< Jesajas 10 >

1 Ak vai, tiem, kas ceļ netaisnus likumus, un tiem rakstītājiem, kas raksta grūtu tiesu,
Ole wao wawekao sheria zisizo za haki, kwa wale watoao amri za kuonea,
2 Ka nabagiem tiesu neizdod un tiesu laupa tiem bēdīgiem starp Maniem ļaudīm, ka atraitnes aplaupa un bāriņus posta!
kuwanyima maskini haki zao na kuzuilia haki za watu wangu walioonewa, kuwafanya wajane mawindo yao na kuwanyangʼanya yatima.
3 Bet ko jūs darīsiet piemeklēšanas dienā un tai postā, kas nāk no tālienes? Pie kā bēgsiet pēc palīdzības, un kur glabāsiet savu godību?
Mtafanya nini siku ya kutoa hesabu, wakati maafa yatakapokuja kutoka mbali? Mtamkimbilia nani awape msaada? Mtaacha wapi mali zenu?
4 Bet jūs locīsities starp gūstītiem un kritīsiet starp nokautiem. Ar visu to Viņa dusmība nenovēršas, un Viņa roka vēl ir izstiepta.
Hakutasalia kitu chochote, isipokuwa kujikunyata miongoni mwa mateka, au kuanguka miongoni mwa waliouawa. Hata kwa haya yote, hasira yake haijageukia mbali, mkono wake bado umeinuliwa juu.
5 Ak vai, Asuram! Tas ir Manas dusmības rīkste, un viņa rokā Manas bardzības zizlis.
“Ole kwa Ashuru, fimbo ya hasira yangu, ambaye mkononi mwake ana rungu ya ghadhabu yangu!
6 Es viņu sūtu pret viltīgiem ļaudīm un viņam pavēlu pret ļaudīm, par kuriem Es apskaities, lai viņš tos laupīdams laupa un postīdams posta, un tos samin kā dubļus uz ielām.
Ninamtuma dhidi ya taifa lisilomjua Mungu, ninamtuma dhidi ya taifa linalonikasirisha, kukamata mateka na kunyakua nyara, pia kuwakanyaga chini kama matope ya barabarani.
7 Bet viņam tā nešķiet, un viņa sirds tā nedomā; jo viņš apņēmies izdeldēt un izsakņot daudz tautas.
Lakini hili silo analokusudia, hili silo alilo nalo akilini; kusudi lake ni kuangamiza, kuyakomesha mataifa mengi.
8 Jo viņš saka: vai mani virsnieki visi kopā nav ķēniņi?
Maana asema, ‘Je, wafalme wote si majemadari wangu?
9 Vai Kalno nav kā Karķemis? Vai Hamata nav kā Arvada? Vai Samarija nav kā Damaskus?
Je, Kalno hakutendwa kama Karkemishi? Hamathi si kama Arpadi, nayo Samaria si kama Dameski?
10 Tā kā mana roka dabūjusi tās elku dievu valstis, jebšu viņu dievekļu bija vairāk nekā to, kas Jeruzālemē un Samarijā, -
Kama vile mkono wangu ulivyotwaa falme za sanamu, falme ambazo vinyago vyao vilizidi vile vya Yerusalemu na Samaria:
11 Vai es nevarētu darīt pie Jeruzālemes un pie viņas elkiem tāpat, kā esmu darījis pie Samarijas un viņas elkiem?
je, nisiishughulikie Yerusalemu na sanamu zake kama nilivyoshughulikia Samaria na vinyago vyake?’”
12 Bet kad Tas Kungs visu Savu darbu būs pabeidzis Ciānas kalnā un Jeruzālemē, tad (sacīs): Es piemeklēšu to sirds lepnības augli pie Asīrijas ķēniņa un viņa acu augsto greznību.
