< Ecechiela 3 >
1 Un Viņš sacīja uz mani: Cilvēka bērns, ēd, kas tavā priekšā, ēd šo satīto grāmatu, un ej un runā uz Israēla namu.
Naye akaniambia, “Mwanadamu, kula kile kilichoko mbele yako, kula huu ukurasa wa kitabu, kisha uende ukaseme na nyumba ya Israeli.”
2 Tad es atdarīju savu muti, un Viņš man deva ēst to satīto grāmatu.
Ndipo nikafungua kinywa changu, naye akanilisha ule ukurasa wa kitabu.
3 Un Viņš sacīja uz mani: Cilvēka bērns, dod savam vēderam ēst un pildi savas iekšas ar šo satīto grāmatu, ko Es tev dodu. Tad es ēdu, un tas bija manā mutē tik salds kā medus.
Ndipo akaniambia, “Mwanadamu, kula ukurasa huu wa kitabu ninaokupa ujaze tumbo lako.” Kwa hiyo nikaula, ulikuwa mtamu kama asali kinywani mwangu.
4 Un Viņš sacīja uz mani: Cilvēka bērns, ej pie Israēla nama un runā uz tiem Manus vārdus.
Kisha akaniambia, “Mwanadamu, sasa nenda katika nyumba ya Israeli ukaseme nao maneno yangu.
5 Jo tu netopi sūtīts pie ļaudīm, kam tumša valoda un grūta mēle, bet uz Israēla namu,
Hukutumwa kwa taifa lenye maneno ya kutatiza na lugha ngumu, bali kwa nyumba ya Israeli.
6 Ne pie lielām tautām, kam tumšas valodas un grūtas mēles, kuru vārdus tu nevari saprast; bet pie tiem Es tevi esmu sūtījis, tie tevi var saprast.
Sikukutuma kwa mataifa mengi yenye maneno ya kutatiza na lugha ngumu ambao maneno yao hutayaelewa. Hakika ningekutuma kwa watu hao, wangekusikiliza.
7 Bet Israēla nams negribēs tevi klausīt, tāpēc ka tie Mani negrib klausīt. Jo visam Israēla namam ir bieza piere un cieta sirds.
Lakini nyumba ya Israeli haitakusikiliza kwa kuwa hawako radhi kunisikiliza mimi, kwa kuwa nyumba yote ya Israeli ni wenye vipaji vya nyuso vigumu na mioyo ya ukaidi.
8 Redzi, tavu vaigu Es daru cietu kā viņu vaigu, un tavu pieri biezu kā viņu pieri
Tazama nimefanya uso wako mgumu dhidi ya nyuso zao na kipaji cha uso wako kigumu dhidi ya vipaji vya nyuso zao.
9 Tavu pieri Es esmu darījis kā dimantu, cietāku pār klinti. Nebīsties no tiem un neiztrūksties no viņu vaiga; jo tie ir atkāpēju suga.
Kama vile almasi ilivyo ngumu kuliko gumegume, ndivyo nilivyokifanya kipaji cha uso wako. Usiwaogope wala usiwahofu, ijapokuwa ni nyumba ya kuasi.”
10 Un Viņš sacīja uz mani: Cilvēka bērns, ņem pie sirds visus Manus vārdus, ko Es uz tevi runāšu, un klausies tos ar savām ausīm.
Naye akaniambia, “Mwanadamu, sikiliza kwa makini na uyatie moyoni mwako maneno yote nitakayosema nawe.
11 Un ej pie tiem aizvestiem, pie savu ļaužu bērniem, un runā uz tiem un saki uz tiem: tā saka Tas Kungs Dievs; - vai tie nu klausa, vai neklausa.
Kisha nenda kwa watu wa taifa lako walio uhamishoni, ukaseme nao. Waambie, ‘Hivi ndivyo Bwana Mwenyezi asemavyo,’ kwamba watasikiliza au hawatasikiliza.”
12 Tad Tas Gars mani pacēla, un es dzirdēju aiz sevis liela trokšņa balsi, kad Tā Kunga godība pacēlās no savas vietas,
Ndipo Roho akaniinua, nikasikia sauti kubwa nyuma yangu ya ngurumo. (Utukufu wa Bwana na utukuzwe katika mahali pa makao yake!)
13 Un (es dzirdēju) to dzīvo spārnus, kas viens pie otra sniedzās, un to skrituļu rībēšanu viņiem līdzās un liela trokšņa skaņu.
Ilikuwa ni sauti ya mabawa ya wale viumbe hai yakisuguana moja kwa jingine, sauti kama ya ngurumo.
14 Tad Tas Gars mani pacēla un mani aizņēma, un es gāju rūgts sava gara karstumā, bet Tā Kunga roka bija pār mani stipra.
Ndipo Roho aliponiinua na kunipeleka mbali. Nikaenda nikiwa na uchungu na hasira moyoni mwangu, nao mkono wa Bwana ukiwa juu yangu.
15 Un es nonācu uz Telabību pie tiem aizvestiem, kas dzīvoja pie Ķebaras upes, un paliku tur, kur tie dzīvoja, un paliku tur viņu vidū septiņas dienas ļoti noskumis.
