< प्रेरितों के काम 26 >

1 अग्रिप्पे पौलुसो खे बोलेया, “ताखे आपणे बारे रे बोलणे री आज्ञा आए।” तेबे पौलुस आथ आगे करी की जवाब देणे लगेया,
Ndipo Agripa akamwambia Paulo, “Unayo ruhusa kujitetea.” Hivyo Paulo akawaashiria kwa mkono wake, akaanza kujitetea, akasema:
2 “ओ अग्रिप्पा राजा! जितणी गल्ला रा यहूदी अगुवे मां पाँदे दोष लगाणे लगी रे, आज तां सामणे तिना रा जवाब देणे खे आऊँ आपू खे धन्य समजूँआ।
“Mfalme Agripa, najiona kuwa na heri kusimama mbele yako leo ninapojitetea kuhusu mashtaka yote ya Wayahudi,
3 खास कर इजी खे कि तूँ यहूदिया रे सब व्यवहार और बईसा खे जाणेया। तेबे आऊँ बिनती करूँआ कि शान्त ऊई की मेरी सुणो।
hasa kwa sababu unajua vyema desturi zote za Kiyahudi na ya kuwa wewe unajua kwa undani mila na masuala ya mabishano. Kwa hiyo, nakusihi unisikilize kwa uvumilivu.
4 “जेड़ा मेरा चाल-चलण शुरूओ ते आपणी जातिया बीचे और यरूशलेमो रे था, ये सब यहूदिया रे अगुवा जाणोए।
“Wayahudi wote wanajua jinsi nilivyoishi tangu nilipokuwa mtoto, kuanzia mwanzo wa maisha yangu katika nchi yangu na pia huko Yerusalemu.
5 सेयो जे गवाई देणा चाओए, तो शुरूओ ते माखे पछयाणोए कि आऊँ फरीसी ऊई की आपणे तर्मो रे सबी ते खरे पन्थो रे मुताबिक चलेया।
Wao wamefahamu kwa muda mrefu na wanaweza kushuhudia kama wakipenda, ya kwamba kutokana na misimamo mikali sana ya dhehebu letu kwenye dini yetu, niliishi nikiwa Farisayo.
6 और एबे तेस वादे री उम्मीदा री बजअ ते, जो परमेशरे आसा रे बाप-दादेया साथे कित्ती थी, मां पाँदे मुकद्दमा चली रा।
Nami sasa ni kwa sababu ya tumaini langu katika kile ambacho Mungu aliwaahidi baba zetu, ninashtakiwa leo.
7 तेसी वादे रे पूरे ऊणे री उम्मीद लगाए रे आसा रे बारा गोत्र, आपणे सारे मनो ते रात-दिन परमेशरो री सेवा करदे आयी रे। ओ राजा! इजी उम्मीदा रे बारे रे यहूदी मां पाँदे दोष लगाणे लगी रे।
Hii ndiyo ahadi ambayo makabila yetu kumi na mawili yanatarajia kuiona ikitimizwa wanapomtumikia Mungu kwa bidii usiku na mchana. Ee mfalme, ninashtakiwa na Wayahudi kwa ajili ya tumaini hili.
8 जबकि जादातर यहूदी ये विश्वास करोए कि परमेशर मरे रेया खे जिऊँदा करोआ, तो तुसा रे एती, ये गल्ल कऊँ विश्वासो जोगी नि समजी जांदी?
Kwa nini yeyote miongoni mwenu afikiri kwamba ni jambo lisilosadikika Mungu kufufua wafu?
9 “मैं बी सोचेया था कि यीशु नासरियो रे नाओं रे बिरोदो रे माखे बऊत कुछ करना चाईयो।
“Mimi pia nilikuwa nimeshawishika kwamba imenipasa kufanya yote yale yaliyowezekana kupinga Jina la Yesu wa Nazareti.
10 और मैं यरूशलेमो रे एड़ा ई कित्तेया और बड़े पुरोईता ते अक्क पाई की बऊत सारे पवित्र लोक जेला रे पाए और जेबे सेयो काए जाओ थे, तो आऊँ बी तिना रे बिरोदो रे आपणी सलाह देऊँ था।
Nami hayo ndiyo niliyoyafanya huko Yerusalemu. Kwa mamlaka ya viongozi wa makuhani, niliwatia wengi wa watakatifu gerezani na walipokuwa wakiuawa, nilipiga kura yangu kuunga mkono.
