< प्रेरितों के काम 10 >
1 कैसरिया म कुरनेलियुस नाम को एक आदमी होतो, जो इतालियानी नाम को पलटन को सूबेदार होतो।
Kulikuwa na mtu mmoja huko Kaisarea aitwaye Kornelio, Jemadari wa kikosi kimoja kiitwacho “Kikosi cha Italia.”
2 ऊ भक्त होतो, अऊर अपनो पूरो घरानों को संग परमेश्वर सी डरत होतो, अऊर यहूदी गरीब लोगों ख बहुत दान देत होतो, अऊर बराबर परमेश्वर सी प्रार्थना करत होतो।
Alikuwa mtu mwema; naye pamoja na jamaa yake yote walimcha Mungu; alikuwa anafanya mengi kusaidia maskini wa Kiyahudi na alikuwa anasali daima.
3 ओन दोपहर लगभग तीन बजे दर्शन म साफ तरह सी देख्यो कि परमेश्वर को एक स्वर्गदूत ओको जवर अन्दर आय क कह्य हय, “हे कुरनेलियुस!”
Yapata saa tisa mchana, aliona dhahiri katika maono malaika wa Mungu akiingia ndani na kumwambia, “Kornelio!”
4 ओन ओख ध्यान सी देख्यो अऊर डर क कह्यो, “हे प्रभु, का आय?” स्वर्गदूत न ओको सी कह्यो, “तोरी प्रार्थनाये अऊर तोरो दान परमेश्वर को जवर याद लायी पहुंच्यो हंय;
Kornelio alimkodolea macho huyo malaika kwa hofu, akamwambia, “Kuna nini Mheshimiwa?” Huyo malaika akamwambia, “Mungu amezipokea sala na sadaka zako kwa maskini.
5 अऊर अब याफा म आदमी भेज क शिमोन ख, जो पतरस कहलावय हय, बुलाय लेवो।
Sasa, watume watu Yopa wakamwite mtu mmoja aitwaye Simoni, kwa jina lingine Petro.
6 ऊ शिमोन, चमड़ा को धन्दा करन वालो को इत मेहमान हय, जेको घर समुन्दर को किनार पर हय।”
Yeye yumo nyumbani kwa Simoni mtengenezaji wa ngozi ambaye nyumba yake iko karibu na bahari.”
7 जब ऊ स्वर्गदूत जेन ओको सी बाते करी होती चली गयो, त ओन दोय सेवक, अऊर जो ओको जवर मौजूद रहत होतो उन्म सी एक भक्त सिपाही ख बुलायो,
Huyo malaika aliyesema hayo alipokwisha kwenda zake, Kornelio aliwaita watumishi wawili wa nyumbani na mmoja wa askari zake ambaye alikuwa mcha Mungu,
8 अऊर उन्न सब बाते बताय क याफा ख भेज्यो।
akawaeleza yote yaliyotukia, akawatuma Yopa.
9 दूसरों दिन जब हि चलतो चलतो नगर को जवर पहुंच्यो, त दोपहर को समय पतरस छत पर प्रार्थना करन चढ़्यो।
Kesho yake, hao watu watatu wakiwa bado safarini, lakini karibu kufika Yopa, Petro alipanda juu ya paa la nyumba yapata saa sita mchana ili kusali.
10 ओख भूख लगी अऊर कुछ खानो चाहत होतो, पर जब हि तैयारी कर रह्यो होतो त ऊ बेहोश भय गयो;
Aliona njaa, akatamani kupata chakula. Chakula kilipokuwa kinatayarishwa, alipatwa na usingizi mzito akaona maono.
11 अऊर ओन देख्यो, कि आसमान खुल गयो; अऊर एक पात्र बड़ी चादर को जसो चारों कोना सी लटकतो हुयो, धरती को तरफ उतर रह्यो हय।
Aliona mbingu zimefunguliwa na kitu kama shuka kubwa inateremshwa chini ikiwa imeshikwa pembe zake nne.
12 जेको म धरती को सब तरह को चार पाय वालो जीव अऊर रेंगन वालो जन्तु अऊर आसमान को पक्षी होतो।
Ndani ya shuka hiyo kulikuwa na kila aina ya wanyama: wanyama wenye miguu minne, wanyama watambaao na ndege wa angani.
13 ओख एक असो आवाज सुनायी दियो, “हे पतरस उठ, मार अऊर खा।”
Akasikia sauti ikimwambia: “Petro, amka uchinje, ule!”