Bwana atakapokuwa amemaliza kazi yake yote dhidi ya Mlima Sayuni na Yerusalemu, atasema, “Nitamwadhibu mfalme wa Ashuru kwa ajili ya majivuno ya ukaidi wa moyo wake na kutazama kwa macho yenye dharau.”
13 Jo tas saka: caur savas rokas spēku es to esmu darījis un caur savu gudrību, jo es esmu prātīgs. Es esmu atņēmis tautu robežas un laupījis viņu mantas un kā varonis zemē gāzis valdniekus.
Kwa kuwa anasema: “‘Kwa nguvu za mkono wangu nimefanya hili, kwa hekima yangu, kwa sababu nina ufahamu. Niliondoa mipaka ya mataifa, niliteka nyara hazina zao, kama yeye aliye shujaa niliwatiisha wafalme wao.
14 Un mana roka atradusi tautu bagātību kā ligzdu, un es esmu sagrābis visu pasauli, kā sagrābj atstātas olas, un neviens nav bijis, kas spārnu būtu kustinājis vai muti atdarījis vai pīkstējis.
Kama mtu atiavyo mkono kwenye kiota, ndivyo mkono wangu ulivyochukua utajiri wa mataifa; kama watu wakusanyavyo mayai yaliyoachwa, ndivyo nilivyokusanya nchi zote; wala hakuna hata mmoja aliyepiga bawa au kufungua kinywa chake kutoa mlio.’”
15 Vai tad cirvis lai lielās pret to, kas ar to cērt? Jeb vai zāģis lai turas pretī tam, kas to velk! tā kā zizlis to turētu, kas viņu paceļ, tā kā rīkste to cilātu, kas nav koks!
Je, shoka laweza kujigamba kuwa na nguvu zaidi kuliko yule anayelitumia, au msumeno kujisifu dhidi ya yule anayeutumia? Ni kana kwamba fimbo ingeweza kumwinua yeye aichukuaye, au mkongojo ungemwinua mwenye kuutumia!
16 Tādēļ Tas Kungs Dievs Cebaot sūtīs diloni starp viņa (Asura) trekniem, un apakš viņa godības dedzin degs, kā uguns deg.
Kwa hiyo Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, atatuma ugonjwa wa kudhoofisha kwa askari wake walio hodari, katika fahari yake moto utawaka kama mwali wa moto.
17 Un Israēla gaišums būs uguns, un viņa Svētais būs liesma, kas sadedzinās un norīs viņa ērkšķus un dadžus vienā dienā.
Nuru ya Israeli itakuwa moto, Aliye Mtakatifu wao mwali wa moto; katika siku moja utaunguza na kuteketeza miiba na michongoma yake.
18 Un viņš aprīs viņa meža un viņa dārza godību, līdz ar dvēseli un miesu, un tas novārgs kā vārgulis.
Fahari ya misitu yake na mashamba yenye rutuba utateketeza kabisa, kama vile mtu mgonjwa adhoofikavyo.
19 Un viņa meža atlikušie koki būs mazs pulciņš, ka zēns tos varētu sarakstīt.
Nayo miti inayobaki katika misitu yake itakuwa michache sana hata mtoto mdogo angeweza kuihesabu.
20 Tanī dienā Israēla atlikušie, un Jēkaba nama izglābtie nepaļausies vairs uz to, kas viņu sitis, bet uzticībā paļausies uz To Kungu, to Svēto iekš Israēla.
Katika siku ile, mabaki ya Israeli, walionusurika wa nyumba ya Yakobo, hawatamtegemea tena yeye aliyewapiga, lakini watamtegemea kwa kweli Bwana Aliye Mtakatifu wa Israeli.
21 Tie atlikušie atgriezīsies, Jēkaba atlikušie, pie tā visuvarenā Dieva.
Mabaki watarudi, mabaki wa Yakobo watamrudia Mungu Mwenye Nguvu.
22 Jo jebšu tavi ļaudis, Israēl, ir kā jūras smiltis, tomēr (tikai) viņu atlikums atgriezīsies. Jo gals ir nospriests pilnīgā taisnībā.
