< Jesajas 7 >
1 Un notikās Ahaza, Jūda ķēniņa, dienās, - tas bija Uzijas dēla Jotama dēls, - ka Recins, Sīrijas ķēniņš, un Pekas, Remalijas dēls, Israēla ķēniņš, uz Jeruzālemi cēlās, pret viņu karot, bet karodami pret viņu tie nekā neiespēja.
Wakati Ahazi mwana wa Yothamu, mwana wa Uzia, alipokuwa mfalme wa Yuda, Mfalme Resini wa Aramu, na Peka mwana wa Remalia mfalme wa Israeli walipanda kupigana dhidi ya Yerusalemu, lakini hawakuweza kuushinda.
2 Un Dāvida namam teica un sacīja: Sīrieši apmetušies pret Efraīmu. Tad viņa sirds un viņa ļaužu sirds drebēja, tā kā meža koki dreb no vēja.
Wakati huu nyumba ya Daudi iliambiwa, “Aramu wameungana na Efraimu.” Kwa hiyo mioyo ya Ahazi na watu wake ilitikiswa, kama miti ya msituni inavyotikiswa na upepo.
3 Un Tas Kungs sacīja uz Jesaju: izej jel Ahazam pretī, tu un tavs dēls ŠearJašubs, augšēja dīķa grāvja galā, ceļmalā, pie vadmalnieku tīruma,
Ndipo Bwana akamwambia Isaya, “Toka uende, wewe na mwanao Shear-Yashubu, mkutane na Ahazi huko mwisho wa mfereji wa Bwawa la Juu, kwenye barabara iendayo Shamba la Dobi.
4 Un saki uz viņu: sargies un esi klusu, nebīsties, un lai tava sirds nebaiļojās no šiem diviem kūpošiem prauliem, no Recina un Sīriešu un Remalijas dēla karstām dusmām.
Mwambie, ‘Uwe mwangalifu, utulie na usiogope. Usife moyo kwa ajili ya watu hawa wawili walio kama visiki vya kuni vifukavyo moshi, kwa ajili ya hasira kali ya Resini na Aramu na ya mwana wa Remalia.
5 Tādēļ ka Sīrieši pret tevi ļaunu sadomājuši ar Efraīmu un Remalijas dēlu sacīdami:
Aramu, Efraimu na mwana wa Remalia wamepanga shauri baya ili wakuangamize, wakisema,
6 Celsimies pret Jūdu un izbiedēsim to un uzņemsim to un celsim tur Tabeala dēlu par ķēniņu; -
“Tuishambulie Yuda, naam, tuirarue vipande vipande na kuigawa miongoni mwetu, na kumtawaza mwana wa Tabeeli awe mfalme juu yake.”
7 Tā saka Tas Kungs Dievs: tas nenotiks un nebūs.
Lakini Bwana Mwenyezi asema hivi: “‘Jambo hili halitatendeka, halitatokea,
8 Bet Damaskus būs Sīrijas galva, un Recins Damaskus galva, un vēl būs sešdesmit pieci gadi, tad Efraīms taps satriekts, ka vairs nebūs tauta.
kwa kuwa kichwa cha Aramu ni Dameski, na kichwa cha Dameski ni Resini peke yake. Katika muda wa miaka sitini na mitano, Efraimu atakuwa ameharibiwa kiasi kwamba hataweza tena kuwa taifa.
9 Un Samarija būs Efraīma galva, un Remalijas dēls Samarijas galva. Ja neticēsiet, tad nepastāvēsiet.
Kichwa cha Efraimu ni Samaria, na kichwa cha Samaria ni mwana wa Remalia peke yake. Kama hamtasimama thabiti katika imani yenu, hamtaimarika kamwe.’”
10 Un Tas Kungs runāja vēl uz Ahazu un sacīja:
Bwana akasema na Ahazi tena,
11 Prasies kādu zīmi no Tā Kunga, sava Dieva, prasi to, vai dziļi dziļumā vai augsti augstumā! (Sheol )
“Mwombe Bwana Mungu wako ishara, iwe kwenye vina virefu sana, au kwenye vimo virefu sana.” (Sheol )
12 Tad Ahazs sacīja: es neprasīšu, es arī To Kungu nekārdināšu.
Lakini Ahazi akasema, “Sitaomba; sitamjaribu Bwana.”
13 Tad viņš sacīja: klausiet jel, jūs no Dāvida nama, vai tas jums vēl maz, kaitināt cilvēkus, ka nu arī kaitinājiet manu Dievu?