14 पर पतरस न कह्यो, “नहीं प्रभु, कभीच नहीं; कहालीकि मय न कभी कोयी अपवित्र या अशुद्ध चिज नहीं खायी हय।”
Petro akajibu, “La, Bwana; mimi sijaonja kamwe chochote ambacho ni najisi au kichafu.”
15 तब दूसरी बार ओख आवाज सुनायी दियो, “जो कुछ परमेश्वर न शुद्ध ठहरायो हय, ओख तय अशुद्ध मत कह्य।”
Ile sauti ikasikika tena ikimwambia: “Usiviite najisi vitu ambavyo Mungu amevitakasa!”
16 तीन बार असोच भयो; तब तुरतच ऊ पात्र आसमान पर उठाय लियो गयो।
Jambo hili lilifanyika mara tatu, kisha ile shuka ikarudishwa juu mbinguni.
17 जब पतरस अपनो मन म संका म होतो, कि यो दर्शन जो मय न देख्यो ऊ का होय सकय हय, त देखो, हि आदमी जिन्ख कुरनेलियुस न भेज्यो होतो, शिमोन को घर को पता लगाय क द्वार पर आय खड़ो भयो,
Petro alipokuwa bado anashangaa juu ya maana ya hilo maono alilokuwa ameliona, wale watu waliotumwa na Kornelio, baada ya kuigundua nyumba ya Simoni, walifika mlangoni,
18 अऊर बुलाय क पूछन लग्यो, “का शिमोन जो पतरस कहलावय हय, इतच मेहमान हय?”
Wakaita kwa sauti: “Je, kuna mgeni humu aitwaye Simoni Petro?”
19 पतरस त ऊ दर्शन पर सोचत रह्यो होतो, कि आत्मा न ओको सी कह्यो, “देख, तीन आदमी तोरी खोज म हंय।
Petro alikuwa bado anajaribu kuelewa lile maono, na hapo Roho akamwambia, “Sikiliza! kuna watu watatu hapa, wanakutafuta.
20 येकोलायी उठ क खल्लो जा, अऊर बिन शक सी उन्को संग होय जा; कहालीकि मय नच उन्ख भेज्यो हय।”
Shuka upesi na wala usisite kwenda pamoja nao kwa maana ni mimi niliyewatuma.”
21 तब पतरस न उतर क उन आदमियों सी कह्यो, “देखो, जेकी खोज तुम कर रह्यो हय, ऊ मयच आय। तुम्हरो आवन को का वजह हय?”
Basi, Petro akateremka chini, akawaambia hao watu, “Mimi ndiye mnayemtafuta. Kwa nini mmekuja?”
22 उन्न कह्यो, “कुरनेलियुस सूबेदार जो सच्चो अऊर परमेश्वर सी डरन वालो अऊर पूरी यहूदी जाति म सुनाम आदमी हय, ओन एक पवित्र स्वर्गदूत सी यो निर्देश पायो हय कि तोख अपनो घर बुलाय क तोरो सी वचन सुने।”
Wao wakamjibu, “Jemadari Kornelio ambaye ni mtu mwema, mcha Mungu na mwenye kuheshimika mbele ya Wayahudi wote ametutuma. Aliambiwa na malaika mtakatifu akualike nyumbani kwake ili asikilize chochote ulicho nacho cha kusema.”
23 तब ओन उन्ख अन्दर बुलाय क उन्की मेहमानी करी। दूसरों दिन ऊ उन्को संग गयो, अऊर याफा नगर को भाऊ म सी कुछ ओको संग भय गयो।
Petro akawaalika ndani, akawapa mahali pa kulala usiku ule. Kesho yake, Petro alianza safari pamoja nao, na baadhi ya ndugu wa huko Yopa walifuatana naye.
24 दूसरों दिन हि कैसरिया पहुंच्यो, अऊर कुरनेलियुस अपनो कुटुम्बियों अऊर प्रिय संगियों ख जमा कर क् उन्की रस्ता देख रह्यो होतो।
Siku ya pili yake, walifika Kaisarea na huko Kornelio alikuwa anawangojea pamoja na jamaa na marafiki aliokuwa amewaalika.
25 जब पतरस अन्दर आय रह्यो होतो, त कुरनेलियुस न ओको सी भेंट करी, अऊर ओको घुटना को बल पर गिर क ओख नमस्कार करयो;
Petro alipokuwa anaingia, Kornelio alitoka nje kumlaki, akapiga magoti mbele yake na kuinama chini kabisa.
