< Otra Mozus 9 >
1 Tad Tas Kungs sacīja uz Mozu: ej pie Faraona un runā uz to: tā saka Tas Kungs, tas Ebreju Dievs: atlaid Manus ļaudis, ka tie Man kalpo;
Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Nenda kwa Farao ukamwambie, ‘Hili ndilo Bwana, Mungu wa Waebrania asemalo: “Waachie watu wangu waende ili wapate kuniabudu.”
2 Jo ja tu liegsies, tos atlaist un tos vēl ilgāki aizturēsi,
Kama ukikataa kuwaachia waende, nawe ukiendelea kuwashikilia,
3 Redzi, tad Tā Kunga roka būs pār tavu ganāmupulku, kas ir laukā, pār zirgiem, pār ēzeļiem, pār kamieļiem, pār vēršiem un pār sīkiem lopiem ar varen grūtu mēri.
mkono wa Bwana utaleta pigo baya kwa mifugo yako, juu ya farasi wako, punda, ngamia, ngʼombe wako, kondoo na mbuzi.
4 Un Tas Kungs darīs brīnišķu starpību starp Israēla lopiem un ēģiptiešu lopiem, ka tur no visa, kas Israēla bērniem pieder, nevienam nebūs mirt.
Lakini Bwana ataweka tofauti kati ya mifugo ya Israeli na ile ya Misri, kwamba hakuna mnyama wa Mwisraeli atakayekufa.’”
5 Un Tas Kungs nolika īpašu laiku un sacīja: rītu Tas Kungs to darīs šinī zemē.
Bwana akaweka wakati na kusema, “Kesho Bwana atalitenda hili katika nchi.”
6 Un Tas Kungs to darīja tai nākošā dienā, un visi ēģiptiešu lopi nomira, bet no Israēla bērnu lopiem nemira neviens.
Siku iliyofuata Bwana akalitenda: Mifugo yote ya Wamisri ikafa, lakini hakuna hata mnyama mmoja wa wana wa Israeli aliyekufa.
7 Un Faraons nosūtīja, un redzi (patiesi), no Israēla lopiem nebija neviens nomiris. Bet Faraona sirds apcietinājās un viņš neatlaida tos ļaudis.
Farao akatuma watu kuchunguza, nao wakakuta kuwa hakuna hata mnyama mmoja wa Waisraeli aliyekufa. Lakini moyo wa Farao haukukubali kuwaachia watu waende.
8 Tad Tas Kungs sacīja uz Mozu un Āronu: ņemat pilnas saujas pelnu no krāsns, un lai Mozus tos kaisa pret debesīm Faraonam redzot,
Kisha Bwana akamwambia Mose na Aroni, “Chukueni majivu ya tanuru, naye Mose ayarushe angani mbele ya Farao.
9 Ka tie izput pār visu Ēģiptes zemi un paliek par trumiem, kas izsitās ar pūtēm pie cilvēkiem un pie lopiem pa visu Ēģiptes zemi.
Yatakuwa vumbi jepesi juu ya nchi yote ya Misri, pia yatatokea majipu yenye kufura juu ya watu na wanyama katika nchi yote.”
10 Un tie ņēma pelnus no krāsns un stājās Faraona priekšā, un Mozus tos kaisīja pret debesīm, - tad izsitās trumi ar pūtēm pie cilvēkiem un pie lopiem.
Basi wakachukua majivu kwenye tanuru na kusimama mbele ya Farao. Mose akayarusha hewani, nayo majipu yenye kufura yakatokea miilini mwa watu na wanyama.
11 Tā ka tie burvji priekš Mozus nevarēja stāvēt to trumu dēļ, jo trumi bija pie tiem burvjiem un pie visiem ēģiptiešiem.
Waganga hawakuweza kusimama mbele ya Mose kwa sababu ya majipu yale yaliyokuwa miilini mwao na juu ya miili ya Wamisri wote.
12 Bet Tas Kungs apcietināja Faraona sirdi, ka tas tiem neklausīja, kā Tas Kungs uz Mozu bija runājis.
Lakini Bwana akaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu, naye hakuwasikiliza Mose na Aroni, sawasawa kama vile Bwana alivyokuwa amemwambia Mose.
