< Trešā Mozus 14 >

1 Un Tas Kungs runāja uz Mozu un sacīja:
Bwana akamwambia Mose,
2 Šis būs tas likums par spitālīgo viņa šķīstīšanas laikā:
“Haya ndiyo masharti yamhusuyo mtu mgonjwa wakati wa kufanyiwa ibada ya utakaso wakati aletwapo kwa kuhani:
3 To būs vest pie priestera, un priesterim būs iziet ārā aiz lēģera, un ja priesteris redz, un raugi, spitālības vaina no spitālīgā ir sadzijusi,
Kuhani atakwenda kumchunguza nje ya kambi. Kama mtu huyo atakuwa amepona ugonjwa wake wa ngozi wa kuambukiza,
4 Tad priesterim būs pavēlēt, ka priekš tā, kas jāšķīstī, būs ņemt divus dzīvus šķīstus putnus un ciedra koku un sarkanus dzīparus un īzapu.
kuhani ataagiza vitu vifuatavyo viletwe kwa ajili ya mtu atakayetakaswa: ndege wawili safi walio hai, mti wa mwerezi, kitani nyekundu, na hisopo.
5 Un priesterim būs pavēlēt, ka tas viens putns top nokauts iekš kāda māla trauka pār tekošu ūdeni.
Kisha kuhani ataagiza kwamba mmoja wa ndege wale achinjwe kwenye chungu chenye maji safi.
6 To dzīvo putnu viņam tad būs ņemt un to ciedra koku un tos sarkanos dzīparus un to īzapu, un tos līdz ar to dzīvo putnu būs iemērcēt tā otra putna asinīs, kas ir nokauts pār to tekošo ūdeni,
Kisha kuhani atamchukua ndege aliye hai na kumtumbukiza pamoja na mti wa mwerezi, kitani nyekundu na hisopo ndani ya damu ya yule ndege aliyechinjiwa kwenye maji safi.
7 Un to, kas no spitāļiem šķīstās, būs septiņreiz apslacīt un šķīstīt, un to dzīvo putnu palaist laukā.
Atamnyunyizia yule mwenye ugonjwa wa kuambukiza maji hayo mara saba, na kumtangaza kuwa safi. Kisha atamwachia yule ndege aliye hai aende zake kwenye mashamba.
8 Un tam, kas šķīstās, būs mazgāt savas drēbes un nocirpt visus savus matus un ūdenī mazgāties, tad tas būs šķīsts; pēc tam lai viņš nāk lēģerī, bet lai paliek sava dzīvokļa ārpusē septiņas dienas.
“Huyo mtu atakayetakaswa ni lazima afue nguo zake, anyoe nywele zake zote, na aoge kwa maji; ndipo atakapokuwa safi kwa desturi ya ibada. Baada ya hili anaweza kuingia kambini, lakini ni lazima akae nje ya hema lake kwa siku saba.
9 Septītā dienā tam būs nodzīt savus matus, savu galvu un savu bārdu, to spalvu savās uzacīs; visus savus matus tam būs nodzīt un savas drēbes mazgāt un savu miesu ar ūdeni mazgāt, tad tas būs šķīsts.
Siku ya saba ni lazima anyoe nywele zake zote; yaani anyoe nywele za kichwa, ndevu zake, kope zake na nywele nyingine zote. Ni lazima afue nguo zake, na aoge kwa maji, naye atakuwa safi.
10 Un astotā dienā tam būs ņemt divus jērus, kas bez vainas, un gada vecu aitiņu, kas bez vainas, līdz ar trim desmitiem kviešu miltu par ēdamo upuri, ar eļļu sajauktu, un vienu logu(glāze) eļļas.
“Siku ya nane, ni lazima alete kondoo dume wawili na kondoo jike mmoja, wote wa mwaka mmoja na wasio na dosari, pamoja na sehemu tatu za kumi za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta, kwa ajili ya sadaka ya nafaka, na logi moja ya mafuta.
11 Tad tam priesterim, kas šķīsti, to vīru, kas šķīstās, līdz ar tām lietām būs stādīt Tā Kunga priekšā, priekš saiešanas telts durvīm.
