< Salamana Pamācības 10 >
1 Salamana sakāmie vārdi. Gudrs dēls ir tēva prieks, bet ģeķīgs mātes sirdēsti.
Mithali za Solomoni: Mwana mwenye hekima huleta furaha kwa baba yake, lakini mwana mpumbavu huleta huzuni kwa mama yake.
2 Netaisnas mantas nelīdz nenieka, bet taisnība izpestī no nāves.
Hazina zilizopatikana kwa njia mbaya hazifai, lakini uadilifu huokoa kutoka mautini.
3 Tas Kungs taisnai dvēselei neliek bada ciest; bet bezdievīga negausību viņš izšķiež.
Bwana hawaachi waadilifu kukaa njaa, lakini hupinga tamaa ya mtu mwovu.
4 Kas slinku roku strādā, top nabags; bet čakla roka dara bagātu.
Mikono mivivu hufanya mtu kuwa maskini lakini mikono yenye bidii huleta utajiri.
5 Kas vasarā sakrāj, ir prātīgs; bet kas pļaujamā laikā guļ, paliek kaunā.
Yeye akusanyaye mazao wakati wa kiangazi ni mwana mwenye hekima, lakini yeye alalaye wakati wa mavuno ni mwana mwenye kuaibisha.
6 Svētība pār taisna galvu, bet bēdas aizbāzīs bezdievīgiem muti.
Baraka huwa taji kichwani mwa mwenye haki, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
7 Taisnam piemiņa paliek svētīta, bet bezdievīgiem slava iznīks.
Kumbukumbu ya mwenye haki itakuwa baraka, lakini jina la mwovu litaoza.
8 Kam gudra sirds, tas pieņem mācību, bet kas muti palaiž, ies bojā.
Mwenye hekima moyoni hupokea maagizo, lakini mpumbavu apayukaye huangamia.
9 Kas skaidrībā staigā, tas staigā ar mieru; bet kas savus ceļus groza, to pienāks.
Mtu mwadilifu hutembea salama, lakini mtu aendaye katika njia zilizopotoka atagunduliwa.
10 Kas ar acīm met, tas pieved bēdas; un kas muti palaiž, ies bojā.
Yeye akonyezaye kwa nia mbaya husababisha huzuni, naye mpumbavu apayukaye huangamia.
11 Taisnam mute ir dzīvības avots; bet bēdas aizbāzīs bezdievīgiem muti.
Kinywa cha mwenye haki ni chemchemi ya uzima, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
12 Ienaids ceļ bāršanos; bet mīlestība apklāj visus pārkāpumus.
Chuki huchochea faraka, lakini upendo husitiri mabaya yote.
13 Uz prātīga lūpām rodas gudrība, bet pār ģeķa muguru nāk rīkste.
Hekima hupatikana katika midomo ya wenye kupambanua, lakini fimbo ni kwa ajili ya mgongo wake asiye na ufahamu.
14 Prātīgie pietur savu padomu, bet ģeķu mute ir briesmas tuvumā.
Wenye hekima huhifadhi maarifa, bali kinywa cha mpumbavu hualika maangamizi.
15 Bagātam manta ir viņa stiprā pils, bet tukšinieku briesmas ir viņu nabadzība.
Mali ya tajiri ni mji wake wenye ngome, bali ufukara ni maangamizi ya maskini.
16 Taisna krājumiņš ir uz dzīvību, bet bezdievīga ienākums uz grēku.
Ujira wa wenye haki huwaletea uzima, lakini mapato ya waovu huwaletea adhabu.
17 Pārmācīšanu pieņemt ir ceļš uz dzīvību, bet kas par mācību nebēdā, tas maldās.
Anayekubali kuadibishwa yuko katika njia ya uzima, lakini yeyote anayepuuza maonyo hupotosha wengine.
18 Viltīgas lūpas slēpj ienaidu, un kas niknu slavu ceļ, ir nelga.
Yeye afichaye chuki yake ana midomo ya uongo, na yeyote anayeeneza uchonganishi ni mpumbavu.
19 Vārdu pulkā netrūkst grēku, bet kas savas lūpas valda, ir gudrs.
Wakati maneno ni mengi, dhambi haikosekani, lakini yeye ambaye huzuia ulimi wake ni mwenye busara.
20 Taisnam mēle ir tīrs sudrabs, bezdievīgā sirds neder nekam.
Ulimi wa mwenye haki ni fedha iliyo bora, bali moyo wa mwovu una thamani ndogo.
21 Taisna lūpas daudziem ganība, bet ģeķi nomirs savā sirds ģeķībā.
Midomo ya mwenye haki hulisha wengi, lakini wapumbavu hufa kwa kukosa ufahamu.
22 Tā Kunga svētība dara bagātu, un rūpes tur nekā nepieliek.
Baraka ya Bwana hutajirisha, wala haichanganyi huzuni.
23 Ģeķim prieks, blēņas darīt, bet prātīgam vīram gudrība.
Mpumbavu hufurahia tabia mbaya, lakini mtu mwenye ufahamu hupendezwa na hekima.
24 No kā bezdievīgais bīstas, tas viņam uziet, un ko taisnie vēlās, to Viņš tiem dod.
Kile anachoogopa mwovu ndicho kitakachompata; kile anachoonea shauku mwenye haki atapewa.
25 Tā kā vētra pārskrien, tāpat bezdievīgā vairs nebūs, bet taisnais pastāv mūžīgi.
Tufani inapopita, waovu hutoweka, lakini wenye haki husimama imara milele.
26 Kā skābums zobiem un dūmi acīm, tā sliņķis tiem, kas to sūta.
Kama siki ilivyo kwa meno na moshi kwa macho, ndivyo alivyo mvivu kwa wale waliomtuma.
27 Tā Kunga bijāšana vairo dienas, bet bezdievīgo gadi top paīsināti.
Kumcha Bwana huongeza urefu wa maisha, lakini miaka ya mwovu inafupishwa.
28 Ko taisnie gaida, būs līksmība, bet bezdievīgo cerība zudīs.
Tarajio la mwenye haki ni furaha, bali matumaini ya mwovu huwa si kitu.
29 Tā Kunga ceļš sirdsskaidriem ir par stiprumu, bet ļauna darītājiem par izbailēm.
Njia ya Bwana ni kimbilio kwa wenye haki, lakini ni maangamizi ya wale watendao mabaya.
30 Taisnais nešaubīsies ne mūžam, bet bezdievīgie nepaliks zemes virsū.
Kamwe wenye haki hawataondolewa, bali waovu hawatasalia katika nchi.
31 No taisnā mutes zaļo gudrība, bet netikla mēle taps izdeldēta.
Kinywa cha mwenye haki hutoa hekima, bali ulimi wa upotovu utakatwa.
32 Taisnā lūpas zin, kas pieklājās, bet bezdievīgo mute ir netikla.
Midomo ya wenye haki inajua kile kinachofaa, bali kinywa cha mwovu hujua kile kilichopotoka tu.