26 पर पतरस न ओख उठाय क कह्यो, “खड़ो हो, मय भी त आदमी आय।”
Lakini Petro alimwinua, akamwambia, “Simama, kwa maana mimi ni binadamu tu.”
27 अऊर ओको संग बातचीत करतो हुयो अन्दर गयो, अऊर बहुत सो लोगों ख जमा देख क
Petro aliendelea kuongea na Kornelio wakiwa wanaingia nyumbani ambamo aliwakuta watu wengi wamekusanyika.
28 ओन कह्यो, “तुम जानय हय कि गैरयहूदी की संगति करनो यां ओको इत जानो यहूदी लायी अधर्म हय, पर परमेश्वर न मोख बतायो हय कि कोयी आदमी ख अपवित्र या अशुद्ध नहीं कहूं।
Petro akawaambia, “Ninyi wenyewe mnajua kwamba Myahudi yeyote amekatazwa na Sheria yake ya dini kushirikiana na watu wa mataifa mengine. Lakini Mungu amenijulisha nisimfikirie mtu yeyote kuwa najisi au mchafu.
29 येकोलायी मय जब बुलायो गयो त बिना कुछ कह्यो चली आयो। अब मय पूछू हय कि मोख कौन्सो काम लायी बुलायो गयो?”
Kwa sababu hiyo, mliponiita nimekuja bila kusita. Basi, nawaulizeni: kwa nini mmeniita?”
30 कुरनेलियुस न कह्यो, “योच घड़ी, पूरो चार दिन भयो, मय अपनो घर म दोपहर तीन बजे को लगभग प्रार्थना कर रह्यो होतो; त देखो, एक पुरुष चमकदार कपड़ा पहिन्यो हुयो, मोरो आगु आय खड़ो भयो
Kornelio akasema, “Siku tatu zilizopita saa kama hii, saa tisa alasiri, nilikuwa nikisali chumbani mwangu. Ghafla, mtu aliyekuwa amevaa mavazi yenye kun'gaa alisimama mbele yangu,
31 अऊर कहन लग्यो, ‘हे कुरनेलियुस, तोरी प्रार्थना सुन ली गयी हय अऊर तोरो दान परमेश्वर को आगु याद करयो गयो हंय।
akasema: Kornelio! Sala yako na sadaka zako kwa maskini vimekubaliwa na Mungu.
32 येकोलायी कोयी ख याफा नगर भेज क शिमोन ख जो पतरस कहलावय हय, बुलाव। ऊ समुन्दर को किनार शिमोन, चमड़ा को धन्दा करन वालो को घर म मेहमान हय।’
Mtume mtu Yopa akamwite mtu mmoja aitwaye Simoni, kwa jina lingine Petroi; yuko nyumbani kwa Simoni mtengenezaji wa ngozi karibu na bahari.
33 तब मय न तुरतच तोरो जवर लोग भेज्यो, अऊर तय न अच्छो करयो जो आय गयो। अब हम सब इत परमेश्वर को आगु हंय, ताकि जो कुछ परमेश्वर न तोरो सी कह्यो हय ओख सुनबो।”
Kwa hiyo nilikutumia ujumbe bila kuchelewa, nawe umefanya vyema kuja. Sasa, sisi tuko mbele ya Mungu, kusikiliza chochote ambacho bwana amekuamuru kusema.”
34 तब पतरस न कह्यो, “अब मोख निश्चय भयो कि परमेश्वर कोयी को पक्षपात नहीं करय,
Hapo Petro akaanza kusema: “Sasa nimetambua kwamba hakika Mungu hana ubaguzi.
35 बल्की हर जाति म जो ओको सी डरय अऊर सच्चायी को काम करय हय, ऊ ओख भावय हय।
Mtu wa taifa lolote anayemcha Mungu na kutenda haki anapokelewa naye.
36 जो वचन ओन इस्राएलियों को जवर भेज्यो, जब ओन यीशु मसीह को द्वारा जो सब को प्रभु हय शान्ति को सुसमाचार सुनायो,
Huu ndio ule ujumbe Mungu alioupeleka kwa watu wa Israeli, akitangaza Habari Njema iletayo amani kwa njia ya Yesu Kristo ambaye ni Bwana wa wote.
37 ऊ वचन तुम जानय हय, जो यूहन्ना को बपतिस्मा को प्रचार को बाद गलील सी सुरूवात होय क पूरो यहूदिया प्रदेश म फैल गयो:
Ninyi mnajua jambo lililotukia katika nchi yote ya Wayahudi kuanzia Galilaya baada ya ule ubatizo aliohubiri Yohane.
