< Sog̒u 9 >
1 Un Abimeleks, JerubBaāla dēls, gāja uz Šehemi pie savas mātes brāļiem un runāja uz tiem un uz visiem savas mātes tēva nama radiem un sacīja:
Siku moja Abimeleki mwana wa Yerub-Baali akaenda kwa ndugu ya mama yake huko Shekemu na kuwaambia yeye na ukoo wote wa mama yake,
2 Runājiet lūdzami priekš visu namnieku ausīm Šehemē: kas jums ir labāki, vai ka septiņdesmit vīri, visi JerubBaāla dēli, pār jums valda, vai ka viens vīrs pār jums valda? Pieminiet, mani arīdzan esam jūsu kaulu un jūsu miesu.
“Waulizeni watu wote wa Shekemu, ‘Lipi lililo bora kwenu: Kutawaliwa na wana wote sabini wa Yerub-Baali, au mtu mmoja peke yake?’ Kumbukeni kwamba, mimi ni mfupa wenu nyama yenu hasa.”
3 Tad viņa mātes brāļi viņa dēļ runāja priekš visu namnieku ausīm Šehemē visus šos vārdus un viņu sirds nesās uz Abimeleku, jo tie sacīja: viņš ir mūsu brālis.
Ndugu za mama yake walipowaeleza watu wote wa Shekemu, wakaelekea kumkubali Abimeleki, kwa kuwa walisema, “Yeye ni ndugu yetu.”
4 Un tie viņam deva septiņdesmit sudraba sēķeļus no BaālBerita nama, un Abimeleks ar tiem saderēja neliešus un nebēdniekus, kas viņam staigāja pakaļ.
Wakampa shekeli sabini za fedha kutoka hekalu la Baal-Berithi, naye Abimeleki akaitumia kuajiri watu ovyo wasiojali, wakawa ndio wafuasi wake.
5 Un viņš nāca sava tēva namā uz Ovru un nokāva savus brāļus, JerubBaāla bērnus, septiņdesmit vīrus uz viena akmens; bet Jotams, JerubBaāla jaunākais dēls, atlika, jo viņš bija paslēpies.
Akaenda nyumbani kwa baba yake huko Ofra, na juu ya jiwe moja wakawaua ndugu zake sabini, ambao ni wana wa Yerub-Baali. Lakini Yothamu, mwana mdogo wa wote wa Yerub-Baali, akaokoka kwa kujificha.
6 Tad visi Šehemes namnieki sapulcējās un viss Millus nams, un tie nogāja un iecēla Abimeleku par ķēniņu pie tā piemiņas ozola, kas ir Šehemē.
Ndipo watu wote wa Shekemu na Beth-Milo wakakusanyika pamoja chini ya mti mkubwa wa mwaloni penye nguzo iliyoko Shekemu wakamvika Abimeleki taji kuwa mfalme.
7 Kad to Jotamam teica, tad viņš nogāja un nostājās Gerizima kalna paša galā un pacēla savu balsi un sauca un sacīja: klausāties mani, jūs Šehemes namnieki, tad Dievs arī jūs klausīs.
Yothamu alipoambiwa hayo, akapanda juu ya kilele cha mlima Gerizimu, akawapazia sauti yake akawaambia, “Nisikilizeni enyi watu wa Shekemu, ili Mungu naye apate kuwasikiliza ninyi.
8 Koki gāja, ķēniņu pār sevi svaidīt, un sacīja uz eļļas koku: esi ķēniņš pār mums.
Siku moja miti ilitoka ili kwenda kujitawazia mfalme. Ikauambia mzeituni, ‘Wewe uwe mfalme wetu.’
9 Bet eļļas koks uz tiem sacīja: vai man būs atstāt savu taukumu, ko Dievs un cilvēki pie manis slavē, un noiet un līgoties pa koku virsu?
“Lakini mzeituni ukaijibu, ‘Je, niache kutoa mafuta yangu ambayo kwake miungu na wanadamu huheshimiwa, ili nikawe juu ya miti?’
10 Tad tie koki sacīja uz vīģes koku: nāc tu, esi ķēniņš pār mums.
“Kisha miti ikauambia mtini, ‘Njoo na uwe mfalme wetu!’
11 Bet vīģes koks uz tiem sacīja: vai man būs atstāt savu saldumu un savus labos augļus un noiet un līgoties pa koku virsu?
“Lakini mtini ukaijibu, ‘Je, niache kutoa matunda yangu mazuri na matamu, ili niende nikawe juu ya miti?’
