< Ījaba 5 >

1 Sauc jel, vai būs kāds, kas tev atbild? Un pie kura no svētiem tu gribi griezties?
“Ita kama unataka, lakini ni nani atakayekujibu? Ni yupi kati ya hao watakatifu utakayemgeukia?
2 Jo sirdēsti nokauj ģeķi, un pārsteigšanās nonāvē nejēgu.
Kuweka uchungu moyoni humuua mpumbavu, nao wivu humchinja mjinga.
3 Es redzēju ģeķi iesakņotu, bet piepeši nolādēju viņa namu.
Mimi mwenyewe nimemwona mpumbavu akistawi, lakini ghafula nyumba yake ikawa imelaaniwa.
4 Viņa bērni palika tālu no pestīšanas un tapa satriekti vārtos, un nebija glābēja.
Watoto wake wako mbali na usalama, hushindwa mahakamani bila mtetezi.
5 Viņa pļāvumu ēda izsalkuši, un pat no ērkšķu vidus to lasīja, un laupītāji aprija viņa padomu.
Wenye njaa huyala mavuno yake, wakiyatoa hata katikati ya miiba, nao wenye kiu huitamani sana mali yake.
6 Jo no pīšļiem neizaug nelaime, un no zemes neizplaukst grūtums.
Kwa maana taabu haioti kutoka kwenye udongo, wala udhia hauchipui kutoka ardhini.
7 Bet cilvēks uz grūtumu piedzimst, kā dzirksteles no oglēm paceļas skraidīt.
Lakini mwanadamu huzaliwa ili kutaabika, kwa hakika kama cheche za moto zirukavyo kuelekea juu.
8 Bet es meklētu to stipro Dievu un Dievam pavēlētu savas lietas.
“Lakini ingekuwa ni mimi, ningemlalamikia Mungu, ningeliweka shauri langu mbele zake.
9 Viņš dara lielas lietas, kas nav izprotamas, un brīnumus, ko nevar skaitīt.
Yeye hutenda maajabu yasiyoweza kutambuliwa, miujiza isiyoweza kuhesabika.
10 Viņš dod lietu virs zemes un ūdenim liek nākt pār druvām.
Yeye huipa nchi mvua, huyapeleka maji kunyesha mashamba.
11 Zemos Viņš liek augstā vietā, un bēdīgie tiek celti laimē.
Huwainua juu wanyonge, nao wale waombolezao huinuliwa wakawa salama.
12 Viņš iznīcina viltniekiem padomu, ka viņu rokas nekā derīga nevar padarīt.
Huipinga mipango ya wenye hila, ili mikono yao isifikie ufanisi.
13 Viņš satver gudros viņu viltībā, un netikliem padoms ātri krīt.
Yeye huwanasa wenye hekima katika hila yao, nayo mipango ya wadanganyifu huifagilia mbali.
14 Pa dienu tie skraida tumsā, un dienas vidū tie grābstās kā naktī.
Giza huwapata wakati wa mchana; wakati wa adhuhuri hupapasa kama vile usiku.
15 Bet Viņš izglābj no zobena, no viņu mutes, un to bēdīgo no varenā rokas.
Humwokoa mhitaji kutokana na upanga ulioko kinywani mwao; huwaokoa kutokana na makucha ya wenye nguvu.
16 Tā nabagam nāk cerība, bet blēdībai būs turēt muti.
Kwa hiyo maskini analo tarajio, nao udhalimu hufumba kinywa chake.
17 Redzi, svētīgs tas cilvēks, ko Dievs pārmāca, tāpēc neņem par ļaunu tā Visuvarenā pārmācību.
“Heri mtu yule ambaye Mungu humrudi; kwa hiyo usidharau adhabu yake Mwenyezi.
18 Jo Viņš ievaino un atkal sasien, Viņš sadauza, un Viņa roka dziedina.
Kwa kuwa hutia jeraha, lakini pia huyafunga; huumiza, lakini mikono yake pia huponya.
19 Sešās bēdās Viņš tevi izglābs, un septītā tevi ļaunums neaizskars.
Kutoka majanga sita atakuokoa; naam, hata katika saba hakuna dhara litakalokupata wewe.
20 Bada laikā Viņš tevi izpestīs no nāves, un kara laikā no zobena cirtieniem.
Wakati wa njaa atakukomboa wewe na kifo, naye katika vita atakukomboa na pigo la upanga.
21 No ļaunām mēlēm tu tapsi paglābts, un nebīsies no posta, kad tas nāks.
Utalindwa kutokana na kichapo cha ulimi, wala hutakuwa na sababu ya kuogopa maangamizi yatakapokujia.
22 Postīšanā un badā tu smiesies, un no zemes zvēriem tu nebīsies.
Utayacheka maangamizo na njaa, wala hutakuwa na sababu ya kuwaogopa wanyama wakali wa mwituni.
23 Jo tev būs derība ar akmeņiem tīrumā, un zvēri laukā turēs ar tevi mieru.
Kwa kuwa utakuwa na agano na mawe ya mashamba, nao wanyama wa mwitu watakuwa na amani nawe.
24 Un tu samanīsi, ka tavs dzīvoklis mierā, un apraudzīsi savu namu un trūkuma nebūs.
Utajua ya kwamba hema lako li salama; utahesabu mali zako wala hutakuta chochote kilichopungua.
25 Un tu samanīsi, ka tava dzimuma būs daudz, un tavi pēcnākamie kā zāle virs zemes.
Utajua ya kuwa watoto wako watakuwa wengi, nao wazao wako wengi kama majani ya nchi.
26 Vecumā tu iesi kapā, tā kā kūlīšus ieved savā laikā.
Utaingia kaburini ukiwa na umri wa uzee mtimilifu, kama masuke ya ngano yakusanywapo kwa wakati wake.
27 Redzi, to mēs esam izmeklējuši, tā tas ir; klausi tu un ņem to labi vērā.
“Tumelichunguza hili, nalo ni kweli. Hivyo lisikie na ulitendee kazi.”

< Ījaba 5 >