< Michas 7 >

1 Vai man, jo es esmu, kā kad koku augļi sakrāti, kā kad vīna ogas otru reiz nolasītas; neviena ķekara ko ēst, nevienas agrīnās vīģes, kas manai dvēselei gribās.
Ole wangu! Kwangu mimi ni kama msimu wa mavuno ulipokwisha, na pia makombo ya mavuno ya zabibu kwenye shamba la mizabibu: Hakuna tena kishamba cha matunda kinachoonekana, hakuna matini ya malimbuka ambayo ninayoyatamani.
2 Dievbijīgie iznīkuši no zemes, un taisna nav cilvēku vidū; tie visnotaļ glūn uz asinīm, cits citam tie met tīklus.
Watu waaminifu wamepotelea kutoka kwenye nchi, hakuna mtu mwadilifu katika wanadamu wote. Wote hudanganya katika kusubiri kumwaga damu; kila mtu humuwinda ndugu yake mwenyewe kwa wavu.
3 Abām rokām tie dara ļaunu cik spēdami; valdnieks prasa un soģis tiesā par maksu, un lielskungs izrunā savas sirds kārību, un tā tie to sapin.
Mikono yao ni mizuri mno kwa kufanya madhara. watawala huuliza pesa, hakimu yuko tayari kwa rushwa, na mtu mwenye nguvu anawaambia wengine kile anachokitaka kujipatia. Hivyo ndivyo waundavyo kwa pamoja.
4 Tas labākais no tiem ir kā ērkšķis, un tas taisnākais kā ērkšķu krūms. Tavu sargu diena, tava piemeklēšana nāk - tad tie būs izsamisuši.
Mtu bora kwao ni kama mitemba, mwadilifu sana ni kama mche wa miba. Imefika siku iliyosemwa nyuma na walinzi wako, siku ya hukumu. Sasa ni mda wa machafuko.
5 Neticat tuvākam un nepaļaujaties uz draugu; pasargi savas mutes durvis priekš tās, kas guļ tavā klēpī.
Msimwamini kila jirani; msimuweke kiongozi katika rafiki yeyote. Kuweni makini kuhusiana na kile msemacho hata kwa mwanamke ambaye adanganyaye kwenye mikono yenu.
6 Jo dēls nicina tēvu, meita ceļas pret savu māti, vedekla pret savu vīra māti, cilvēka ienaidnieki ir viņa paša mājas ļaudis.
Kwa kuwa mwana humfedhehesha baba yake, binti huinuka kushindana na mama yake, na mke wa mwana wa kiume hushindana na mama mkwe wake. Adui wa watu ni watu wa nyumba yake mwenyewe.
7 Bet es cerēšu uz To Kungu, es gaidīšu uz Dievu, savu Pestītāju; mans Dievs mani paklausīs.
Lakini kama kwangu mimi, nitamtazama Yahwe. Nitamsubiri Mungu wa wokovu wangu; Mungu wangu ataniskia.
8 Nepriecājies, mana ienaidniece! Kad es esmu kritis, es atkal celšos; kad es sēžu tumsībā, tad Tas Kungs ir mans gaišums.
Usifurahi juu yangu, adui yangu. Niangukapo, nitainuka. Wakati nitakapokuwa nimekaa katika giza, Yahwe atakuwa mwanga kwangu.
9 Es nesīšu Tā Kunga dusmību, jo es pret Viņu esmu grēkojis, tiekams Viņš iztiesās manu tiesas lietu un man nesīs tiesu. Viņš mani vedīs gaismā, es redzēšu ar prieku Viņa taisnību.
Kwasababu nimetenda dhambi dhidi ya Yahwe, nitachukua ghadhabu yake hata aniteteapo kosa langu, na kutekeleza hukumu kwa ajili yangu. Atanileta kwenye nuru, na nitamwona akiniokoa kwenye haki yake.