12 Tad tie koki sacīja uz vīnakoku: nāc tu un esi ķēniņš pār mums.
“Ndipo miti ikauambia mzabibu, ‘Njoo na uwe mfalme wetu.’
13 Bet vīnakoks uz tiem sacīja: vai man būs atstāt savu vīnu, kas dievus un cilvēkus iepriecina, un noiet un līgoties pa koku virsu?
“Lakini mzabibu ukaijibu, ‘Je, niache kutoa divai yangu inayofurahisha miungu na wanadamu ili nikawe juu ya miti?’
14 Tad visi koki sacīja uz ērkšķu krūmu: nāc tu un esi ķēniņš pār mums.
“Mwishoni miti yote ikauambia mti wa miiba, ‘Njoo na uwe mfalme wetu.’
15 Tad ērkšķu krūms uz tiem kokiem sacīja: kad jūs tiešām mani svaidiet sev par ķēniņu, tad nāciet un uzticaties manai paēnai, bet ja ne, tad lai uguns iziet no ērkšķu krūma un norij Lībanus ciedru kokus.
“Nao mti wa miiba ukaijibu, ‘Kama kweli mnataka niwe mfalme wenu, basi njooni mpate kupumzika chini ya kivuli changu. Lakini kama sivyo, moto na utoke kwenye mti wa miiba ukateketeze mierezi ya Lebanoni!’
16 Un nu, vai jūs esat taisni un pareizi darījuši, Abimeleku celdami par ķēniņu, un vai jūs esat labi darījuši pie JerubBaāla un viņa nama un viņam darījuši pēc viņa roku nopelna?
“Basi ikiwa mmetenda kwa uaminifu na heshima kumfanya Abimeleki kuwa mfalme, na kama mmetendea vyema Yerub-Baali na jamaa yake kama ilivyostahili:
17 Jo mans tēvs jūsu dēļ karojis un savu dzīvību nometis un jūs izglābis no Midijaniešu rokas,
kwa kuwa baba yangu aliwapigania ninyi na kuhatarisha nafsi yake na kuwaokoa ninyi kutoka mikononi mwa Wamidiani
18 Bet jūs šodien esat cēlušies pret mana tēva namu un nokāvuši viņa dēlus, septiņdesmit vīrus uz viena akmens, un esat iecēluši Abimeleku,
(lakini leo mmeasi dhidi ya jamaa ya baba yangu, na kuwaua wanawe sabini juu ya jiwe moja, nanyi mkamfanya Abimeleki mwana wa mwanamke mtumwa kuwa mfalme juu ya Shekemu, kwa kuwa yeye ni ndugu yenu),
19 Ja nu jūs šodien taisni un pareizi esat darījuši pie JerubBaāla un pie viņa nama, tad priecājaties par Abimeleku, un lai viņš arīdzan priecājās par jums.
nanyi kama basi mmemtendea Yerub-Baali na jamaa yake kwa heshima na uaminifu, basi Abimeleki na awe furaha yenu, nanyi mwe furaha yake pia!
20 Bet ja ne, tad lai uguns iziet no Abimeleka un norij Šehemes namniekus un Millus namu, un lai uguns iziet no Šehemes namniekiem un no Millus nama un norij Abimeleku.
Lakini kama sivyo, moto na utoke kwa Abimeleki na uwateketeze, ninyi watu wa Shekemu na Beth-Milo, nao moto utoke kwenu, watu wa Shekemu na Beth-Milo umteketeze Abimeleki!”
21 Tad Jotams bēga un aizbēga uz Beru un dzīvoja tur, no sava brāļa Abimeleka bīdamies.
Ndipo Yothamu akakimbia, akatoroka akaenda Beeri, akaishi huko, kwa sababu alimwogopa ndugu yake Abimeleki.
22 Kad nu Abimeleks trīs gadus bija valdījis pār Israēli,
Baada ya Abimeleki kutawala Israeli kwa muda wa miaka mitatu,
23 Tad Dievs sūtīja ļaunu garu starp Abimeleku un Šehemes namniekiem, un Šehemes namnieki turējās viltīgi pret Abimeleku,
Mungu akaruhusu roho mbaya kati ya Abimeleki na watu wa Shekemu, nao watu wa Shekemu wakamtendea Abimeleki kwa hila.
