< Salamana Pamācības 24 >

1 Neiekarsies uz nelabiem cilvēkiem un nekāro būt ar viņiem;
Usiwaonee wivu watu waovu, usitamani ushirika nao;
2 Jo viņu sirds domā uz postu, un viņu lūpas runā mokas.
kwa maana mioyo yao hupanga mambo ya jeuri, nayo midomo yao husema juu ya kuleta madhara.
3 Ar gudrību uzceļ namu un ar saprašanu to stiprina,
Kwa hekima nyumba hujengwa, nayo kwa njia ya ufahamu huimarishwa
4 Un ar samaņu pilda kambarus ar visādu dārgu un jauku bagātību.
kwa njia ya maarifa vyumba vyake hujazwa vitu vya thamani na vya kupendeza.
5 Gudrs vīrs ir spēcīgs, un vīrs, kam atzīšana, ir varens spēkā;
Mtu mwenye hekima ana uwezo mkubwa, naye mtu mwenye maarifa huongeza nguvu,
6 Jo ar gudriem padomiem tu izvedīsi savu karu, un uzvarēšana ir, kur padoma devēju papilnam.
kwa kufanya vita unahitaji uongozi na kwa ushindi washauri wengi.
7 Ģeķim gudrība ir neaizsniedzama; savu muti lai tas neatdara pilsētas vārtos.
Hekima i juu mno kwa mpumbavu, katika kusanyiko langoni hana lolote la kusema.
8 Kas tīšām ļaunu dara, tas jāsauc blēdis pār visiem blēžiem.
Yeye apangaye mabaya atajulikana kama mtu wa hila.
9 Ģeķības nodomi ir grēks, un mēdītājs cilvēkiem ir negantība.
Mipango ya upumbavu ni dhambi, watu huchukizwa na mwenye dhihaka.
10 Ja tu bēdu dienā nogursi, tad tavs spēks pagalam.
Ukikata tamaa wakati wa taabu, jinsi gani nguvu zako ni kidogo!
11 Glāb, kas uz nāvi pazudināti, un kas pie kaušanas top vesti, vai tu no tiem atrausies?
Okoa wale wanaoongozwa kwenye kifo; wazuie wote wanaojikokota kuelekea machinjoni.
12 Ja tu saki: „Redzi, mēs to nezinām!“Vai tad tas, kas sirdis pārmana, to nemana, un kas tavu dvēseli pasargā, to nezin un cilvēkiem neatmaksās pēc viņu darba?
Kama mkisema, “Lakini hatukujua lolote kuhusu hili,” je, yule apimaye mioyo halitambui hili? Je, yule awalindaye maisha yenu halijui hili? Je, hatamlipa kila mtu kulingana na aliyotenda?
13 Ēd, mans dēls, medu, jo tas ir labs, un tīrs medus ir salds tavā mutē;
Ule asali mwanangu, kwa kuwa ni nzuri; asali kutoka kwenye sega ni tamu kwa kuonja.
14 Tāpat tavai dvēselei būs gudrības atzīšana, ja tu to atrodi; jo ir pastara diena, un tava gaidīšana nebūs veltīga.
Ujue pia kwamba hekima ni tamu kwa nafsi yako, kama ukiipata, kuna matumaini kwako ya siku zijazo, nalo tumaini lako halitakatiliwa mbali.
15 Neglūn, tu bezdievīgais, uz taisnā dzīvokli, neposti viņa vietu;
Usivizie kama haramia afanyavyo ili kuyashambulia makao ya mwenye haki, wala usiyavamie makazi yake,
16 Jo taisnais krīt septiņ reiz un ceļas augšām; bet bezdievīgie nogrimst nelaimē.
Kwa maana ingawa mtu mwenye haki huanguka mara saba, huinuka tena, lakini waovu huangushwa chini na maafa.
