< Ecechiela 43 >
1 Un viņš mani noveda pie tiem vārtiem, kas pret rīta pusi.
Kisha yule mtu akanileta kwenye lango linaloelekea upande wa mashariki,
2 Un redzi, Israēla Dieva godība nāca no rīta puses, un viņa rībēšana bija kā varenu ūdeņu rūkšana, un zeme tapa apgaismota no Viņa godības.
nami nikaona utukufu wa Mungu wa Israeli ukija kutoka upande wa mashariki. Sauti yake ilikuwa kama ya ngurumo ya maji yaendayo kasi, nayo nchi ikangʼaa kwa utukufu wake.
3 Un viņa parādīšanās bija tāda pati, kādu es redzēju, kad es nācu, to pilsētu postīt, un tā parādīšanās bija tā kā tā, ko es redzēju pie Ķebaras upes, un es kritu uz savu vaigu.
Maono niliyoyaona yalikuwa kama maono yale niliyokuwa nimeyaona wakati Mungu alipokuja kuangamiza mji na kama maono niliyokuwa nimeyaona kando ya Mto wa Kebari, nami nikaanguka kifudifudi.
4 Un Tā Kunga godība nāca tai namā pa tiem vārtiem, kas pret rīta pusi.
Utukufu wa Bwana ukaingia hekaluni kwa kupitia lango linaloelekea upande wa mashariki.
5 Un Tas Gars mani pacēla un mani ieveda iekšējā pagalmā, un redzi, Tā Kunga godība piepildīja to namu.
Kisha Roho akanichukua na kunileta katika ule ua wa ndani, nao utukufu wa Bwana ulilijaza Hekalu.
6 Un no tā nama es dzirdēju vienu ar mani runājam, un viens vīrs stāvēja pie manis.
Wakati yule mtu akiwa amesimama kando yangu, nilisikia mtu mmoja akisema nami kutoka ndani ya Hekalu.
7 Un Tas uz mani sacīja: “Cilvēka bērns, šī ir Mana godības krēsla vieta un Manu pēdu vieta, kur Es Israēla bērnu vidū dzīvošu mūžīgi. Un Israēla nams, viņi ar saviem ķēniņiem vairs nesagānīs Manu svēto Vārdu ar savu maucību un ar savu ķēniņu mirušām miesām pie viņu miršanas,
Akasema, “Mwanadamu, hapa ni mahali pa kiti changu cha enzi na mahali pa kuweka nyayo za miguu yangu. Hapa ndipo nitakapoishi miongoni mwa Waisraeli milele. Kamwe nyumba ya Israeli hawatalinajisi tena Jina langu takatifu, yaani, wao wala wafalme wao, kwa ukahaba wao na kwa sanamu zao zisizokuwa na uhai za wafalme wao katika mahali pao pa juu pa kuabudia miungu.
8 Kad tie savu slieksni lika pie mana sliekšņa un savus stabus pie maniem stabiem, ka tikai siena bija starp mani un viņiem, un sagānīja manu svēto vārdu ar savām negantībām, ko tie darīja; tāpēc es tos esmu aprijis savā dusmībā.
Walipoweka kizingiti chao karibu na kizingiti changu na miimo yao ya milango karibu na miimo yangu, pakiwa na ukuta tu kati yangu na wao, walilinajisi Jina langu takatifu kwa matendo yao ya machukizo. Kwa sababu hiyo niliwaangamiza kwa hasira yangu.
9 Nu tie atņems savu maucību un savu ķēniņu mirušās miesas tālu nost no manis un es dzīvošu viņu vidū mūžīgi.
Basi sasa na waweke mbali nami ukahaba wao na sanamu za wafalme wao zisizo na uhai, nami nitakaa miongoni mwao milele.
10 Tu cilvēka bērns, dari zināmu Israēla namam šo namu, lai tie kaunas savu noziegumu dēļ, un lai tie to ēku mēro.
“Mwanadamu, elezea hilo Hekalu kwa watu wa Israeli, ili wapate kuona aibu kwa ajili ya dhambi zao. Wao na wapime hicho kielelezo.
