< Psalmi 59 >
1 Dāvida sirds dziesma, pēc: „nesamaitā“; kad Sauls nosūtīja, vaktēt to namu, ka viņu nokautu. Izglāb mani, mans Dievs, no maniem ienaidniekiem, pasargi mani no tiem, kas pret mani ceļas.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Utenzi wa Daudi. Wakati Sauli alipotuma wapelelezi nyumbani mwa Daudi ili wamuue. Ee Mungu, uniokoe na adui zangu, unilinde kutokana na hao wanaoinuka dhidi yangu.
2 Izglāb mani no ļauna darītājiem un atpestī mani no asins ļaudīm.
Uniponye na watu watendao mabaya, uniokoe kutokana na wamwagao damu.
3 Jo redzi tie glūn uz manu dvēseli, vareni sapulcējās pret mani, lai gan neesmu grēkojis nedz noziedzies, ak Kungs!
Tazama wanavyonivizia! Watu wakali wananifanyia hila, ingawa Ee Bwana, mimi sijakosea wala kutenda dhambi.
4 Bez vainas tie tek un sataisās. Uzmosties man palīgā un skaties!
Sijatenda kosa; hata hivyo wako tayari kunishambulia. Inuka unisaidie, uone hali yangu mbaya!
5 Tu, ak Kungs, Dievs Cebaot, Israēla Dievs, uzmosties, piemeklēt visus pagānus, neapžēlojies par nevienu, kas tik viltīgi dodas uz netaisnību. (Sela)
Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli! Zinduka uyaadhibu mataifa yote, usionyeshe huruma kwa wasaliti.
6 Vakarā tie atnāk, rūc kā suņi, un tekā(skraida) apkārt pa pilsētu.
Hurudi wakati wa jioni, wakibweka kama mbwa, wakiuzurura mji.
7 Redzi, tie ar savu muti plukšķ, zobeni ir viņu lūpās, jo - kas to dzird?
Tazama yale wanayotema kutoka vinywa vyao, hutema upanga kutoka midomo yao, nao husema, “Ni nani atakayetusikia?”
8 Bet Tu, Kungs, par tiem smiesies, Tu apmēdīsi visus pagānus.
Lakini wewe, Bwana, uwacheke; unayadharau mataifa hayo yote.
9 Pret viņu varu es gaidīšu uz Tevi, jo Dievs ir mans patvērums.
Ee nguvu yangu, ninakutazama wewe, wewe, Ee Mungu, ndiwe ngome yangu,
10 Dievs man bagātīgi parāda Savu žēlastību, Dievs man liek ar prieku uzlūkot savus pretiniekus.
Mungu wangu unipendaye. Mungu atanitangulia, naye atanifanya niwachekelee wale wanaonisingizia.
11 Nenokauj tos, ka mani ļaudis to neaizmirst, izklīdini tos ar Savu varu, un nogāz tos, ak Kungs, mūsu priekšturamās bruņas!
Lakini usiwaue, Ee Bwana, ngao yetu, au sivyo watu wangu watasahau. Katika uwezo wako wafanye watangetange na uwashushe chini.
12 Tīri grēks ir viņu lūpu vārdi, tāpēc lai tie top sagūstīti savā lepnībā, viņu lādēšanas un to melu pēc, ko tie runā.
Kwa ajili ya dhambi za vinywa vyao, kwa ajili ya maneno ya midomo yao, waache wanaswe katika kiburi chao. Kwa ajili ya laana na uongo wanaotamka,
13 Izdeldē tos dusmībā, izdeldē tos, ka to vairs nav, un lai atzīst, ka Dievs ir valdītājs iekš Jēkaba līdz pasaules galam. (Sela)
wateketeze katika ghadhabu, wateketeze hadi wasiwepo tena. Ndipo itakapofahamika katika miisho ya dunia kwamba Mungu anatawala juu ya Yakobo.
14 Vakarā tie atnāk, rūc kā suņi, un tekā apkārt pa pilsētu.
Hurudi jioni, wakibweka kama mbwa, wakiuzurura mji.
15 Tie skraida šurp un turp barības pēc, un kad nav paēduši, paliek pa nakti.
Wanatangatanga wakitafuta chakula, wasipotosheka hubweka kama mbwa.
16 Bet es dziedāšu no Tava stipruma un teikšu rītos Tavu žēlastību, jo Tu man esi bijis augsts patvērums un glābšana bēdu dienā.
Lakini mimi nitaziimba nguvu zako, asubuhi nitaimba juu ya upendo wako; kwa maana wewe ndiwe ngome yangu na kimbilio langu wakati wa shida.
17 No Tevis es dziedāšu, mans stiprums, jo Tu, Dievs, esi mans patvērums, mans žēlīgais Dievs!
Ee uliye Nguvu zangu, ninakuimbia sifa. Wewe, Ee Mungu, ndiwe ngome yangu, Mungu unipendaye.