Ndipo Isaya akasema, “Sikia sasa, ewe nyumba ya Daudi! Je, haitoshi kujaribu uvumilivu wa wanadamu? Je, mtaujaribu uvumilivu wa Mungu wangu pia?
14 Tādēļ Tas Kungs pats jums dos zīmi: redzi, jumprava būs grūta un dzemdēs dēlu un nosauks viņa vārdu Immanuel (Dievs ar mums).
Kwa hiyo Bwana mwenyewe atawapa ishara: Bikira atachukua mimba, naye atamzaa mwana, na ataitwa Imanueli.
15 Sviestu un medu viņš ēdīs, kad viņš zin ļaunu atmest un labu uzņemt.
Atakula jibini na asali atakapokuwa ameweza kukataa mabaya na kuchagua mema.
16 Jo pirms tas puisītis zin ļaunu atmest un labu uzņemt, zeme būs izpostīta, no kuras diviem ķēniņiem tev bailes.
Lakini kabla mtoto hajajua kukataa mabaya na kuchagua mema, nchi ya wafalme hao wawili unaowaogopa itafanywa ukiwa.
17 Un Tas Kungs atvedīs pār tevi un pār taviem ļaudīm un pār tavu tēva namu dienas, kādas nav nākušas no tā brīža, kamēr Efraīms no Jūda ir atkāpies, proti Asīrijas ķēniņu.
Bwana ataleta juu yako, juu ya watu wako, na juu ya nyumba ya baba yako wakati ambao haujawahi kuwako tangu Efraimu alipojitenga na Yuda: yeye atawaleteeni mfalme wa Ashuru.”
18 Jo tai dienā Tas Kungs pasvilps tām mušām, kas ir Ēģiptes upju galā, un to biti, kas Asīrijas zemē.
Katika siku ile Bwana atawapigia filimbi mainzi kutoka vijito vya mbali vya Misri, na nyuki kutoka nchi ya Ashuru.
19 Un tie nāks un apmetīsies visi dziļās ielejās un kalnu gravās un visos ērkšķu krūmos un visās ganībās.
Wote watakuja na kukaa kwenye mabonde yenye miteremko, na kwenye nyufa za miamba, kwenye vichaka vyote vyenye miiba, na kwenye mashimo yote ya maji.
20 Tai dienā Tas Kungs ar derētu dzenamu nazi, kas viņpus upes, caur Asīrijas ķēniņu, nodzīs galvu un kāju matus, ir visu bārdu Viņš nodzīs.
Katika siku ile Bwana atatumia wembe ulioajiriwa kutoka ngʼambo ya Mto, yaani mfalme wa Ashuru, kunyoa nywele za kichwa chako na malaika ya miguu yako, na kuziondoa ndevu zako pia.
21 Un tai dienā cilvēks turēs kādu gotiņu un kādas divas aitiņas.
Katika siku ile, mtu atahifadhi hai ndama mmoja na kondoo wawili.
22 Un tie tik daudz piena dos, ka tas sviestu ēdīs, jo ikkatrs, kas tai zemē atliks, tas ēdīs sviestu un medu.
Kwa ajili ya wingi wa maziwa watakayotoa, atapata jibini ya kula. Wote watakaobakia katika nchi watakula jibini na asali.
23 Un tai dienā notiks, ka ikkatrā vietā, kur bijuši tūkstoš vīna koki, kas maksāja tūkstoš sudraba gabalus, tur būs ērkšķi un krūmi,
Katika siku ile, kila mahali palipokuwa na mizabibu elfu moja yenye thamani ya shekeli 1,000 za fedha, patakuwa na michongoma na miiba tu.
24 Ka ar bultām un stopiem tur būs jāiet, jo visa tā zeme būs ērkšķi un krūmi.
Watu watakwenda huko wakiwa na upinde na mshale, kwa maana nchi itafunikwa na michongoma na miiba.
25 Un uz visiem tiem kalniem, ko citkārt apkapāja ar kapļiem, tur tu neiesi, bīdamies no ērkšķiem un krūmiem, bet lieli lopi tur staigās, un sīki lopi tos mīdīs.
Kuhusu vilima vyote vilivyokuwa vikilimwa kwa jembe, hamtakwenda huko tena kwa ajili ya hofu ya michongoma na miiba. Patakuwa mahali ambapo ngʼombe wataachiwa huru, na kondoo kukimbia kimbia.