< Ecechiela 14 >
1 Un pie manis atnāca kādi Israēla vecaji un apsēdās manā priekšā.
Baadhi ya wazee wa Israeli walinijia na kuketi mbele yangu.
2 Tad Tā Kunga vārds uz mani notika sacīdams:
Ndipo neno la Bwana likanijia kusema:
3 Cilvēka bērns, šie vīri savus elkadievus uzņēmuši savā sirdī un to, kas viņus apgrēcina, cēluši priekš savām acīm; vai tad tādiem bija Mani jautāt?
“Mwanadamu, watu hawa wameweka sanamu katika mioyo yao na kuweka vitu viovu vya kukwaza mbele ya macho yao. Je, kweli niwaruhusu waniulize jambo lolote?
4 Tādēļ runā ar tiem un saki uz tiem: tā saka Tas Kungs Dievs: ikviens no Israēla nama, kas savā sirdī uzņem elkudievus un ceļ priekš savām acīm, kas viņus apgrēcina, un nāk pie pravieša, - tad Es Tas Kungs viņam atbildēšu pēc viņu elkadievu pulka,
Kwa hiyo sema nao uwaambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Wakati Mwisraeli yeyote anapoweka sanamu moyoni mwake na kuweka kitu kiovu cha kukwaza mbele ya macho yake na kisha akaenda kwa nabii, Mimi Bwana nitamjibu peke yangu sawasawa na ukubwa wa ibada yake ya sanamu.
5 Lai Es Israēla namam sirdi aizgrābju, jo tie visi no Manis ir atkāpušies caur saviem elkadieviem.
Nitafanya jambo hili ili kukamata tena mioyo ya watu wa Israeli, ambao wote wameniacha kwa ajili ya sanamu zao.’
6 Tāpēc saki uz Israēla namu: tā saka Tas Kungs Dievs: atgriežaties un nogriežaties no saviem elkadieviem un nogriežat savu vaigu no visām savām negantībām.
“Kwa hiyo iambie nyumba ya Israeli, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Tubuni! Geukeni kutoka kwenye sanamu zenu na mkatae matendo yenu yote ya machukizo!
7 Jo ikviens no Israēla nama un no tiem svešiniekiem, kas Israēla starpā dzīvo, kas no Manis atkāpjas un uzņem savus elkadievus savā sirdī un ceļ priekš savām acīm, kas viņus apgrēcina, un nāk pie pravieša caur viņu Mani vaicāt, - Es esmu Tas Kungs, - tam no Manis kļūs atbilde,
“‘Mwisraeli yeyote au mgeni yeyote anayeishi katika Israeli anapojitenga nami na kujiwekea sanamu katika moyo wake na kwa hivyo kuweka kitu kiovu cha kukwaza mbele ya macho yake na kisha akamwendea nabii kuuliza shauri kwangu, mimi Bwana nitamjibu mwenyewe.
8 Un Es celšu Savu vaigu pret šo vīru un to likšu par zīmi un sakāmu vārdu un to izdeldēšu no viņa ļaužu vidus, un jūs samanīsiet, ka Es esmu Tas Kungs.
Nitaukaza uso wangu dhidi ya mtu huyo na kumwadhibu na kumfanya ishara kwa watu. Nitamkatilia mbali kutoka watu wangu. Ndipo mtakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.
9 Kad nu kāds pravietis pievilsies un kaut ko runās, šim pravietim Es, Tas Kungs, atkal likšu pievilties, un izstiepšu Savu roku pret viņu un to izdeldēšu no Savu Israēla ļaužu vidus.
“‘Naye nabii kama atakuwa ameshawishika kutoa unabii, Mimi Bwana nitakuwa nimemshawishi nabii huyo, nami nitaunyoosha mkono wangu dhidi yake na kumwangamiza kutoka miongoni mwa watu wangu Israeli.
10 Tā tie nesīs savu noziegumu; kā tā vaicātāja noziegums būs, tāpat būs tā pravieša noziegums,
Watachukua hatia yao, nabii atakuwa na hatia sawa na yule mtu aliyekuja kuuliza neno kwake.
11 Lai Israēla nams no Manis vairs nenomaldās un vairs neapgānās ar visiem saviem pārkāpumiem; tad tie Man būs par ļaudīm, un Es tiem būšu par Dievu, saka Tas Kungs, Dievs.
“‘Ndipo watu wa Israeli hawataniacha tena, wala kujitia unajisi tena kwa dhambi zao zote. Ndipo watakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wao, asema Bwana Mwenyezi.’”
12 Atkal Tā Kunga vārds uz mani notika sacīdams:
Neno la Bwana likanijia kusema,
13 Cilvēka bērns, kad kāda zeme pret Mani apgrēkojās un no Manis atkāpjas, tad Es izstiepšu Savu roku pret viņu un viņai atņemšu maizes padomu un tai sūtīšu badu un izdeldēšu no tās cilvēkus un lopus.
