< प्रेरितों के काम 9 >
1 शाऊल जो अब तक प्रभु को चेलां ख धमकान अऊर मार डालन की धुन म होतो, महायाजक को जवर गयो
Wakati huo Saulo alikuwa akizidisha vitisho vikali vya kuwaua wafuasi wa Bwana. Alikwenda kwa Kuhani Mkuu,
2 अऊर ओको सी दमिश्क को आराधनालयों को नाम पर या बात की चिट्ठियां मांगी कि का पुरुष का बाई, जिन्ख ऊ यो पंथ पर पाये उन्ख बान्ध क यरूशलेम ले आये।
akaomba apatiwe barua za utambulisho kwa masunagogi ya Kiyahudi kule Damasko, ili akikuta huko wanaume au wanawake wanaofuata Njia ya Bwana, awakamate na kuwaleta Yerusalemu.
3 पर चलतो चलतो जब ऊ दमिश्क को जवर पहुंच्यो, त अचानक आसमान सी ओको चारयी तरफ ज्योति चमकी,
Lakini alipokuwa njiani karibu kufika Damasko, ghafla mwanga kutoka angani ulimwangazia pande zote.
4 अऊर ऊ जमीन पर गिर पड़्यो अऊर यो आवाज सुन्यो, “हे शाऊल, हे शाऊल, तय मोख कहाली सतावय हय?”
Akaanguka chini na kusikia sauti ikimwambia: “Saulo, Saulo! Kwa nini unanitesa?”
5 ओन पुच्छ्यो, “हे प्रभु, तय कौन आय?” ओन कह्यो, “मय यीशु आय, जेक तय सतावय हय
Naye Saulo akauliza, “Ni nani wewe Bwana?” Na ile sauti ikajibu, “Mimi ni Yesu ambaye wewe unamtesa.
6 पर अब उठ क नगर म जाव, अऊर जो तोख करनो हय ऊ तोरो सी कह्यो जायेंन।”
Lakini simama sasa, uingie mjini na huko utaambiwa unachopaswa kufanya.”
7 जो आदमी ओको संग होतो, हि सन्न रह्य गयो; कहालीकि आवाज त सुनत होतो पर कोयी ख देखत नहीं होतो।
Wale watu waliokuwa wanasafiri pamoja na Saulo walisimama pale, wakiwa hawana la kusema; walisikia ile sauti lakini hawakumwona mtu.
8 तब शाऊल जमीन पर सी उठ्यो, पर जब आंखी खोली त ओख कुछ नहीं दिख्यो, अऊर हि ओको हाथ पकड़ क दमिश्क म ले गयो।
Saulo aliinuka, na alipofumbua macho yake hakuweza kuona chochote; hivyo wale watu wakamwongoza kwa kumshika mkono mpaka mjini Damasko.
9 ऊ तीन दिन तक नहीं देख सक्यो, अऊर नहीं खायो अऊर नहीं पीयो।
Saulo alikaa siku tatu bila kuona, na wakati huo hakula au kunywa chochote.
10 दमिश्क म हनन्याह नाम को एक चेला होतो, ओन दर्शन देख्यो कि प्रभु न ओको सी कह्यो, “हे हनन्याह!” “हव मय, प्रभु आय।”
Basi, huko Damasko kulikuwa na mfuasi mmoja aitwaye Anania. Bwana akamwambia katika maono, “Anania!” Anania akaitika, “Niko hapa, Bwana.”
11 तब प्रभु न ओको सी कह्यो, “उठ क वा गली म जाव जो ‘सीधी’ कहलावय हय, अऊर यहूदा को घर म शाऊल नाम को एक तरसुस वासी ख पूछ; कहालीकि देख, ऊ प्रार्थना कर रह्यो हय,
Naye Bwana akamwambia, “Jitayarishe uende kwenye barabara inayoitwa Barabara ya Moja kwa Moja, na katika nyumba ya Yuda umtake mtu mmoja kutoka Tarso aitwaye Saulo. Sasa anasali;
12 अऊर ओन हनन्याह नाम को एक पुरुष ख अन्दर आवतो अऊर अपनो ऊपर हाथ रखतो देख्यो हय; ताकि फिर सी देख पाये।”
na katika maono ameona mtu aitwaye Anania akiingia ndani na kumwekea mikono ili apate kuona tena.”
