< Pirmā Mozus 42 >
1 Kad nu Jēkabs redzēja, ka labība bija Ēģiptes zemē, tad viņš saviem dēliem sacīja: ko jūs skatāties?
Wakati Yakobo alipofahamu kuwa kuna nafaka huko Misri, akawaambia wanawe, “Mbona mnakaa tu hapa mnatazamana?”
2 Un viņš sacīja: redzi, es esmu dzirdējis, labību esam Ēģiptes zemē, noejat turp un pērciet mums no turienes, lai dzīvojam un nemirstam.
Akaendelea kuwaambia, “Nimesikia kuwa huko Misri kuna nafaka. Telemkeni huko mkanunue chakula kwa ajili yetu, ili tuweze kuishi wala tusife.”
3 Tad desmit Jāzepa brāļi nogāja, labības pirkt no Ēģiptes zemes.
Ndipo wale ndugu kumi wa Yosefu, wakateremka huko Misri kununua nafaka.
4 Bet Benjaminu, Jāzepa brāli, Jēkabs nesūtīja ar viņa brāļiem, jo tas sacīja: ka to kāda nelaime neaizņem.
Lakini Yakobo hakumtuma Benyamini, ndugu yake Yosefu, pamoja na wengine, kwa sababu aliogopa asije akapatwa na madhara.
5 Tā Israēla dēli nāca, labības pirkt līdz ar citiem, kas turp gāja, jo bads bija arī Kanaāna zemē.
Hivyo wana wa Israeli walikuwa miongoni mwa wale waliokwenda Misri kununua nafaka, kwani njaa ilikuwa katika nchi ya Kanaani pia.
6 Un Jāzeps bija tas valdītājs pār zemi un pārdeva visiem tās zemes ļaudīm, un Jāzepa brāļi nāca un klanījās viņa priekšā ar vaigu pie zemes.
Wakati huo Yosefu alikuwa mtawala wa nchi ya Misri, naye alikuwa ndiye aliwauzia watu wote nafaka. Kwa hiyo wakati ndugu zake Yosefu walipofika, wakamsujudia hadi nyuso zao zikagusa ardhi.
7 Tad Jāzeps redzēja savus brāļus un tos pazina, bet viņš likās pret tiem svešs, un runāja ar tiem bargi un sacīja uz tiem: no kurienes jūs nākat? Un tie sacīja: no Kanaāna zemes, maizes pirkt.
Mara Yosefu alipowaona ndugu zake, akawatambua, lakini akajifanya mgeni na kuzungumza nao kwa ukali, akiwauliza, “Ninyi mnatoka wapi?” Wakamjibu, “Tumetoka katika nchi ya Kanaani kuja kununua chakula.”
8 Un Jāzeps pazina savus brāļus, bet tie viņu nepazina.
Ingawa Yosefu aliwatambua ndugu zake, wao hawakumtambua.
9 Un Jāzeps pieminēja savus sapņus, ko viņš par tiem bija sapņojis, un viņš uz tiem sacīja: jūs esat izlūki, jūs esat nākuši raudzīt, kur zemei var piekļūt.
Ndipo Yosefu alipokumbuka ndoto zake kuwahusu wao, akawaambia, “Ninyi ni wapelelezi! Mmekuja kuangalia mahali ambapo nchi yetu haina ulinzi.”
10 Un tie uz viņu sacīja: nē, mans kungs, tavi kalpi ir nākuši, maizes pirkt.
Wakamjibu, “Sivyo bwana wangu. Watumishi wako wamekuja kununua chakula.
11 Mēs visi esam viena vīra dēli, mēs esam taisni ļaudis, tavi kalpi nav izlūki.
Sisi sote ni wana wa baba mmoja. Watumishi wako ni watu waaminifu, wala sio wapelelezi.”
12 Un viņš uz tiem sacīja: nē, bet jūs esat nākuši izlūkot, kur zemei var piekļūt.
Akawaambia, “La hasha! Mmekuja kuangalia mahali ambapo nchi yetu haina ulinzi.”
13 Un tie sacīja: mēs tavi kalpi bijām divpadsmit brāļi, viena paša vīra dēli Kanaāna zemē, un redzi, tas jaunākais vēl šodien ir pie mūsu tēva, bet tā viena vairs nav.
Lakini wakamjibu, “Watumishi wako walikuwa kumi na wawili, wana wa mtu mmoja ambaye anaishi katika nchi ya Kanaani. Sasa mdogo wetu wa mwisho yupo na baba yetu na mwingine alikufa.”
14 Tad Jāzeps uz tiem sacīja: tā tas ir, kā es uz jums esmu runājis un sacījis: jūs esat izlūki.
Yosefu akawaambia, “Ni sawa kabisa kama nilivyowaambia: Ninyi ni wapelelezi!
