Wazabuloni: Ishmaya mwana wa Obadia; kwa Wanaftali: Yeremothi mwana wa Azrieli;
20 amo ana’ i Efraimeo, i Hoseà ana’ i Azazià; amy vakim-pifokoa’ i Menasèy, Ioele ana’ i Pedaià;
kwa Waefraimu: Hoshea mwana wa Azazia; kwa nusu ya kabila la Manase: Yoeli mwana wa Pedaya;
21 amy vakim-pifokoa’ i Menasè e Giladey, Idò ana’ i Zekarià; amy Beniamine, Iaasiele, ana’ i Abnere;
kwa nusu nyingine ya kabila la Manase huko Gileadi: Ido mwana wa Zekaria; kwa Wabenyamini: Yaasieli mwana wa Abneri;
22 amy Dane, i Azarele, ana’ Ierokame. Ie ro mpiaolo o fifokoa’ Israeleo.
kwa Wadani: Azareli mwana wa Yerohamu. Hao ndio waliokuwa maafisa wa makabila ya Israeli.
23 Tsy niahe’ i Davide ze ambane ty roapolo taoñe, ami’ty nafè’ Iehovà te hampitomboe’e manahake o vasian-dikerañeo t’Israele.
Daudi hakuwahesabu watu waliokuwa chini ya miaka ishirini, kwa sababu Bwana alikuwa ameahidi kuwafanya Israeli kuwa wengi kama nyota za angani.
24 Toe niorotse nañiake t’Ioabe ana’ i Tseroià fe tsy nahatafetetse naho nifetsak’ am’ Israele ty haviñerañe vaho tsy nazilik’ amo talili’ i Davide, mpanjakao, i iakey.
Yoabu mwana wa Seruya alianza kuwahesabu watu lakini hakumaliza. Kwa sababu ya kuwahesabu watu, hasira ya Mungu iliwaka juu ya Israeli, nayo hiyo hesabu yao haikuingizwa katika kitabu cha kumbukumbu za Mfalme Daudi.
25 Nifehe o fanontonam-bara’ i mpanjakaio t’i Azmavete ana’ i Adiele; le nifehe o trañom-bara an-kivok’ ey naho amo rovao naho amo tanàñeo vaho amo fitalakesañ’ aboo t’Iehonatane, ana’ i Otsià.
Azmawethi mwana wa Adieli ndiye alikuwa msimamizi wa hazina za mfalme. Msimamizi wa hazina katika mashamba, miji, vijiji na kwenye ngome alikuwa Yonathani mwana wa Uzia.
26 Le nifehe o nitoloñe an-tetek’ ao o mpiava-taneo, t’i Etsrý ana’ i Kelobe;
Ezri mwana wa Kelubu alikuwa msimamizi wa wafanyakazi waliolima katika mashamba.
27 le nifehe o tanem-baheo t’i Simeý nte Ramà; le nifehe ty voka’ o tanembaheo ho amo lakaton-divaio t’i Zabdý nte-Sifmý;
Shimei Mramathi alikuwa msimamizi wa mashamba ya mizabibu. Zabdi Mshifmi alikuwa msimamizi wa zabibu, utengenezaji na uhifadhi wa divai katika mapipa makubwa.
28 nifehe o zaite naho sakoañe amo vavataneoo t’i Baale-kanane nte-Gedere; naho nifehe o lakato-menakeo t’Ioase.
Baal-Hanani Mgederi ndiye alikuwa mwangalizi wa mashamba ya mfalme ya mizeituni na mikuyu katika tambarare za vilima vya magharibi. Yoashi alikuwa msimamizi wa ghala za mafuta ya zeituni.
29 Le nifehe o mpirai-troke nandrazeñe e Saroneo t’i Sitraý nte-Sarone; naho nifehe o mpirai-troke am-bavataneo t’i Safate, ana’ i Adlaý;
Shitrai Msharoni alikuwa msimamizi wa makundi ya ngʼombe waliojilisha huko Sharoni. Shafati mwana wa Adlai alikuwa msimamizi wa yale makundi ya ngʼombe yaliyokuwa makondeni.
30 nifehe o ramevao ka t’i Obile nte-Ismaele; naho nifehe o birìkeo t’Iekdeià nte-Meronote;
Obili Mwishmaeli alikuwa msimamizi wa ngamia. Yedeya Mmeronothi alikuwa msimamizi wa punda.
31 le nifehe o lia-raikeo t’Iazize, nte-Hagrý. Ie ro mpifehe ty vara’ i Davide mpanjaka.
Yazizi Mhagri alikuwa msimamizi wa makundi ya kondoo na mbuzi. Hawa wote ndio waliokuwa maafisa wasimamizi wa mali alizokuwa nazo Mfalme Daudi.
32 Nimpanoro-kevetse naho ondaty mahihitse vaho mpanokitse t’Ionatane rahalahin-drae’ i Davide; mpañabey o anam-panjakao t’Iekiele ana’ i Kakmoný.
Yonathani mjomba wa Daudi alikuwa mshauri, mtu mwenye ufahamu mkubwa na mwandishi. Yehieli mwana wa Hakmoni alikuwa akiwahudumia wana wa mfalme.
33 Nimpanolo-heve’ i mpanjakay t’i Akitofele naho mpiamy mpanjakay t’i Kosay nte-Ereke;
Ahithofeli alikuwa mshauri wa mfalme. Hushai Mwariki alikuwa rafiki wa mfalme.
34 nandimbe i Akitofele t’Iehoiadà ana’ i Benaià naho i Abiatare; vaho nimpifehe o lahindefo’ i mpanjakaio t’Ioabe.
Baada ya Ahithofeli, Yehoyada mwana wa Benaya aliingia mahali pake kama mshauri wa mfalme pamoja na Abiathari. Yoabu alikuwa ndiye jemadari wa majeshi ya mfalme.