24 Ka tas varas darbs pie tiem septiņdesmit JerubBaāla dēliem nāktu un viņa asinis grieztos uz Abimeleku, viņu brāli, kas tos bija nokāvis, un tos, kas bija stiprinājuši, savus brāļus nokaut.
Hili lilitokea ili ule ukatili waliotendewa hao wana sabini wa Yerub-Baali upatilizwe, na damu yao iwe juu ya Abimeleki ndugu yao aliyewaua, na pia iwe juu ya watu wa Shekemu, ambao walimsaidia kuua ndugu zake.
25 Un Šehemes namnieki sūtīja kādus, kas ar viltu uz viņu glūnēja kalna galos, un tie visus aplaupīja, kas pa to ceļu gāja, un tas Abimelekam tapa sacīts.
Hivyo, kutokana na uadui juu yake watu wa Shekemu wakaweka watu wa kumvizia katika vilele vya milima. Wakawanyangʼanya watu wote waliopita karibu nao, nayo haya yakaarifiwa kwa Abimeleki.
26 Un Gaāls, Ebeda dēls, nāca ar saviem brāļiem un gāja uz Šehemi, un Šehemes namnieki viņam uzticējās,
Basi Gaali mwana wa Ebedi akaenda pamoja na ndugu zake wakaingia Shekemu, nao watu wa huko wakamtumainia yeye.
27 Un izgāja uz lauku un nolasīja savus vīna kalnus un spaidīja ogas un svinēja prieka svētkus, un gāja sava dieva namā un ēda un dzēra un lādēja Abimeleku.
Wakaenda mashambani mwao kuvuna zabibu na kuzisindika hizo zabibu, wakafanya sikukuu katika hekalu la mungu wao. Wakati wakila na kunywa, wakamlaani Abimeleki.
28 Un Gaāls, Ebeda dēls, sacīja: kas ir Abimeleks, un kas ir Šehems, ka mums viņam būs kalpot? Vai tas nav JerubBaāla dēls un Zebuls viņa uzraugs? Kalpojiet labāki, Hamora, Šehema tēva, vīriem, jo kāpēc lai mēs viņam kalpojam?
Gaali mwana wa Ebedi akasema, “Abimeleki ni nani, na Shekemu ni nani, hata tumtumikie? Je, yeye si mwana wa Yerub-Baali? Naye Zebuli si ndiye msaidizi wake? Basi watumikieni watu wa Hamori, babaye Shekemu. Kwa nini tumtumikie Abimeleki?
29 Ak kaut šie ļaudis būtu manā rokā, gan es Abimeleku izdzītu. Un uz Abimeleku viņš sacīja: vairo savu karaspēku un nāc ārā.
Laiti watu hawa wangekuwa chini ya amri yangu! Basi mimi ningemwondoa huyo Abimeleki. Ningemwambia Abimeleki, ‘Ondoa jeshi lako lote.’”
30 Kad Zebuls, tās pilsētas virsnieks, Gaāla, Ebeda dēla, vārdus dzirdēja, tad viņš apskaitās,
Zebuli aliyekuwa mtawala wa mji aliposikia aliyosema Gaali mwana wa Ebedi, akakasirika sana.
31 Un sūtīja slepeni vēstnešus pie Abimeleka un sacīja: redzi, Gaāls, Ebeda dēls, un viņa brāļi ir nākuši uz Šehemi, un redzi, tie ceļ dumpi pret tevi pilsētā.
Akatuma ujumbe uende kwa Abimeleki kwa siri na kusema, “Gaali mwana wa Ebedi na ndugu zake wamekuja Shekemu, na wanauchochea mji huu kinyume chako.
32 Un nu celies naktī, tu un tie ļaudis, kas pie tevis, un paslēpies laukā;
Sasa, basi, usiku huu wewe uondoke na watu wako ili mje kuwavizia mashambani.
33 Un rītā agri, kad saule lec, tad celies un uzbrūc tai pilsētai, un redzi, kad viņš un tie ļaudis, kas pie viņa, ies ārā tev pretī, tad dari viņam, kā tava roka māk.
Kisha asubuhi wakati wa kuchomoza jua, amka mapema na ujipange dhidi ya huo mji. Wakati yeye na jeshi lililo pamoja naye watakapotoka kukabiliana nanyi, mwaweza kuwatendea kwa kadiri mnavyoweza.”
34 Tad Abimeleks un visi ļaudis, kas pie viņa bija, cēlās naktī un paslēpās pret Šehemi četros pulkos.
Kwa hiyo Abimeleki pamoja na jeshi lake lote wakaondoka usiku na kujificha karibu na Shekemu wakiwa vikosi vinne.
