< Hozejas 10 >

1 Israēls ir kupls vīna koks, kas nes augļus; jo vairāk bija viņa augļu, jo vairāk viņš cēla altāru; jo labāka viņa zeme, jo labāki viņš iztaisīja elku stabus.
Israeli alikuwa mzabibu uliostawi sana, alijizalia matunda mwenyewe. Kadiri matunda yake yalivyoongezeka, alijenga madhabahu zaidi; kadiri nchi yake ilivyostawi, alipamba mawe yake ya ibada.
2 Viņu sirds ir viltīga; nu tiks atmaksāts. Viņš salauzīs viņu altārus, postīs viņu elku stabus.
Moyo wao ni mdanganyifu, nao sasa lazima wachukue hatia yao. Bwana atabomoa madhabahu zao na kuharibu mawe yao ya ibada.
3 Nu tie sacīs: ķēniņa mums nav, jo mēs To Kungu neesam bijušies; ko mums ķēniņš var darīt?
Kisha watasema, “Hatuna mfalme kwa sababu hatukumheshimu Bwana. Lakini hata kama tungelikuwa na mfalme, angeweza kutufanyia nini?”
4 Tie runāja vārdus, nepatiesi zvērēdami un derības derēdami, tāpēc sodība zaļos kā nāves zāle uz tīruma vagām.
Wanaweka ahadi nyingi, huapa viapo vya uongo wanapofanya mapatano; kwa hiyo mashtaka huchipuka kama magugu ya sumu katika shamba lililolimwa.
5 Samarijas iedzīvotāji iztrūcinājās par BetAvenas teļu, viņa ļaudis par to bēdājās un viņa priesteri par to trīc, jo viņa godība no tā aiziet.
Watu wanaoishi Samaria huogopa kwa ajili ya sanamu ya ndama ya Beth-Aveni. Watu wake wataiombolezea, vivyo hivyo kuhani wake wa kuabudu sanamu, wale waliokuwa wamefurahia fahari yake, kwa sababu itaondolewa kutoka kwao kwenda uhamishoni.
6 Arī to pašu(elka teļu) vedīs uz Asīriju par dāvanu priekš ķēniņa Jareba; Efraīms paliks kaunā, un Israēls taps apkaunots sava padoma dēļ.
Itachukuliwa kwenda Ashuru kama ushuru kwa mfalme mkuu. Efraimu atafedheheshwa; Israeli ataaibika kwa ajili ya sanamu zake za mti.
7 Samarijas ķēniņš ir izzudis kā putas ūdens virsū.
Samaria na mfalme wake wataelea kama kijiti juu ya uso wa maji.
8 Un Avenas kalni, kur Israēls apgrēkojās, taps izdeldēti, ērkšķi un dadži augs uz viņu altāriem, un tie sacīs uz tiem kalniem: apklājiet mūs! - un uz tiem pakalniem: krītiet pār mums!
Mahali pa kuabudia sanamu pa uovu pataharibiwa: ndiyo dhambi ya Israeli. Miiba na mibaruti itaota na kufunika madhabahu zao. Kisha wataiambia milima, “Tufunikeni!” na vilima, “Tuangukieni!”
9 No Ģibejas dienām tu esi grēkojis, Israēl: tur tie pastāvējuši; tā kauja Ģibejā pret tiem negantības bērniem tos neaizņēma.
“Tangu siku za Gibea, mmetenda dhambi, ee Israeli, huko ndiko mlikobaki. Je, vita havikuwapata watenda mabaya huko Gibea?
10 Pēc Sava prāta Es tos pārmācīšu, un tautas pret tiem sapulcināsies, kad Es tos sodīšu viņu divēju grēku dēļ.
Wakati nitakapopenda, nitawaadhibu; mataifa yatakusanywa dhidi yao ili kuwaweka katika vifungo kwa ajili ya dhambi zao mbili.
11 Jo Efraīms ir teļš, ieradis labprāt kult, bet Es nākšu par viņa kakla skaistumu, Es Efraīmu iejūgšu, Jūda ars, un Jēkabs ecēs.
Efraimu ni mtamba wa ngʼombe aliyefundishwa ambaye hupenda kupura, hivyo nitamfunga nira juu ya shingo yake nzuri. Nitamwendesha Efraimu, Yuda lazima alime, naye Yakobo lazima avunjavunje mabonge ya udongo.
12 Sējiet sev pēc taisnības, pļaujiet pēc žēlastības, plēsiet sev jaunu zemi, jo laiks ir, To Kungu meklēt, tiekams tas nāk un jums māca taisnību.
Jipandieni wenyewe haki, vuneni matunda ya upendo usio na kikomo, vunjeni ardhi yenu isiyolimwa; kwa kuwa ni wakati wa kumtafuta Bwana, mpaka atakapokuja na kuwanyeshea juu yenu haki.
13 Jūs arat bezdievību, ļaunumu jūs pļaujat un ēdat melu augļus.
Lakini mmepanda uovu, mkavuna ubaya, mmekula tunda la udanganyifu. Kwa sababu mmetegemea nguvu zenu wenyewe na wingi wa mashujaa wenu,
14 Jo tu paļaujies uz savu ceļu, uz savu varoņu pulku. Tāpēc liels troksnis celsies pret taviem ļaudīm, un visas tavas stiprās vietas taps postītas, tā kā Zalmans BetArbeli postīja kara laikā, kur māte līdz ar bērniem tapa satriekta.
mngurumo wa vita utainuka dhidi ya watu wako, ili kwamba ngome zako zote zitaharibiwa: kama Shalmani alivyoharibu Beth-Arbeli katika siku ile ya vita, wakati mama pamoja na watoto wao walipotupwa kwa nguvu ardhini.
15 Tāpat jums notiks caur Bēteli jūsu niknās blēdības dēļ; Israēla ķēniņš dienai austot nīcin iznīks.
Ndivyo itakavyotokea kwako, ee Betheli, kwa sababu uovu wako ni mkuu. Siku ile itakapopambazuka, mfalme wa Israeli ataharibiwa kabisa.

< Hozejas 10 >