< Jāņa Evaņg̒elijs 21 >
1 Pēc tam Jēzus tiem mācekļiem atkal parādījās pie Tiberijas jūras, un Viņš tā parādījās.
Baada ya haya Yesu akawatokea tena wanafunzi wake kando ya Bahari ya Tiberia. Yeye alijionyesha kwao hivi:
2 Tur bija kopā Sīmanis Pēteris un Toms, dvīnis saukts, un Natanaēls no Kānas iekš Galilejas un tie Cebedeja dēli un divi citi no Viņa mācekļiem.
Simoni Petro, Tomaso aitwaye Didimasi, yaani Pacha, Nathanaeli wa Kana ya Galilaya, wana wa Zebedayo na wanafunzi wengine wawili walikuwa pamoja.
3 Sīmanis Pēteris uz tiem saka: “Es iešu zvejot.” Tad tie uz viņu saka: “Mēs arī iesim tev līdz!” Tad tie izgāja un tūdaļ iekāpa laivā un nekā nedabūja tajā naktī.
Simoni Petro akawaambia wenzake, “Mimi naenda kuvua samaki.” Nao wakamwambia, “Tutakwenda pamoja nawe.” Wakatoka, wakaingia ndani ya mashua, lakini usiku ule hawakupata chochote.
4 Bet kad gaisma jau bija aususi, Jēzus stāvēja malā, un tie mācekļi nezināja, to esam Jēzu.
Mara baada ya kupambazuka, Yesu akasimama ufuoni, lakini wanafunzi hawakumtambua kwamba alikuwa Yesu.
5 Tad Jēzus uz tiem saka: “Bērni, vai jums nav ko ēst?” Tie Viņam atbildēja: “Nav nekā!”
Yesu akawaambia, “Wanangu, je, mna samaki wowote?” Wakamjibu, “La.”
6 Bet Viņš uz tiem sacīja: “Metiet tīklu pa laivas labo pusi, tad jūs atradīsiet.” Tad tie izmeta tīklu un vairs nespēja to vilkt tā pulka zivju dēļ.
Akawaambia, “Shusheni nyavu upande wa kuume wa mashua yenu nanyi mtapata samaki.” Wakashusha nyavu na tazama wakapata samaki wengi mno hata wakashindwa kuvutia zile nyavu zilizojaa samaki ndani ya mashua.
7 Tad tas māceklis, ko Jēzus mīlēja, uz Pēteri saka: “Tas ir Tas Kungs!” Tad Pēteris dzirdēdams, ka Tas esot Tas Kungs, drēbi apvilka (jo viņš bija noģērbies) un iemetās jūrā.
Yule mwanafunzi aliyependwa na Yesu akamwambia Petro, “Huyu ni Bwana!” Simoni Petro aliposikia haya, akajifunga nguo yake kwa kuwa alikuwa uchi, naye akajitosa baharini.
8 Bet tie citi mācekļi nāca ar laivu, jo tie nebija tālu no malas, bet pie divsimt olekšu nost, un vilka to tīklu ar tām zivīm.
Wale wanafunzi wengine wakaja kwa ile mashua huku wakikokota ule wavu uliyojaa samaki, maana hawakuwa mbali na nchi kavu, ilikuwa yapata dhiraa 200
9 Kad tie nu izkāpa pie malas, tad tie redzēja ogles liktas un zivis uz tām un maizi.
Walipofika ufuoni, wakaona moto wa makaa na samaki wakiokwa juu yake na mikate.
10 Jēzus uz tiem saka: “Atnesiet šurp no tām zivīm, ko jūs tagad esat dabūjuši.”
Yesu akawaambia, “Leteni baadhi ya hao samaki mliovua sasa hivi.”
11 Sīmanis Pēteris iekāpa un to tīklu izvilka malā pilnu ar lielām zivīm, pusotru simts un trīs. Un jebšu to tik daudz bija, tomēr tas tīkls nesaplīsa.
Simoni Petro akapanda kwenye mashua na kuukokota ule wavu pwani. Ulikuwa umejaa samaki wakubwa 153. Ingawa samaki walikuwa wengi kiasi hicho, ule wavu haukuchanika.
12 Jēzus uz tiem saka: “Nāciet un turiet azaidu.” Bet neviens no tiem mācekļiem nedrīkstēja Viņam jautāt, kas Tu esi? Jo tie gan zināja, ka Viņš bija Tas Kungs.
Yesu akawaambia, “Njooni mpate kifungua kinywa.” Hakuna hata mmoja wa wanafunzi aliyethubutu kumuuliza, “Wewe ni nani?” Kwa sababu walijua ya kuwa ni Bwana.
13 Tad Jēzus nāk un to maizi ņem un tiem to dod, tā arī no tām zivīm.
Yesu akaja, akachukua ule mkate, akawapa na vivyo hivyo akawagawia pia wale samaki.
14 Šī nu trešā reize, ka Jēzus Saviem mācekļiem parādījies pēc Savas augšām celšanās no miroņiem.
Hii ilikuwa mara ya tatu Yesu kuwatokea wanafunzi wake baada yake kufufuliwa kutoka kwa wafu.