11 आऊँ हर प्रार्थना रे कअरो रे तिना खे कूटी-कूटी की यीशुए री निन्दा करवाऊँ था, एथो तक कि रोषो रे मारे इतणा पागल ऊईगा कि बारले नगरो रे जाई की बी तिना खे सताऊँ था।
Mara nyingi nilikwenda kutoka sinagogi moja hadi ingine nikiamuru waadhibiwe, nami nilijaribu kuwalazimisha wakufuru. Katika shauku yangu dhidi yao, hata nilikwenda miji ya kigeni ili kuwatesa.
12 “एसी धुना रे जेबे आऊँ बड़े पुरोईता ते अक्क और आज्ञा-पत्र लयी की दमिश्को नगरो खे जाणे लगी रा था,
“Siku moja nilipokuwa katika mojawapo ya safari hizi nikiwa ninakwenda Dameski, nilikuwa na mamlaka na agizo kutoka kwa kiongozi wa makuhani.
13 तेबे ओ राजा! बाटा रे त्याड़िया जे, मैं सर्गो ते एक सूरजो री चमका ते बी बढ़ी की एक जोति आपू पाँदे और साथे चलणे वाल़ेया रे चऊँ कनारे चमकदी ऊई देखी।
Ilikuwa yapata adhuhuri, ee mfalme, nilipokuwa njiani, niliona nuru kutoka mbinguni kali kuliko jua, ikingʼaa kunizunguka pande zote mimi na wale niliokuwa pamoja nao.
14 और जेबे आसे सब जमीना पाँदे रूड़ी गे, तेबे मैं इब्रानी पाषा (भाषा) रे मां साथे बोलदे ऊए ये शब्द सुणेया, ‘ओ शाऊल! ओ शाऊल! तूँ माखे कऊँ सताणे लगी रा? पईने पाँदे लाते बाणी ईदे तेरा ई नुकशाण ए।’
Wote tulipokuwa tumeanguka chini, nikasikia sauti ikisema nami kwa lugha ya Kiebrania, ‘Sauli, Sauli, mbona unanitesa? Ni vigumu kwako kuupiga teke mchokoo.’
15 मैं बोलेया, ‘ओ प्रभु! तूँ कुण ए?’ प्रभुए बोलेया, ‘आऊँ यीशु ए, जेसखे तूँ सताएया।
“Nikauliza, ‘Ni nani wewe, Bwana?’ “Naye Bwana akajibu, ‘Ni Mimi Yesu unayemtesa.
16 पर तूँ उठ, आपणे पैरा पाँदे खड़ा ओ, कऊँकि मैं ताखे इजी री खातर दर्शन देई राखेया, ताकि ताखे तिना गल्ला रा सेवक और गवा ठराऊँ, जो तैं देखी राखिया और तिना रा बी, जिना री तंईं मां ताखे दर्शन देणा
Sasa inuka usimame kwa miguu yako. Nimekutokea ili nikuteue uwe mtumishi na shahidi wa mambo ambayo umeyaona, na yale nitakayokuonyesha.
17 यहूदियो और दुजिया जातिया ते, जिना बीचे आँऊ ताखे पेजणे लगी रा मां तूँ तिना ते बचाणा।
Nitakuokoa kutoka kwa watu wako na watu wa Mataifa ambao ninakutuma kwao,
18 ताकि तूँ तिना री आखी खोल, ताकि सेयो न्हेरे ते जोतिया री तरफा खे और शैतानो रे अक्को ते परमेशरो रे राज्य री तरफा खे फिरो। ताकि सेयो पापो री माफी और तिना लोका साथे जो मां पाँदे विश्वास करने ते पवित्र कित्ते रे ए, जायदात पाओ।’
uyafumbue macho yao ili wageuke kutoka gizani waingie nuruni, na kutoka kwenye nguvu za Shetani wamgeukie Mungu, ili wapate msamaha wa dhambi na sehemu miongoni mwa wale waliotakaswa kwa kuniamini mimi.’
19 “तो ओ अग्रिप्पा राजा! मैं तेस स्वर्गिय दर्शनो री गल्ल मानी ली।
“Hivyo basi, Mfalme Agripa, sikuacha kuyatii yale maono yaliyotoka mbinguni,
20 पर पईले दमिश्क नगरो रे और तेबे यरूशलेमो रे रणे वाल़ेया खे, तेबे यहूदिया रे सारे देशो रे और दुजिया जातिया खे समजयांदा रया कि मन फिराओ और परमेशरो री तरफा खे फिरी की मन फिराणे जोगा काम करो।
bali niliyatangaza kwanza kwa wale wa Dameski, kisha Yerusalemu na katika vijiji vyote vya Uyahudi na pia kwa watu wa Mataifa, kwamba inawapasa kutubu na kumgeukia Mungu na kuthibitisha toba yao kwa matendo yao.