Ingawa watu wako, ee Israeli, ni wengi kama mchanga wa pwani, ni mabaki yao tu watakaorudi. Maangamizi yamekwisha amriwa, ni mengi tena ni haki.
23 Jo Tas Kungs Dievs Cebaot nolikto gala spriedumu izdarīs pa visu zemes virsu.
Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, atatekeleza maangamizi yaliyoamriwa juu ya nchi yote.
24 Tāpēc Tas Kungs Dievs Cebaot saka tā: Mani ļaudis, kas dzīvojat Ciānā, nebīstaties no Asura, kad tas jūs sit ar rīksti, un savu zizli paceļ pret jums, kā notika Ēģiptē.
Kwa hiyo, hili ndilo Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: “Enyi watu wangu mkaao Sayuni, msiwaogope Waashuru, wanaowapiga ninyi kwa fimbo na kuinua rungu dhidi yenu, kama Misri ilivyofanya.
25 Jo vēl mazs brīdis, tad dusmība būs pagalam, un Mana bardzība tos izdeldēs.
Bado kitambo kidogo sana hasira yangu dhidi yenu itakoma, na ghadhabu yangu itaelekezwa kwenye maangamizi yao.”
26 Jo Tas Kungs Cebaot pacels pātagu pret to, kā Viņš sita Midijanu pie Horeba kalna, un Ciņa zizlis ir pār jūru un viņš to paceļ kā Ēģiptes zemē.
Bwana Mwenye Nguvu Zote atawachapa kwa mjeledi, kama alivyowapiga Wamidiani katika mwamba wa Orebu, naye atainua fimbo yake juu ya maji, kama alivyofanya huko Misri.
27 Un tai dienā viņa nasta atstāsies no tava kamieša un viņa jūgs no tava kakla, un tas jūgs šķīdīs no treknuma.
Katika siku hiyo mzigo wao utainuliwa kutoka mabegani mwenu, na nira yao kutoka shingoni mwenu; nira itavunjwa kwa sababu ya kutiwa mafuta.
28 Tas nāk uz Ajatu, tas iet caur Migronu, Mikmasā tas atstāj savas lietas.
Wanaingia Ayathi, wanapita katikati ya Migroni, wanahifadhi mahitaji huko Mikmashi.
29 Tie iet caur šaurumu, Ģebā tie paliek par nakti, Rāma dreb, Saula Ģibeja bēg.
Wanavuka kivukoni, nao wanasema, “Tutapiga kambi huko Geba usiku kucha.” Rama inatetemeka; Gibea ya Sauli inakimbia.
30 Kliedz stiprā balsī, Galima meita! Klausies, Laīša! nabaga Anatota!
Piga kelele, ee Binti Galimu! Sikiliza, ee Laisha! Maskini Anathothi!
31 Madmena bēg, Ģebimas iedzīvotāji glābjās.
Madmena inakimbia; watu wa Gebimu wanajificha.
32 Vēl šodien tas apmetīsies Nobā, pacels roku pret Ciānas meitas kalnu, pret Jeruzālemes pakalnu.
Siku hii ya leo watasimama Nobu; watatikisa ngumi zao kwa mlima wa Binti Sayuni, kwa kilima cha Yerusalemu.
33 Redzi, Tas Kungs Dievs Cebaot nokapā tos zarus ar briesmīgu varu, un tie, kas ir augsti augumā, top nocirsti, un tie lielie pazemoti.
Tazama, Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, atayakata matawi kwa nguvu kuu. Miti mirefu sana itaangushwa, ile mirefu itashushwa chini.
34 Un Viņš nocērt ar dzelzi biezos meža krūmus, un Lībanus krīt caur vareno.
Atakata vichaka vya msitu kwa shoka; Lebanoni itaanguka mbele zake yeye Mwenye Nguvu.

< Jesajas 10 >