< Salamana Pamācības 6 >
1 Mans bērns, ja tu priekš sava tuvākā galvojis un roku devis priekš cita,
Mwanangu, kama umekuwa mdhamini wa jirani yako, ikiwa umeshika mikono kwa kuweka ahadi kwa ajili ya mwingine,
2 Tad tu esi sasaistīts ar savas mutes valodu un savaldzināts ar savas mutes vārdiem.
kama umetegwa na ulichosema, umenaswa kwa maneno ya kinywa chako,
3 Tad dari jel tā mans bērns, un izglābies, ja tu savam tuvākam rokā esi nācis; ej, meties zemē priekš viņa un spied savu tuvāko;
basi fanya hivi mwanangu, ili ujiweke huru, kwa kuwa umeanguka mikononi mwa jirani yako: Nenda ukajinyenyekeshe kwake; msihi jirani yako!
4 Nedod savām acīm miega, nedod savām acīm dusas;
Usiruhusu usingizi machoni pako, usiruhusu kope zako zisinzie.
5 Izglābies kā stirna no viņa rokas un kā putns no mednieka rokas!
Jiweke huru, kama swala mkononi mwa mwindaji, kama ndege kutoka kwenye mtego wa mwindaji.
6 Ej pie skudras, sliņķi, skaties viņas ceļus un topi gudrs!
Ewe mvivu, mwendee mchwa; zitafakari njia zake ukapate hekima!
7 Lai tai nav valdnieka, ne virsnieka, ne kunga,
Kwa maana yeye hana msimamizi, wala mwangalizi, au mtawala,
8 Tā tomēr savu maizi sagādā vasarā, savu barību sakrāj pļaujamā laikā.
lakini hujiwekea akiba wakati wa kiangazi na hukusanya chakula chake wakati wa mavuno.
9 Cik ilgi tu gulēsi, sliņķi? Kad tu celsies no sava miega?
Ewe mvivu, utalala hata lini? Utaamka lini kutoka usingizi wako?
10 Guli maķenīt, snaudi maķenīt, saliec maķenīt rokas miegā;
Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, bado kukunja mikono kidogo upate kupumzika:
11 Tad tava nabadzība tev pienāks nākdama, un tavs trūkums, kā apbruņots vīrs.
hivyo umaskini utakuja juu yako kama mnyangʼanyi, na kupungukiwa kutakujia kama mtu mwenye silaha.
12 Nelieša cilvēks ir tāds negants vīrs, kas staigā ar netiklu muti,
Mtu mbaya sana na mlaghai, ambaye huzungukazunguka na maneno ya upotovu,
13 Met ar acīm, piegrūž ar kājām, zīmē ar pirkstiem.
ambaye anakonyeza kwa jicho lake, anayetoa ishara kwa miguu yake na kuashiria kwa vidole vyake,
14 Netiklība ir viņa sirdī, viņš domā vienmēr uz ļaunu, saceļ ķildas.
ambaye hupanga ubaya kwa udanganyifu moyoni mwake: daima huchochea fitina.
15 Tādēļ viņam nelaime nāks piepeši, viņš ātri taps satriekts un dziedināšanas nebūs.
Kwa hiyo maafa yatamkumba ghafula; ataangamizwa mara, pasipo msaada.
16 Šās sešas lietas Tas Kungs ienīst, un tā septītā viņam ir negantība:
Kuna vitu sita anavyovichukia Bwana, naam, viko saba vilivyo chukizo kwake:
17 Lepnas acis, melu mēle un rokas, kas nenoziedzīgas asinis izlej,
macho ya kiburi, ulimi udanganyao, mikono imwagayo damu isiyo na hatia,
18 Sirds, kas negantus nodomus perē; kājas, kas mudīgas uz ļaunu skriet;
moyo uwazao mipango miovu, miguu iliyo myepesi kukimbilia uovu,
19 Viltīgs liecinieks, kas droši melus runā, un kas ķildu ceļ starp brāļiem. -
shahidi wa uongo ambaye humwaga uongo, na mtu ambaye huchochea fitina kati ya ndugu.
20 Mans bērns, glabā sava tēva pamācīšanu un nepamet savas mātes mācību.
Mwanangu, zishike amri za baba yako, wala usiyaache mafundisho ya mama yako.
21 Sasien to allažiņ uz savas sirds un sien to ap savu kaklu.
Yafunge katika moyo wako daima, yakaze kuizunguka shingo yako.
22 Kad tu staigā, tad tā tevi pavadīs; kad tu apgulies, tad tā tevi apsargās, un kad tu uzmodies, tad tā ar tevi runās;
Wakati utembeapo, yatakuongoza; wakati ulalapo, yatakulinda; wakati uamkapo, yatazungumza nawe.
23 Jo pamācīšana ir spīdeklis, un mācība gaišums, un kad pārmāca un rāj, tas ir dzīvības ceļš;
Kwa maana amri hizi ni taa, mafundisho haya ni mwanga na maonyo ya maadili ni njia ya uzima,
24 Ka tās tev izsargā no negodīgas sievas, no svešas sievietes mīkstās mēles.
yakikulinda na mwanamke aliyepotoka, kutokana na maneno laini ya mwanamke aliyepotoka.
25 Nekāro savā sirdī pēc viņas skaistuma, un lai viņa tevi nesagūsta ar savām acīm;
Moyo wako usitamani uzuri wake wala macho yake yasikuteke,
26 Jo caur mauku tiek līdz maizes drupekļiem, un vīra sieva tev notvers pat dārgo dzīvību.
kwa maana kahaba atakufanya uwe maskini, hata ukose kipande cha mkate, naye mwanamke mzinzi huwinda maisha yako hasa.
27 Vai arī uguni var klēpī ņemt, un drēbes nesadegtu?
Je, mtu aweza kuchotea moto kwenye paja lake bila nguo zake kuungua?
28 Vai uz kvēlošām oglēm var iet un nesadedzinātu kājas?
Je, mtu aweza kutembea juu ya makaa ya moto yanayowaka bila miguu yake kuungua?
29 Tāpat, kas ieiet pie otra sievas; nesodīts nepaliks, kas to aizskar.
Ndivyo alivyo mtu alalaye na mke wa mwanaume mwingine; hakuna yeyote amgusaye huyo mwanamke ambaye hataadhibiwa.
30 Zaglim nepiedod vis, ka zog izsalcis, vēderu pildīt.
Watu hawamdharau mwizi kama akiiba kukidhi njaa yake wakati ana njaa.
31 Bet pieķerts tas septiņkārt atlīdzinās, visu sava nama padomu tas atdos.
Pamoja na hayo, kama akikamatwa, lazima alipe mara saba, ingawa inamgharimu utajiri wote wa nyumba yake.
32 Kas ar sievu laulību pārkāpj, tam prāta nav; to tik dara, kas sev dzīvību grib nogalināt.
Lakini mwanaume aziniye na mwanamke hana akili kabisa; yeyote afanyaye hivyo hujiangamiza mwenyewe.
33 Tam būs kāviens un kauns un negods bez gala;
Mapigo na aibu ni fungu lake na aibu yake haitafutika kamwe;
34 Jo viņas vīra dusmas iekarsušās netaupīs atriebšanas laikā.
kwa maana wivu huamsha ghadhabu ya mume, naye hataonyesha huruma alipizapo kisasi.
35 Tas nebēdās ne par kādu līdzību(izpirkumu), un nebūs miera, cik dāvanu arī nedotu.
Hatakubali fidia yoyote; atakataa malipo, hata yakiwa makubwa kiasi gani.