13 हनन्याह न उत्तर दियो, “हे प्रभु, मय न यो आदमी को बारे म बहुत सो सी सुन्यो हय कि येन यरूशलेम म तोरो पवित्र लोगों को संग बड़ी-बड़ी बुरायी करी हंय;
Lakini Anania akajibu, “Bwana, nimesikia habari za mtu huyu kutoka kwa watu wengi; nimesikia juu ya mabaya aliyowatendea watu wako huko Yerusalemu.
14 अऊर इत भी येख महायाजक को तरफ सी अधिकार मिल्यो हय कि जो लोग तोरो नाम लेवय हंय, उन पूरो ख बान्ध लेवो।”
Na amekuja hapa akiwa na mamlaka kutoka kwa makuhani wakuu kuwatia nguvuni wote wanaoomba kwa jina lako.”
15 पर प्रभु न ओको सी कह्यो, “तय चली जा; कहालीकि उत गैरयहूदियों अऊर राजावों अऊर इस्राएलियों को आगु मोरो नाम प्रगट करन लायी मोरो चुन्यो हुयो पात्र हय।
Lakini Bwana akamwambia, “Nenda tu, kwa maana nimemchagua awe chombo changu, alitangaze jina langu kwa mataifa na wafalme wao na kwa watu wa Israeli.
16 अऊर मय ओख बताऊ कि मोरो नाम लायी ओख कसो कसो दु: ख उठावनो पड़ेंन।”
Mimi mwenyewe nitamwonyesha mengi yatakayomlazimu kuteswa kwa ajili ya jina langu.”
17 तब हनन्याह उठ क ऊ घर म गयो, अऊर ओको पर अपनो हाथ रख क कह्यो, “हे भाऊ शाऊल, प्रभु, यानेकि यीशु, जो ऊ रस्ता म, जित सी तय आयो तोख दिखायी दियो होतो, ओनच मोख भेज्यो हय कि तय फिर नजर पाये अऊर पवित्र आत्मा सी परिपूर्न होय जाये।”
Basi, Anania akaenda, akaingia katika hiyo nyumba. Kisha akaweka mikono yake juu ya Saulo, akasema, “Ndugu Saulo, Bwana ambaye ndiye Yesu mwenyewe aliyekutokea ulipokuwa njiani kuja hapa, amenituma ili upate kuona tena na kujazwa Roho Mtakatifu.”
18 अऊर तुरतच ओकी आंखी सी छिलका को जसो गिरयो अऊर ऊ देखन लग्यो, अऊर उठ क बपतिस्मा लियो।
Mara vitu kama magamba vikaanguka kutoka macho ya Saulo, akaweza kuona tena. Akasimama, akabatizwa.
19 फिर जेवन कर क् ताकत पायो। ऊ कुछ दिन उन चेलां को संग रह्यो जो दमिश्क म होतो।
Na baada ya kula chakula, nguvu zake zikamrudia. Saulo alikaa siku chache pamoja na wafuasi huko Damasko.
20 अऊर ऊ तुरतच आराधनालयों म यीशु को प्रचार करन लग्यो कि ऊ परमेश्वर को बेटा हय।
Mara alianza kuhubiri katika masunagogi kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu.
21 सब सुनन वालो चकित होय क कहन लग्यो, “का यो उच आदमी नोहोय जो यरूशलेम म उन्ख जो यो नाम ख लेत होतो, नाश करत होतो; अऊर इत भी येकोलायी आयो होतो कि उन्ख बान्ध क महायाजक को जवर लिजाये?”
Watu wote waliomsikia walishangaa, wakasema, “Je, mtu huyu si yuleyule aliyewaua wale waliokuwa wanaomba kwa jina hili kule Yerusalemu? Tena alikuja hapa akiwa na madhumuni ya kuwatia nguvuni watu hao na kuwapeleka kwa makuhani!”