15 Pie tam jūs tapsiet pārbaudīti; tik tiešām kā Faraons dzīvo, jūs no šejienes netiksiet projām, ja jūsu jaunākais brālis nenāk šurpu.
Na hivi ndivyo mtakavyojaribiwa: Hakika kama Farao aishivyo, hamtaondoka mahali hapa mpaka ndugu yenu mdogo aje hapa.
16 Sūtiet vienu no jums, kas atved jūsu brāli, bet jūs paliekat cietumā, tad jūsu vārdi taps pārbaudīti, vai pie jums ir patiesība, un ja ne, tik tiešām kā Faraons dzīvo, tad jūs esat izlūki.
Tumeni mmoja wenu akamlete huyo ndugu yenu, wengine mtawekwa gerezani, ili maneno yenu yajaribiwe kuona kama mnasema kweli. La sivyo, hakika kama Farao aishivyo ninyi ni wapelelezi!”
17 Un viņš tos kopā lika trīs dienas cietumā.
Akawaweka wote chini ya ulinzi kwa siku tatu.
18 Un trešā dienā Jāzeps uz tiem sacīja: dariet tā, tad jūs dzīvosiet; es bīstos Dievu.
Siku ya tatu Yosefu akawaambia, “Fanyeni hili nanyi mtaishi, kwa maana namwogopa Mungu:
19 Ja jūs esat taisni ļaudis, tad lai viens no jūsu brāļiem paliek saistīts cietumā, un jūs ejat, pārvediet to labību, tādēļ ka bads jūsu mājās.
Ikiwa ninyi ni watu waaminifu, mmoja wa ndugu zenu na abaki kifungoni, nanyi wengine pelekeni nafaka kwa jamaa yenu wanaoteseka kwa njaa.
20 Un atvediet savu jaunāko brāli pie manis, tad jūsu vārdi taps atrasti taisni, un jūs nemirsiet; un tie tā darīja.
Lakini ni lazima mniletee ndugu yenu mdogo hapa, ili maneno yenu yathibitike na kwamba msife.” Wakakubali kufanya hivyo.
21 Tad tie sacīja viens uz otru: patiesi, mēs esam noziegušies pret savu brāli, ka mēs viņa dvēseles bēdas redzējām, kad viņš no mums žēlastības lūdzās, un neklausījām; tādēļ šās bēdas nāk pār mums.
Wakaambiana wao kwa wao, “Hakika tunaadhibiwa kwa sababu ya ndugu yetu. Tuliona jinsi alivyohuzunika alipokuwa anatusihi kuponya maisha yake, lakini hatukumsikiliza, hiyo ndiyo sababu dhiki hii imetupata.”
22 Un Rūbens tiem atbildēja un sacīja: vai es jums to neteicu sacīdams: neapgrēkojaties pret to bērnu, bet jūs neklausījāt? Un nu redzi, viņa asinis top meklētas.
Reubeni akawajibu, “Sikuwaambieni msitende dhambi dhidi ya kijana? Lakini hamkunisikiliza! Sasa ni lazima tuadhibiwe kwa ajili ya damu yake.”
23 Un tie nezināja, ka Jāzeps to saprata, jo tur bija tulks viņu starpā.
Hawakujua kuwa Yosefu angewaelewa, kwa sababu alitumia mkalimani.
24 Un viņš no tiem novērsās un raudāja, un atkal pie tiem atgriezās un ar tiem runāja, un ņēma no viņu vidus Sīmeanu un to saistīja priekš viņu acīm.
Yosefu akajitenga nao akaanza kulia, kisha akawarudia na kuzungumza nao tena. Akataka Simeoni akamatwe na kufungwa mbele yao.
25 Un Jāzeps pavēlēja viņu maisus pildīt ar labību un viņu naudu atlikt ikkatram savā maisā, un tiem dot ceļa barību uz ceļu; un tiem tā tapa darīts.
Yosefu akatoa amri ya kujaza magunia yao nafaka na kuweka fedha ya kila mmoja ndani ya gunia lake, kisha wapewe mahitaji ya njiani. Baada ya kufanyiwa hayo yote,
26 Un tie uzkrāva savu labību uz saviem ēzeļiem un aizgāja no turienes.
wakapakiza nafaka juu ya punda zao, wakaondoka.
27 Kad nu viens no tiem savu maisu atraisīja, savu ēzeli barot mājas vietā, tad tas ieraudzīja savu naudu, un redzi, tā bija viņa maisa virsgalā.
Walipofika mahali pa kulala huko njiani mmoja wao akafungua gunia lake ili amlishe punda wake, akakuta fedha yake kwenye mdomo wa gunia lake.
28 Un tas sacīja uz saviem brāļiem: mana nauda man ir atlikta, un redzi, tā ir manā maisā. Tad tiem sirds iztrūkās un tie pārbijās viens uz otru sacīdami: kas tas ir, ko Dievs mums ir darījis?
