< Ecechiela 36 >

1 Un tu cilvēka bērns, sludini par Israēla kalniem un saki: Israēla kalni, klausiet Tā Kunga vārdu.
“Mwanadamu, itabirie milima ya Israeli na useme, ‘Ee milima ya Israeli, sikieni neno la Bwana.
2 Tā saka Tas Kungs Dievs: tādēļ ka ienaidnieks par jums saka: redzi, tie mūžīgie kalni mums ir tikuši par mantību,
Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kwa sababu adui wanasema juu yako, “Aha! Mahali palipoinuka pa zamani pamekuwa milki yetu.”’
3 Tādēļ sludini un saki: tā saka Tas Kungs Dievs: Tāpēc ka jūs visapkārt esat postīti un aprīti, ka jūs tiem atlikušiem pagāniem esat par mantību un esat nākuši ļaužu mēlēs un valodās,
Kwa hiyo tabiri na useme, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kwa sababu wamewafanya ukiwa na kuwagandamiza kila upande ili mpate kuwa milki ya mataifa mengine na kuwa kitu cha kusimangwa na kudhihakiwa miongoni mwa watu,
4 Tāpēc, Israēla kalni, klausiet Tā Kunga Dieva vārdu. Tā saka Tas Kungs Dievs uz kalniem un pakalniem, gravām un ielejām, tukšām posta vietām un atstātām pilsētām, kas ir palikušas par laupījumu un apsmieklu visām atlikušām tautām visapkārt, -
kwa hiyo, ee milima ya Israeli, sikieni neno la Bwana Mwenyezi: Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo kwa milima na vilima, kwa makorongo na mabonde, kwa mahame yaliyo ukiwa, miji iliyoachwa ambayo imetekwa nyara na kudharauliwa na mataifa mengine yanayowazunguka,
5 Tāpēc tā saka Tas Kungs Dievs: tiešām, Es Sava karstuma ugunī runāju pret tām atlikušām tautām un pret visu Edomu, kas Manu zemi sev ņēmuši par mantību ar visas sirds prieku, ar lielu nicināšanu, to izpostīt un aplaupīt.
hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika wivu wangu uwakao nimenena dhidi ya mataifa mengine na dhidi ya Edomu yote, kwa maana kwa furaha na hila katika mioyo yao waliifanya nchi yangu kuwa milki yao ili wapate kuteka nyara sehemu yake ya malisho.’
6 Tāpēc sludini Israēla zemei un saki uz kalniem un pakalniem, gravām un ielejām: tā saka Tas Kungs Dievs: redzi, Es Savā karstumā un Savā bardzībā esmu runājis, tāpēc ka jums apsmiekls bija jānes no pagāniem.
Kwa hiyo tabiri kuhusu nchi ya Israeli na uiambie milima na vilima, makorongo na vijito na mabonde: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ninanena katika wivu wa ghadhabu yangu kwa sababu mmedharauliwa na mataifa.
7 Tādēļ Tas Kungs Dievs tā saka: Es, Es paceļu Savu roku, tiešām, tām tautām, kas visapkārt ap jums, pašām būs nest savu apsmieklu.
Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ninaapa kwa mkono wangu ulioinuliwa kwamba mataifa wanaowazunguka nao pia watadharauliwa.
8 Bet jūs, jūs Israēla kalni, atkal zaļosiet un nesīsiet savus augļus Maniem Israēla ļaudīm, jo īsā laikā tie pārnāks.
“‘Lakini ninyi, ee milima ya Israeli, mtatoa matawi na matunda kwa ajili ya watu wangu Israeli, kwa sababu hivi karibuni watakuja nyumbani.
9 Jo redzi, Es būšu pie jums, un Es skatīšos uz jums, un jūs tapsiet kopti un apsēti.
Mimi ninawajibika nanyi na nitawaangalia kwa upendeleo, mtalimwa na kupandwa mbegu,
10 Un Es vairošu pie jums cilvēkus, visu Israēla namu visnotaļ: un pilsētās dzīvos un postītas vietas uztaisīs.
nami nitaizidisha idadi ya watu kwenu, naam, nyumba yote ya Israeli. Miji itakaliwa na watu na magofu yatajengwa upya.
11 Un Es pie jums vairošu cilvēkus un lopus, tie vairosies un vaislosies, un Es iekš jums likšu dzīvot kā jūsu vecos laikos, un Es jums darīšu vairāk labuma nekā jūsu senajos laikos, un jūs samanīsiet, ka Es esmu Tas Kungs.
Nitaongeza idadi ya watu na wanyama juu yenu, nao watazaana sana na kuwa wengi mno. Nitawakalisha watu ndani yenu kama ilivyokuwa wakati uliopita, nami nitawafanya mfanikiwe kuliko hapo kwanza. Ndipo mtakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.
12 Un Es pie jums atvedīšu cilvēkus, Savus Israēla ļaudis, tie tevi iemantos, un tu tiem būsi par mantību un tiem vairs nelaupīsi bērnus.
Nitawafanya watu, watu wangu Israeli, kutembea juu yenu. Watawamiliki ninyi, nanyi mtakuwa urithi wao, kamwe hamtawaondolea tena watoto wao.