11 Kad tie nu kaunas par visu, ko tie darījuši, tad rādi tiem tā nama izskatu un viņa kārtību un viņa izejamās un ieejamās durvis un visu viņa izskatu un visus viņa likumus un visu viņa stāvu, un visu viņa bauslību dari tiem zināmu un raksti priekš viņu acīm, ka tie visu viņa izskatu un visus viņa likumus patur un tos dara.”
Wakishaona aibu kwa ajili ya yale yote waliyotenda, wafahamishe kielelezo cha hilo Hekalu, yaani mpangilio wake, maingilio yake ya kutoka na kuingia, kielelezo chake chote, na masharti yake yote na sheria zake zote. Yaandike haya mbele yao ili wapate kuwa waaminifu kwa hicho kielelezo chake na kufuata masharti yake yote.
12 Šī ir Tā Dieva nama bauslība: kalna galā visapkārt līdz viņa robežām ir vissvētākā vieta; redzi, šī ir tā nama bauslība.
“Hii ndiyo sheria ya Hekalu: Eneo lote linalozunguka Hekalu juu ya mlima litakuwa takatifu kuliko yote. Hii ndiyo sheria ya Hekalu.
13 Un šie ir altāra mēri pēc tās olekts, kas ir lielāka nekā cita olekts par vienu plaukstu. Viņa pamats ir vienu olekti (augstumā) un vienu olekti garumā, un viņa malas zimze(apmale) ir vienu sprīdi visapkārt; un tas ir altāra augstums:
“Hivi ndivyo vipimo vya madhabahu kwa dhiraa ndefu, yaani, dhiraa moja na nyanda nne: Tako lake liwe na kina cha hiyo dhiraa moja na upana wa hiyo dhiraa moja, ikiwa na ukingo wa shibiri moja kuizunguka pembeni. Hiki kitakuwa ndicho kimo cha madhabahu:
14 No pamata pie zemes līdz apakšējai pakāpei bija divas olektis un platums viena olekts. Bet no tās mazās pakāpes līdz tai lielai ir četras olektis un platums viena olekts.
Kimo cha msingi kuanzia usawa wa ardhi mpaka kwenye mfereji sehemu ya chini kimo chake ni dhiraa mbili na upana wake ni dhiraa moja na kuanzia kwenye ukingo mdogo hadi kwenye ukingo mpana kimo chake ni dhiraa nne na upana wake ni dhiraa moja.
15 Un altāra ugunskurs bija četras olektis augstumā, un no ugunskura uz augšu bija tie četri ragi.
Pale pawashwapo moto madhabahuni kimo chake kitakuwa dhiraa nne, na pembe nne zinazoelekeza juu kutoka pale pawashwapo moto.
16 Un altāra ugunskurs bija divpadsmit olektis garumā un divpadsmit olektis platumā, četrkantīgs uz saviem četriem sāniem.
Pale pawashwapo moto pa madhabahu ni mraba, urefu wake ni dhiraa kumi na mbili na upana wa dhiraa kumi na mbili.
17 Un tā (augšēja) pakāpe bija četrpadsmit olektis garumā un četrpadsmit olektis platumā savos četros sānos, un tā mala ap viņu bija vienu pusolekti, un tas pamats pie tās bija viena olekts visapkārt, un uzkāpšana bija no rīta puses.
Pia sehemu ya juu ni mraba, urefu wake dhiraa kumi na nne na upana wa dhiraa kumi na nne, ikiwa na ukingo wa nusu dhiraa na mfereji kuizunguka madhabahu. Ngazi za kupandia madhabahuni zitaelekea upande wa mashariki.”
18 Un viņš uz mani sacīja: cilvēka bērns, tā saka Tas Kungs Dievs: šie ir altāra likumi tai dienā, kad viņš taps taisīts, uz tā upurēt dedzināmos upurus un uz to slacināt asinis.