10 Un mana ienaidniece to redzēs un taps apsegta ar kaunu, - kas uz mani saka: kur ir Tas Kungs, tavs Dievs? Manas acis redzēs, ka viņu samīs kā dubļus ielā.
Kisha adui yangu atakapoliona hilo, na aibu itamfunika yule aliyeniambia, “Yahwe Mungu wako yuko wapi?” macho yangu yatamtazama; atakanyagwa chini kama tope kwenye mitaa.
11 Nāks diena, tad tavi mūri taps uzcelti, tanī dienā robeža tālu sniegsies.
Siku ya ya kujenga kuta zako zitafika; siku hiyo mipaka itasogezwa mbali sana.
12 Tanī dienā pie tevis nāks no Asura un Ēģiptes pilsētām, un no Ēģiptes līdz lielupei, un no vienas jūras līdz otrai un no viena kalna līdz otram.
Siku hiyo watu watakuja kwako, kutoka Ashuru na miji katika Misri, kutoka Misri hata mto mkubwa, kutoka bahari kwenda bahari, na kutoka mlima kwenda mlima.
13 Bet zeme taps postā savu iedzīvotāju dēļ, viņu darba augļu dēļ.
Hizo nchi zitakuwa zimejitenga kwasababu ya watu ambao wanaishi huko sasa, kwasababu ya tunda la matendo yao.
14 Tu tad gani Savus ļaudis ar Savu zizli, Savas mantības ganāmo pulku, kas savrup dzīvo Karmeļa mežā; lai tie gana pa Basanu un Gileādu tā kā vecos laikos.
Chunga watu wako kwa fimbo yako, kundi la urithi wako. Wanaishi wenyewe kwenye msitu, katikati ya msitu. Wachunge katika Bashani na Gileadi kama siku za zamani.
15 Es tiem likšu brīnumus redzēt, kā tanīs dienās, kad jūs izgājāt no Ēģiptes zemes.
Kama katika siku wakati mlipotoka nje ya nchi ya Misri, nitawaonyesha maajabu.
16 Pagāni to redzēs un taps kaunā ar visu savu varu, tie roku liks uz muti, viņu ausis taps kurlas.
Mataifa yataona na kuwa na aibu ya nguvu zao zote. Wataweka mikono yao kwenye midomo yao; masikio yao yatakuwa kiziwi.
17 Tie laizīs pīšļus kā čūska, kā zemes tārpi tie trīcēs savās pilīs, tie bīsies To Kungu, mūsu Dievu, un baiļosies no Tevis.
Watalamba vumbi kama nyoka, kama viumbe vitaambavyo juu ya nchi. Watatoka nje kwenye maficho kwa hofu; watakuja kwako kwa hofu, Yahwe Mungu wetu, na wataogopa kwa sababu yako.
18 Kur ir tāds Dievs kā Tu? Kas piedod noziegumu un pamet pārkāpumu Savas mantības atlikušiem; Viņš nepatur Savu dusmību mūžīgi, jo Viņam ir labs prāts žēlot.
Ni nani aliye Mungu kama wewe, wewe uchukuaye dhambi, wewe upitaye juu ya kosa la mabaki ya mrithi wako? Hutunzi hasira yako milele, kwa sababu unapenda kutuonyesha agano lako la aminifu.
19 Viņš atkal par mums apžēlosies, Viņš deldēs mūsu noziegumus. Tiešām, Tu visus viņu grēkus metīsi jūras dziļumos.
Tena utakuwa na huruma juu yetu; utayakanyaga maovu chini ya miguu yako. Utazitupa dhambi zetu zote kwenye vilindi vya bahari.
20 Jēkabam Tu parādīsi uzticību, Ābrahāmam žēlastību, ko mūsu tēviem esi zvērējis no vecām dienām.
Utampatia ukweli Yakobo na agano aminifu kwa Abrahamu, ulipoapa kwa babu zetu katika siku za kale.

< Michas 7 >