21 इना गल्ला री बजअ ते यहूदी माखे मन्दरो रे पकड़ने और काणे री कोशिश करो थे।
Ni kwa sababu hii Wayahudi walinikamata nilipokuwa Hekaluni, wakataka kuniua.
22 पर परमेशरो री मइरबानिया ते आऊँ आजो तक बणी रा और छोटे-बड़े सबी सामणे गवाई देऊँआ और तिना गल्ला खे छाडी की ओर कुछ नि बोलदा, जो भविष्यबक्ते और मूसे बी बोलेया कि ऊणे वाल़िया ए
Hadi leo nimepata msaada kutoka kwa Mungu, na hivyo nasimama hapa nikishuhudia kwa wakubwa na wadogo. Sisemi chochote zaidi ya yale ambayo manabii na Mose walisema yatatukia:
23 कि मसीह खे दु: ख ऊणा और तेस ई सबी ते पईले मरे देया बीचा ते जिऊँदे ऊई की यहूदी लोका बीचे और दुजिया जातिया बीचे जोतिया रा प्रचार करना।”
kwamba Kristo atateswa, na kwamba yeye atakuwa wa kwanza kufufuka kutoka kwa wafu, na atatangaza nuru kwa watu wake na kwa watu wa Mataifa.”
24 जेबे पौलुस ईंयां जवाब देणे लगी रा था, तेबे फेस्तुसे जोरे की बोलेया, “ओ पौलुस, तूँ पागल ऊईगा रा, जादा पढ़ाईये तूँ पागल बणाई ता दा।”
Paulo alipokuwa akifanya utetezi huu, Festo akasema kwa sauti kubwa, “Paulo, wewe umerukwa na akili! Kusoma kwingi kunakufanya uwe kichaa!”
25 पर पौलुसे बोलेया, “ओ महाप्रतापी फेस्तुस! आऊँ पागल निए, पर सच्चाई और बुद्धि री गल्ल करूँआ।
Lakini Paulo akajibu, “Mimi sijarukwa na akili, mtukufu sana Festo, bali nanena kweli nikiwa na akili zangu timamu.
26 राजा बी जेस सामणे आऊँ निडर ऊई की बोलणे लगी रा, इना गल्ला खे जाणोआ और माखे विश्वास ए कि इना गल्ला बीचा ते कोई एसते छीपी दी निए, कऊँकि ये घटणा कोई कूणे रे नि ऊई री।
Naam, Mfalme anajua kuhusu mambo haya yote, nami nasema naye kwa uhuru. Kwa sababu nina hakika kwamba hakuna hata mojawapo ya mambo haya asilolijua, kwa kuwa hayakufanyika mafichoni.
27 ओ अग्रिप्पा राजा! क्या तूँ भविष्यबक्तेया पाँदे विश्वास करेया? आ, आऊँ जाणूंआ कि तूँ विश्वास करेया।”
Mfalme Agripa, je, unaamini manabii? Najua kuwa unaamini.”
28 तेबे अग्रिप्पे पौलुसो खे बोलेया, “तूँ थोड़ा जा ई समजयाणे ते माखे मसीह बनाणा चाएया?”
Agripa akamwambia Paulo, “Je, unanishawishi kwa haraka namna hii niwe Mkristo?”
29 पौलुसे बोलेया, “मेरी परमेशरो ते ये प्रार्थना ए कि क्या थोड़े जे, क्या बऊत जे, बस तूँई नि, पर जितणे लोक आज मेरी सुणने लगी रे, इना बन्दना खे छाडी की सेयो मां जेड़े मसीह बणी जाओ।”
Paulo akasema, “Ikiwa ni kwa haraka au la, namwomba Mungu, si wewe peke yako bali pia wale wote wanaonisikiliza leo, wawe kama mimi nilivyo, kasoro minyororo hii.”
30 तेबे राजा, हाकिम और बिरनिके और तिना साथे बैठणे वाल़े खड़े ऊईगे
Baada ya kusema hayo, mfalme akainuka pamoja na mtawala na Bernike na wale waliokuwa wameketi pamoja nao.
31 और लग जे जाई की आपू बीचे बोलणे लगे, “ये मांणू एड़ा कुछ तो नि करदा, जो मौत या फसणे जोगा ओ।”
Walipokuwa wakiondoka, wakaambiana, “Mtu huyu hafanyi jambo lolote linalostahili kufa au kufungwa.”
32 अग्रिप्पे फेस्तुसो खे बोलेया, “जे ये मांणू कैसरो री दुहाई नि देंदा, तो छूटी सको था।”
Agripa akamwambia Festo, “Mtu huyu angeachwa huru kama hangekuwa amekata rufaa kwa Kaisari.”

< प्रेरितों के काम 26 >