< Salamana Pamācības 11 >

1 Viltīgs svars Tam Kungam ir negantība, bet pilnīgs svara akmens Viņam patīk.
Yehova huchukia vipimo ambavyo havipo sahihi, bali hufurahia uzani dhahiri.
2 Kur nāk lepnība, tur arī nāk kauns, bet pie pazemīgiem ir gudrība.
Kinapokuja kiburi, ndipo aibu huja, bali unyenyekevu huleta hekima.
3 Taisno sirdsskaidrība tos vada, bet neliešu netiklība tos posta.
Uadilifu wa wenye haki huwaongoza, bali udanganyifu wa njia za wajanja utawaangamiza.
4 Manta nepalīdz atriebšanas dienā, bet taisnība izpestī no nāves.
Utajiri hauna thamani siku ya ghadhabu, bali kwa kutenda haki hujilinda na mauti.
5 Skaidram taisnība līdzina ceļu, bet bezdievīgais kritīs caur savu bezdievību.
Mwenendo wa mtu mwema huinyosha njia yake, bali waovu wataanguka kwa sababu ya uovu wao.
6 Taisno taisnība tos izglābs, bet nebēdnieki savaldzināsies savā kārībā.
Mwenendo mwema wa wale wampendezao Mungu utawalinda salama, bali wadanganyifu hunaswa katika shauku zao.
7 Kad bezdievīgs cilvēks mirst, tad viņa cerība iznīkst, un netaisno gaidīšana ir pagalam.
Mtu mwovu anapokufa, tumaini lake hupotea na tumaini lililokuwa katika nguvu zake linakuwa si kitu.
8 Taisnais tiek izglābts no bēdām, un bezdievīgais nāk viņa vietā.
Yule atendaye haki hulindwa katika taabu na badala yake taabu humjia mwovu.
9 Blēdis savu tuvāko bendē ar muti, bet taisnie, to manot, paglābjas.
Kwa kinywa chake asiyeamini Mungu humwangamiza jirani yake, bali kwa maarifa wale watendao haki hulindwa salama.
10 Kad taisnam labi klājās, tad pilsēta priecājās, un gavilē, kad bezdievīgais iet postā.
Wanapofanikiwa watendao haki, mji hufurahi, waovu wanapoangamia, kunakuwa na kelele za furaha.
11 Caur taisna svētību pilsēta ceļas, bet caur bezdievīga muti tā top nopostīta.
Kwa zawadi nzuri za wale wanaompendeza Mungu, mji unakuwa mkubwa; kwa kinywa cha waovu mji huvurugwa.
12 Kas savu tuvāko nicina, tam nav saprašanas; bet gudrs vīrs cieš klusu.
Mtu mwenye dharau kwa rafiki yake hana akili, bali mtu mwenye ufahamu hunyamaza.
13 Mēlnesis apkārt lienot izmuld, kas slēpjams; bet kam uzticīgs prāts, tas to apklāj.
Anayekwenda akizunguka kwa kukashifu hufunua siri, bali mtu mwaminifu hustiri jambo.
14 Kur vadīšanas nav, tur ļaudis nīkst; bet kur padoma devēju papilnam, tur labi izdodas.
Pasipokuwa na uongozi wenye busara, taifa huanguka, bali ushindi huja kwa kushauriana washauri wengi.
15 Kas par svešu galvo, tam būs bēdu gan; bet kas galvošanu ienīst, tas paliek mierā.
Anayemdhamini mkopo wa mgeni ataumia kwa usumbufu, bali anayechukia kutoa rehani kwa namna ya ahadi yupo salama.
16 Mīlīga sieva panāk godu, tā kā varenie panāk bagātību.
Mwanamke mwenye rehema hupata heshima, bali watu wakorofi hufumbata utajiri.
17 Žēlīgs vīrs savai paša dvēselei dara labu, bet niknais savai paša miesai dara grūti.
Mtu mkarimu hufaidika mwenyewe, bali mkatili hujiumiza mwenyewe.
18 Bezdievīgais pelnās tukšu algu, bet kas taisnību sēj, tam alga pastāvīga.
Mtu mwovu husema uongo kupata mishahara yake, bali yeye apandaye haki anavuna mishahara ya kweli.
19 Kā taisnība ir uz dzīvību, tā ļaunam pakaļ dzīties ir uz nāvi.
Mtu mwaminifu atendaye haki ataishi, bali yeye atendaye uovu atakufa.
20 Kam netikla sirds, tas Tam Kungam ir negantība; bet kam skaidrs ceļš, tas Viņam patīk.
Yehova anawachukia wenye ukaidi mioyoni, bali anawapenda wale ambao njia zao hazina makosa.
21 Uz radu radiem paliek blēža vaina; bet taisno dzimums taps izglābts.
Uwe na uhakika juu ya hili- watu waovu hawatakosa adhabu, bali uzao wa wale watendao haki watawekwa salama.
22 Skaista sieva, kas goda neprot, ir zelta gredzens cūkas purnā.
Kama pete ya dhahabu kwenye pua ya nguruwe ndiyo alivyo mwanamke mzuri asiye na busara.
23 Ko taisnie vēlās, ir visnotaļ labums; bet bezdievīgo cerība ir pārgalvība.
Shauku ya wale watendao haki ni matokeo mema, bali watu waovu wanaweza kutumainia ghadhabu tu.
24 Cits izkaisa, un tam vēl krājās; un cits taupa pārlieku, bet tik uz trūcību.
Kuna yule ambaye hupanda mbegu- atakusanya zaidi; mwingine hapandi- huyo anakuwa masikini.
25 Tā dvēsele, kas svētī, tiks trekna, un kas dzirdina, tas atkal taps dzirdināts.
Mtu mkarimu atafanikiwa na yule awapaye maji wengine atapata maji yake mwenyewe.
26 Kas aiztur labību, to ļaudis lād, bet svētība būs pār pārdevēja galvu.
Watu wanamlaani mtu ambaye hukataa kuuza nafaka, bali zawadi njema hufunika kichwa chake ambaye huuza nafaka.
27 Kas dzenās pēc laba, tas ir patīkams, bet kas meklē ļaunu, tam tas arī nāks.
Yule ambaye hutafuta mema kwa bidii pia anatafuta kibali, bali yule atafutaye ubaya atapata ubaya.
28 Kas uz savu bagātību palaižās, tas iznīks, bet taisnie zaļos kā lapas,
Wale wanaotumaini utajiri wataanguka, bali kama jani, wale watendao haki watasitawi.
29 Kas savu namu pilda ar nemieru, tas mantos vēju, un ģeķis būs par kalpu tam, kam ir gudra sirds.
Yule ambaye analeta taabu kwenye kaya yake ataurithi upepo na mpumbavu atakuwa mtumishi wa wenye moyo wa hekima.
30 Taisna auglis ir dzīvības koks, un gudrais manto sirdis.
Wale watendao haki watakuwa kama mti wa uzima, lakini vurugu huondoa uzima.
31 Redzi, taisnam virs zemes top atmaksāts, cik vairāk vēl bezdievīgam un grēciniekam.
Tazama! Ikiwa wale watendao haki hupokea wanachositahili, je si zaidi kwa waovu na wenye dhambi!

< Salamana Pamācības 11 >