22 पर शाऊल अऊर भी सामर्थी होत गयो, अऊर या बात को सबूत दे क कि मसीह योच आय, दमिश्क को रहन वालो यहूदियों को मुंह बन्द करतो रह्यो।
Saulo alizidi kupata nguvu, na kwa jinsi alivyothibitisha wazi kwamba Yesu ndiye Kristo, Wayahudi wa huko Damasko walivurugika kabisa.
23 जब बहुत दिन भय गयो, त यहूदियों न मिल क ओख मार डालन की साजीश रचा।
Baada ya siku nyingi kupita, Wayahudi walikusanyika na kufanya mpango wa kumwua Saulo.
24 पर उन्को साजीश शाऊल ख मालूम भय गयो। हि त ओख मार डालन लायी रात दिन द्वारों पर मारन की ताक म लग्यो रहत होतो।
Lakini Saulo alipata habari ya mpango huo. Usiku na mchana walilinda milango ya kuingia mjini ili wapate kumwua.
25 पर रात को ओको चेलां न ओख टोकनी म बैठायो, अऊर दिवार पर सी उतार दियो।
Lakini wakati wa usiku wanafunzi wake walimchukua, wakamteremsha chini ndani ya kapu kubwa kwa kupitia nafasi iliyokuwako ukutani.
26 यरूशलेम म पहुंच क ओन चेलां को संग मिल जान को कोशिश करयो; पर सब ओको सी डरत होतो, कहालीकि उन्ख विश्वास नहीं होत होतो, कि ऊ भी चेला आय।
Saulo alipofika Yerusalemu alijaribu kujiunga na wale wanafunzi. Lakini wote walimwogopa, na hawakuweza kuamini kwamba yeye amekuwa mfuasi.
27 पर बरनबास न ओख अपनो संग प्रेरितों को जवर लिजाय क उन्ख बतायो कि येन कसो तरह सी रस्ता म प्रभु ख देख्यो, अऊर ओन येको सी बाते करी; तब दमिश्क म येन कसो हिम्मत सी यीशु को नाम सी प्रचार करयो।
Hapo, Barnaba alikuja akamchukua Saulo, akampeleka kwa mitume na kuwaeleza jinsi Saulo alivyomwona Bwana njiani na jinsi Bwana alivyoongea naye. Aliwaambia pia jinsi Saulo alivyokuwa amehubiri bila uoga kule Damasko.
28 ऊ उन्को संग यरूशलेम म आतो-जातो रह्यो
Basi, Saulo alikaa pamoja nao, akatembelea Yerusalemu yote akihubiri neno la Bwana bila hofu.
29 अऊर बेधड़क होय क प्रभु को नाम सी प्रचार करत होतो; अऊर यूनानी भाषा बोलन वालो यहूदियों को संग बातचीत अऊर वाद-विवाद करत होतो; पर हि ओख मार डालन की कोशिश करन लग्यो।
Pia aliongea na kubishana na Wayahudi wasemao Kigiriki, lakini wao walijaribu kumwua.
30 यो जान क भाऊ ओख कैसरिया ले आयो, अऊर तरसुस ख भेज दियो।
Wale ndugu walipogundua jambo hilo walimchukua Saulo, wakampeleka Kaisarea, wakamwacha aende zake Tarso.
31 यो तरह पूरो यहूदिया, अऊर गलील, अऊर सामरियां म मण्डली ख सन्तुष्ट भयो, अऊर ओकी उन्नति होत गयी; अऊर ऊ प्रभु को डर अऊर पवित्र आत्मा की शान्ति म चलती अऊर बढ़ती गयी।
Wakati huo kanisa likawa na amani popote katika Yudea, Galilaya, na Samaria. Lilijengwa na kukua katika kumcha Bwana, na kuongezeka likitiwa moyo na Roho Mtakatifu.
32 तब असो भयो कि पतरस हर जागा फिरतो हुयो, उन पवित्र लोगों को जवर भी पहुंच्यो जो लुद्दा म रहत होतो।
Petro alipokuwa anasafirisafiri kila mahali alifika pia kwa watu wa Mungu waliokuwa wanaishi Luda.
