< Salamana Pamācības 8 >

1 Vai gudrība nesauc, un atzīšana nepaceļ savu balsi?
Je hekima haiti? Je ufahamu hapazi sauti yake?
2 Kalnu virsgalā tā stāv, ceļmalā uz ceļu jūtīm;
Juu ya kilima kando ya barabara, kwenye njia panda, hekima anasimama.
3 Pie vārtiem pilsētas priekšā, kur pa vārtiem ieiet, viņa skaņi sauc:
Kando ya njia ya kuingilia mjini, karibu na milango ya mji, anaita kwa sauti.
4 „Uz jums, vīri, es saucu, un mana balss iet pie cilvēku bērniem.
Watu, ninawaita ninyi na ninapaza sauti yangu kwa wana wa wanadamu.
5 Ņemiet vērā, nejēgas, gudrību, un, ģeķi, paliekat prātīgi!
Ninyi wajinga, jifunzeni hekima, na ninyi mnaochukia maarifa, lazima mjipatieni moyo wa ufahamu.
6 Klausāties, jo es runāšu augstas lietas un atdarīšu savu muti ar skaidriem vārdiem.
Sikiliza na mimi nitasema mambo mazuri na nifumbuapo midomo yangu nitaongea haki.
7 Jo mana mute runās patiesību, un bezdievība manām lūpām ir negantība.
Maana kinywa changu hunena uaminifu na midomo yangu huchukia uovu.
8 Visi manas mutes vārdi stāv taisnībā, iekš tiem nav netiklības, nedz viltības.
Maneno ya kinywa changu yote ni haki; hakuna kilichogeuzwa wala kupotoshwa.
9 Tie ir visnotaļ taisni tam, kas tos saprot un skaidri tiem, kas atzīšanu atraduši.
Maneno yangu yote yamenyooka kwa yule mwenye kuelewa; maneno yangu ni haki kwa wale wanaotafuta maarifa.
10 Pieņemiet manu mācību labāki nekā sudrabu, un atzīšanu vairāk nekā tīru zeltu;
Chagua fundisho langu badala ya fedha na maarifa kuliko dhahabu safi.
11 Jo gudrība ir labāka pār pērlēm, un viss, ko tu kārotu, tai netiek līdz.
Maana mimi, hekima ni bora kuliko vito; hakuna unachokitamani kinaweza kulinganishwa na mimi.
12 Es, tā gudrība, mītu pie samaņas un atrodu vērtīgu padomu.
Mimi, hekima, naishi kwa utaratibu, na ninamiliki maarifa na busara.
13 Tā Kunga bijāšana ir: ienīdēt ļaunu, lepnību, augstprātību un ļaunu ceļu, un es ienīstu netiklu muti.
Hofu ya Mungu ni kuchukia uovu- nachukia majivuno na kiburi, njia ya uovu, na kauli iliyopotoka- hivyo ninavichukia.
14 Pie manis ir padoms un palīgs; es esmu atzīšana, man ir spēks.
Ninaushauri mzuri na hekima sahihi; mimi ni busara; nguvu zipo kwangu.
15 Caur mani valda ķēniņi, un dod taisnus likumus valdītāji;
Kwa njia yangu wafalme hutawala- pia na waungwana, na wote ambao hutawala kwa haki.
16 Caur mani valda varenie un lielkungi, visi zemes soģi.
Kwa njia yangu wafalme hutawala na waungwana na wote wanaotawala kwa haki.
17 Es mīlēju tos, kas mani mīl, un kas mani tikuši(centīgi) meklē, tie mani atrod.
Nawapenda wale wanaonipenda, na wale wanaonitafuta kwa bidii, wataniona.
18 Bagātība un gods ir pie manis, paliekama manta un taisnība.
Kwangu kunautajiri na heshima, utajiri wa kudumu na haki.
19 Mani augļi ir labāki nekā zelts un tīrs zelts, un mans ienākums nekā šķīsts sudrabs.
Tunda langu ni bora kuliko dhahabu, bora hata kuliko dhahabu safi.
