< Augstā Dziesma 1 >
1 Salamana augstā dziesma.
Wimbo ulio bora wa Solomoni.
2 Lai viņš mani skūpsta ar savas mutes skūpstīšanu; jo tava mīlestība ir jo mīlīgāka nekā vīns.
Unibusu kwa busu la kinywa chako, kwa maana upendo wako unafurahisha kuliko divai.
3 Tavai eļļai ir salda smarža; tavs vārds ir izlieta eļļa, tāpēc jaunavas tevi mīl.
Manukato yako yananukia vizuri, jina lako ni kama manukato yaliyomiminwa. Ndiyo sababu wanawali wanakupenda!
4 Velc mani, tad mēs tev tecēsim pakaļ; ķēniņš mani ved savos kambaros; mēs līksmosimies un priecāsimies par tevi; mēs pieminēsim tavu mīlestību vairāk nekā vīnu; patiesīgi tevi mīl.
Nichukue twende nawe, na tufanye haraka! Mfalme na anilete ndani ya vyumba vyake. Marafiki Tunakushangilia na kukufurahia, tutasifu upendo wako zaidi kuliko divai. Mpendwa Tazama jinsi ilivyo bora wakupende!
5 Es esmu melna, bet mīlīga, jūs Jeruzālemes meitas, tā kā Ķedara teltis, kā Salamana gardīnes(aizkari).
Mimi ni mweusi, lakini napendeza, enyi binti za Yerusalemu, mweusi kama mahema ya Kedari, kama mapazia ya hema la Solomoni.
6 Neuzlūkojiet mani, ka esmu pamelna, jo saulē esmu nodegusi; manas mātes bērni pret mani apskaitušies, tie mani likuši par vīna dārzu sargātāju; savu pašu vīna dārzu neesmu apsargājusi.
Usinikazie macho kwa sababu mimi ni mweusi, kwa sababu nimefanywa mweusi na jua. Wana wa mama yangu walinikasirikia na kunifanya niwe mtunza mashamba ya mizabibu. Shamba langu mwenyewe la mizabibu nimeliacha.
7 Saki man, tu, ko mana dvēsele mīl, kur tu gani, kur tu gulies pusdienā? Jo kāpēc man būs aloties pie tavu biedru ganāmiem pulkiem?
Niambie, wewe ambaye ninakupenda, unalisha wapi kundi lako la kondoo na ni wapi unapowapumzisha kondoo wako adhuhuri. Kwa nini niwe kama mwanamke aliyefunikwa shela karibu na makundi ya rafiki zako?
8 Ja tu to nezini, tu visu skaistākā starp sievām, tad ej jel pa avju pēdām un gani savus kazlēnus pie ganu teltīm.
Kama hujui, ewe mwanamke mzuri kuliko wote, fuata nyayo za kondoo, na kulisha wana-mbuzi wako karibu na hema za wachungaji.
9 Es tevi līdzināju, mana draudzene, ar tiem zirgiem pie Faraona ratiem.
Mpenzi wangu, ninakufananisha na farasi jike aliyefungwa katika mojawapo ya magari ya vita ya Farao.
10 Tavi vaigi ir mīlīgi sprādzēs, tavs kakls pērļu rotā.
Mashavu yako yanapendeza yakiwa na vipuli, shingo yako ikiwa na mikufu ya vito.
11 Mēs tev taisīsim zelta sprādzes ar sudraba podziņām.
Tutakufanyia vipuli vya dhahabu, vyenye kupambwa kwa fedha.
12 Kamēr ķēniņš pie galda, mana nardes puķīte dod savu smaržu.
Wakati mfalme alipokuwa mezani pake, manukato yangu yalisambaza harufu yake nzuri.
13 Mans draugs man ir mirru pušķis, pie manām krūtīm piesprausts.
Mpenzi wangu kwangu mimi ni kifuko cha manemane kati ya matiti yangu.
14 Mans draugs man ir vīna ķekars Enģedi vīna dārzos.
Mpenzi wangu kwangu mimi ni kama kishada cha maua ya mhina kutoka mashamba ya mizabibu ya En-Gedi.
15 Redzi, tu esi skaista, mana draudzene, redzi, tu esi skaista, tavas acis ir kā baložu acis.
Tazama jinsi ulivyo mzuri, mpenzi wangu! Tazama jinsi ulivyo mzuri! Macho yako ni kama ya hua.
16 Redzi, tu esi skaists, mans draugs, un mīlīgs, un mūsu dusas vieta zaļo.
Tazama jinsi ulivyo mzuri, mpenzi wangu! Ee, tazama jinsi unavyopendeza! Na kitanda chetu ni cha majani mazuri.
17 Mūsu namu baļķi ir ciedri, mūsu sijas ir cipreses.
Nguzo za nyumba yetu ni mierezi, na mapao yetu ni miberoshi.