< Ecechiela 6 >
1 Un Tā Kunga vārds notika uz mani sacīdams:
Neno la Bwana likanijia kusema,
2 Cilvēka bērns! Griez savu vaigu pret Israēla kalniem un sludini pret tiem
“Mwanadamu, elekeza uso wako kukabili milima ya Israeli, utabiri dhidi yake
3 Un saki: Israēla kalni, klausāties Tā Kunga Dieva vārdu! Tā saka Tas Kungs Dievs uz kalniem un pakalniem, uz upēm un ielejām: redzi! Es vedu pār jums zobenu un izdeldu jūsu elku altārus.
na useme: ‘Ee milima ya Israeli, sikia neno la Bwana Mwenyezi. Hili ndilo Bwana Mwenyezi aliambiayo milima na vilima, magenge na mabonde: Ninakaribia kuleta upanga dhidi yenu, nami nitapaharibu mahali penu pote pa juu pa kuabudia miungu.
4 Un jūsu altāri taps nopostīti un jūsu saules stabi nolauzti, un es gāzīšu jūsu nokautos jūsu elku priekšā.
Madhabahu yenu yatabomolewa na madhabahu yenu ya kufukizia uvumba yatavunjavunjwa, nami nitawachinja watu wenu mbele ya sanamu zenu.
5 Un Es nodošu Israēla bērnu trūdus viņu elku priekšā un kaisīšu jūsu kaulus ap jūsu altāriem.
Nitazilaza maiti za Waisraeli mbele ya sanamu zao, nami nitatawanya mifupa yenu kuzunguka madhabahu yenu.
6 Visur, kur jūs mājojat, pilsētas būs postītas un elku kalni atstāti, jo jūsu altāri būs sagāzti un nopostīti un jūsu elki būs salauzti un izdeldēti, un jūsu saules stabi tiks nocirsti un jūsu darījumi iznīcināti.
Popote mnapoishi, miji hiyo itafanywa ukiwa na mahali pa juu pa kuabudia miungu patabomolewa, ili madhabahu yenu ifanywe ukiwa na kuharibiwa, sanamu zenu zitavunjavunjwa na kuharibiwa, madhabahu yenu ya kufukizia uvumba yatabomolewa na kila mlichokifanya kitakatiliwa mbali.
7 Un jūsu vidū gulēs nokauti, un jūs samanīsiet, ka Es esmu Tas Kungs.
Watu wenu watachinjwa katikati yenu, nanyi mtatambua Mimi ndimi Bwana.
8 Bet Es (kādus) atlicināšu, ka jums paliek, kas zobenam izmūk starp pagāniem, kad jūs tapsiet izkaisīti pa zemēm.
“‘Lakini nitawabakiza hai baadhi yenu, kwa kuwa baadhi yenu watanusurika kuuawa watakapokuwa wametawanyika katika nchi na mataifa.
9 Tad jūsu izglābtie mani pieminēs starp pagāniem, kur tie būs cietumā, kad Es būšu salauzis viņu mauku sirdis, kas no Manis atkāpušās, un viņu acis, kas mauko pakaļ viņu elkiem, un tiem riebsies tas ļaunums, ko tie darījuši visās savās negantībās.
Ndipo katika mataifa ambamo watakuwa wamechukuliwa mateka, wale ambao watanusurika watanikumbuka, jinsi ambavyo nimehuzunishwa na mioyo yao ya uzinzi, ambayo imegeukia mbali nami na macho yao ambayo yametamani sanamu zao. Watajichukia wenyewe kwa ajili ya uovu walioutenda na kwa ajili ya desturi zao za kuchukiza.
10 Un tiem būs samanīt, ka Es esmu Tas Kungs; Es nebūt neesmu velti runājis, ka viņiem darīšu šo ļaunumu.
Nao watajua kuwa Mimi ndimi Bwana, sikuwaonya bure kuwa nitaleta maafa hayo yote juu yao.
11 Tā saka Tas Kungs Dievs: sasit savas rokas un sit ar kāju pie zemes un sauc: ak vai! Pār visām niknām Israēla nama negantībām, jo tie kritīs caur zobenu, caur badu un caur mēri.
“‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Piga makofi, kanyaga chini kwa mguu na upige kelele, “Ole!” kwa sababu ya maovu yote na machukizo yote yanayofanywa na nyumba ya Israeli, kwa kuwa wataanguka kwa upanga, njaa na tauni.
12 Kas tālu, tas kritīs caur mēri, un kas tuvu, tas kritīs caur zobenu, bet kas atliksies un izglābsies, nomirs badā. Tā Es pret tiem izdarīšu savu bardzību.
Yeye aliye mbali sana atakufa kwa tauni, naye aliye karibu atauawa kwa upanga, naye yule atakayenusurika na kubaki atakufa kwa njaa. Hivyo ndivyo nitakavyotimiza ghadhabu yangu dhidi yao.
13 Tad jūs samanīsiet, ka Es esmu Tas Kungs, kad viņu nokautie gulēs viņu elku priekšā ap viņu altāriem pa visiem augstiem pakalniem, pa visiem kalnu galiem un apakš visiem zaļiem kokiem un apakš visiem kupliem ozoliem, tais vietās, kur tie saldu smaržu upurēja visiem saviem elkiem.
Nao watajua kwamba Mimi ndimi Bwana, wakati maiti za watu wao zitakapokuwa zimelala katikati ya sanamu zao kuzunguka madhabahu yao, juu ya kila kilima kilichoinuka na juu ya vilele vyote vya milima, chini ya kila mti uliotanda na kila mwaloni wenye majani, yaani, sehemu walizofukizia uvumba kwa sanamu zao zote.
14 Un Es izstiepšu savu roku pār viņiem, un darīšu zemi par postažu un tuksnesi vairāk nekā Diblas tuksnesi, visur, kur viņi mājo; un tie samanīs, ka Es esmu Tas Kungs.
Nami nitanyoosha mkono wangu dhidi yao na kuifanya nchi yao ukiwa, kuanzia jangwani hadi Dibla, kila mahali wanapoishi. Ndipo watakapojua ya kwamba Mimi ndimi Bwana.’”