Kuhani atakayemtangaza kuwa safi atahitaji kumkabidhi mgonjwa aliyepona pamoja na sadaka zake zote mbele za Bwana katika ingilio la Hema la Kukutania.
12 Un priesterim būs ņemt to vienu jēru un to upurēt par nozieguma upuri ar to logu (glāze) eļļas, un par līgojamu upuri to upurēt Tā Kunga priekšā.
“Kisha kuhani atamchukua mmoja wa wale kondoo dume na kumtoa kuwa sadaka ya hatia, pamoja na ile logi moja ya mafuta; ataviinua mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa.
13 Tad viņam to jēru būs nokaut tai vietā, kur top nokauts tas grēku upuris un dedzināmais upuris, svētā vietā, jo tas nozieguma upuris pieder tāpat kā tas grēku upuris priesterim; tas ir augsti svēts.
Atamchinja huyo kondoo katika mahali patakatifu ambapo sadaka ya dhambi na ile ya kuteketezwa huchinjiwa. Kama ilivyo sadaka ya dhambi, sadaka ya hatia ni ya kuhani; nayo ni takatifu sana.
14 Un priesterim būs ņemt no tā nozieguma upura asinīm, un to būs likt uz labās auss skripstiņu tam, kas jāšķīstī, un uz viņa labās rokas īkšķi un uz viņa labās kājas lielo pirkstu.
Kuhani atachukua sehemu ya damu ya sadaka ya hatia na kuitia kwenye ncha ya sikio la kuume la yule atakayetakaswa, kwenye kidole gumba cha mkono wake wa kuume, na kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume.
15 Un priesterim arī būs ņemt eļļu no tā loga un liet savā kreisā saujā.
Kuhani atachukua sehemu ya ile logi ya mafuta, ayamimine kwenye kiganja cha mkono wake mwenyewe wa kushoto,
16 Un būs iemērcēt savu labo pirkstu tai eļļā, kas kreisajā saujā, un ar savu pirkstu no tās eļļas septiņreiz slacīt Tā Kunga priekšā.
na achovye kidole chake cha shahada cha mkono wake wa kuume kwenye mafuta yaliyoko kwenye kiganja chake, na kwa kidole hicho anyunyize mafuta hayo mara saba mbele za Bwana.
17 Un no tās atlikušās eļļas, kas viņa saujā, priesterim būs likt uz labās auss skripstiņu tam, kas jāšķīstī, un uz viņa labās rokas īkšķi un uz viņa labās kājas lielo pirkstu virsū uz tām nozieguma upura asinīm.
Kuhani atampaka yule anayetakaswa sehemu ya mafuta yaliyobaki kiganjani kwenye ncha ya sikio lake la kuume, kwenye kidole gumba cha mkono wake wa kuume, na kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume, mahali palepale alipompaka damu ya sadaka ya kuondoa hatia.
18 Un kas vēl atlicis no tās eļļas, kas bija priestera saujā, to viņam būs likt uz galvu tam, tas jāšķīstī; tā priesterim viņu būs salīdzināt Tā Kunga priekšā.
Kuhani atayapaka mafuta yaliyobaki kwenye kiganja chake juu ya kichwa cha yule anayetakaswa, na kufanya upatanisho kwa ajili yake mbele za Bwana.
19 Un priesterim arī būs sataisīt grēku upuri un to šķīstīto salīdzināt viņa nešķīstības dēļ.
“Kisha kuhani atatoa dhabihu ya sadaka ya dhambi na kufanya upatanisho kwa ajili ya yule atakayetakaswa kutoka unajisi wake. Baada ya hayo, kuhani atachinja sadaka ya kuteketezwa
20 Tad viņam būs nokaut to dedzināmo upuri un to dedzināmo upuri un to ēdamo upuri būs celt uz altāri; tā priesterim viņu būs salīdzināt, tad tas ir šķīsts.
na kuitoa juu ya madhabahu, pamoja na sadaka ya nafaka ili kumfanyia upatanisho, naye atakuwa safi.