13 Tā saka Tas Kungs Dievs: tādēļ ka uz jums saka: tu esi cilvēku rijēja un savu ļaužu bērnu aplaupītāja,
“‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kwa sababu watu wanakuambia, “Unawala watu na kuliondolea taifa lako watoto wake,”
14 Tādēļ tu cilvēkus vairs nerīsi un saviem ļaudīm vairs nelaupīsi bērnus, saka Tas Kungs Dievs.
kwa hiyo hutakula tena watu wala kulifanya tena taifa lako lisiwe na watoto, asema Bwana Mwenyezi.
15 Un Es tev vairs nelikšu dzirdēt pagānu apsmieklu, un tu nenesīsi vairs tautu negodu un saviem ļaudīm vairs nelaupīsi bērnus, saka Tas Kungs Dievs.
Sitakufanya tena usikie dhihaka za mataifa, wala kudharauliwa na kabila za watu, wala kulifanya taifa lako lianguke, asema Bwana Mwenyezi.’”
16 Atkal Tā Kunga vārds uz mani notika sacīdams:
Neno la Bwana likanijia tena, kusema:
17 Cilvēka bērns, Israēla nams, kad tie savā zemē dzīvoja, tad tie to sagānīja ar savu ceļu un ar saviem darbiem; viņu ceļš bija Manā priekšā kā sārņainas sievas nešķīstība.
“Mwanadamu, nyumba ya Israeli walipokuwa wakiishi katika nchi yao wenyewe, waliinajisi kwa mwenendo wao na matendo yao. Mwenendo wao mbele zangu ulikuwa kama mwanamke aliye katika hedhi.
18 Tādēļ Es Savu bardzību pār viņiem izgāzu to asiņu dēļ, ko tie tai zemē bija izlējuši, un viņu elku dēļ ar ko to bija sagānījuši.
Hivyo nilimwaga ghadhabu yangu juu yao kwa sababu walikuwa wamemwaga damu katika nchi na kwa sababu walikuwa wameitia nchi unajisi kwa sanamu zao.
19 Un Es tos izkaisīju starp tautām, un tie tapa izputināti pa valstīm, Es tos sodīju pēc viņu ceļa un pēc viņu darbiem.
Nikawatawanya miongoni mwa mataifa, nao wakaenda huku na huko katika nchi mbalimbali, nikawahukumu sawasawa na mwenendo wao na matendo yao.
20 Kad tie nu pie tām tautām nonāca, kurp tie bija gājuši, tad tie sagānīja manu svēto vārdu, tāpēc ka no tiem tapa sacīts: šie ir Tā Kunga ļaudis un izgājuši no viņa zemes.
Tena popote walipokwenda miongoni mwa mataifa walilitia unajisi Jina langu takatifu, kwa kuwa watu walisema kuwahusu, ‘Hawa ndio watu wa Bwana, lakini imewapasa kuondoka katika nchi yake.’
21 Bet Man ir žēl Sava svētā Vārda, ko Israēla bērni sagānījuši starp tām tautām, kur tie bija nākuši.
Lakini niliwahurumia kwa ajili ya Jina langu takatifu, ambalo nyumba ya Israeli imelitia unajisi miongoni mwa mataifa huko walikokwenda.
22 Tāpēc saki uz Israēla namu: tā saka Tas Kungs Dievs: Es to nedaru jūsu dēļ, Israēla nams, bet Sava svētā Vārda dēļ, ko jūs esat sagānījuši starp tām tautām, kur esat nākuši.
“Kwa hiyo iambie nyumba ya Israeli, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Si kwa ajili yako, ee nyumba ya Israeli, kwamba ninafanya mambo haya, bali ni kwa ajili ya Jina langu takatifu, ambalo mmelitia unajisi miongoni mwa mataifa mliyoyaendea.
23 Jo Es pagodināšu Savu lielo Vārdu, kas starp pagāniem ir sagānīts, ko jūs viņu vidū esat sagānījuši. Un pagāni samanīs, ka Es esmu Tas Kungs, saka Tas Kungs Dievs, kad Es pie jums svēts parādīšos priekš viņu acīm.
Nitauonyesha utakatifu wa Jina langu kuu, ambalo limetiwa unajisi miongoni mwa mataifa, jina ambalo limetiwa unajisi miongoni mwao. Ndipo mataifa watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana, asema Bwana Mwenyezi, nitakapojionyesha mwenyewe kuwa mtakatifu kwa kuwapitia ninyi mbele ya macho yao.
24 Jo Es jūs atvedīšu no tām tautām un jūs sapulcināšu no visām valstīm, un Es jūs atvedīšu atkal jūsu zemē.
“‘Kwa kuwa nitawaondoa ninyi toka mataifa, nitawakusanya kutoka nchi zote na kuwarudisha kwenye nchi yenu wenyewe.
25 Un Es uz jums slacināšu šķīstu ūdeni, ka topat šķīsti; no visas jūsu nešķīstības un no visiem jūsu elkiem Es jūs šķīstīšu.
