< Ecechiela 41 >
1 Un viņš mani noveda Dieva namā, un viņš mēroja tos pīlārus, sešas olektis bija platums no šīs puses un sešas olektis platums no viņas puses, tik plats bija tas dzīvoklis.
Kisha yule mtu akanileta katika sehemu ya nje ya patakatifu, naye akaipima miimo; upana wake ulikuwa dhiraa sita kila upande.
2 Un durvju platums bija desmit olektis, un durvīm sānis piecas olektis no šīs un piecas olektis no viņas puses. Un viņš mēroja viņa garumu četrdesmit olektis un platumu divdesmit olektis.
Ingilio lilikuwa la upana wa dhiraa kumi na kuta zilizojitokeza kila upande zilikuwa na upana wa dhiraa tano. Pia akapima sehemu ya nje ya patakatifu, nayo ilikuwa na urefu wa dhiraa arobaini na upana wa dhiraa ishirini.
3 Tad viņš iegāja iekšā un mēroja durvju pīlārus divas olektis un durvis sešas olektis, un durvju platums bija septiņas olektis.
Kisha akaingia sehemu takatifu ndani ya Hekalu na kupima miimo ya ingilio, kila mmoja ulikuwa na upana wa dhiraa mbili. Ingilio lilikuwa na upana wa dhiraa sita, na kuta zilizotokeza kila upande zilikuwa na upana wa dhiraa saba.
4 Un viņš mēroja to garumu divdesmit olektis un to platumu divdesmit olektis Dieva nama priekšā. Un viņš uz mani sacīja: šī ir tā visusvētākā vieta.
Naye akapima urefu wa sehemu takatifu ndani, nao ulikuwa dhiraa ishirini, na upana wake ulikuwa dhiraa ishirini hadi mwisho wa sehemu ya nje ya sehemu takatifu. Akaniambia, “Hapa ndipo Patakatifu pa Patakatifu.”
5 Un viņš mēroja tā nama sienu sešas olektis, ikkatra sānu kambara platumu četras olektis visapkārt tam namam.
Kisha akapima ukuta wa Hekalu, nao ulikuwa na unene wa dhiraa sita, na kila chumba cha pembeni kuzunguka Hekalu kilikuwa na upana wa dhiraa nne.
6 Un tie sānu kambari bija viens pie otra trīsdesmit un trīs sānu kambari, un tie satecēja tai sienā, kas pie tā nama bija priekš sānu kambariem visapkārt, ka tie taptu stipri turēti, jo tie nebija stiprināti tā nama sienā.
Vyumba vya pembeni vilikuwa na ghorofa tatu, kimoja juu ya kingine, kila ghorofa ilikuwa na vyumba thelathini. Kulikuwa na boriti katika ukuta wote wa Hekalu ili kuimarisha vyumba vya pembeni, kwa hiyo boriti hizo hazikushikamanishwa kwenye ukuta wa Hekalu.
7 Un tie sānu kambari izplētās jo augstāki jo platāki, jo tas nams tapa allažiņ uz augšu aptaisīts visapkārt, tāpēc tas nams uz augšu bija platāks, un no apakšas kambara bija jāiet uz augškambari caur vidējo.
Vyumba vya pembeni vilivyozunguka Hekalu vilizidi kupanuka kulingana na sakafu zilivyokwenda juu. Ujenzi uliozunguka Hekalu ulijengwa kukwea juu, kwa hiyo vyumba vilipanuka kwa kadiri ya kila kimoja kilivyokwenda juu. Ngazi za kupandia zilianzia sakafu ya chini hadi sakafu ya juu kabisa kwa kupitia sakafu ya kati.
8 Un es redzēju tā nama augstumu visapkārt: sānu kambaru pamati bija vesela kārts, sešas lielas olektis no zemes līdz augšai.
Nikaona pia kuwa Hekalu lilikuwa na kitako kilichoinuliwa pande zote, huu ulikuwa ndio msingi wa vile vyumba vya pembeni ambao ulikuwa na urefu wa ule ufito mmoja wa kupimia, yaani, dhiraa ndefu sita.
9 Un tās sienas platums, kas priekš tiem sānu kambariem bija uz ārpusi, bija piecas olektis, un kas atlikās, bija sānu kambaru iekšpusē.
Ukuta wa nje wa vyumba vya pembeni ulikuwa na unene wa dhiraa tano. Eneo la wazi katikati ya vyumba vya pembeni vya Hekalu
10 Un starp tiem kambariem bija platums divdesmit olektis visapkārt tam namam.
na vyumba vya makuhani lilikuwa na upana wa dhiraa ishirini kuzunguka Hekalu pande zote.
11 Un sānu kambaru durvis bija pie tā atlikuma, vienas durvis pret ziemeli un otras durvis pret dienvidiem, un tā atlikuma platums bija piecas olektis visapkārt.
Kulikuwa na maingilio kwenye vyumba vya pembeni kutokea eneo lililo wazi, moja upande wa kaskazini na lingine upande wa kusini, nao msingi uliounganisha lile eneo la wazi ulikuwa na upana wa dhiraa tano ukilizunguka lote.
12 Tai ēkai, kas tā atlikuma priekšā bija pret vakara pusi, platums bija septiņdesmit olektis, un tās ēkas siena piecas olektis platumā visapkārt, un viņas garums deviņdesmit olektis.