21 Bet ja viņš ir nabags un viņam maz pie rokas, tad lai ņem vienu jēru nozieguma upurim par līgojamu upuri, sevi salīdzināt, un desmito tiesu kviešu miltu ar eļļu sajauktu par ēdamu upuri un vienu logu (glāze) eļļas,
“Hata hivyo, kama ni maskini na hawezi kupata vitu hivi, lazima achukue mwana-kondoo mmoja kama sadaka ya hatia ipate kuinuliwa ili kumfanyia upatanisho, pamoja na sehemu ya kumi ya efa ya unga laini uliochanganywa na logi moja ya mafuta kwa ajili ya sadaka ya nafaka,
22 Un divas ūbeles jeb divus jaunus baložus, cik viņa roka paspēj; no tiem lai ir viens par grēku upuri un otrs par dedzināmo upuri.
na hua wawili au makinda mawili ya njiwa, kile atakachoweza kupata, mmoja kwa sadaka ya dhambi, na mwingine kwa sadaka ya kuteketezwa.
23 Un astotā šķīstīšanas dienā tos būs nest pie priestera, pie saiešanas telts durvīm Tā Kunga priekšā.
“Katika siku ya nane, lazima avilete vitu hivyo kwa kuhani, kwa ajili ya kutakaswa kwake kwenye ingilio la Hema la Kukutania mbele za Bwana.
24 Un priesterim būs ņemt to nozieguma upura jēru un to logu (glāze) eļļas, un tos būs līgot par līgojamu upuri Tā Kunga priekšā.
Kuhani atamchukua mwana-kondoo kwa ajili ya sadaka ya hatia, pamoja na ile logi ya mafuta ya kuinuliwa mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa.
25 Tad nozieguma upura jēru būs nokaut un ņemt no nozieguma upura asinīm, un to likt uz labās auss skripstiņu tam, kas šķīstās un uz viņa labās rokas īkšķi un uz viņa labās kājas lielo pirkstu.
Atamchinja huyo mwana-kondoo kwa ajili ya sadaka ya hatia. Pia ataichukua sehemu ya damu yake na kuipaka kwenye ncha ya sikio la kuume la yule anayetakaswa, na aipake pia kwenye kidole gumba cha mkono wa kuume wa huyo mtu, na kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume.
26 Un priesterim no tās eļļas būs liet savā kreisajā saujā.
Kuhani atamiminia sehemu ya mafuta kwenye kiganja chake cha mkono wa kushoto,
27 Un no tās eļļas, kas kreisajā saujā, priesterim septiņreiz būs slacīt Tā Kunga priekšā.
na kwa kidole chake cha shahada cha mkono wa kuume, atamnyunyizia yule anayetakaswa yale mafuta yaliyo kwenye kiganja chake mara saba mbele za Bwana.
28 Un no tās eļļas, kas viņa saujā, priesterim būs likt uz labās auss skripstiņu tam, kas šķīstās, un uz viņa labās kājas lielo pirkstu, virsū uz tām nozieguma upura asinīm.
Atampaka mafuta yaliyobaki kwenye kiganja chake katika sehemu zote, kama alivyompaka damu ya sadaka ya hatia: yaani, kwenye ncha ya sikio la kuume la yule anayetakaswa, kwenye kidole gumba cha mkono wake wa kuume, na kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume.
29 Un to atlikumu no tās eļļas, kas priestera saujā, būs likt uz galvu tam, kas šķīstās, par salīdzināšanu Tā Kunga priekšā.
Kuhani atayapaka mafuta yaliyobaki katika kiganja chake kwenye kichwa cha yule anayetakaswa, na kufanya upatanisho kwa ajili yake mbele za Bwana.
30 Tad viņam būs sataisīt vienu no tām ūbelēm jeb no tiem jauniem baložiem, cik viņa roka paspēj,
Kisha atatoa dhabihu wale hua ama yale makinda ya njiwa ambayo mtu ataweza kuwapata,
31 Cik viņa roka paspēj, vienu par grēku upuri un otru par dedzināmo upuri līdz ar ēdamo upuri; tā priesterim to, kas šķīstās, būs salīdzināt Tā Kunga priekšā,
mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi, na mwingine kuwa sadaka ya kuteketezwa, pamoja na sadaka ya nafaka. Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho mbele za Bwana kwa ajili ya yule anayetakaswa.”