38 परमेश्वर न कौन्सो रीति सी यीशु नासरी ख पवित्र आत्मा अऊर सामर्थ सी अभिषेक करयो; ऊ भलायी करतो अऊर सब ख जो शैतान को सतायो हुयो होतो, अच्छो करतो फिरयो, कहालीकि परमेश्वर ओको संग होतो।
Mnajua Yesu wa Nazareti na jinsi Mungu alivyomteua kwa kummiminia Roho Mtakatifu na nguvu. Mungu alikuwa pamoja naye; yeye alikwenda huko na huko akitenda mema na kuwaponya wote waliokuwa wamevamiwa na Ibilisi.
39 हम उन सब कामों को गवाह हंय; जो ओन यहूदियों को देश अऊर यरूशलेम म भी करयो, अऊर उन्न ओख क्रूस पर लटकाय क मार डाल्यो।
Sisi ni mashahidi wa mambo yote aliyotenda katika nchi ya Wayahudi na katika Yerusalemu. Walimuua kwa kumtundika msalabani;
40 ओख परमेश्वर न तीसरो दिन जीन्दो करयो, अऊर प्रगट भी कर दियो हय;
lakini Mungu alimfufua siku ya tatu, akamfanya aonekane
41 सब लोगों पर नहीं बल्की उन गवाहों पर जिन्ख परमेश्वर न पहिले सी चुन लियो होतो, यानेकि हम पर जिन्न ओको मरयो हुयो म सी जीन्दो होन को बाद ओको संग खायो-पीयो;
si kwa watu wote ila kwa wale Mungu aliokwisha wachagua wawe mashahidi wake, yaani sisi tuliokula na kunywa pamoja naye baada ya kufufuka kwake kutoka wafu.
42 अऊर ओन हम्ख आज्ञा दियो कि लोगों म प्रचार करो अऊर गवाही दे, कि यो उच आय जेक परमेश्वर न जीन्दो अऊर मरयो हुयो को न्यायकर्ता ठहरायो हय।
Alituamuru kuihubiri Habari Njema kwa watu wote na kushuhudia kwamba yeye ndiye aliyeteuliwa na Mungu awe Mwamuzi wa wazima na wafu.
43 ओकी सब भविष्यवक्ता गवाही देवय हंय कि जो कोयी ओको पर विश्वास करेंन, ओख ओको नाम को द्वारा पापों की माफी मिलेंन।”
Manabii wote waliongea juu yake kwamba kila mtu atakayemwamini atasamehewa dhambi zake zote kwa jina lake.”
44 पतरस या बाते कहतच रह्यो होतो कि पवित्र आत्मा वचन को सब सुनन वालो पर उतर आयो।
Wakati Petro alipokuwa bado anasema maneno hayo, Roho Mtakatifu aliwashukia wote waliokuwa wanasikiliza ujumbe huo.
45 अऊर जितनो खतना करयो हुयो विश्वासी पतरस को संग आयो होतो, हि सब अचम्भित हुयो कि गैरयहूदियों पर भी पवित्र आत्मा को दान कुड़ायो गयो हय।
Wale Wayahudi waumini waliokuja pamoja na Petro kutoka Yopa walishangaa kuona kuwa Mungu aliwamiminia zawadi ya Roho Mtakatifu watu wa mataifa mengine pia;
46 कहालीकि उन्न उन्ख अलग-अलग तरह की भाषा बोलत अऊर परमेश्वर की बड़ायी करतो सुन्यो। येको पर पतरस न कह्यो,
maana waliwasikia wakiongea kwa lugha mbalimbali wakimtukuza Mungu. Hapo Petro akasema,
47 “का कोयी उन्ख रोक सकय हय कि हि बपतिस्मा नहीं पाये, जिन्न हमरो जसो पवित्र आत्मा पायो हय?”
“Watu hawa wamempokea Roho Mtakatifu kama sisi wenyewe tulivyompokea. Je, kuna yeyote atakayeweza kuwazuia wasibatizwe kwa maji?”
48 अऊर ओन आज्ञा दियो कि उन्ख यीशु मसीह को नाम म बपतिस्मा दियो जाये। तब उन्न ओको सी बिनती करी कि ऊ कुछ दिन अऊर उन्को संग रहे।
Basi, akaamuru wabatizwe kwa jina la Yesu Kristo. Kisha wakamwomba akae nao kwa siku chache.