Nikafika kwa wale watu waliokuwa uhamishoni huko Tel-Abibu karibu na Mto Kebari. Nikakaa miongoni mwao kwa muda wa siku saba, nikiwa nimejawa na mshangao.
16 Un pēc septiņām dienām Tā Kunga vārds uz mani notika sacīdams:
Mwishoni mwa hizo siku saba neno la Bwana likanijia kusema:
17 Cilvēka bērns, Es tevi esmu licis par sargu Israēla namam, ka tev no Manas mutes būs klausīties to vārdu un viņiem no Manas puses piekodināt.
“Mwanadamu, nimekufanya uwe mlinzi wa nyumba ya Israeli, kwa hiyo sikia neno nisemalo, ukawape onyo litokalo kwangu.
18 Kad Es saku uz bezdievīgo: tu mirdams mirsi, - un tu viņu nepamāci un nerunā, ka tu bezdievīgo atgriezi no viņa bezdievīgā ceļa un viņu paturi dzīvu, tad bezdievīgais nomirs savā noziegumā, bet viņa asinis Es prasīšu no tavas rokas.
Nimwambiapo mtu mwovu, ‘Hakika utakufa,’ na wewe usipomwonya mtu huyo au kumshauri aache njia zake mbaya ili kuokoa maisha yake, huyo mtu mwovu atakufa katika dhambi yake na damu yake nitaidai mkononi mwako.
19 Bet kad tu bezdievīgo pamāci un viņš neatgriežas no savas bezdievības un no sava bezdievīgā ceļa, tad viņš nomirs savā noziegumā, bet tu savu dvēseli esi izglābis.
Lakini ukimwonya mtu mwovu naye akakataa kuacha uovu wake na njia zake mbaya, atakufa katika dhambi yake, lakini wewe utakuwa umejiokoa nafsi yako.
20 Un kad taisnais nogriežas no savas taisnības un dara ļaunu, tad Es viņam likšu piedauzīties, un tas mirs; kad tu viņu neesi pamācījis, tad viņš nomirs savos grēkos, un viņa taisnība, ko viņš darījis, netaps pieminēta, bet viņa asinis Es prasīšu no tavas rokas.
“Tena, mtu mwenye haki akiacha haki yake na kutenda maovu, nami nikaweka kikwazo mbele yake mtu huyo atakufa. Kwa kuwa hukumwonya, atakufa katika dhambi yake. Mambo ya haki aliyotenda, hayatakumbukwa, damu yake nitaidai mkononi mwako.
21 Bet kad tu taisno pamāci, ka tam taisnam nebūs grēkot, un viņš negrēko, tad viņš tiešām dzīvos, tāpēc ka tas ir tapis pamācīts, un tu savu dvēseli esi izglābis.
Lakini ukimwonya mwenye haki asitende dhambi na akaacha kutenda dhambi, hakika ataishi kwa sababu alipokea maonyo na utakuwa umejiokoa nafsi yako.”
22 Un Tā Kunga roka bija tur uz manis, un Viņš uz mani sacīja: celies, ej ārā ielejā, un tur Es ar tevi runāšu.
Mkono wa Bwana ulikuwa juu yangu huko, naye akaniambia, “Simama uende mpaka sehemu tambarare, nami nitasema nawe huko.”
23 Tad es cēlos un izgāju ielejā, un redzi, tur stāvēja Tā Kunga godība, tā kā tā godība, ko es biju redzējis pie Ķebaras upes. Un es nokritu uz savu vaigu.
Kwa hiyo niliinuka nikaenda mpaka mahali pa tambarare. Utukufu wa Bwana ulikuwa umesimama huko, kama utukufu ule niliouona kando ya Mto Kebari, nami nikaanguka kifudifudi.
24 Tad gars nāca iekš manis un mani cēla kājās, un Viņš runāja uz mani un sacīja uz mani: ej, ieslēdzies savā namā.
Ndipo Roho akaja ndani yangu akanisimamisha kwa miguu yangu. Akasema nami akaniambia: “Nenda ukajifungie ndani ya nyumba yako.
25 Un redzi, tu cilvēka bērns, tev apliks virves, un tevi ar tām saistīs, un tu no tām nevarēsi noiet viņu vidū.
Nawe, ee mwanadamu, watakufunga kwa kamba, watakufunga ili usiweze kutoka na kuwaendea watu.
26 Un Es tavai mēlei likšu pielipt pie zoda, un tu paliksi mēms un tiem nebūsi par pārmācītāju; jo tie ir atkāpēju suga.
Nitaufanya ulimi wako ushikamane kwenye kaa la kinywa chako, ili uwe kimya usiweze kuwakemea, wajapokuwa ni nyumba ya kuasi.
27 Bet kad Es ar tevi runāšu, tad Es atdarīšu tavu muti, un tev būs sacīt uz tiem: tā saka Tas Kungs Dievs! Kas klausa, lai klausa, un kas neklausa, lai neklausa; jo tie ir atkāpēju suga.
Lakini nitakaposema nawe, nitafungua kinywa chako nawe utawaambia, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo.’ Yeyote atakayesikiliza na asikilize, na yeyote atakayekataa na akatae; kwa kuwa wao ni nyumba ya kuasi.