32 Šis ir tas likums par to, kam ir spitāļi, kam roka nepaspēj, cik viņa šķīstīšanas pēc vajag.
Haya ndiyo masharti kwa mtu yeyote mwenye ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza, na ambaye hana uwezo wa kutoa sadaka za kawaida kwa ajili ya kutakaswa kwake.
33 Un Tas Kungs runāja uz Mozu un uz Āronu un sacīja:
Bwana akawaambia Mose na Aroni,
34 Kad jūs nāksiet Kanaāna zemē, ko Es jums došu par īpašumu, un kad Es spitālības vainu piesūtīšu kādam jūsu zemes namam,
“Mtakapoingia katika nchi ya Kanaani ambayo ninawapa kuwa milki yenu, nami nikaweka upele ueneao kwenye nyumba katika nchi ile,
35 Tad tam, kam tas nams pieder, būs nākt un priesterim dot ziņu un sacīt: man šķiet, kādu vainu esam manā namā.
ni lazima mwenye nyumba hiyo akamwambie kuhani, ‘Nimeona kitu fulani kinachofanana na upele kwenye nyumba yangu.’
36 Un priesterim būs pavēlēt, ka to namu izkravā, pirms priesteris nāk, to vainu apraudzīt, lai netop nešķīsti visi, kas tai namā, un tad priesterim būs nākt un to namu apraudzīt.
Kuhani ataagiza vitu vyote vitolewe ndani ya nyumba, kabla hajaenda kuchunguza kama ina ugonjwa huo, ili kitu chochote ndani ya nyumba kisitangazwe kuwa najisi. Baada ya hili, kuhani ataingia ndani na kuikagua hiyo nyumba.
37 Kad viņš nu to vainu aplūkojis un redz, ka tai vainai pie nama sienām ir pazaļas vai pasarkanas dobītes, un tās dziļāki izraugās nekā tā siena,
Atachunguza upele huo katika kuta za nyumba hiyo, nazo kama zina rangi ya kijani kibichi au wekundu, na kuna mibonyeo ndani ya ukuta,
38 Tad priesterim no nama būs iziet pie nama durvīm un to namu aizslēgt septiņas dienas.
kuhani atatoka na kufunga mlango wa nyumba hiyo kwa siku saba.
39 Un septītā dienā priesterim atkal būs nākt un lūkot, un raugi, ja tā vaina pie nama sienām ir izpletusies,
Siku ya saba, kuhani atarudi kuikagua nyumba. Kama upele umeenea juu ya kuta,
40 Tad priesterim būs pavēlēt, ka tos akmeņus izlauž, kur tā vaina, un tos ārā izmet aiz pilsētas kādā nešķīstā vietā.
ataagiza kwamba mawe yote yaliyoambukizwa yaondolewe na kutupwa katika eneo lililo najisi nje ya mji.
41 Un to namu no iekšienes visapkārt būs nokasīt, un to nokasījumu, ko tie nokasījuši, būs izmest ārā aiz pilsētas uz kādu nešķīstu vietu.
Kuta zote za ndani ya nyumba hiyo ni lazima zikwanguliwe, na kifusi chake kitupwe mahali najisi nje ya mji.
42 Tad tiem būs ņemt citus akmeņus un likt viņu akmeņu vietā, un citus mālus ņemt un to namu apmest.
Kisha watachukua mawe mengine na kujenga palipobomolewa kwa udongo mpya wa mfinyanzi, na kuipiga nyumba hiyo lipu mpya.
43 Bet ja tā vaina tajā namā izplešas, pēc tam kad tie akmeņi ir izlauzti, tas nams nokasīts un atkal apmests,
“Ikiwa upele huo utatokea tena ndani ya ile nyumba baada ya mawe kuondolewa na nyumba kukwanguliwa na kuwekwa lipu mpya,
44 Tad priesterim būs nākt un raudzīt, un redzi, ja tā vaina pie tā nama ir izpletusies, tad ēdoti spitālības vaina ir tanī namā; - tas ir nešķīsts.
kuhani atakwenda kuikagua, na kama upele umeenea ndani ya nyumba, basi ni upele uharibuo; nyumba hiyo ni najisi.
