< Amosa 7 >
1 Tas Kungs Dievs man šādu lietu lika redzēt, un redzi, Viņš rādīja siseņus, kad atāls sāka augt, un redzi, atāls bija audzis pēc ķēniņa pļaušanas.
Hili ndilo alilonionyesha Bwana Mwenyezi katika maono: Alikuwa anaandaa makundi ya nzige baada ya kuvunwa fungu la mfalme na wakati ule tu mimea ya pili ilipokuwa ikichipua.
2 Un kad tie zāli zemes virsū visnotaļ bija aprijuši, tad es sacīju: Kungs Dievs, piedod jel! Kā Jēkabs varēs pastāvēt, jo viņš ir mazs.
Wakati nzige walikuwa wamekula mimea yote ya nchi, nililia kwa sauti kuu, “Bwana Mwenyezi, samehe! Je, Yakobo atawezaje kuendelea kuishi? Yeye ni mdogo sana!”
3 Tad Tam Kungam bija žēl; tas nenotiks, sacīja Tas Kungs. -
Kwa hiyo Bwana akaghairi. Kisha Bwana akasema, “Hili halitatokea.”
4 Atkal Tas Kungs Dievs man šādu lietu lika redzēt, un redzi, Tas Kungs Dievs sauca un gribēja ar uguni sodīt, un tas jau norija to lielo jūru un aprija arī vienu zemes gabalu.
Hili ndilo Bwana Mwenyezi alilonionyesha katika maono: Bwana Mwenyezi alikuwa akiita hukumu ya moto; nao ulikausha vilindi vikuu, ukateketeza nchi.
5 Tad es sacīju: Kungs Dievs, mitējies jel! Kā Jēkabs varēs pastāvēt, jo viņš ir mazs.
Ndipo nikalia, “Bwana Mwenyezi, nakusihi, zuia! Je, Yakobo atawezaje kuendelea kuishi? Yeye ni mdogo sana!”
6 Tad tas Tam Kungam bija žēl; ir tas nenotiks, - sacīja Tas Kungs Dievs.
Kwa hiyo Bwana akaghairi. Bwana Mwenyezi akasema, “Hili nalo halitatokea.”
7 Atkal viņš man šādu lietu lika redzēt, un redzi, Tas Kungs stāvēja uz stāva mūra, un lote(svina svērtenis) bija Viņa rokā.
Hili ndilo alilonionyesha katika maono: Bwana alikuwa amesimama karibu na ukuta ambao ulikuwa umejengwa kwa timazi, akiwa na uzi wa timazi mkononi mwake.
8 Un Tas Kungs sacīja uz mani: ko tu redzi, Amos? Tad es sacīju: loti. Tad Tas Kungs sacīja: redzi, Es pielikšu loti vidū Maniem Israēla ļaudīm, un viņus vairs netaupīšu;
Naye Bwana akaniuliza, “Je, Amosi unaona nini?” Nikamjibu, “Uzi wa timazi.” Kisha Bwana akasema, “Tazama, ninaweka uzi wa timazi miongoni mwa watu wangu Israeli; sitawahurumia tena.
9 Bet Īzaka elku kalni taps iznīcināti, un Israēla svētās vietas taps nopostītas, un Es celšos pret Jerobeama namu ar zobenu.
“Mahali pa Isaki pa juu pa kuabudia miungu pataangamizwa, na mahali patakatifu pa Israeli pa kuabudia pataharibiwa; kwa upanga wangu nitainuka dhidi ya nyumba ya Yeroboamu.”
10 Tad Amacīja, Bēteles priesteris, sūtīja pie Jerobeama, Israēla ķēniņa, un sacīja: Amos ceļ dumpi pret tevi Israēla nama vidū, zeme nevar panest visus viņa vārdus.
Kisha Amazia kuhani wa Betheli akatuma ujumbe kwa Yeroboamu mfalme wa Israeli, akisema: “Amosi analeta fitina juu yako katikati ya Israeli. Nchi haiwezi kuvumilia maneno yake yote.
11 Jo tā saka Amos: Jerobeams nomirs caur zobenu, un Israēls vešus no savas zemes taps aizvests.
Kwa kuwa hili ndilo Amosi analosema: “‘Yeroboamu atakufa kwa upanga, na kwa hakika Israeli watakwenda uhamishoni, mbali na nchi yao.’”
12 Un Amacīja sacīja uz Amosu: tu redzētāj, ej, bēdz uz Jūda zemi, un ēd tur savu maizi,
Kisha Amazia akamwambia Amosi, “Nenda zako, ewe mwonaji! Urudi katika nchi ya Yuda. Ujipatie riziki yako huko na kutoa unabii wako.
13 Un sludini tur, bet Bētelē tev joprojām vairs nebūs sludināt, jo te ir ķēniņa svētā vieta, un te ir valsts pilsēta.
Usiendelee kutoa unabii katika Betheli, kwa sababu hapa ni mahali pa mfalme pa kuabudia na Hekalu la ufalme huu.”
14 Tad Amos atbildēja un sacīja uz Amacīju: es neesmu pravietis nedz pravieša dēls, bet es esmu lopu gans un lasu meža vīģes;
Amosi akamjibu Amazia, “Mimi sikuwa nabii wala mwana wa nabii, lakini nilikuwa mchungaji wa kondoo na mtunza mikuyu.
15 Bet Tas Kungs mani ņēmis no ganāmā pulka, un Tas Kungs uz mani sacījis: ej, sludini Maniem Israēla ļaudīm.
Lakini Bwana akanitoa kutoka kuchunga kondoo na kuniambia, ‘Nenda, ukawatabirie watu wangu Israeli.’
16 Nu tad, klausi Tā Kunga vārdu! Tu saki: nesludini pret Israēli un nemāci pret Īzaka namu.
Sasa basi, sikieni neno la Bwana. Ninyi mnasema, “‘Usitabiri dhidi ya Israeli, na uache kuhubiri dhidi ya nyumba ya Isaki.’
17 Tādēļ, tā saka Tas Kungs: tava sieva pilsētā taps par mauku, un tavi dēli un tavas meitas kritīs caur zobenu, un tava zeme taps mērota un izdalīta, un tu mirsi nešķīstā zemē, un Israēls vešus no savas zemes taps aizvests.
“Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana: “‘Mke wako atakuwa kahaba mjini, nao wana wako na binti zako watauawa kwa upanga. Shamba lako litapimwa na kugawanywa, na wewe mwenyewe utafia katika nchi ya kipagani. Nayo Israeli kwa hakika itakwenda uhamishoni, mbali na nchi yao.’”