< Salamana Pamācības 18 >

1 Kas ar citiem kopā neturas, tas savu gribu tik meklē, un ir kavēklis visās lietās.
Yule ambaye hujitenga hutafuta matakwa yake mwenyewe na hupingana na hukumu zote za kweli.
2 Ģeķim netīk gudra valoda, bet tik vien atklāt savu paša sirdi.
Mpumbavu hapati raha katika ufahamu, lakini hufunua kile kilichopo katika moyo wake.
3 Bezdievīgam staigā līdz negods un ar apsmieklu kauns.
Mtu mwovu anapokuja, dharau huja pamoja naye- sambamba na aibu na shutuma.
4 Vārdi cilvēka mutē ir dziļš ūdens, un gudrības avots ir tekoša ūdens upīte.
Maneno ya kinywa cha mtu ni maji yenye kina kirefu; chemchemi ya hekima ni mkondo unaotiririka.
5 Nav labi bezdievīga vaigu cienīt un nospiest taisno tiesā.
Si vema kuwa na upendeleo kwa mwovu, wala haifai kukana haki kwa wale watendao mema.
6 Ģeķa lūpas ieved ķildā, un viņa mute brēc pēc sitieniem.
Midomo ya mpumbavu huletea mafarakano na kinywa chake hukaribisha mapigo.
7 Ģeķa mute sev pašai par postu, un viņa lūpas paša dvēselei par slazda valgu.
Kinywa cha mpumbavu ni uharibifu wake na hujinasa mwenye kwa midomo yake.
8 Lišķa vārdi ir kā saldi kumosi un iet visai pie sirds.
Maneno ya mmbea ni kama chembe tamu na hushuka katika sehema za ndani sana kwenye mwili.
9 Kas laisks pie darba, tas palaidņa brālis.
Basi, ambaye ni mzembe katika kazi yake ni ndugu yake anayeharibu wengi.
10 Tā Kunga vārds ir stipra pils; tur taisnais glābjas un top izglābts.
Jina la Yehova ni mnara imara; atendaye haki hukimbilia na kuwa salama.
11 Bagātam manta ir viņa stiprā pils un viņam šķiet augsts mūris.
Mali ya tajiri ni mji wake imara na katika fikira zake ni kama ukuta mrefu.
12 Priekš bojāiešanas cilvēka sirds top lepna, bet pazemība ved godā.
Moyo wa mtu huwa na kiburi kabla ya anguko lake, bali unyenyekevu hutangulia kabla ya heshima.
13 Kas atbild, pirms dzirdējis, tas tam par ģeķību un kaunu.
Anayejibu kabla ya kusikiliza- ni upuuzi na aibu yake.
14 Vīra gars panes savas bēdas, bet kad gars izmisis, kas to var panest?
Roho ya mtu itajinusuru na madhara, bali roho iliyopondeka nani anaweza kuivumilia?
15 Prātīga sirds iemanto atzīšanu, un gudra auss meklē atzīšanu.
Moyo wa mwenye akili hujipatia maarifa na usikivu wa mwenye busara huitafuta.
16 Dāvanas cilvēkam līdzina ceļu un viņu ved kungu priekšā.
Zawadi ya mtu inaweza kufungua njia na kumleta mbele ya mtu muhimu.
17 Kas pirmais sūdz, tam taisnība; kad nu nāk viņa pretinieks, tad to tirda.
Wa kwanza kujitetea katika shitaka lake huonekana kuwa na haki hadi mpinzani wake aje na kumuuliza maswali.
18 Mesli nobeidz ķildas un izšķir varenos.
Kupiga kura kunamaliza mabishano na kuwatawanya wapinzani imara.
19 Apkaitināts brālis ir cietāks nekā stipra pils, un ķilda nekā pils vārtu aizšaujamais.
Ndugu aliyechukizwa ni mgumu kushawishiwa kuliko mji wenye nguvu, na kugombana ni kama makomeo ya ngome.
20 No mutes augļiem ikkatrs savu vēderu pildīs, un viņa lūpu padoms to ēdinās.
Tumbo la mtu litashiba kutoka kwenye tunda la kinywa chake; atatoshelezwa kwa mavuno ya midomo yake.
21 Nāve un dzīvība stāv mēles galā; kā kurš runā, tā tam būs.
Uzima na kifo hutawaliwa kwa ulimi, na wale wenye kuupenda ulimi watakula tunda lake.
22 Kas sievu atradis, tas atradis labumu un mantojis žēlastību no Tā Kunga.
Yeye apataye mke anapata kitu chema na kupokea fadhila kutoka kwa Yehova.
23 Nabags runā lūgdamies, bet bagāts atbild bargi.
Mtu masikini huomba rehema, lakini mtu tajiri hujibu kwa ukali.
24 Citam daudz draugu uz postu; bet ir draugi, kas labāki nekā brālis.
Anayejidai kwa marafiki wengi watamleta katika uharibifu, bali yupo rafiki ambaye huwa karibu kuliko ndugu.

< Salamana Pamācības 18 >