Akawaambia ndugu zake, “Fedha yangu imerudishwa. Iko ndani ya gunia langu.” Mioyo yao ikazimia, na kila mmoja akamgeukia mwenzake wakitetemeka, wakaulizana, “Ni nini hiki Mungu alichotufanyia?”
29 Un tie nāca pie Jēkaba, sava tēva, uz Kanaāna zemi un teica tam visu, kas tiem bija noticis, un sacīja:
Walipofika kwa Yakobo baba yao katika nchi ya Kanaani, wakamweleza mambo yote yaliyowapata. Wakasema,
30 Tas vīrs, tas zemes kungs, runāja bargi ar mums un mūs turēja par zemes izlūkiem.
“Huyo mtu ambaye ndiye bwana katika nchi hiyo alisema nasi kwa ukali, akatutendea kana kwamba sisi tulikuwa tunaipeleleza nchi.
31 Tad mēs tam sacījām: mēs esam taisni ļaudis, mēs neesam izlūki bijuši.
Lakini tulimwambia, ‘Sisi ni watu waaminifu, sio wapelelezi.
32 Mēs bijām divpadsmit brāļi, sava tēva dēli, viena vairs nav, un tas jaunākais vēl šodien ir pie mūsu tēva Kanaāna zemē.
Tulizaliwa ndugu kumi na wawili, wana wa baba mmoja. Mmoja alikufa, na mdogo wetu wa mwisho yupo na baba yetu huko Kanaani.’
33 Un tas vīrs, tas zemes kungs, mums sacīja: pie tam es nomanīšu, jūs esam taisnus: pametiet vienu no saviem brāļiem pie manis un ņemiet, ko jums vajag, un noejat,
“Ndipo huyo mtu aliye bwana katika nchi hiyo alipotuambia, ‘Hivi ndivyo nitafahamu kuwa ninyi ni watu waaminifu: Mwacheni mmoja wa ndugu zenu pamoja nami hapa, kisha nendeni mpeleke chakula kwa ajili ya jamaa yenu inayoteseka kwa njaa.
34 Un atvediet savu jaunāko brāli pie manis, tad es manīšu, jūs neesam izlūkus, bet taisnus ļaudis. Jūsu brāli es jums atdošu un jums ļaušu šinī zemē pirkt un pārdot.
Lakini mleteni huyo ndugu yenu mdogo kwangu, ndipo nitajua kuwa ninyi sio wapelelezi, ila ni watu waaminifu. Kisha nitamrudisha ndugu yenu, nanyi mtaweza kufanya biashara katika nchi hii.’”
35 Un kad tie savus maisus izbēra, redzi, tad ikviens atrada savu naudas mučkuli(maisiņu) savā maisā, un tie ieraudzīja savus naudas mučkuļus, viņi un viņu tēvs, un tie izbijās.
Walipokuwa wanamimina nafaka kutoka kwenye magunia yao, ndani ya gunia la kila mtu kulikuwa na mfuko wa fedha! Wakati wao na baba yao walipoona mifuko ya fedha, wakaogopa.
36 Tad Jēkabs, viņu tēvs, uz tiem sacīja: jūs man paņemat manus bērnus: Jāzepa vairs nav un Sīmeana vairs nav, un Benjaminu jūs ņemsiet; viss tas nāk man virsū.
Yakobo baba yao akawaambia, “Ninyi mmenipokonya watoto wangu. Yosefu hayupo na Simeoni hayupo tena na sasa mnataka kumchukua Benyamini. Kila kitu ni kinyume nami!”
37 Tad Rūbens runāja ar savu tēvu un sacīja: ja es to pie tevis neatvedīšu atpakaļ, tad nokauj manus divus dēlus; dod viņu manā rokā, tad es viņu pie tevis atvedīšu atpakaļ.
Ndipo Reubeni akamwambia baba yake, “Waweza kuwaua wanangu wote wawili, ikiwa sitamrudisha Benyamini kwako. Mkabidhi Benyamini katika uangalizi wangu, nami nitamrudisha.”
38 Bet viņš sacīja: manam dēlam nebūs noiet ar jums, jo viņa brālis ir miris, un tas ir viens pats atlicis. Ja tam kāda nelaime notiks uz ceļa, kur jūs iesiet, tad jūs manus sirmos matus ar sirdēstiem novedīsiet bedrē. (Sheol )
Lakini Yakobo akasema, “Mwanangu hatashuka huko pamoja nanyi; ndugu yake amekufa naye ndiye peke yake aliyebaki. Ikiwa atapatwa na madhara katika safari mnayoiendea, mtashusha kichwa changu chenye mvi kaburini kwa masikitiko.” (Sheol )