35 Un Gaāls, Ebeda dēls, izgāja ārā un stāvēja priekš pilsētas vārtiem. Tad Abimeleks un tie ļaudis, kas pie viņa bija, cēlās, kur bija apslēpušies.
Basi Gaali mwana wa Ebedi alikuwa ametoka nje akawa amesimama katika ingilio la mji wakati ule ule ambao Abimeleki na watu wake walipokuwa wanatoka sehemu zao za maficho.
36 Kad nu Gaāls tos ļaudis ieraudzīja, tad viņš sacīja uz Zebulu: redzi, no kalnu galiem nāk ļaudis. Bet Zebuls uz to sacīja: tev šķiet kalna ēnu cilvēkus esam.
Gaali alipowaona, akamwambia Zebuli, “Tazama, watu wanashuka kutoka kwenye vilele vya milima!” Zebuli akajibu, “Wewe unaona vivuli vya milima kana kwamba ni watu.”
37 Tad Gaāls vēl runāja un sacīja: redzi, ļaudis nāk no augšgala un viens pulks nāk pa ceļu no burvju ozola.
Lakini Gaali akasema tena, “Tazama, watu wanashuka kutoka katikati ya nchi na kikosi kimoja kinakuja kutoka Tabur-Ezeri na kikosi kingine kutoka upande wa Elon-Meonenimu.”
38 Tad Zebuls uz viņu sacīja: kur nu ir tava mute, ar ko tu sacīji: kas ir Abimeleks, ka lai tam kalpojam? Vai šie nav tie ļaudis, ko tu esi apsmējis? Izej jel nu ārā un karo pret viņu.
Ndipo Zebuli akamwambia, “Kuko wapi kujivuna kwako sasa, wewe uliyesema, ‘Huyo Abimeleki ni nani hata tumtumikie?’ Hawa si wale watu uliowadharau? Toka nje sasa ukapigane nao!”
39 Un Gaāls izgāja Šehemes namnieku priekšā un karoja pret Abimeleku.
Basi Gaali akatoka akawaongoza watu wa Shekemu kupigana na Abimeleki.
40 Un Abimeleks tam dzinās pakaļ, un tas bēga no viņa, un daudz krita nokauti līdz vārtiem.
Abimeleki akamfukuza, watu wengi wakajeruhiwa katika kukimbia huko, njia nzima hadi kwenye ingilio la lango.
41 Un Abimeleks palika Arumā, bet Zebuls izdzina Gaālu un viņa brāļus, ka tie Šehemē nepalika.
Abimeleki akakaa Aruma, naye Zebuli akawafukuza Gaali na ndugu zake watoke Shekemu.
42 Un notika otrā dienā, ka tie ļaudis gāja uz lauku, un tas Abimelekam tapa sacīts.
Kesho yake watu wa Shekemu wakatoka wakaenda mashambani, Abimeleki akaambiwa juu ya jambo hili.
43 Tad viņš ņēma tos (kara) ļaudis un tos dalīja trijos pulkos un paslēpās laukā. Un viņš skatījās, un redzi, tie ļaudis izgāja no pilsētas; tad viņš cēlās pret tiem un tos nokāva.
Hivyo akawachukua watu wake, akawagawanya katika vikosi vitatu na kuwaweka waviziao huko mashambani. Alipowaona watu wanatoka kwenda nje ya mji, akainuka dhidi yao na kuwashambulia.
44 Un Abimeleks un tie pulki, kas pie viņa bija, uzbruka un nostājās priekš pilsētas vārtiem, bet tie divi pulki uzbruka visiem, kas bija laukā, un tos nokāva.
Abimeleki pamoja na vile vikosi wakaharakisha kwenda mbele kwenye nafasi, mahali pa ingilio la lango la mji. Vile vikosi viwili vikawawahi wale waliokuwa mashambani na kuwaua.
45 Un Abimeleks karoja pret to pilsētu visu to dienu un uzņēma to pilsētu un nokāva tos ļaudis, kas tanī bija, un nopostīja to pilsētu un apsēja to ar sāli.
Siku hiyo nzima Abimeleki akazidisha mashambulizi yake dhidi ya mji hadi akawa ameuteka na kuwaua watu wa huo mji. Kisha akauangamiza mji na kusambaza chumvi juu yake.