33 उत ओख एनियास नाम को एक लकवा को रोगी मिल्यो, जो आठ साल सी खटिया पर पड़्यो होतो।
Huko alimkuta mtu mmoja aitwaye Enea ambaye kwa muda wa miaka minane alikuwa amelala kitandani kwa sababu alikuwa amepooza.
34 पतरस न ओको सी कह्यो, “हे एनियास! यीशु मसीह तोख चंगो करय हय। उठ, अपनो बिस्तर बिछाव।” तब ऊ तुरतच उठ खड़ो भयो।
Basi, Petro akamwambia, “Enea, Yesu Kristo anakuponya. Amka utandike kitanda chako.” Enea akaamka mara.
35 तब लुद्दा अऊर शारोन को सब रहन वालो ओख देख क प्रभु को तरफ फिरे।
Wakazi wote wa Luda na Saroni walimwona Enea, na wote wakamgeukia Bwana.
36 याफा म तबीता यानेकि दोरकास नाम को एक विश्वासिनी रहत होती। वा बहुत सो अच्छो अच्छो काम अऊर दान करत होती।
Kulikuwa na mfuasi mmoja mwanamke mjini Yopa aitwaye Tabitha (kwa Kigiriki ni Dorka, maana yake, Paa). Huyo mwanamke alikuwa akitenda mema na kuwasaidia maskini daima.
37 उन दिन म वा बीमार होय क मर गयी; अऊर उन्न ओख नहलाय क ऊपर को कमरा म रख दियो।
Wakati huo ikawa kwamba aliugua, akafa. Watu wakauosha mwili wake, wakauzika katika chumba ghorofani.
38 येकोलायी कि लुद्दा याफा को जवर होतो, चेलां न यो सुन क कि पतरस उत हय, दोय आदमी भेज क ओको सी बिनती करी, “हमरो जवर आवनो म देर मत कर।”
Yopa si mbali sana na Luda; kwa hiyo wafuasi waliposikia kwamba Petro alikuwa Luda, wakawatuma watu wawili kwake na ujumbe: “Njoo kwetu haraka iwezekanavyo.”
39 तब पतरस उठ क उन्को संग भय गयो, अऊर जब ऊ पहुंच्यो त हि ओख वा ऊपर को कमरा म लिजायो। पूरी विधवा रोवती हुयी ओको जवर आय क खड़ी भयी, अऊर जो कुरता अऊर कपड़ा दोरकास न उन्को संग रहतो हुयो बनायो होतो, दिखान लगी।
Basi, Petro akaenda pamoja nao. Alipofika alipelekwa ghorofani katika kile chumba. Huko wajane wengi walimzunguka Petro wakilia na kumwonyesha makoti na nguo ambazo Dorka alikuwa akitengeneza wakati alipokuwa hai.
40 तब पतरस न सब क् बाहेर कर दियो, अऊर घुटना टेक क प्रार्थना करी अऊर लाश को तरफ देख क कह्यो, “हे तबीता, उठ।” तब ओन अपनी आंखी खोल दी; अऊर पतरस ख देख क उठ बैठी।
Petro aliwatoa nje wote, akapiga magoti, akasali. Kisha akamgeukia yule maiti, akasema, “Tabitha, amka” Naye akafumbua macho yake na alipomwona Petro, akaketi.
41 ओन हाथ दे क ओख उठायो, अऊर पवित्र लोगों अऊर विधवावों ख बुलाय क ओख जीन्दो दिखाय दियो।
Petro akamsaidia kusimama, halafu akawaita wale watu wa Mungu na wale wajane, akamkabidhi kwao akiwa mzima.
42 या बात पूरो याफा म फैल गयी; अऊर बहुत सो न प्रभु पर विश्वास करयो।
Habari ya tukio hili ilienea kila mahali huko Yopa, na watu wengi wakamwamini Bwana.
43 अऊर पतरस याफा म शिमोन नाम को कोयी चमड़ा को धन्दा करन वालो को इत बहुत दिन तक रह्यो।
Petro alikaa siku kadhaa huko Yopa, akiishi kwa mtu mmoja mtengenezaji wa ngozi aitwaye Simoni.