Nitawanyunyizia maji safi, nanyi mtakuwa safi, nitawatakasa kutoka uchafu wenu wote na kutoka sanamu zenu zote.
26 Un Es jums došu jaunu sirdi un došu jums jaunu garu, un atņemšu to akmens sirdi no jūsu miesām un došu jums miesīgu sirdi.
Nitawapa moyo mpya na kuweka roho mpya ndani yenu, nitaondoa ndani yenu moyo wenu wa jiwe na kuwapa moyo wa nyama.
27 Un Es jums došu Savu Garu un darīšu, ka jūs staigāsiet Manos likumos un sargāsiet un darīsiet Manas tiesas.
Nami nitaweka Roho yangu ndani yenu na kuwafanya ninyi mfuate amri zangu na kuwafanya kuwa waangalifu kuzishika sheria zangu.
28 Un jūs dzīvosiet tai zemē, ko Es jūsu tēviem esmu devis, un jūs Man būsiet par ļaudīm, un Es jums būšu par Dievu.
Mtaishi katika nchi niliyowapa baba zenu, ninyi mtakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wenu.
29 Un Es jūs atpestīšu no visas jūsu nešķīstības un aicināšu labību un to vairošu un nevedīšu pār jums badu.
Nitawaokoa ninyi kutoka unajisi wenu wote. Nitaiita nafaka na kuiongeza iwe nyingi sana nami sitaleta njaa juu yenu.
30 Un Es vairošu koku augļus un tīruma augļus, ka jūs bada dēļ starp tautām vairs netopat nicināti.
Nitaongeza matunda ya miti na mazao ya mashamba, ili kwamba msipate tena aibu miongoni mwa mataifa kwa ajili ya njaa.
31 Tad jūs pieminēsiet savus ļaunos ceļus un savus nelabos darbus un būsiet paši sev riebīgi par saviem noziegumiem un par savām negantībām.
Ndipo mtakapozikumbuka njia zenu za uovu na matendo yenu maovu, nanyi mtajichukia wenyewe kwa ajili ya dhambi zote na matendo yenu ya kuchukiza.
32 Un to Es nedaru jūsu dēļ, saka Tas Kungs Dievs, to jums būs zināt. Kaunaties un nosarkstiet savu ceļu dēļ, jūs, Israēla nams!
Ninataka ninyi mjue kwamba sifanyi hili kwa ajili yenu, asema Bwana Mwenyezi. Oneni aibu na mkatahayari kwa ajili ya mwenendo wenu, ee nyumba ya Israeli!
33 Tā saka Tas Kungs Dievs: tai dienā, kad Es jūs šķīstīšu no visas jūsu nešķīstības, tad Es pilsētās likšu dzīvot, un postažas taps uztaisītas.
“‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Siku ile nitakapowasafisha kutoka dhambi zenu zote, nitarudisha watu waishi katika miji yenu na magofu yatajengwa upya.
34 Un tā tukšā zeme atkal taps apkopta, kur posts bija priekš ikviena acīm, kas gāja garām.
Nchi iliyokuwa ukiwa italimwa badala ya kukaa ukiwa machoni mwa wale wote wanaopita ndani yake.
35 Un sacīs: šī zeme, kas bija postā, ir palikusi kā Ēdenes dārzs, un tās iztukšotās un izpostītās un sagruvušās pilsētas ir stipras un apdzīvotas.
Watasema, “Hii nchi iliyokuwa imeachwa ukiwa sasa imekuwa kama bustani ya Edeni, miji ile iliyokuwa magofu, ukiwa na kuangamizwa, sasa imejengewa ngome na kukaliwa na watu.”
36 Tad tās tautas, kas atlikušas visapkārt ap jums, samanīs, ka Es, Tas Kungs, uztaisu sagruvušas vietas un apdēstu, kas ir izpostīts; Es, Tas Kungs, to esmu runājis, un Es to darīšu.
Ndipo mataifa yanayowazunguka yaliyobakia watakapojua kuwa Mimi Bwana nimejenga tena kile kilichoharibiwa na nimepanda tena kile kilichokuwa ukiwa. Mimi Bwana nimenena, nami nitalifanya.’
37 Tā saka Tas Kungs Dievs: Es ļaušos atkal pielūgties no Israēla nama, ka Es tiem parādos; Es vairošu tos ļaudis kā ganāmu pulku.
“Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mara nyingine tena nitasikia maombi ya nyumba ya Israeli na kuwatendea jambo hili: Nitawafanya watu wake kuwa wengi kama kondoo,
38 Tā kā tās svētās avis, kā Jeruzālemes avis savos svētkos, tā būs tās tukšās vietas ar cilvēkiem kā ar ganāmu pulku pilnas, un tie samanīs, ka Es esmu Tas Kungs.
kuwa wengi kama kundi la kondoo kwa ajili ya dhabihu huko Yerusalemu wakati wa sikukuu zao za wakati ulioamriwa. Hivyo ndivyo miji iliyokuwa magofu itajazwa na makundi ya watu. Ndipo watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.”

< Ecechiela 36 >