46 Kad nu visi Šehemes pils namnieki to dzirdēja, tad tie gāja tai stiprā Berita dieva nama tornī.
Kwa kusikia jambo hili watu wote katika mnara wa Shekemu, wakaingia kwenye ngome ya hekalu la El-Berithi.
47 Un Abimelekam tas tapa sacīts, ka visi Šehemes pils namnieki bija sapulcējušies.
Abimeleki aliposikia kuwa wamekusanyika huko,
48 Tad Abimeleks gāja uz Calmon kalnu, viņš un visi ļaudis, kas pie viņa bija, un Abimeleks ņēma cirvi savā rokā un nocirta koka zaru un to uzcēla un lika uz savu kamiesi un sacīja uz tiem ļaudīm, kas pie tā bija: ko esat redzējuši mani darām, to dariet steigšus tāpat.
yeye na watu wake wote wakakwea kwenye Mlima Salmoni. Abimeleki akachukua shoka, akakata baadhi ya matawi, ambayo aliyachukua mabegani. Akawaagiza wale watu waliokuwa pamoja naye kuwa, “Fanyeni kile mlichoona mimi nikifanya!”
49 Tad arī visi ļaudis nocirta ikkatrs zaru un gāja Abimelekam pakaļ, un tos pielika pie tā stiprā torņa un iededzināja pār tiem to torni ar uguni, ka visi Šehemes pils ļaudis nomira līdz tūkstoš vīru un sievu.
Basi watu wote wakakata matawi na kumfuata Abimeleki. Wakayakusanya hayo matawi juu ya ngome na kuitia moto ili kuwachoma wale watu wote waliokuwa ndani yake. Hivyo watu wote katika mnara wa Shekemu, karibia watu 1,000 waume kwa wake, pia wakafa.
50 Un Abimeleks gāja uz Tebecu un apmetās pret Tebecu un to uzņēma.
Baadaye Abimeleki akaenda Thebesi na kuuzingira kwa jeshi na kuuteka.
51 Bet pilsētas vidū bija stipra pils, uz turieni visi vīri un sievas un visi pilsētas namnieki bēga un ieslēdzās un uzkāpa uz pils jumtu.
Hata hivyo, ndani ya huo mji kulikuwa na mnara imara, ambako watu wote wa mji wanaume na wanawake, watu wote wa mji, walikimbilia ndani yake. Wakajifungia ndani yake na kupanda juu ya paa la mnara.
52 Tad Abimeleks nāca pie tās pils un karoja pret to un piegāja pie pils durvīm, viņu ar uguni sadedzināt.
Abimeleki akaja kwenye ule mnara na kuushambulia, lakini alipokaribia kwenye ingilio la mnara ili kuuchoma kwa moto,
53 Tad viena sieva nometa dzirnu akmens gabalu uz Abimeleka galvu un satrieca viņa galvas kausu.
mwanamke mmoja akaangusha sehemu ya juu ya jiwe la kusagia juu ya kichwa cha Abimeleki, likapasua fuvu la kichwa chake.
54 Tad viņš steigšus piesauca to puisi, savu bruņu nesēju, un uz to sacīja: izvelc savu zobenu un nokauj mani, lai no manis nesaka: viena sieva viņu nokāvusi. Un viņa puisis to nodūra, ka nomira.
Akamwita kwa haraka kijana yule aliyechukua silaha zake, na kumwambia, “Chukua upanga wako na uniue, watu wasije wakasema kwamba, ‘Mwanamke amemuua.’” Basi yule kijana akamchoma upanga, naye akafa.
55 Kad nu Israēla vīri redzēja, ka Abimeleks bija nomiris, tad tie gāja ikkatrs uz savām mājām.
Waisraeli walipoona kuwa Abimeleki amekufa, kila mtu akaenda nyumbani kwake.
56 Tā Dievs Abimelekam maksāja to ļaunumu, ko viņš bija darījis savam tēvam, nokaudams savus septiņdesmit brāļus.
Hivyo ndivyo Mungu alivyolipiza uovu ule ambao Abimeleki alikuwa ameutenda kwa baba yake kwa kuwaua ndugu zake sabini.
57 Un Dievs Šehemes vīriem atmaksāja visu ļaunumu uz viņu galvām, un Jotama, JerubBaāla dēla, lāsti nāca pār tiem.
Mungu akawapatiliza watu wa Shekemu uovu wao juu ya vichwa vyao, na juu yao ikaja laana ya Yothamu mwana wa Yerub-Baali.