< Vēstule Ebrējiem 7 >

1 Jo šis Melhizedeks bija Salemes ķēniņš, Dieva tā visu augstākā priesteris, kas Ābrahāmam, kad tas pārnāca no tās ķēniņu kaušanas, gāja pretī un viņu svētīja;
Melkisedeki alikuwa mfalme wa Salemu, na kuhani wa Mungu Mkuu. Abrahamu alipokuwa anarudi kutoka vitani ambako aliwaua wafalme, Melkisedeki alikutana naye akambariki,
2 Tam Ābrahāms arī deva to desmito tiesu no visa. Tas pirmā kārtā top tulkots: taisnības ķēniņš, - bet tad arīdzan: Salemes ķēniņš, tas ir, miera ķēniņš;
naye Abrahamu akampa sehemu ya kumi ya vitu vyote alivyokuwa navyo. (Maana ya kwanza ya jina hili Melkisedeki ni “Mfalme wa Uadilifu”; na, kwa vile yeye alikuwa mfalme wa Salemu, jina lake pia lina maana ya “Mfalme wa Amani.”)
3 Bez tēva, bez mātes, bez radu raksta; kam nav nedz dienu iesākuma, nedz dzīvības gala, bet Dieva Dēlam līdzināts viņš paliek priesteris mūžam.
Baba yake na mama yake hawatajwi, wala ukoo wake hautajwi; haisemwi alizaliwa lini au alikufa lini. Anafanana na Mwana wa Mungu, na anaendelea kuwa kuhani daima.
4 Bet lūkojiet, cik liels šis ir, ka pats Ābrahāms, tas vectēvs, viņam desmito tiesu no tā laupījuma devis.
Basi, mwaona jinsi mtu huyu alivyokuwa maarufu. Baba Abrahamu alimpa sehemu moja ya kumi ya vitu vyote alivyoteka vitani.
5 Un tiem Levja bērniem, kas to svēto amatu dabū, ir gan viens likums, desmito tiesu ņemt no tiem ļaudīm pēc bauslības, tas ir, no saviem brāļiem, jebšu tie cēlušies no Ābrahāma gurniem;
Tunajua vilevile kwamba kufuatana na Sheria, wana wa Lawi ambao ni makuhani, wanayo haki ya kuchukua sehemu ya kumi kutoka kwa watu, yaani ndugu zao, ingawaje nao ni watoto wa Abrahamu.
6 Bet viņš, kas nebija cēlies no viņu cilts, to desmito tiesu ir ņēmis no Ābrahāma un svētījis to, kam tās apsolīšanas bija.
Lakini huyo Melkisedeki hakuwa wa ukoo wa Lawi, hata hivyo alipokea sehemu ya kumi kutoka kwa Abrahamu; tena akambariki yeye ambaye alikuwa amepewa ahadi ya Mungu.
7 Bet nu bez nekādas pretī runāšanas tas mazākais top svētīts no tā lielākā.
Hakuna mashaka hata kidogo kwamba anayebariki ni mkuu zaidi kuliko yule anayebarikiwa.
8 Un še mirstīgi cilvēki ņem to desmito tiesu, bet tur tas, par ko liecība top dota, ka tas dzīvo.
Tena, hao makuhani wanaopokea sehemu ya kumi, ni watu ambao hufa; lakini hapa anayepokea sehemu ya kumi, yaani Melkisedeki, anasemekana kwamba hafi.
9 Un (tā sakot): arī Levi, kas to desmito tiesu ņem, to desmito tiesu ir devis caur Ābrahāmu.
Twaweza, basi, kusema kwamba Abrahamu alipotoa sehemu moja ya kumi, Lawi (ambaye watoto wake hupokea sehemu moja ya kumi) alitoa sehemu moja ya kumi pia.
10 Jo viņš vēl bija tēva gurnos, kad Melhizedeks šim gāja pretī.
Maana Lawi hakuwa amezaliwa bado, bali ni kama alikuwa katika mwili wa baba yake, Abrahamu, wakati Melkisedeki alipokutana naye.
11 Ja tad nu tā pilnība būtu caur to priestera amatu no Levja cilts, (jo līdz ar to tie ļaudis bauslību ir dabūjuši), kam tad vēl vajadzēja citam priesterim celties pēc Melhizedeka kārtas, un netikt sauktam pēc Ārona kārtas?
Kutokana na ukuhani wa Walawi, watu wa Israeli walipewa Sheria. Sasa, kama huduma ya Walawi ingalikuwa kamilifu hapangekuwa tena na haja ya kutokea ukuhani mwingine tofauti, ukuhani ambao umefuata utaratibu wa ukuhani wa Melkisedeki, na si ule wa Aroni.
12 Jo kad priesteru amats tiek pārcelts, tad arīdzan bauslībai jātiek pārceltai.
Maana ukuhani ukibadilika ni lazima Sheria nayo ibadilike.
13 Jo Tas, par ko tas sacīts, piederēja pie citas cilts, no kuras neviens nebija kalpojis pie altāra.
Naye Bwana wetu ambaye mambo hayo yote yanasemwa juu yake, alikuwa wa kabila lingine, na wala hakuna hata mmoja wa kabila lake aliyepata kutumikia madhabahuni akiwa kuhani.