15 Kad tie nu to azaidu bija noturējuši, tad Jēzus uz Sīmani Pēteri saka: “Sīmani, Jonas dēls, vai tu Mani vairāk mīli nekā šie?” Tas uz Viņu saka: “Tiešām, Kungs, Tu zini, ka es Tevi mīlēju.” Viņš uz to saka: “Gani Manus jērus!”
Walipokwisha kula, Yesu akamuuliza Simoni Petro, “Je, Simoni mwana wa Yohana, unanipenda kweli kuliko hawa?” Yeye akamjibu, “Ndiyo Bwana, wewe unajua ya kuwa ninakupenda.” Yesu akamwambia, “Lisha wana-kondoo wangu.”
16 Atkal otru reiz Viņš uz to saka: “Sīmani, Jonas dēls, vai tu Mani mīli?” Tas uz Viņu saka: “Tiešām, Kungs, Tu zini, ka es Tevi mīlēju.” Viņš uz to saka: “Gani Manas avis!”
Yesu akamwambia tena, “Simoni, mwana wa Yohana, wanipenda?” Petro akamjibu, “Ndiyo Bwana, wewe unajua ya kuwa ninakupenda.” Yesu akamwambia, “Chunga kondoo zangu.”
17 Trešo reiz Viņš uz to saka: “Sīmani, Jonas dēls, vai tu Mani mīli?” Pēteris noskuma, ka Viņš trešo lāgu uz to sacīja: “Vai tu Mani mīli?” Un sacīja uz Viņu: “Kungs Tu visas lietas zini; Tu zini, ka es Tevi mīlēju.” Jēzus uz to saka: “Gani Manas avis!
Kwa mara ya tatu Yesu akamuuliza Petro, “Simoni mwana wa Yohana, unanipenda?” Petro akahuzunika sana kwa kuwa Yesu alimuuliza mara ya tatu, “Unanipenda?” Akamjibu, “Bwana, wewe unajua yote, unajua ya kuwa ninakupenda.” Yesu akamwambia, “Lisha kondoo wangu.
18 Patiesi, patiesi, Es tev saku: tu, jaunāks būdams, pats esi jozies un esi gājis, kur gribēdams; bet, vecs tapis, tu savas rokas izstiepsi, un cits tevi jozīs un tevi vedīs, kur tu negribi.”
Amin, amin nakuambia, ulipokuwa kijana ulivaa na kwenda unakotaka, lakini utakapokuwa mzee utanyoosha mikono yako na mtu mwingine atakuvika na kukupeleka usipotaka kwenda.”
19 Bet to Viņš sacīja, gribēdams rādīt, ar kādu nāvi tam bija Dievu godāt. Un to runājis Viņš uz to saka: “Nāc Man pakaļ!”
Yesu alisema haya ili kuashiria ni kifo cha aina gani Petro atakachomtukuza nacho Mungu. Kisha Yesu akamwambia Petro, “Nifuate!”
20 Un Pēteris apgriezies redz to mācekli, ko Jēzus mīlēja, pakaļ nākam, kas arī pie tā vakariņa pie Viņa krūtīm bija gulējis un sacījis: Kungs, kurš ir tas, kas Tevi nodos?
Petro akageuka, akamwona yule mwanafunzi aliyependwa na Yesu akiwafuata. (Huyu ndiye yule mwanafunzi aliyeegama kifuani mwa Yesu walipokula naye chakula cha mwisho na kuuliza, “Bwana, ni nani atakayekusaliti?”)
21 Kad Pēteris to redzēja, tad viņš saka uz Jēzu: “Kungs, kas tad būs ar šo?”
Petro alipomwona huyo mwanafunzi, akamuuliza Yesu, “Bwana na huyu je?”
22 Jēzus uz to saka: “Ja Es gribu, ka šis paliek, kamēr Es nāku, kas tev par to? Nāc tu Man pakaļ!”
Yesu akamjibu, “Ikiwa nataka aishi mpaka nitakaporudi, inakuhusu nini? Wewe inakupasa unifuate!”
23 Tad šī valoda cēlās starp tiem brāļiem: “Šis māceklis nemirs.” Bet Jēzus viņam nebija sacījis, ka viņš nemirs, bet: “Ja Es gribu, ka viņš paliek, kamēr Es nāku, kas tev par to?”
Kwa sababu ya maneno haya ya Yesu, uvumi ukaenea miongoni mwa ndugu kwamba huyu mwanafunzi hangekufa. Lakini Yesu hakusema kuwa hangekufa. Yeye alisema tu kwamba, “Ikiwa nataka aishi mpaka nitakaporudi, inakuhusu nini?”
24 Šis ir tas māceklis, kas liecību dod par šīm lietām un tās ir sarakstījis; un mēs zinām, ka viņa liecība uzticama.
Huyu ndiye yule mwanafunzi anayeshuhudia mambo haya na ndiye ambaye ameandika habari hizi. Nasi tunajua ya kuwa ushuhuda wake ni kweli.
25 (Un vēl daudz citas lietas Jēzus ir darījis, un ja visas tās pēc kārtas uzrakstītu, tad man šķiet, ka arī visa pasaule tās sarakstītas grāmatas nevarētu saņemt. Āmen.)
Lakini kuna mambo mengine mengi ambayo Yesu alifanya. Kama yote yangeliandikwa, nadhani hata ulimwengu wote usingekuwa na nafasi ya kutosha kuweka vitabu vyote ambavyo vingeandikwa. Amen.