13 Tad Tas Kungs sacīja uz Mozu: celies rīt agri un stājies Faraona priekšā un runā uz to: tā saka Tas Kungs, tas Ebreju Dievs, atlaid Manus ļaudis, ka tie Man kalpo.
Kisha Bwana akamwambia Mose, “Amka mapema asubuhi, usimame mbele ya Farao, umwambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Waebrania: Waachie watu wangu waende, ili kwamba waweze kuniabudu,
14 Jo šo brīdi Es sūtīšu visas Savas mocības tavā sirdī un pār taviem kalpiem un pār taviem ļaudīm, ka tev būs atzīt, ka neviens nav tāds kā Es pa visu zemes virsu.
au wakati huu nitaleta mapigo yangu yenye nguvu dhidi yako, maafisa wako na watu wako, ili upate kujua kuwa hakuna mwingine kama Mimi katika dunia yote.
15 Jo Es Savu roku jau būtu izstiepis un tevi un tavus ļaudis sitis ar mēri, ka tu no zemes būtu izdeldēts;
Kwa kuwa mpaka sasa ningelikuwa nimenyoosha mkono wangu na kukupiga wewe na watu wako kwa pigo ambalo lingekufutilia mbali juu ya nchi.
16 Bet patiesi, tāpēc Es tevi esmu taupījis, ka Es Savu spēku pie tevis parādītu, un ka Mans vārds taptu teikts pa visu zemes virsu.
Lakini nimekuinua wewe kwa kusudi hili hasa, ili nipate kukuonyesha uwezo wangu, na ili Jina langu lipate kutangazwa duniani yote.
17 Vai tu vēl celies pret Maniem ļaudīm, negribēdams tos atlaist?
Bado unaendelea kujiinua juu ya watu wangu, wala hutaki kuwaachia waende.
18 Redzi, rīt ap šo laiku Es likšu krist varen lielai krusai, kāda vēl nav bijusi Ēģiptes zemē no tās dienas, kamēr tā ir celta, līdz šim.
Kwa hiyo, kesho wakati kama huu nitaleta mvua mbaya sana ya mawe ambayo haijapata kunyesha katika nchi ya Misri, tangu siku ilipoumbwa mpaka leo.
19 Un nu sūti un sadzen savus lopus, un visu, kas tev ir uz lauka; visi cilvēki un lopi, kas laukā atradīsies un pajumtā nebūs sadzīti, tie nomirs, kad šī krusa uz viņiem kritīs.
Sasa toa amri urudishe wanyama wote watoke malishoni na chochote ambacho kipo mashambani waje mpaka mahali pa usalama, kwa sababu mvua ya mawe itanyesha juu ya kila mtu na kila mnyama ambaye hajaletwa ndani ambao bado wako nje mashambani, nao watakufa.’”
20 Kurš nu no Faraona kalpiem Tā Kunga vārdu bijās, tas saviem kalpiem un saviem lopiem lika bēgt pajumtā.
Wale maafisa wa Farao ambao waliliogopa neno la Bwana wakafanya haraka kuwaleta watumwa wao na mifugo yao ndani.
21 Bet kurš savā sirdi Tā Kunga vārdu nelika vērā, tas savus kalpus un savus lopus pameta laukā.
Lakini wale waliopuuza neno la Bwana wakawaacha watumwa wao na mifugo yao shambani.
22 Tad Tas Kungs sacīja uz Mozu: izstiep savu roku pret debesīm, un lai krusa nāk visā Ēģiptes zemē pār cilvēkiem un pār lopiem un pār visiem lauka augļiem Ēģiptes zemē.
Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Nyoosha mkono wako kuelekea angani ili kwamba mvua ya mawe inyeshe juu ya Misri yote, juu ya watu, wanyama na juu ya kila kitu kiotacho katika mashamba ya Misri.”
23 Un Mozus izstiepa savu zizli pret debesīm. Un Tas Kungs izlaida pērkonus un krusu, un uguns nošāvās uz zemi.
Mose alipoinyoosha fimbo yake kuelekea angani, Bwana akatuma ngurumo na mvua ya mawe, umeme wa radi ulimulika hadi nchi. Kwa hiyo Bwana akaifanya mvua ya mawe kunyesha juu ya nchi ya Misri,
24 Un Tas Kungs lika krusai līt pār Ēģiptes zemi, un tur bija krusa un uguns laistījās krusā, ļoti briesmīgs, kāds nav bijis Ēģiptes zemē, kamēr ļaudis tur bijuši.
mvua ya mawe ikanyesha na radi ikamulika pote. Ikawa dhoruba ya kutisha ambayo haijakuwako katika nchi ya Misri, tangu nchi hiyo iwe taifa.
