< Psalmi 86 >
1 Dāvida lūgšana. Kungs, atgriez Savas ausis, paklausi mani, jo es esmu bēdīgs un nabags.
Maombi ya Daudi. Ee Bwana, sikia na unijibu, kwa maana mimi ni maskini na mhitaji.
2 Pasargi manu dvēseli, jo es esmu bezvainīgs; palīdz, mans Dievs, Savam kalpam, kas uz Tevi paļaujas.
Linda maisha yangu, kwa maana nimejiweka kwako, wewe ni Mungu wangu, mwokoe mtumishi wako anayekutumaini.
3 Esi man žēlīgs, ak Kungs! jo es saucu uz Tevi cauru dienu.
Ee Bwana, nihurumie mimi, kwa maana ninakuita mchana kutwa.
4 Iepriecini Sava kalpa dvēseli, jo mana dvēsele, Kungs, nesās uz Tevi.
Mpe mtumishi wako furaha, kwa kuwa kwako wewe, Ee Bwana, ninainua nafsi yangu.
5 Jo Tu, Kungs, esi labs, un piedod labprāt no lielas žēlastības visiem, kas Tevi piesauc.
Ee Bwana, wewe ni mwema na mwenye kusamehe, umejaa upendo kwa wote wakuitao.
6 Kungs, klausies uz manu lūgšanu un ņem vērā manas piesaukšanas balsi.
Ee Bwana, sikia maombi yangu, sikiliza kilio changu unihurumie.
7 Bēdu laikā es Tevi piesaucu, jo Tu mani paklausi.
Katika siku ya shida yangu nitakuita, kwa maana wewe utanijibu.
8 Neviens starp tiem dieviem nav kā Tu, Kungs, un tā nav nekas kā Tavi darbi.
Ee Bwana, katikati ya miungu hakuna kama wewe, hakuna matendo ya kulinganishwa na yako.
9 Visas tautas, Kungs, ko Tu esi radījis, nāks un pielūgs Tavā priekšā, un godās Tavu vārdu.
Ee Bwana, mataifa yote uliyoyafanya yatakuja na kuabudu mbele zako; wataliletea utukufu jina lako.
10 Jo Tu esi liels un dari brīnumus, Tu esi Dievs, Tu vien.
Kwa maana wewe ni mkuu, na unafanya mambo ya ajabu; wewe peke yako ndiwe Mungu.
11 Māci man, Kungs, Tavu ceļu, es staigāšu iekš Tavas patiesības; valdi manu sirdi pie tā viena, Tavu vārdu bīties.
Ee Bwana, nifundishe njia yako, nami nitakwenda katika kweli yako; nipe moyo usiositasita, ili niweze kulicha jina lako.
12 Kungs, mans Dievs, es Tevi slavēšu no visas sirds, un godāšu Tavu vārdu mūžīgi.
Ee Bwana wangu, nitakusifu kwa moyo wote; nitaliadhimisha jina lako milele.
13 Jo Tava žēlastība ir liela pār mani un Tu manu dvēseli esi atpestījis no tās dziļās elles. (Sheol )
Kwa maana upendo wako ni mkuu kwangu; umeniokoa kutoka kwenye vilindi vya kaburi. (Sheol )
14 Ak Dievs, lepni ļaudis ceļas pret mani un varas darītāju bars meklē manu dvēseli un Tevi netur priekš savām acīm.
Ee Mungu, wenye majivuno wananishambulia; kundi la watu wakatili linatafuta uhai wangu: watu wasiokuheshimu wewe.
15 Bet Tu, Dievs Kungs, esi sirds žēlīgs un lēnprātīgs, pacietīgs un no lielas žēlastības un uzticības.
Lakini wewe, Ee Bwana, ni Mungu wa huruma na neema, si mwepesi wa hasira, bali ni mwingi wa upendo na uaminifu.
16 Atgriezies pie manis un esi man žēlīgs, dod Savu spēku Savam kalpam, un atpestī Savas kalpones dēlu.
Nigeukie na unihurumie; mpe mtumishi wako nguvu zako, mwokoe mwana wa mtumishi wako wa kike.
17 Dari zīmi pie manis, ka man labi klājās, ka mani nīdētāji to redz un kaunas, ka Tu, Kungs, man palīdzi un mani iepriecini.
Nipe ishara ya wema wako, ili adui zangu waione nao waaibishwe, kwa kuwa wewe, Ee Bwana, umenisaidia na kunifariji.