20 Es vadu uz taisnības ceļa, taisnas tiesas pēdās,
Ninazalisha kilicho bora kuliko fedha safi. Natembea katika njia ya haki,
21 Ka tiem, kas mani mīl, dodu iemantot pilnību un pildu viņu mantu.
katika mapito ambayo huelekea kwenye haki, ili niwape urithi wale wanaonipenda na kuzijaza hazina zao.
22 Tas Kungs mani nolika par sava ceļa iesākumu, par savu radījumu pirmaju no mūžības.
Yehova aliniumba tokea mwanzo- mwazoni mwa matendo yake ya nyakati za kale.
23 No mūžības es esmu iecelta, no iesākuma, no pasaules gala.
Tokea enzi za kale niliwekwa katika nafasi- tokea kwanza, tokea mwanzo wa dunia.
24 Kad dziļumi vēl nebija, tad es piedzimu, kad avoti vēl nebija, no ūdeņiem grūti.
Kabla ya bahari, mimi nilizaliwa- kabla ya kuwepo chemchemi zenye maji tele.
25 Pirms kalnu pamati tapa nolikti, priekš pakalniem, tad es piedzimu.
Kabla ya milima na vilima kuwekwa, mimi nilizaliwa.
26 Viņš vēl nebija radījis zemi nedz klajumus, nedz sācis pasaules pīšļus;
Nilizaliwa kabla ya Yehova hajaiumba dunia wala makonde, hata mavumbi ya kwanza katika dunia.
27 Kad viņš debesis sataisīja, tad es tur biju; kad viņš izplatīja debess velvi pār dziļumiem,
Nilikuwepo alipoziimarisha mbingu, wakati alipochora mstari katika sura ya kilindi.
28 Kad viņš padebešus augšām nostiprināja, kad dziļumu avoti krākdami krāca,
Nilikuwepo alipoimarisha anga la juu na wakati wa kutengeneza kina cha chemchemi.
29 Kad viņš jūrai lika robežas, ka ūdeņi neplūstu pār viņas malām, kad viņš nostiprināja zemes pamatus:
Nilikuwepo alipotengeneza mipaka ya bahari, ili maji yasisambae kuvuka pale alipoyaamuru, na wakati anaamuru misingi ya dunia sehemu ya kukaa.
30 Tad es biju pie viņa tā izdarītāja un biju viņa prieks dienu dienas un līksmojos viņa priekšā vienmēr:
Nilikuwa kando yake, kama fundistadi mkuu, na mimi nilikuwa furaha yake siku kwa siku, nikifurahi mbele zake daima.
31 Es līksmojos viņa pasaules virsū un mans prieks ir pie cilvēku bērniem.
Nilikuwa nikifurahi katika dunia yake yote na furaha yangu ilikuwa kwa wana wa wanadamu.
32 Tad klausiet nu mani, mani bērni; jo svētīgs, kas manus ceļus sargā.
Na sasa, wanangu, nisikilizeni, maana wale wazishikao njia zangu watakuwa na furaha.
33 Klausiet pamācīšanai un topiet gudri, un neatmetat viņu.
Sikilizeni fundisho langu na mpate hekima; wala msilipuuze.
34 Svētīgs tas cilvēks, kas mani klausa, kas kavējās pie manām durvīm dienu no dienas, sargāt manu durvju stenderus;
Anisikilizaye atakuwa na furaha- kila siku akitazama katika malango yangu, akinisubiri pembeni mwa milango ya masikani yangu.
35 Jo kas mani atrod, tas atrod dzīvību un dabūs žēlastību no Tā Kunga.
Maana yeyote anionaye mimi, anapata uzima, naye atapata kibali kwa Yehova.
36 Bet kas pret mani grēko, tas dara varu savai dvēselei; kas mani ienīst, tie visi līdz mīļo nāvi.“
Na yeyote asiyeniona mimi, hujiumiza mwenyewe, wote wanaonichukia hupenda mauti.

< Salamana Pamācības 8 >