“Mwanadamu, kama nchi itanitenda dhambi kwa kutokuwa waaminifu nami nikinyoosha mkono wangu dhidi yake kukatilia mbali upatikanaji wake wa chakula na kuipelekea njaa na kuua watu wake na wanyama wao,
14 Jebšu šie trīs vīri, Noa, Daniēls un Ījabs būtu viņas vidū, tad tie caur savu taisnību tikai izglābtu savas dvēseles, saka Tas Kungs Dievs.
hata kama watu hawa watatu: Noa, Danieli na Ayubu wangekuwa ndani ya nchi hiyo, ndio hao tu wangeweza kujiokoa wenyewe kwa uadilifu wao, asema Bwana Mwenyezi.
15 Un ja Es sūtītu niknus zvērus tai zemē, ka tā paliktu bez ļaudīm un par tuksnesi un to zvēru dēļ neviens tur nestaigātu,
“Au kama nikipeleka wanyama pori katika nchi hiyo yote na kuifanya isiwe na watoto, nayo ikawa ukiwa kwamba hakuna mtu apitaye katika nchi hiyo kwa sababu ya wanyama pori,
16 Un šie trīs vīri būtu viņas vidū, - tik tiešām kā Es dzīvoju, saka Tas Kungs Dievs, tie neizglābtu nedz dēlus nedz meitas; tie paši vien izglābtos, bet tā zeme paliktu par tuksnesi.
hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, hata kama watu hawa watatu wangekuwa humo ndani yake, wasingeweza kuokoa wana wao wala binti zao. Wao peke yao wangeokolewa, lakini nchi ingekuwa ukiwa.
17 Jeb kad Es zobenu sūtītu pār šo zemi un sacītu: zoben, ej pa to zemi! Un Es no tās izdeldētu cilvēkus un lopus,
“Au kama nikileta upanga dhidi ya nchi hiyo na kusema, ‘Upanga na upite katika nchi yote,’ nami nikiua watu wake na wanyama wao,
18 Jebšu tie trīs vīri būtu viņas vidū, tik tiešām kā Es dzīvoju, saka Tas Kungs Dievs, tie neizglābtu nedz dēlus nedz meitas, bet paši vien izglābtos.
hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, hata kama watu hawa watatu wangekuwa humo ndani yake, wasingeweza kuokoa wana wao wala binti zao. Wao wenyewe tu wangeokolewa.
19 Jeb kad Es mēri sūtītu šai zemē, un pār to izgāztu savu bardzību ar asinīm, un izdeldētu no tās cilvēkus un lopus,
“Au kama nikipeleka tauni katika nchi hiyo na kumwaga ghadhabu yangu juu yake kwa njia ya kumwaga damu, kuua watu wake na wanyama wao,
20 Jebšu Noa, Daniēls un Ījabs būtu viņas vidū, tik tiešām kā Es dzīvoju, saka Tas Kungs Dievs, tie neizglābtu nedz dēlus nedz meitas, bet caur savu taisnību tie izglābtu tikai savu dvēseli.
hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, hata kama Noa, Danieli na Ayubu wangekuwa humo ndani yake, wasingeweza kumwokoa mwana wala binti. Wao wangeweza kujiokoa wenyewe tu kwa uadilifu wao.
21 Bet tā saka Tas Kungs Dievs: jebšu Es pret Jeruzālemi sūtīšu Savas četras sodības, zobenu un badu un niknus zvērus un mēri, un izdeldēšu cilvēkus un lopus no turienes,
“Kwa maana hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Itakuwa vibaya kiasi gani nitakapopeleka dhidi ya Yerusalemu hukumu zangu nne za kutisha, yaani, upanga, njaa, wanyama pori na tauni, ili kuua watu wake na wanyama wao!
22 Tomēr redzi, tur atliks kādi izglābti, kas taps izvesti, dēli un meitas; redzi, tie nāks pie jums, un jūs redzēsiet, kā tiem klājās un ko tie dara, un tapsiet iepriecināti pār to ļaunumu, ko Es esmu vedis pār Jeruzālemi ar visu to citu, ko Es pār to esmu vedis.
Lakini watakuwepo wenye kuokoka, wana na binti wataletwa kutoka nje ya nchi hiyo. Watawajia ninyi, nanyi mtakapoona mwenendo wao na matendo yao, mtafarijika kuhusu maafa niliyoleta juu ya Yerusalemu, kwa ajili ya yale yote niliyoleta juu yake.
23 Tie jūs iepriecinās, kad jūs redzēsiet, kā tiem klājās un ko tie dara, un jūs redzēsiet, ka Es neesmu darījis bez iemesla, ko Es tur esmu darījis, saka Tas Kungs Dievs.
Mtafarijika wakati mtakapoona mwenendo wao na matendo yao, kwa kuwa mtajua kwamba sikufanya lolote ndani yake bila sababu, asema Bwana Mwenyezi.”