25 Un krusa apsita visā Ēģiptes zemē visu, kas bija laukā, cilvēkus līdz ar lopiem, un visus lauka augļus krusa apsita un salauzīja visus kokus laukā.
Mvua ya mawe ikaharibu kila kitu katika nchi ya Misri kilichokuwa katika mashamba, watu na wanyama, ikaharibu kila kitu kinachoota mashambani na kuvunja kila mti.
26 Tik Gošenes zemē vien, kur Israēla bērni dzīvoja, krusas nebija.
Mahali pekee ambapo mvua ya mawe haikunyesha ni nchi ya Gosheni, ambako Waisraeli waliishi.
27 Tad Faraons sūtīja un aicināja Mozu un Āronu un tiem sacīja: es šo brīdi esmu grēkojis; Tas Kungs ir taisns, bet es un mani ļaudis esam bezdievīgi.
Ndipo Farao akawaita Mose na Aroni akawaambia, “Wakati huu nimetenda dhambi. Bwana ni mwenye haki, mimi na watu wangu ni wakosaji.
28 Lūdziet To Kungu, lai ir gan (pietiek), ka Dieva pērkoni un krusa apstātos, tad es jūs atlaidīšu un jums vairs nebūs palikt.
Mwombeni Bwana, kwa kuwa tumepata ngurumo na mvua za mawe za kututosha. Nitawaachia mwondoke; hamtahitaji kungoja zaidi.”
29 Tad Mozus uz viņu sacīja: kad no pilsētas iziešu, es savas rokas izstiepšu uz To Kungu, tad pērkoni mitēsies, un krusas vairs nebūs, lai tu atzīsti, ka tā zeme pieder Tam Kungam.
Mose akamjibu, “Nitakapokuwa nimetoka nje ya mji, nitanyoosha mikono yangu juu kumwomba Bwana. Ngurumo zitakoma na hapatakuwepo mvua ya mawe tena, ili upate kujua kuwa, nchi ni mali ya Bwana.
30 Tomēr tevi un tavus kalpus es zinu, ka jūs vēl nebīsities Dievu, To Kungu.
Lakini ninajua kuwa wewe na maafisa wako bado hammwogopi Bwana Mungu.”
31 Tā tapa apsisti lini un mieži, jo mieži bija izplaukuši, un liniem jau bija galviņas.
(Kitani na shayiri viliharibiwa, kwa kuwa shayiri ilikuwa na masuke, na kitani ilikuwa katika kutoa maua.
32 Bet kvieši un rudzi netapa apsisti, jo tie bija vēlu sēti.
Hata hivyo, ngano na jamii nyingine ya ngano hazikuharibiwa kwa sababu zilikuwa hazijakomaa bado.)
33 Tad Mozus aizgāja no Faraona, no pilsētas ārā, un izstiepa savas rokas uz To Kungu, un pērkoni un krusa mitējās, un lietus vairs negāzās zemē.
Kisha Mose akaondoka kwa Farao akaenda nje ya mji. Mose akanyoosha mikono yake kuelekea kwa Bwana, ngurumo na mvua ya mawe vikakoma, mvua haikuendelea tena kunyesha nchini.
34 Kad nu Faraons redzēja, ka lietus un krusa un pērkoni mitējās, tad viņš vēl vairāk apgrēkojās un apcietināja savu sirdi, viņš un viņa kalpi.
Farao alipoona kwamba mvua ya mawe na ngurumo zimekoma, akafanya dhambi tena. Yeye na maafisa wake wakafanya mioyo yao kuwa migumu.
35 Tā Faraona sirds apcietinājās, ka viņš Israēla bērnus neatlaida, kā Tas Kungs caur Mozu bija runājis.
Kwa hiyo moyo wa Farao ukawa mgumu, wala hakuwaachia Waisraeli waende, kama vile Bwana alivyokuwa amesema kupitia Mose.