17 Nepriecājies, kad tavs ienaidnieks krīt, un lai tava sirds nelīksmojās, kad viņš klūp,
Usitazame kwa kufurahia adui yako aangukapo; wakati ajikwaapo, usiruhusu moyo wako ushangilie.
18 Ka Tas Kungs to neredz, un tas viņa acīm neriebj, un viņš savu dusmību no tā nenovērš.
Bwana asije akaona na kuchukia akaiondoa ghadhabu yake mbali naye.
19 Neapskaities par ļauniem un neiekarsies par bezdievīgiem!
Usikasirike kwa sababu ya watu wabaya wala usiwaonee wivu waovu,
20 Jo ļaunam nenāk cerētais gals; bezdievīgo spīdeklis izdzisīs.
kwa maana mtu mbaya hana tumaini la siku zijazo, nayo taa ya waovu itazimwa.
21 Mans dēls, bīsties To Kungu un ķēniņu, un nejaucies ar dumpiniekiem.
Mwanangu, mche Bwana na mfalme, wala usijiunge na waasi,
22 Jo piepeši nāks viņiem nediena, - un abēju sodu, kas to zin!
kwa maana hao wawili watatuma maangamizi ya ghafula juu yao, naye ni nani ajuaye maafa wawezayo kuleta?
23 Arī šie ir gudro vārdi: Tiesā cilvēka vaigu uzlūkot nav labi.
Hii pia ni misemo ya wenye hekima: Kuonyesha upendeleo katika hukumu si vyema:
24 Kas uz vainīgo saka: „Tev taisnība!“to cilvēki lād un ļaudis ienīst.
Yeyote amwambiaye mwenye hatia, “Wewe huna hatia,” Kabila zitamlaani na mataifa yatamkana.
25 Bet tie (viņiem) mīļi, kas (tādu) pārmāca, un pār tiem nāks visu labākā svētība.
Bali itakuwa vyema kwa wale watakaowatia hatiani wenye hatia, nazo baraka tele zitawajilia juu yao.
26 Kas pareizi atbildējis, ir kā saldu muti devis.
Jawabu la uaminifu ni kama busu la midomoni.
27 Padari savu darbu laukā un apkopies tīrumā, un tad vēl uztaisi savu namu.
Maliza kazi zako za nje, nawe uweke mashamba yako tayari, baada ya hayo, jenga nyumba yako.
28 Nedod velti liecību pret savu tuvāko! Vai tu mānīsi ar savām lūpām?
Usishuhudie dhidi ya jirani yako bila sababu, au kutumia midomo yako kudanganya.
29 Nesaki: „Kā viņš man darījis, tā es viņam darīšu; es tam atmaksāšu pēc viņa darba!“
Usiseme, “Nitamtenda kama alivyonitenda mimi; nitamlipiza mtu yule kwa kile alichonitendea.”
30 Es gāju gar sliņķa tīrumu un gar ģeķa vīna kalnu.
Nilipita karibu na shamba la mvivu, karibu na shamba la mizabibu la mtu asiye na akili,
31 Un redzi, tur auga tik nātres vien, un dadži pārņēma visu, un viņa akmeņu mūris bija sagruvis.
miiba ilikuwa imeota kila mahali, ardhi ilikuwa imefunikwa na magugu, na ukuta wa mawe ulikuwa umebomoka.
32 Un es to ieraudzīju, to liku vērā: es to redzēju, ņēmos mācību:
Nikatafakari moyoni mwangu lile nililoliona, nami nikajifunza somo kutokana na niliyoyaona:
33 Guli maķenīt, snaud maķenīt, saliec maķenīt rokas miegā;
Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, bado kukunja mikono kidogo upate kupumzika:
34 Tad tava nabadzība tev pienāks nākdama, un tavs trūkums kā apbruņots vīrs.
hivyo umaskini utakuja juu yako kama mnyangʼanyi, na kupungukiwa kutakujia kama mtu mwenye silaha.

< Salamana Pamācības 24 >