< Salamana Pamācības 18 >
1 Kas ar citiem kopā neturas, tas savu gribu tik meklē, un ir kavēklis visās lietās.
Mtu ajitengaye na wengine hufuata matakwa yake mwenyewe; hupiga vita kila shauri jema.
2 Ģeķim netīk gudra valoda, bet tik vien atklāt savu paša sirdi.
Mpumbavu hafurahii ufahamu, bali hufurahia kutangaza maoni yake mwenyewe.
3 Bezdievīgam staigā līdz negods un ar apsmieklu kauns.
Wakati uovu unapokuja, dharau huja pia, pamoja na aibu huja lawama.
4 Vārdi cilvēka mutē ir dziļš ūdens, un gudrības avots ir tekoša ūdens upīte.
Maneno ya kinywa cha mwanadamu ni kina cha maji, bali chemchemi ya hekima ni kijito kinachobubujika.
5 Nav labi bezdievīga vaigu cienīt un nospiest taisno tiesā.
Sio vizuri kumpendelea mtu mwovu, au kumnyima haki asiye na hatia.
6 Ģeķa lūpas ieved ķildā, un viņa mute brēc pēc sitieniem.
Midomo ya mpumbavu humletea ugomvi na kinywa chake hualika kipigo.
7 Ģeķa mute sev pašai par postu, un viņa lūpas paša dvēselei par slazda valgu.
Kinywa cha mpumbavu ni uharibifu wake na midomo yake ni mtego kwa nafsi yake.
8 Lišķa vārdi ir kā saldi kumosi un iet visai pie sirds.
Maneno ya mchongezi ni kama chakula kitamu; huingia sehemu za ndani sana za mtu.
9 Kas laisks pie darba, tas palaidņa brālis.
Mtu aliye mlegevu katika kazi yake ni ndugu na yule anayeharibu.
10 Tā Kunga vārds ir stipra pils; tur taisnais glābjas un top izglābts.
Jina la Bwana ni ngome imara, wenye haki huikimbilia na kuwa salama.
11 Bagātam manta ir viņa stiprā pils un viņam šķiet augsts mūris.
Mali ya tajiri ni mji wake wenye ngome, wanaudhania kuwa ukuta usioweza kurukwa.
12 Priekš bojāiešanas cilvēka sirds top lepna, bet pazemība ved godā.
Kabla ya anguko moyo wa mtu hujaa kiburi, bali unyenyekevu hutangulia heshima.
13 Kas atbild, pirms dzirdējis, tas tam par ģeķību un kaunu.
Yeye ajibuye kabla ya kusikiliza, huo ni upumbavu wake na aibu yake.
14 Vīra gars panes savas bēdas, bet kad gars izmisis, kas to var panest?
Roho ya mtu itastahimili katika ugonjwa bali roho iliyovunjika ni nani awezaye kuistahimili?
15 Prātīga sirds iemanto atzīšanu, un gudra auss meklē atzīšanu.
Moyo wa mwenye ufahamu hujipatia maarifa, masikio ya mwenye hekima huyatafuta maarifa.
16 Dāvanas cilvēkam līdzina ceļu un viņu ved kungu priekšā.
Zawadi humfungulia njia mtoaji, nayo humleta mbele ya wakuu.
17 Kas pirmais sūdz, tam taisnība; kad nu nāk viņa pretinieks, tad to tirda.
Yeye aliye wa kwanza kuleta mashtaka huonekana sahihi, hadi mwingine ajitokezapo na kumuuliza maswali.
18 Mesli nobeidz ķildas un izšķir varenos.
Kupiga kura hukomesha mashindano na kutenganisha wapinzani wakuu wanaopingana.
19 Apkaitināts brālis ir cietāks nekā stipra pils, un ķilda nekā pils vārtu aizšaujamais.
Ndugu aliyechukizwa ni mgumu kuridhika kuliko mji uliozungushiwa ngome, nayo mabishano ni kama malango ya ngome yenye makomeo.
20 No mutes augļiem ikkatrs savu vēderu pildīs, un viņa lūpu padoms to ēdinās.
Tumbo la mtu litajaa kutokana na tunda la kinywa chake, atashibishwa mavuno yanayotokana na midomo yake.
21 Nāve un dzīvība stāv mēles galā; kā kurš runā, tā tam būs.
Mauti na uzima viko katika uwezo wa ulimi, nao waupendao watakula matunda yake.
22 Kas sievu atradis, tas atradis labumu un mantojis žēlastību no Tā Kunga.
Apataye mke apata kitu chema naye ajipatia kibali kwa Bwana.
23 Nabags runā lūgdamies, bet bagāts atbild bargi.
Mtu maskini huomba kuhurumiwa bali tajiri hujibu kwa ukali.
24 Citam daudz draugu uz postu; bet ir draugi, kas labāki nekā brālis.
Mtu mwenye marafiki wengi wanaweza kumharibu, bali yuko rafiki aambatanaye na mtu kwa karibu kuliko ndugu.