14 Jo tas ir zināms, ka mūsu Kungs cēlies no Jūda cilts un uz šo cilti Mozus neko nav runājis par priesteru amatu.
Inafahamika wazi kwamba yeye alizaliwa katika kabila la Yuda ambalo Mose hakulitaja alipokuwa anasema juu ya makuhani.
15 Un tas vēl jo skaidri ir zināms, ja pēc Melhizedeka līdzības cits priesteris ceļas,
Tena jambo hili ni dhahiri zaidi: kuhani mwingine anayefanana na Melkisedeki amekwisha tokea.
16 Kas tāds tapis ne pēc miesīga likuma bauslības, bet pēc neiznīcīgas dzīvības spēka.
Yeye hakufanywa kuwa kuhani kwa sheria na maagizo ya kibinadamu, bali kwa nguvu ya uhai ambao hauna mwisho.
17 Jo Viņš apliecina: Tu esi priesteris mūžīgi pēc Melhizedeka kārtas. (aiōn g165)
Maana Maandiko yasema: “Wewe ni kuhani milele, kufuatana na utaratibu wa ukuhani wa Melkisedeki.” (aiōn g165)
18 Jo iepriekšēja baušļa atcelšana notiek tāpēc, ka tas nespēcīgs un nederīgs.
Basi, ile amri ya zamani ilifutwa kwa sababu ilikuwa hafifu na isiyofaa kitu.
19 Jo bauslība neko nav darījusi pilnīgu, bet tā labākas cerības ievešana, caur ko mēs tuvu nākam pie Dieva.
Maana Sheria ya Mose haikuweza kukamilisha jambo lolote. Lakini sasa, mahali pake pamewekwa tumaini lililo bora zaidi ambalo kwalo tunaweza kumkaribia Mungu.
20 Un kad tas nav noticis bez zvērēšanas, -
Zaidi ya hayo hapa pana kiapo cha Mungu. Wakati wale wengine walipofanywa makuhani hapakuwako kiapo.
21 (Jo viņi bez zvērēšanas palikuši par priesteriem, bet Šis ar zvērēšanu, caur To, kas uz Viņu saka: Tas Kungs ir zvērējis - un tas Tam nebūs žēl - Tu esi priesteris mūžīgi pēc Melhizedeka kārtas) - (aiōn g165)
Lakini Yesu alifanywa kuhani kwa kiapo wakati Mungu alipomwambia: “Bwana ameapa, wala hataigeuza nia yake: Wewe ni kuhani milele.” (aiōn g165)
22 Tad Jēzus par vienas daudz labākas derības galvinieku ir palicis.
Basi, kutokana na tofauti hii, Yesu amekuwa mdhamini wa agano lililo bora zaidi.
23 Un viņi gan daudzi ir tapuši par priesteriem, tāpēc ka nāve tiem neļāva palikt.
Kuna tofauti nyingine pia: hao makuhani wengine walikuwa wengi kwa sababu walikufa na hawakuweza kuendelea na kazi yao.
24 Bet Šim caur to, ka Viņš mūžīgi paliek, ir neiznīcīgs priestera amats. (aiōn g165)
Lakini Yesu si kama wao, yeye anaishi milele; ukuhani wake hauondoki kwake. (aiōn g165)
25 Tādēļ Viņš arī pilnīgi var izglābt tos, kas caur Viņu pie Dieva nāk, vienmēr dzīvodams, ka Viņš tos aizstāvētu.
Hivyo, yeye anaweza daima kuwaokoa kabisa wote wanaomwendea Mungu kwa njia yake, maana yeye anaishi milele kuwaombea kwa Mungu.
26 Jo tāds augsts priesteris mums arī pienācās, kas ir svēts, nenoziedzīgs, neapgānīts, atšķirts no grēciniekiem un augstāks pār debesīm;
Basi, Yesu ndiye Kuhani Mkuu ambaye anatufaa sana katika mahitaji yetu. Yeye ni mtakatifu, hana hatia wala dhambi ndani yake; hayumo katika kundi la wenye dhambi na ameinuliwa mpaka juu mbinguni.
27 Kam nevajag, tā kā tiem augstiem priesteriem, ikdienas upurus nest papriekš par saviem pašu grēkiem un pēc par tiem ļaužu grēkiem; jo to Viņš ir darījis vien' reiz, kad Viņš pats Sevi upurējis.
Yeye si kama wale makuhani wakuu wengine; hana haja ya kutoa dhabihu kila siku, kwanza kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe, kisha kwa ajili ya dhambi za watu. Yeye alifanya hivyo mara moja tu wakati alipojitoa yeye mwenyewe, na hiyo yatosha kwa nyakati zote.
28 Jo bauslība ieceļ par augstiem priesteriem cilvēkus, kam ir vājība, bet tas zvērēšanas vārds, kas nāca pēc bauslības, tas To Dēlu ieceļ mūžīgi pilnīgu. (aiōn g165)
Sheria ya Mose huwateua watu waliokuwa dhaifu kuwa makuhani wakuu; lakini ahadi ya Mungu aliyoifanya kwa kiapo na ambayo imefika baada ya sheria imemteua Mwana ambaye amefanywa mkamilifu milele. (aiōn g165)

< Vēstule Ebrējiem 7 >