< Psalmi 116 >

1 Es mīlu(to Kungu), ka Tas Kungs klausa manu balsi un manu pielūgšanu.
Ninampenda Bwana kwa maana amesikia sauti yangu; amesikia kilio changu ili anihurumie.
2 Jo Viņš griež Savu ausi pie manis, tādēļ es Viņu piesaukšu visu mūžu.
Kwa sababu amenitegea sikio lake, nitamwita siku zote za maisha yangu.
3 Nāves saites mani bija apņēmušas, un elles bēdas man bija uzgājušas, bēdas un bailes man nāca virsū. (Sheol h7585)
Kamba za mauti zilinizunguka, maumivu makuu ya kuzimu yalinipata, nikalemewa na taabu na huzuni. (Sheol h7585)
4 Bet es piesaucu Tā Kunga vārdu: ak Kungs, izglāb manu dvēseli!
Ndipo nikaliitia jina la Bwana: “Ee Bwana, niokoe!”
5 Tas Kungs ir žēlīgs un taisns, un mūsu Dievs ir sirds žēlīgs.
Bwana ni mwenye neema na haki, Mungu wetu ni mwingi wa huruma.
6 Tas Kungs pasargā vientiesīgos; kad es biju bēdās, tad Viņš man palīdzēja.
Bwana huwalinda wanyenyekevu, nilipokuwa katika shida kubwa, aliniokoa.
7 Esi atkal mierā, mana dvēsele, jo Tas Kungs tev dara labu.
Ee nafsi yangu, tulia tena, kwa kuwa Bwana amekuwa mwema kwako.
8 Jo tu manu dvēseli esi izglābis no nāves, manas acis no asarām, manu kāju no slīdēšanas.
Kwa kuwa wewe, Ee Bwana, umeniokoa nafsi yangu na mauti, macho yangu kutokana na machozi, miguu yangu kutokana na kujikwaa,
9 Es staigāšu Tā Kunga priekšā dzīvo zemē.
ili niweze kutembea mbele za Bwana, katika nchi ya walio hai.
10 Es ticu, tāpēc es runāju. Es biju ļoti apbēdināts;
Niliamini, kwa hiyo nilisema, “Mimi nimeteseka sana.”
11 Es sacīju savās bailēs: visi cilvēki ir melkuļi.
Katika taabu yangu nilisema, “Wanadamu wote ni waongo.”
12 Kā es Tam Kungam maksāšu visas labdarīšanas, ko Viņš pie manis darījis?
Nimrudishie Bwana nini kwa wema wake wote alionitendea?
13 Es pacelšu to pestīšanas biķeri un piesaukšu Tā Kunga vārdu.
Nitakiinua kikombe cha wokovu na kulitangaza jina la Bwana.
14 Es maksāšu Tam Kungam savus solījumus visu Viņa ļaužu priekšā.
Nitazitimiza nadhiri zangu kwa Bwana mbele za watu wake wote.
15 Viņa svēto nāve ir dārga Tā Kunga acīs.
Kifo cha watakatifu kina thamani machoni pa Bwana.
16 Ak Kungs, es esmu tiešām Tavs kalps, es esmu Tavs kalps, Tavas kalpones dēls, Tu manas saites esi atraisījis.
Ee Bwana, hakika mimi ni mtumishi wako, mimi ni mtumishi wako, mwana wa mjakazi wako; umeniweka huru toka katika minyororo yangu.
17 Tev es upurēšu pateicības upurus un piesaukšu Tā Kunga vārdu.
Nitakutolea dhabihu ya kukushukuru na kuliita jina la Bwana.
18 Es maksāšu Tam Kungam savus solījumus visu Viņa ļaužu priekšā,
Nitazitimiza nadhiri zangu kwa Bwana mbele za watu wake wote,
19 Tā Kunga nama pagalmos, tavā vidū, Jeruzāleme. Alleluja!
katika nyua za nyumba ya Bwana, katikati yako, ee Yerusalemu. Msifuni Bwana.

< Psalmi 116 >