< Nachuma 3 >
1 Ak vai, tai asins pilsētai, kas visa pilna melu un varas darbu; laupīšana tur nemitās.
Ole wa mji umwagao damu, uliojaa uongo, umejaa nyara, usiokosa kuwa na vitu vya kuteka nyara.
2 Klau, pātagas plīkšķ, riteņi rīb, zirgi skraida un rati rūc!
Kelele za mijeledi, vishindo vya magurudumu, farasi waendao mbio na mshtuo wa magari ya vita!
3 Jātnieki jāj, zobeni zib, šķēpi spīd! Bez skaita nokauto, pulkiem mirušo, bez gala līķu, ka krīt pār līķiem.
Wapanda farasi wanaenda mbio, panga zinameremeta, na mikuki inangʼaa! Majeruhi wengi, malundo ya maiti, idadi kubwa ya miili isiyohesabika, watu wanajikwaa juu ya mizoga:
4 Viss tas notiks caur tās daiļās maukas, tās gudrās burves, lielo maucību, kas ar savu maukošanu tautas apmānījusi un ciltis ar savu buršanu.
yote haya kwa sababu ya wingi wa tamaa za kahaba, anayeshawishi, bibi wa mambo ya uchawi, anayewatia utumwani mataifa kwa ukahaba wake na pia jamaa za watu kwa ulozi wake.
5 Redzi, Es esmu pret tevi, saka Tas Kungs Cebaot, un Es atsegšu tavas (drēbju) vīles tavā priekšā, un rādīšu pagāniem tavu plikumu un valstīm tavu kaunu.
Bwana Mwenye Nguvu Zote anasema, “Mimi ni kinyume na ninyi. Nitafunika uso wako kwa gauni lako. Nitaonyesha mataifa uchi wako na falme aibu yako.
6 Es metīšu uz tevi gānekļus un tevi sagānīšu un likšu tevi par biedēkli,
Nitakutupia uchafu, nitakufanyia dharau na kukufanya kioja.
7 Ka visi, kas tevi redz, no tevis bēgs un sacīs: Ninive ir postīta! Kam tās būs žēl? Kur man tev meklēt iepriecinātājus?
Wote wanaokuona watakukimbia na kusema, ‘Ninawi ipo katika kuangamia: ni nani atakayeomboleza kwa ajili yake?’ Nitampata wapi yeyote wa kukufariji?”
8 Vai tu esi labāka nekā NoAmona, kas sēdēja pie upēm, kam visapkārt bija ūdeņi, kam jūra bija par stiprumu un jūra par mūri?
Je, wewe ni bora kuliko No-Amoni, uliopo katika Mto Naili, uliozungukwa na maji? Mto ulikuwa kinga yake, nayo maji yalikuwa ukuta wake.
9 Moru(Etiopiešu) zeme bija viņas stiprums un Ēģipte bez gala, Puts un Libija tev bija par palīgu.
Kushi na Misri walikuwa nguvu zake zisizo na mpaka; Putu na Libia walikuwa miongoni mwa wale walioungana naye.
10 Viņa arīdzan ir aizvesta un gājusi cietumā, arī viņas bērni ir nokauti visu ielu stūros, un par viņas goda vīriem meta meslus, un visus viņas lielkungus slēdza ķēdēs.
Hata hivyo alichukuliwa mateka na kwenda uhamishoni. Watoto wake wachanga walivunjwa vunjwa vipande kwenye mwanzo wa kila barabara. Kura zilipigwa kwa watu wake wenye heshima, na watu wake wote wakuu walifungwa kwa minyororo.
11 Tāpat tev būs piedzerties un krist tumsā un meklēt patvērumu no saviem ienaidniekiem.
Wewe pia utalewa; utakwenda mafichoni na kutafuta kimbilio kutoka kwa adui.
12 Visas tavas stiprās pilis ir kā vīģes koki ar pirmiem augļiem; kad tos krata, tad tie krīt mutē ēdējam.
Ngome zako zote ni kama mitini yenye matunda yake ya kwanza yaliyoiva; wakati inapotikiswa, tini huanguka kwenye kinywa chake alaye.
13 Redzi, tavi ļaudis tavā vidū ir bābas, tavas zemes vārti atveras taviem ienaidniekiem, uguns aprij tavus aizšaujamos.
Tazama vikosi vyako: wote ni wanawake! Malango ya nchi yako yamekuwa wazi kwa adui zako; moto umeteketeza mapingo yake.
14 Smelies ūdeni, jo tu tapsi apsēsta, stiprini savas pilis, ej uz ķieģeļu cepli un min mālus, taisi stiprus ķieģeļus.
Teka maji kwa ajili ya kuzingirwa kwako, imarisha ulinzi wako, Ufanyie udongo wa mfinyanzi kazi, yakanyage matope, karabati tanuru la kuchomea matofali!
15 Uguns tevi aprīs, zobens tevi izdeldēs, viņš tevi norīs kā vaboli; vairojies kā vaboles, vairojies kā siseņi.
Huko moto utakuteketeza, huko upanga utakuangusha chini na kama vile panzi, watakumaliza. Ongezeka kama panzi, ongezeka kama nzige!
16 Tev ir vairāk tirgotāju nekā debess zvaigznes; vaboles izpleš spārnus un aizskrien.
Umeongeza idadi ya wafanyabiashara wako mpaka wamekuwa wengi kuliko nyota za angani, lakini kama nzige wanaacha nchi tupu kisha huruka na kwenda zake.
17 Tavi cienīgie ir kā siseņi, un tavi virsnieki kā vaboles, kas apmetās pie sētām dzestrā laikā, bet kad saule uzlec, tad tie aizskrien, tā ka viņu vietu nezin, kur tie ir.
Walinzi wako ni kama nzige, maafisa wako ni kama makundi ya nzige watuao kwenye kuta wakati wa siku ya baridi: lakini wakati jua linapotokea wanaruka kwenda zao, na hakuna ajuaye waendako.
18 Tavi gani, ak Asīrijas ķēniņ, guļ, tavi cienīgie dus, tavi ļaudis izklīduši pa kalniem, un neviens tos nesapulcina.
Ee mfalme wa Ashuru, wachungaji wako wanasinzia; wakuu wako wanalala chini mavumbini kupumzika. Watu wako wametawanyika juu ya milima bila kuwa na mtu yeyote wa kuwakusanya.
19 Tavai vainai nav dziedināšanas, tava kaite ir nāvīga; visi, kas par tevi dzird, sasit rokas par tevi. Jo kam tavs niknums nav uzgājis bez mitēšanās?
Hakuna kitu kinachoweza kuponya jeraha lako; jeraha lako ni la kukuua. Kila anayesikia habari zako, hupiga makofi kwa kuanguka kwako, kwa kuwa ni nani ambaye hajaguswa na ukatili wako usio na mwisho?