45 Un to namu, viņa akmeņus un viņa kokus un visus nama mālus būs nolauzīt un ārā izmest aiz pilsētas uz kādu nešķīstu vietu.
Ni lazima ibomolewe: mawe yake, mbao na lipu yake, vyote vikatupwe nje ya mji mahali palipo najisi.
46 Un kas šai namā iet jebkurā dienā, kad tas tapis aizslēgts, tam būs nešķīstam būt līdz vakaram.
“Yeyote atakayeingia katika nyumba hiyo ikiwa imefungwa, atakuwa najisi mpaka jioni.
47 Un kas tajā namā guļ, tam būs mazgāt savas drēbes, un kas tai namā ēd, tam būs mazgāt savas drēbes.
Yeyote atakayelala au kula ndani ya nyumba hiyo ni lazima afue nguo zake.
48 Bet kad priesteris atkal nāks un lūkos un redzi, tā vaina tai namā pēc tam, kad tas apmests, nav izpletusies, tad priesterim to namu būs atzīt par šķīstu, jo tā vaina ir sadzijusi.
“Lakini ikiwa kuhani atakuja kuikagua na kukuta kuwa upele haujaenea tena baada ya nyumba kupigwa lipu, ataitangaza nyumba ile kuwa safi, kwa sababu upele umekwisha.
49 Tad viņam priekš tā nama šķīstīšanas būs ņemt divus putnus un ciedra koku un sarkanus dzīparus un īzapu.
Ili kuitakasa nyumba hiyo, mwenye nyumba ataleta ndege wawili, mti wa mwerezi, kitani nyekundu na hisopo.
50 Un viņam to vienu putnu būs nokaut kādā mālu traukā pār tekošu ūdeni.
Atamchinja mmoja wa wale ndege kwenye chungu chenye maji safi.
51 Un viņam būs ņemt to ciedra koku un to īzapu un tos sarkanos dzīparus un to dzīvo putnu un tos iemērcēt tā nokauta putna asinīs un tai tekošā ūdenī un to namu septiņreiz apslacīt.
Kisha atachukua mti wa mwerezi, hisopo, kitani nyekundu na ndege aliye hai, na kuvitumbukiza ndani ya damu ya ndege aliyechinjwa pamoja na maji safi, na kuinyunyizia nyumba ile mara saba.
52 Tā viņam to namu būs šķīstīt ar tā putna asinīm un ar to tekošo ūdeni un ar to dzīvo putnu un ar to ciedra koku un ar to īzapu un ar tiem sarkaniem dzīpariem.
Ataitakasa nyumba kwa damu ya yule ndege, maji safi, ndege aliye hai, mti wa mwerezi, hisopo na kitani nyekundu.
53 Tad viņam to dzīvo putnu būs palaist ārā aiz pilsētas laukā; tā viņam to namu būs salīdzināt, tad tas taps šķīsts.
Kisha atamwachia yule ndege aliye hai huru mashambani nje ya mji. Kwa njia hii atafanya upatanisho kwa ajili ya nyumba ile, nayo itakuwa safi.”
54 Šis ir tas likums par ikvienu spitālības vainu un par kraupi
Haya ndiyo masharti kuhusu aina yoyote ya ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza, mwasho wowote,
55 Un par drēbju un namu spitāļiem,
upele ndani ya nguo au ndani ya nyumba,
56 Un par tūkumiem un kašķi un baltām pūtēm;
kwa uvimbe, vipele au kipaku kingʼaacho,
57 Par mācību, kad kas ir nešķīsts un kad kas šķīsts; - šis ir tas likums par spitāļiem.
kupambanua wakati kitu fulani ni safi au najisi. Haya ndiyo masharti kuhusu magonjwa ya ngozi ya kuambukiza na upele.

< Trešā Mozus 14 >