Jengo lililoelekeana na ua wa Hekalu upande wa magharibi lilikuwa na upana wa dhiraa sabini. Ukuta wa jengo hilo ulikuwa na unene wa dhiraa tano, kulizunguka lote, urefu ulikuwa wa dhiraa tisini.
13 Tad viņš mēroja to namu, viņa garums bija simts olektis, (proti) tas atlikums un tā ēka un viņas sienas bija simts olektis garumā.
Kisha akapima Hekalu, lilikuwa na urefu wa dhiraa mia moja na ua wa Hekalu na jengo pamoja na kuta zake vilikuwa na urefu wa dhiraa mia moja pia.
14 Un nama priekšas platums un tas atlikums pret rīta pusi bija arīdzan simts olektis.
Upana wa ua wa Hekalu upande wa mashariki, pamoja na upande wa mbele wa Hekalu ulikuwa dhiraa mia moja.
15 Viņš mēroja arī tās ēkas garumu pret to atlikumu, kas aiz viņas bija, līdz ar viņas margām: no šīs un no viņas puses bija simts olektis. Un iekšējais Dieva nams un pagalma priekšnami.
Kisha akapima urefu wa jengo linaloelekeana na ua upande wa nyuma wa Hekalu, pamoja na vyumba vyake kila upande, ilikuwa dhiraa mia moja. Sehemu takatifu ya nje, sehemu takatifu ya ndani, pamoja na baraza inayoelekeana na ukumbi,
16 Līdz ar tiem sliekšņiem un šauriem logiem un tām margām visapkārt trijās rindās, slieksnim pretī bija apklāti ar dēļiem visapkārt no zemes līdz logiem, un tie logi bija apsegti.
pamoja na vizingiti, madirisha membamba na vyumba vyote vitatu, kila kimoja pamoja na kizingiti vilifunikwa kwa mbao. Sakafu, ukuta mpaka kwenye madirisha na madirisha yenyewe vilifunikwa kwa mbao.
17 Un izgriezumi bija virs durvīm un līdz iekšējam namam un ārā un pie visām sienām visapkārt, gan ārā, gan iekšpusē.
Katika nafasi iliyokuwa juu ya upande wa nje wa ingilio la sehemu takatifu ya ndani, na katika kuta zilizozunguka sehemu takatifu ya ndani na sehemu takatifu ya nje, kwa nafasi zilizo sawa,
18 Un bija taisīti ķerubi un palmu koki, tā ka viens palma koks bija starp ķerubu un ķerubu.
kulinakshiwa makerubi na miti ya mitende. Miti ya mitende ilikuwa kati ya kerubi na kerubi. Kila kerubi alikuwa na nyuso mbili:
19 Un ikvienam ķerubam bija divi vaigi, cilvēka vaigs pret šīs puses palma koku, un lauvas vaigs pret viņas puses palma koku; tā tas bija taisīts visā namā visapkārt.
upande mmoja uso wa mwanadamu kuelekea mti wa mtende na upande mwingine uso wa simba ukielekea mti mwingine wa mtende. Ilinakshiwa kuzunguka Hekalu lote.
20 No zemes līdz pāri pār durvīm bija ķerubi un palmu koki taisīti, un pie Dieva nama sienas.
Kuanzia sakafu mpaka eneo lililo juu ya ingilio, palinakshiwa makerubi na miti ya mitende pamoja na kwenye ukuta wa nje wa patakatifu.
21 Un Dieva nama stenderi bija četrām kantīm, un svētās vietas priekša tāpat izskatījās.
Mahali patakatifu pa nje palikuwa na miimo ya mlango uliokuwa mraba na ule uliokuwa katika Patakatifu Pa Patakatifu ulikuwa unafanana na huo mwingine.
22 Altāris bija no koka, trīs olektis augstumā un divas olektis garumā, un viņa virsas un viņa sienas bija no koka. Un viņš uz mani runāja: šis ir tas galds, kas stāv Tā Kunga priekšā.
Kulikuwa na madhabahu ya mbao kimo chake dhiraa tatu na ilikuwa dhiraa mbili mraba pande zote, tako lake na pande zake zilikuwa za mbao. Yule mtu akaniambia, “Hii ni meza ambayo iko mbele za Bwana.”
23 Un Dieva namam un tai svētai vietai bija katram divas durvis.
Mahali patakatifu pa nje na Patakatifu Pa Patakatifu zilikuwa na milango miwili.
24 Un pie tām durvīm bija divi spārni, ko varēja atvērt un aizvērt, divi pie vienām durvīm un divi spārni pie otrām.
Kila mlango ulikuwa na vipande viwili, vipande viwili vilivyoshikwa na bawaba vyenye kufunguka kwa kila mlango.
25 Un pie tām, proti pie Dieva nama durvīm, bija taisīti ķerubi un palmu koki, tā kā bija taisīti pie sienām, un priekšnama priekšā no āra puses bija koka slieksnis.
Juu ya hiyo milango ya Patakatifu palinakshiwa makerubi na miti ya mitende kama yale yaliyonakshiwa kwenye kuta, na kulikuwa na ubao ulioningʼinia mbele ya baraza kwa nje.
26 Un pie tiem šauriem logiem bija arīdzan palmu koki no šīs un no viņas puses priekšnama sānos, un pie tā nama sānu kambariem un pie tiem sliekšņiem.
Katika kuta za pembeni za ukumbi kulikuwa na madirisha membamba yaliyonakshiwa miti ya mitende kila upande. Vyumba vya pembeni vya Hekalu pia vilikuwa vimefunikwa kwa mbao.