Kisha akaniambia, “Mwanadamu, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Haya ndiyo yatakayokuwa masharti ya kutoa dhabihu za kuteketezwa na kunyunyiza damu juu ya madhabahu itakapokuwa imejengwa.
19 Un tiem priesteriem, Levja bērniem, kas ir no Cadoka dzimuma, kas man tuvojās, man kalpot, saka Tas Kungs Dievs: tiem tev būs dot vienu jaunu vērsi par grēku upuri.
Utatoa fahali mchanga kuwa sadaka ya dhambi kwa makuhani, ambao ni Walawi, wa jamaa ya Sadoki, ndio watakaonikaribia kuhudumu mbele zangu, asema Bwana Mwenyezi.
20 Un tev no viņa asinīm būs ņemt un to likt pie viņa četriem ragiem un pie tiem četriem pakāpes stūriem un pie tās apkārtējās malas, tā tev to būs šķīstīt un svētīt.
Itakupasa kuchukua baadhi ya hiyo damu ya mnyama huyo na kuiweka juu ya hizo pembe nne za madhabahu na juu ya ncha zake nne za sehemu ya juu kuzunguka ukingo wote, ili kuitakasa madhabahu na kufanya upatanisho kwa ajili yake.
21 Un tev būs ņemt grēku upura vērsi, un to būs sadedzināt ierādītā nama vietā, ārā no tās svētās vietas.
Itakupasa kumchukua huyo fahali mchanga kwa ajili ya sadaka ya dhambi na kumteketeza mahali palipoagizwa katika eneo la Hekalu nje ya mahali Patakatifu.
22 Un otrā dienā tev būs upurēt vienu āzi, kas bez vainas, par grēku upuri, un altāri būs svētīt, tā kā to svētīja ar to vērsi.
“Siku ya pili yake utamtoa beberu asiye na dosari kwa ajili ya sadaka ya dhambi, nayo madhabahu itatakaswa kama ilivyotakaswa kwa yule fahali.
23 Kad tu nu to svētīšanu būsi pabeidzis, tad tev no ganāmā pulka būs upurēt vienu jaunu vērsi, kas bez vainas, un vienu aunu, kas bez vainas.
Utakapokuwa umemaliza kazi ya kuitakasa, utamtoa fahali mchanga pamoja na kondoo dume toka kwenye kundi, wote wawe hawana dosari.
24 Un tev tos būs upurēt Tā Kunga priekšā, un priesteriem būs sāli uz tiem mest un tos upurēt par dedzināmo upuri Tam Kungam.
Utawatoa mbele za Bwana, nao makuhani watanyunyizia chumvi juu yao na kuwatoa kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana.
25 Septiņas dienas tev būs upurēt ikdienas vienu āzi par grēku upuri, viņiem arī būs upurēt vienu jaunu vērsi un vienu aunu no ganāmā pulka, kas abi bez vainas.
“Kwa siku saba itakupasa kutoa beberu kila siku kwa ajili ya sadaka ya dhambi, pia itakupasa kutoa fahali mchanga na kondoo dume kutoka zizini, wote wawe hawana dosari.
26 Septiņas dienas tiem altāri būs svētīt un viņu šķīstīt un savas rokas pildīt.
Kwa siku saba itawapasa kufanya upatanisho kwa ajili ya madhabahu na kuitakasa na hivyo ndivyo watakavyoiweka wakfu.
27 Un pēc šīm dienām priesteriem astotā dienā un joprojām būs upurēt jūsu dedzināmos upurus un jūsu pateicības upurus uz altāra, un man būs labs prāts pie jums, saka Tas Kungs Dievs.
Mwishoni mwa hizi siku saba, kuanzia siku ya nane na kuendelea, itawapasa makuhani kutoa sadaka zenu za kuteketezwa na sadaka za amani juu ya madhabahu. Kisha nitawakubali ninyi, asema Bwana Mwenyezi.”